WALIOCHAGULIWA TEKU MAJINA YAPO HAPA

Chuo Kikuu Theofilo Kisanji (TEKU) kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho ktk mwaka wa masomo 2016/2017.

BOFYA HAPA KUANAGALIA MAJINA


VENANCE BLOG ITAENDELEA KUSOGEZA SELECTION HIZO ZA VYUO MBALIMBALI KADIRI ZINAVYOTOKA.

SELECTION ZA TUMAINI MAKUMIRA NA UNIVERSITY OF IRINGA ZIPO HAPA

Tumaini Makumira

University of Iringa

Chuo Kikuu cha Iringa na Chuo Kikuu Tumaini Makumira vimetoa majina ya waliochaguliwa katika vyuo hivyo.





Uangaliaji wa majina ktk vyuo hivi ni tofauti kwani wao hawatumii Index ya form 4 wala 6 ni majina tu, hivyo kama uliapply na unataka kuona jina tuma jina lako kwenda namba 0753400208. Huduma hii ni bure kabisa.

WALIOCHAGULIWA BUGANDO (CUHAS) MAJINA HAYA HAPA

Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Kikatoliki (Bugando) (CUHAS) kimetoa majina ya wanafunzi mbalimbali waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho.

BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA

Aidha unaweza kutuma jina lako na index ya form four au six bila kusahau kozi uliyoomba chuoni hapo kwenda namba 0753400208 na utaangaliziwa jina bure kabisa.

WALIOCHAGULIWA UDSM, DUCE NA MKWAWA BATCH 1 MAJINA HAYA HAPA



Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na matawi yake DUCE na MKWAWA (MUCE) kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kozi mbalimbali za shahada chuoni hapo kwa mwaka wa masomo 2016/2017.



Unaweza kutuma jina lako, pamoja na namba ya kidato ya cha 4 au 6 kwenda namba 0753400208 na utaangaliziwa jina BURE. Kumbuka kutuma jina lako, index ya 4 au 6 na chuo unachotaka kuangalia hata kama ni zaidi ya kimoja. Mfano: Venance Gilbert s2509/0575/2012 (iv) au s0494/0141/2015 (vi) Mzumbe, MUHAS, SUA, UDSM, UDOM, SAUT n.k. kwenda 0753400208. Huduma hii ni BURE.

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA UDOM BACHELOR DEGREE YAPO HAPA


Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

Ili kuona matokeo haya kwa njia ya  simu hakikisha simu yako ina WPS Office, Polaris Office n.k. kisha BONYEZA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO

VENANCE BLOG IKO NA WEWE, UKISHINDWA KUANGALIA MAJINA HAYO TUMA UJUMBE MFUPI (SMS) UKIANDIKA JINA LAKO NA INDEX YA KIDATO CHA 4 AU 6 KWENDA NAMBA 0753400208 UTAANGALIZIWA JINA LAKO BURE KABISA KUPEWA MAJIBU.

WALIOCHAGULIWA KOZI ZA SHAHADA CBE KAMPASI YA DAR ES SALAAM

Chuo cha Elimu ya Biashara kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa kwanza wa masomo 2016/2017.
Majina yapo hapa. Kumbuka hili ni toleo la kwanza (First Batch). BOFYA HAPA KUANGALIA

WALIOCHAGULIWA KOZI MBALIMBALI ZA SHAHADA IFM

  Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM) imetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kusoma kozi mbalimbali za Shahada katika fani mbali mbali chuoni hapo.

Majina hayo yako hapa. BOFYA HAPA KUONA MAJINA HAYO

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU TUMAINI MAKUMIRA KAMPAS YA MBEYA HAYA HAPA



Chuo Kikuu Tumaini Makumira kampus ya Mbeya kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Chuo hicho kwa kozi za Shahada ya Elimu na Sanaa (Bachelor of Arts with Education BA.Ed) na Shahada ya Elimu katika Sanaa (Bachelor of Education in Arts BED). Majina hayo yapo kwenye tovuti ya Chuo toka juzi Septemba 15.

KUANGALIA BA.Ed BOFYA HAPA

KUANGALIA BEd BOFYA HAPA

Aidha taarifa zote za Chuo hiko unaweza kuzipata kwa KUBOFYA HAPA

VENANCE BLOG IKO NA WEWE KWA TAARIFA ZOTE ZA VYUO MBALIMBALI NCHINI. ENDELEA KUWA NAMI.

HILLARY CLINTON AMEREJEA KATIKA KAMPENI NA KUMSHAMBULIA TRUMP

Mgombea wa chama cha Democratic katika kinyan'ganyiro cha urais nchini Marekani Hillary Clinton amerejea tena katika kampeni na kutoa kauli ya tahadhari dhidi ya mpinzani wake Donald Trump.

Mgombea wa chama cha Democrats Hillary Clinton akiwahutubia wafuasi wake North Carolina
Mgombea wa chama cha Democrats Hillary Clinton akiwahutubia wafuasi wake North Carolina

Akizungumza katika mikutano miwili tofauti ya kampeni kwenye majimbo mawili, North Carolina na Washington, Hillary Clinton alisema amefurahi kurejea katika kampeni hizo baada ya hapo awali kushauriwa na madaktari kubakia nyumbani hadi atakapopata nafuu kutokana na maradhi ya homa ya mapafu yaliyokuwa yakimkabili.

Hali ya afya ya Hillary Clinton ilidhoofika wakati wa kumbukumbu ya mika 15 tangu yalipofanyika mashambulizi ya kigaidi nchini Marekani tarehe 11/9/ 2001.

"Ni jambo jema kuwa nimerejea katika kampeni" alisema mgombea huyo wa chama cha Democratic huku akishangiliwa na wafuasi wake alipohutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika eneo la Greensboro, North Carolina.

Hillary Clinton alitangaza kuendelea na mikutano ya kampeni katika majimbo ambayo mgombea wa chama cha Republican Donald Trump amekwishafanya mikutano yake ya kampeni ikiwa ni pamoja na jimbo la Florida ambalo kila mgombea anawania kulichukua.

Wakati suala la afya ya wagombea wote wawili likizua mjadala katika mikutano ya kampeni ya viongozi hao , Hillary Clinton alienda mbali zaidi kwa kutoa taarifa zinazohusiana na afya yake akisema ni mwenye afya njema na anaweza vema kutekeleza majukumu ya uongozi. Kwa upande mwingine wakati mgombea wa chama cha Republican Donald Trump akionekana kuwa na uzito mkubwa daktari wake alithibitisha kuwa mgombea huyo ana afya njema.
Hillary Clinton amshambulia Trump
Bildkombo Donald Trump und Hillary Clinton
Akizungumza katika mikutano hiyo ya kampeni Hillary Clinton hakusita kumshambulia kwa maneno Donald Trump kutokana na kauli ya awali aliyoitoa akikataa kusema iwapo ana amini kuwa Rais Barack Obama ni mzaliwa wa Marekani na pia kumkashifu mchungaji mwenye asili ya Afrika ambapo Trump alitembelea kanisa lake mjini Michigan wiki hii.

Kwa miaka kadhaa Donald Trump alikuwa akiendesha harakati akihoji kama Rais Barack Obama amezaliwa nchini Marekani na kutumia majukwaa kutangaza kuwa Rais huyo wa sasa wa Marekani alizaliwa nje ya nchi hiyo na kuwa hakusitahili kuwa Rais wa nchi hiyo kwa mujibu wa katiba ya Marekani.

Hapo jana wakati Trump alipohojiwa na gazeti la Washington Post iwapo ana amini kuwa Rais Obama alizaliwa mjini Hawaii, alishindwa kutoa jibu kwa mara nyingine akisema atajibu swali hilo wakati muafaka utakapowadia. Hata hivyo taarifa iliyotolewa baadaye na waratibu wa mikutano ya kampeni ya mgombea huyo ilisema Trump ana amini kuwa Rais Obama alizaliwa nchini Marekani.

" Baada ya kufanikiwa kupata cheti cha kuzaliwa cha Rais Barack Obama wakati wengine wameshindwa , Donald Trump sasa ana amini kuwa Rais Obama ni mzaliwa wa Marekani " ilisisitiza taarifa hiyo.

Aidha mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton alisema kitendo cha Trump kumshambulia mchungaji kinazidi kumnyima sifa Trump za kuwa Rais wa nchi hiyo na kuwataka wapiga kura kumkataa wakati wa uchaguzi wa mwezi Novemba.


Chanzo: DW

MTU MMOJA AMEJITOA MUHANGA NA KUUA WATU 16 KATIKA MSIKITI WA MOHMAND PAKISTAN

Takribani watu 16 wameuawa na wengine 35 kujeruhiwa katika swala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Mohmand huko Pakistan.

Duru za habari zinasema kuwa mtu huyo aliyejitoa muhanga ameua watu 16 na wengine 35 kujeruhiwa walipokuwa wakihudhuria swala ya Ijumaa kaskazini mashariki mwa  Pakistan.

Shambulio hilo limetokea katika kijiji cha Anbar Tehsil katika wilaya inayokaliwa na kabila la Mohmand ambapo jeshi la Pakistan limekuwa likipambana na kundi la Taliban.

"Swala ya Ijumaa ilikuwa ikiendelea msikitini hapo wakati ambapo mshambuliaji huyo wa kujitoa muhanga alijilipua na kuua waumini 16 na kujeruhi wengine 35" kiongozi mmoja wa Mohmand aliliambia shirika la habari la AFP.

Hakujatokea taarifa zozote kuhusu shambulio hilo, lakini kundi la Taliban linashutumiwa kuhusika na shambulio hilo kwa kuwa limekuwa likifanya mashambulio katika maeneo ya mahakama, shule na misikiti.

Jeshi la Pakistan limekuwa likifanya operesheni toka Juni 2014 kuangamiza makundi yote ya kigaidi yaliweka ngome kaskazini mashariki mwa maeneo hayo ili kuepusha vifo vya watu wasio na hatia toka 2004.


Chanzo: Al Jazeera

LEO SEPTEMBA 14 KATIKA HISTORIA

Rapa Nas Escobar alizaliwa September 13, 1973.
Leo ni Jumatano Septemba 14, 2016. Ni siku ya 258 katika mwaka 2016. Zimesalia siku 108 kuukamilisha mwaka 2016.

MATUKIO

1960 - Iraq, Iran, Kuwait na Saudi Arabia ziliunda jumuiya ya OPEC.

1979 - Nur Muhammad Tarak, Rais na na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Afghanistan aliuawa katika mapinduzi ambapo Waziri Mkuu Hafizullah Amin alishika madaraka.



KUZALIWA

1849 - Mwanasaikolojia wa Urusi, Ivan Pavlov.

1864 - Robert Cecil,  miongoni mwa waanzilishi wa Jumuiya ya Mataifa alizaliwa.

1879 - Margaret Sanger, wakili na muanzilishi wa Uzazi wa mpango.

1973 - Rapa Nas Escobar alizaliwa. 

NEW AUDIO: DOWNLOAD BARAKA DA PRINCE FT ALI KIBA-NISAMEHE MP3

Baraka Da Prince akishirikiana na Ali Kiba wanakusikilizisha kitu hiki hapa kipya, wimbo unaitwa Nisamehe umefanyikwa kwa Imma the Boy.


DOWNLOAD HAPA

TCU IMERUHUSU UDAHILI VYUO VIKUU AWAMU YA PILI

Tume ya Vyuo Vikuu nchini Tanzania (TCU) imeruhusu awamu ya pili ya udahili kwa wanafunzi waliokosa vyuo kwa kukosa sifa katika udahili wa awamu ya kwanza na wale ambao hawakuomba kudahiliwa kabisa.

Aidha TCU inakumbusha kwamba wale waliokwisha omba na hawakupangiwa kwa kukosa sifa stahiki za vyuo walivyopangiwa hawatatakiwa kulipia tena.

Pia wadahiliwa wapya wanatakiwa kulipia kiasi cha fedha za kitanzania Tsh. Elfu Hamsini (50,000/=) kama gharama za udahili. Fedha hii huwa hairudishwi.

Vilevile TCU inakumbusha kwamba kozi ambazo zimejaa tayari hazitaonekana kwenye mfumo wa Udahili (CAS).

Aidha TCU inawakumbusha waombaji kuwa mwisho wa kutuma maombi ya udahili ni Septemba 23 na hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza kwa wale watakaoshindw kuomba vyuo katika muda huo ulioongezwa.


MAELEZO ZAIDI BOFYA HAPA

IGGY AZALEA ASISITIZA YEYE NA FRENCH MONTANA NI MARAFIKI TU

Iggy Azalea amekataa kuwa na uhusiano na French Montana japo wameonekana mara kadhaa wakiwa sehemu za starehe pamoja.
Rapper huyo wa kike ameuambia mtandao wa TMZ kuwa hana mpenzi kwa sasa hivyo yeye na French Montana ni marafiki tu.
“We are Single, I’m single,” amesema Iggy. “just friends.”
Wiki kadhaa zilizopita Iggy alidai kuwa yeye na French Montana kuna wimbo wamefanya ila hawana mahusiano yoyote lakini baada ya wiki moja wawili hao walionekana wakiwa wanakula bata pamoja huko Cabo San Lucas, Mexico. Walionekana pia wakibusiana.

LEO SEPTEMBA 13 KATIKA HISTORIA

Tarehe kama ya leo Septemba 13' Tupac Shakur alifariki.
Leo Septemba 13 siku ya 257 katika mwaka 2016, zimesalia siku 109 kuukamilisha mwaka 2016.


MATUKIO

1759 - Vikosi vya majeshi ya Uingerza viliyashinda majeshi ya Ufaransa katija mapigano kwenye nyanda za Abraham huko Quebec.

1914 - Wanaharakati wa Ireland waliomba msaada kwa wajerumani.

1940 - Italia iliivamia Misri.

1945 - Vikosi vya majeshi ya Uingereza viliingia Japan kupunguza uwezo wa jeshi la Japan.

1993 - Mkataba wa amani kusitisha mapigano Israel na Palestina ulisainiwa.


VIFO

1996 - Mwanamuziki 2Pac Shakur alifariki.


KWA MSAADA WA MTANDAO.

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER


Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi.

KUZALIWA

Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani. 

ELIMU

Alipata Elimu yake katika Village Christian School.

KAZI

Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared.

Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha The Coty Prestige fragrance brand, Davidoff Cool Water for Men na alishiriki katika Chanel zinazoonesha Matukio ya kijiografia chini Marekani katika mfululizo wa vipindi vya Expedition Great White.

Pia alianzisha kikundi cha kusaidia jamii haswa wale wanaokumbwa na majanga ya asili kilichoitwa Reach Out WorldWide (ROWW).

Mpaka mauti yanamfika, Walker alikuwa anaigiza movie 3 ambazo ni Hours (2013), Brick Mansions (2014) na Furious 7 (2015). Wiz Khalifa alimuimbia wimbo wa heshima 'See You Again' ambao ulitumika kama soundtrack ya Furious 7. Wimbo huo ulitajwa kushiriki tuzo za Golden Globe Awards katika kipengele cha Wimbo Bora katika Tuzo ya 73 ya Golden Globe Wards.

MIAKA YA UMAARUFU

Paul Walker alikuwa maarufu kati ya mwaka 1984 hadi mwaka 2013 alipofikwa na mauti.

UTAJIRI ALIOKUWA NAO

Mpaka anafariki alikadiriwa kuwa na utajiri uliofikia dola za kimarekani bilioni 25 kwa makadirio ya mwaka 2014.


MAISHA YAKE

Walker alizaliwa Glendale California na alikuwa ni mtoto wa Cherly ambaye alikuwa mwanamitindo na baba yake Paul William Walker III alikuwa ni mkandarasi na mwanamasumbwi aliyeshinda ubingwa wa Golden Gloves mara mbili.

Paul Walker baada ya kumaliza elimu ya pili (kwa Tanzania kidato cha 5 & 6) alijiunga na vyuo mbali mbali Kusini mwa California akisomea baiolojia ya viumbe wa majini.


DINI

Walker alikuwa ni muumini wa Dini ya Kikristu. Kanisa lake linaitwa Nondenominational Christianity ambalo mwanzo lilijulikana kama The Church of  Jesus Christ of Latter-day Saints.

FAMILIA

Aliacha mtoto mmoja aitwaye Meadow Walker. Pia alikuwa na Ndugu wawili wa kiume; Cody Walker na Caleb Walker.

KIFO

Paul Walker alifariki Novemba 30, 2013 katika ajali mbaya ya gari ambayo alikuwepo yeye na rafiki yake Roger Rodas miaka 38. Siku hiyo Walker akiwa na Roger walikuwa wakielekea katika taasisi yake ya kusaidia watu ROWW ambapo iliwalenga waanga wa kimbunga Typhoon Haiyan (Yolanda). Siku hiyo Roger ndiye aliyekuwa dereva huku Paul akiwa kama abiria. Inadaiwa kuwa Roger aliendesha gari kwa umbali wa maili 45 kwa saa sawa na kilomita 72 kwa saa na baadae gari yao Porsche Carrera GT ilipiga mzinga maeneo ya Kelly Johnson Parkway huko Valencia Santa Clarita California na badae gari yao iliungua. Ajali ilionekana kwenye camera ya ulinzi iliyokuwa maeneo hayo.
Hapa ndipo majivu ya mwili wa Paul Walker yalipozikwa.


Mwaka 2014 uchunguzi zaidi ulionesha kuwa chanzo cha ajali kilikuwa ni mwendokasi ambapo alidaiwa kuwa gari ilikimbizwa katika mwendokasi wa kilomita 103 kwa saa.

Majivu ya mwili wa Paul Walker yalizikwa huko Forest Lawn Memorial Park, Hollywood Hills nchini Marekani.







Hapa akiwa na wenzie wa Fast and Furious.




MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU PAUL WALKER MAHALA PEMA PEPONI.

AMINA!. 

UCHAMBUZI KWA MSAADA WA WIKIPEDIA PICHA KWA HISANI YA MTANDAO.

LEO SEPTEMBA 12 KATIKA HISTORIA

Tarehe kama ya leo Septemba 12, 1973 muigizaji wa Marekani, Paul Walker alizaliwa huko Glendale, Califonia.Alifariki Novemba 30, 2013.
Leo ni tarehe 12 Septemba, siku ya 256 katika mwaka 2016, zimesalia siku 110 kuukamilisha mwaka 2016.

MATUKIO

Leo kuna matukio mengi sana hata hivyo tuyaangalie kama ifuatavyo:

1217 - Mfalme wa Ufaransa Prince Louis na Mfalme wa Uingerza Henry III walisaini mkataba wa amani.

1624 - Meli ya kwanza kupita chini ya maji ilijaribiwa katika Mto Thames kwa ajili ya kutumiwa na Mfalme James I huko Uingereza.

1662 - John Flamsteed aliona nusu ya kupatwa kwa jua na ikampelekea kuvutiwa na elimu ya anga (unajimu)

1703 - Jeshi la Uingereza chini ya Archiduke Charles wa Austria waliwasili nchini Ureno.

1722 - Vikosi vya Urusi viliteka Baku na Derbent huko Persia ambayo kwa sasa ni Iran.

1751 - Amsterdam ilikataa kuanzisha makazi ya Wayahudi.

1753 - Mnajimu wa Ufaransa Charles Messier bila kutarajia aligundua gesi ya miamba (crab nebula) na akaanza utafiti wake (Messier Catalogue)

1848 - Uswisi iliunganisha mataifa yake kupata taifa moja la Uswisi.

1878 - Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alifungua Mkutano wa Kongo.

1885 - Rekodi ya kwanza ya magoli 35 katika mechi ya ligi daraja la kwanza iliwekwa.

1890 - Cecil Rhodes alifika Harare, Zimbabwe kwa wakati ule ikiitwa Fort Salisbury.

1909 - Waarabu walivamia Gedara Palestina.

1919 - Adolf Hitler aliungana na Chama cha Wafanyakazi wa Ujerumani akiwa mwanachama wa saba lakini hakukubaliana na lengo la chama hicho badala yake alisisitiza Utaifa (Harakati za nchi binafsi) na kusisitiza chuki dhidi ya Wayahudi.

1922 - Mwanariadha Paavo Nurmi aliweka rekodi ya dunia kwa kukimbia umbali wa mita 5000 sawa na kilomita 5 kwa daika 14:35.4

1928 - Kimbunga Hurricane kiliua watu 6,000.

1934 - Estonia, Lativia & walisaini mkataba wa Baltic Entente dhidi ya Muungano wa nchi za Kisovieti.

1941 - Meli ya kwanza ya kijerumani katika vita ya pili ya Dunia ilitekwa na meli za Marekani.

1943 - Taifa la Skorzeny lilimuachia Benito Nussolini huko Gran Sasso.

1944 - Vikosi vya Marekani viliingia nchini Ujerumani kwa mara ya kwanza.

1950 - Serikali ya Ubelgiji iliwafukuza wafanyakazi wote wa kikomunisti.

1956 - Wanafunzi weusi waliruhusiwa kusoma shule ya Ckay Ky huko Marekani.

1958 - Marekani ilifanya jaribio lake la Nyuklia katika uwanja wa majaribio wa Nevada.

1958 - Muhandisi Jack Kilby alifanya jaribio la sakiti ya kompyuta aliyogundua kwa msimamizi wake.

1959 - Muungano wa nchi za kisovieti (USSR) ulituma chombo Luna 2 kwenda kwenye mwezi.

1961 - Urusi ilifanya jaribio lake la nyuklia huko Novaya Zemlya.

1971 - Urusi ilituma chombo chake kwenye mwezi Luna 16.

1973 - Urusi ilifanya tena jaribio la Nyuklia huko Novaya Zemlya.

1974 - Mfalme Haile Sellasie alipinduliwa nchini Ethiopia.

1978 - Fidel Castro alitembelea Addis Ababa Ethiopia.

1979 - Indonesia ilikumbwa na tetemeko la ardhi ambalo lilikuwa na ukubwa wa 8.1 katika kipimo cha Richter.

1984 - Ethiopia iliunda Jamhuri ya Kisoshalisti.

1987 - Ethiopia ilianza kufuata utawala wa Katiba.

1992 - Mae Jemison alikuwa mwanamke wa kwanza Mmarwkani mweusi kwenda angani.

1999 - Indonesia ilisema itaruhusu walinzi wa amani Mashariki mwa Timor.

2005 - Israel iliondosha majeshi na vikosi vyake kutoka ukanda wa Gaza.

2007 - Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe alitangaza nia yake ya kujiuzulu wadhifa huo.

2007 - Rais wa zamani wa Ufilipino Joseph Estrada kwa kosa na wizi wa fedha za serikali.

2010 - Lady Gaga na Eminem walichukua tuzo za MTV Video Music.

2012 - Kampuni ya Apple ilitangaza na kuonesha simu zao iPhone 5 na iOS 6.

2015 - Watalii 12 waliuawa bila kukusudia na Jeshi la Misri Magahribi mwa Jangwa la Misri wakidhaniwa kuwa ni waasi.




KUZALIWA

1575 -  Mtafiti wa Uingereza Henry Hudson.

1913 - Mwanaridha Jesse Owen.

1973 - Muigizaji Paul Walker.

1977 - Muigizaji Connor Frante.

1978 - Muigizaji Benjamin McKenzie.

1981 - Muigizaji na Mwanamuziki Jennifer Hudson.



IMEANDALIWA KWA MSAADA WA MTANDAO.

ALI KIBA KUTUMBUIZA TUZO ZA MTV MAMA OKTOBA 22


Mwanamzuki mwenye vionjo vya kipekee Ali Kiba a.k.a. King Kiba amethibitisha katika ukurasa wake wa Facebook kuwa ataperform katika tuzo za MTV MAMA zitakazofanyika Johanesburg Afrika Kusini Octoba 22 mwaka huu.

KATY PERRY AMESEMA ATAFANYA COLLABO NA TAYLOR SWIFT KAMA ATAOMBA MSAMAHA

Katy Perry na Taylor Swift wakiwa Berley Hilton Hotel Januari 30, 2010


Katy Perry na Taylor Swift kufanya  collabo?

 Collabo hiyo inaweza kutokea lakini kwa sharti moja tu kutoka kwa Katy Perry, kama Taylor Swift atakubali kumuomba msamaha.

Hili linakuja baada ya shabiki mmoja wa Katy Perry kuuliza katika mtandao wa Twitter kama Katy Perry anaweza kufanya collabo na Swift, Perry akajibu kwa kifupi "hakika, kama ataomba msamaha"

Mgogoro kati ya mastaa hawa wawili wa Pop ulianza mwaka 2014 kufuatia Swift kumteta Katy katika Mtandao wa The Rolling Stone kuwa wimbo wake "Bad blood" ulikuwa unamhusu Swift.

"Alifanya kitu kibaya sana" alisema Swift. "Ilikuwa kama hivyo. Tumekuwa maadui. Na sababu haikuwa mwanaume. Ni kazi tu. Alijaribu hata kuvuruga tamasha langu. Alijaribu hata kuwapa hela vijana waje kunitoa jukwaani"

JE, KATY PERRY AMETHIBITISHA KUWA WIMBO WA 'BAD BLOOD' UNAMHUSU SWIFT?

Mtandao wa The Internet ulisema kwamba Katy Perry ndiye mwenye makosa, kufuatia baadhi ya madansa wa Swift kuondoka kwenye tour ya Swift kufuatia mpango ulofanywa na Katy Perry.

Muda mfupi baada ya Mahojiano na The Rolling Stone yaliyokuwa ya moja kwa moja, Katy alitweet katika mtandao wa Twitter "Kaa tayari kwa kipindi cha Regina George kuhusu nguo za kondoo".
Baadaye kwenye mahojiano mwaka 2015 na Billboard Perry alisema "kama kuna mtu atajaribu kuniharibia sifa yangu, mtamsikia tu"



Chanzo: Billboard

WALIOKUFA KATIKA TETEMEKO WAFIKIA 16

Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kuaga miili ya waliokufa katika tetemeko la ardhi mkoani Kagera.


Maafa zaidi yameripotiwa katika janga la tetemeko la ardhi, lililotokea juzi mkoani Kagera, ambapo imeripotiwa idadi ya vifo kuongezeka na kufikia watu 16, huku wengine 253 wakijeruhiwa na kusababisha simanzi na masikitiko kwa familia nyingi. Katika tukio hilo, pia nyumba 840 za makazi zimeanguka, nyumba 1,264 zimepata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule yameanguka.

Tukio hilo limemfanya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kulazimika kufanya ziara ya ghafla ya kuwatembelea waathirika wa tetemeko hilo, ambalo limedaiwa kusababisha tafrani pia katika nchi jirani za ukanda wa Afrika Mashariki za Kenya na Rwanda.

Katika hatua nyingine, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimeeleza mpango wa kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga hayo kutokea.

Katika mradi huo maalumu chini ya Kitengo cha Utafiti wa Miamba na Volcano, chuo hicho kitashirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo Ulaya na Marekani, hasa Chuo Kikuu cha Glasgow kilichopo Scotland, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Burton Mwamila. Ziara ya Waziri Mkuu

Akitoa taarifa kwa Waziri Mkuu jana katika Uwanja wa Kaitaba ulioko mjini Bukoba ambapo umeandaliwa maalumu kwa ajili ya kuaga miili ya watu waliopoteza maisha katika tukio hilo la kusikitisha, Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu alisema tukio hilo ni la kwanza kutokea mkoani humo na kwamba limeleta madhara makubwa kwa wananchi na kuacha majonzi makubwa.

Kijuu alisema mpaka taarifa inaandaliwa watu 16 waliripotiwa kupoteza maisha na kusababisha majeruhi 253, huku 170 wakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo na 83 wakitibiwa na kuruhusiwa.

Alisema pia tetemeko hilo limesababisha nyumba 840 za makazi kuanguka, nyumba 1,264 kupata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule kuanguka.

Alisema tetemeko hilo lenye ukubwa wa alama 5.7 uliopimwa kwa kipimo cha Ritcher cha kisayansi cha kupima matetemeko, limeleta madhara makubwa ambapo Serikali ya Mkoa inaendelea kutathmini kwa kina athari zaidi zilizosababishwa na tetemeko hilo na pia uharibifu uliojitokeza kisha kupeleka katika Ofisi ya Waziri Mkuu waone jinsi ya kusaidia.

Alisema hatua zilizochukuliwa na mkoa mpaka sasa ni kuwaokoa na kuwapeleka watu hospitali kwa ajili ya matibabu na kuwapatia makazi ya muda baadhi ya wananchi wenye nyumba zilizoathirika, wakati mipango mingine ikiandaliwa.

Taarifa hiyo ya Mkuu wa Mkoa, ilimfanya Waziri Mkuu kueleza masikitiko yake na serikali kutokana na janga hilo na kutoa salamu za pole kwa wananchi waliopatwa na madhara na kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa na pia maeneo yote yaliyoathirika.

"Leo si siku nzuri kwetu, nimekuja kumwakilisha Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye anawapa pole sana wana Kagera wote na Watanzania kwa ujumla. Pia Makamu wa Rais anawapa pole kwa msiba huu mkubwa, lengo la safari yangu ni kuja kuwapa pole, tukio hili ni kubwa na halijawahi kutokea Tanzania, tumekuwa tukisikia kutoka mataifa ya nje lakini leo limetupata nchini kwetu," alisema Majaliwa.

Aliwasihi na kuwataka wananchi kuwa wavumilivu, kuonesha umoja na ushirikiano, lakini pia kujitokeza kuwafariji wenzao wakati wote wa majonzi, huku akisema Watanzania kwa miaka mingi wamekuwa wakishuhudia mitikisiko midogo, lakini juzi tumeshuhudia mtikisiko mkubwa kabisa ambao umeleta madhara makubwa kwetu.

"Mpaka sasa hatuna uhakika mtikisiko huu utakuwa endelevu kwa kiasi gani, nataka niwahakikishie Watanzania wote, Serikali tunafanya mawasiliano na taasisi zenye uwezo wa kubaini mtikisiko huu ili tuweze kujua jambo hili litakuwa endelevu kwa kiasi gani na kuona dalili na ukubwa wake utakuwaje ili tujipange katika kutoa elimu lakini pia tahadhari pindi jambo kama hili linapoweza kutokea au tunapoona viashiria au dalili za jambo hili," alisema Waziri Mkuu.

Alisema kuwa Mkuu wa Mkoa katika taarifa yake alimweleza kwamba tathmini inaendelea na kwamba ameiagiza Kamati ya Maafa ya Ofisi ya Waziri Mkuu kufika mkoani Kagera mara moja na kuzunguka mkoa mzima kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa kwa lengo la kufanya tathmini ya jumla.

Alisema baada ya tathmini hiyo, utaratibu utafuatwa kwani serikali haiwezi kuwatupa mkono wananchi hao, pia alitumia fursa hiyo kuwaambia wafiwa kuwa Watanzania nchini kote wako pamoja nao katika janga hilo.

Akielezea mkasa huo, majeruhi Happines Apolinary ambaye ni mkazi wa kata ya Buyekera aliyelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera kwa kuumia kichwani na mgongoni, alisema alishtuka kusikia mtikisiko mkubwa wakati akiwa ndani ya nyumba yake na ghafla aliangukiwa na kuta na kumsababishia majeraha. Pamoja na kueleza kuumia vibaya kutokana na tukio hilo, Happines aliwashukuru wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Kagera kwa huduma nzuri waliyompatia tangu juzi alipofikishwa hospitalini hapo.

Majeruhi mwingine, Paulina Spilian aliyelazwa hospitalini hapo akiwa amejeruhiwa miguu alisema akiwa ndani ya nyumba yake ghafla alisikia mtikisiko mkubwa ulioambatana na kishindo cha kuanguka kwa kuta za nyumba na akiwa katika harakati za kutaka kukimbia nje aliangukiwa na ukuta miguuni.

Majeruhi huyo aliiomba Serikali kuwasaidia kwa kuwajengea nyumba na pia kuwapa elimu kuhusiana na matukio kama hayo ili waweze kujiokoa baada ya kuona dalili au viashiria tofauti na ilivyotokea juzi.

Advela Respicius ambaye ni mama wa marehemu, Verdiana Respicius aliyekufa baada ya kufunikwa na kifusi cha nyumba, akizungumza kwa niaba ya familia za wafiwa wa tukio hilo, alitoa shukrani kwa serikali kwa kutoa majeneza, sanda na usafiri wa kuwapeleka marehemu hao mpaka vijijini kwa ajili ya maziko.

Vifaa vya kutabiri kufungwa Wakati hofu ikiwa bado imetawala kutokana na tukio hilo hasa kutokana na wananchi wa Kagera kueleza kutofahamu lolote kabla ya kutokea kwa tetemeko kutokana na kutopewa taarifa zozote na mamlaka za serikali, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimesema kinatarajia kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga hayo kutokea.

Katika mradi huo maalumu chini ya Kitengo cha Utafiti wa Miamba na Volcano, chuo hicho kitashirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo Ulaya na Marekani, lakini hasa Chuo Kikuu cha Glasgow kilichopo Scotland, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Burton Mwamila.

Katika mradi huo wa kwanza nchini unaolenga kutoa utabiri wa matukio ya matetemeko na ulipukaji wa volcano nchini, vifaa maalumu vitakavyokuwa vinapima uwezekano wa kutokea majanga hayo, vitafungwa katika maeneo nyeti kama milima, vilima na sehemu ambazo huwa na volcano hai.

Mtaalamu wa miamba ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya 'Eco Science' inayoshughulika na utafiti wa miamba pamoja na milipuko ya volcano, Dk Ben Beeckmans amefafanua kuwa 'Mlima wa Mungu' (Oldonyo Lengai) uliopo eneo la Ngaresero, wilayani Ngorongoro ndio chanzo kikubwa cha matetemeko ya ardhi katika eneo lote la Afrika Mashariki. Mlima huo wenye volkano hai pia umekuwa ukilipuka mara kwa mara na tukio la mwisho lilirekodiwa mwaka 2007.

Vifaa hivyo vya kutabiri matetemeko ya ardhi vitafungwa kuzunguka eneo la mlima huo, Ziwa Natron, Mlima Meru na hata Mlima Kilimanjaro pamoja na maeneo mengine nchini.

Lakini hatua hiyo si kwamba imetokana na matukio ya tetemeko yaliyoyakumba maeneo mengi ya nchi juzi bali ni mpango uliobuniwa na wataalamu mapema mwaka huu na kwamba kilichobaki ni utekelezaji tu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), Karimu Meshaki alisema atatoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya mpango huo wiki hii.

Hivi karibuni Serikali ilijenga maabara kubwa kabisa ya utafiti wa kisayansi katika Chuo cha Nelson Mandela, Arusha ambayo ilizinduliwa miezi miwili iliyopita.

Serikali ya India pia ilitoa mchango wake kwa kukipatia chuo hicho kompyuta kubwa na yenye uwezo mkubwa zaidi nchini ijulikanayo kama 'Param Kilimanjaro,' ambayo pamoja na shughuli nyingine pia inatarajiwa kutumika katika tafiti za miamba, gesi asilia na pia kwenye huu mradi mpya wa kufuatilia matukio ya tetemeko la ardhi na milipuko ya volkano.



Chanzo: Habarileo

VIDEO: HII NDIYO MAANA HALISI YA SEPTEMBA 11 HUKO MAREKANI

Mnamo mwaka 2001 ndege mbili za abiria za chini Marekani zilitekwa angani na magaidi wanaodhaniwa kuwa ni Al-Qaeda. Ndege hizo mbili aina ya Boeing 767 ziligonga katika majengo pacha ya Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililoko katika jiji la New York nchini Marekani. Hili lilikuwa ni shambulio kubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na magaidi wa Al-Qaeda ambao kwa kipindi hicho kundi hilo lilikuwa likiongozwa na Osama bin Laden ambaye aliuawa miaka ya hivi karibuni na wanajeshi wa jeshi la Marekani (wanavyodai wao Marekani). 

Pia kundi la Al Qaeda lilikuwa limelenga kuteketeza jengo la Idara ya Ulinzi ya Marekani, The Pentagon ambako ndiyo makao makuu ya Idara ya Ulinzi ya nci ya Marekani. Lakini pia ililengwa Ikulu ya Marekani 'The White House'.

Watu wapatao 2,996 pamoja na watekelezaji wa tukio hilo wakiwa 19 waliuawa. Watu zaidi ya 6,000 walijeruhiwa katika tukio hilo.

Pia tukio hilo lilisababisha uharibifu wa mali hasa majengo na miundo mbinu uliofikia dola bilioni 10. Jumla kuu ya uharibifu ilikadiriwa kuwa dola za kimarekani trilioni 3. 

Katika kutekeleza tukio hilo la ugaidi magaidi 19 walihusika ambapo 15 walikuwa ni raia wa Saudi Arabia, 2 kutoka Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE), 1 kutoka Misri na 1 kutoka Lebanon.

Historia ya Al Qaeda inarudi nyuma katika mwaka 1979 ambapo Muungano wa Kisoviet uliivamia Afghanistan. Osama alisafiri hadi Afghanistan na kuunda kikundi cha kiarabu cha wajahideen kupingana na Wasoviet. Osama aliendelea kuwa kinyume na Wamarekani na mwaka 1996 alitoa tamko lililotaka majeshi ya Marekani kuondoka Saudia Arabia

Shambulio hili lilkuwa kama ifuatavyo:
  • Ndege ya Shirika la Marekani (American Airlines Flight 11) aina ya Boeing 767 iliondoka Logan airpot ikiwa na crew ya watu 11 pamoja na abiria 76 (watekaji 5 hawakuhesabiwa) ndege hiyo iligeuzwa ruti ikiwa angani na kugonga katika kituo cha biashara Duniani saa 8:46 am saa za Marekani.
  • Ndege ya pili ya Marekani (American Airlines Flight 77) Boeing 757 iliondoka Washington Dulles Airport kuelekea Los Angels, California ikiwa na crew ya watu 6 na abiria 53 (watekaji wameondolewa katika hesabu hiyo). Watekaji walifanikiwa kuiteka na kugonga jengo la ulinzi la Marekani The Pentagon saa 9:37 am saa za Marekani.
  • Ndege ya tatu (United Airlines Flight 93) Boing 757 iliondoka  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa New York ikielekea San Fransisco kabla ya kutekwa angani na kugonga Stonycreek Township  karibu na Shanksville, Pennsylvania saa 10:03 am saa za Marekani. Abiria walikuwa 33 na crew ya watu 7 huku watekaji wakiwa 4.
  • Ndege nyingine American Airline Flight 11 Boeing 767 ilikuwa na abiria 51 crew ya watu 9 na watekaji 5 iliondoka Los Angels na kutekwa angani hadi WTC saa 9:03 am dakika chache mara baada ya Shambulio la awali.



Hizi ni baadhi ya picha za tukio hilo



WTC kabla ya shambulio


WTC kabla ya shambulio



WTC kabla ya shambulio



Nimekuwekea video pia ambapo unaweza kutazama tukio hilo





Makala hii imeandaliwa kwa Msaada wa Mtandao (Wikipedia, Britannica na YouTube)

LEO SEPTEMBA 11 KATIKA HISTORIA

Leo ni tarehe 11 Septemba, siku ya 255 katika mwaka 2016, zimesalia siku 111 kumaliza mwaka huu 2016.

MATUKIO

1740 - Daktari mweusi aliyetibu meno alitajwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la The Pennsylvania 

1777 - Mapigano ya vita ya Brandywine yalianza huko Pennsylvania ambapo General George Washington na vikosi vyake walishindwa na General Sir William Howe wa Uingereza

1915 - Mkutano wa Zimmerwald uliitishwa kurejesha amani wakati wa vita ya kwanza ya Dunia.

1940 - Adof Hitler alituma vikosi vyake Mashariki mwa Romania katika vita ya pili ya dunia.

1944 - Vikosi vya Marekani viliingia Luxembourg.

1974 - Haile Selassie I aliondolewa madarakani huko Ethiopia.

1997 - Scotland ilipiga kura ya kuwa na Bunge lake kamili baada ya miaka 290 ya Muungano na England.

Jengo la Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililolipuliwa Septemba 11, 2001 na kundi la Al-Qaeda.

2001 - Mnamo majira ya saa 2 na
 dakika 45 asubuhi ikiwa siku ya Jumanne, ndege mbili za abiria za Marekani Boeing 767 zilitekwa angani na kugonga katika jengo la Kituo cha Biashara duniani (WTC) ambapo watu wengi waliuawa. Inasidikika kuwa tukio hilo la ugaidi liliungwa mkono na magaidi wa Kiislamu kutoka Saudi Arabia na kundi la Al Qaeda ilililokuwa chini ya Osama bin Laden kwa kipindi hicho.

2005 - Israel iliwaondoa wananchi wake na vikosi vyake vya jeshi katika mapiagano dhidi ya Palestina katika Ukanda wa Gaza.

2007 - Urusi ilifanya jaribio la kulipua bomu la Nano lililoitwa "Father of Bombs" yaani Baba la Mabomu yote ambalo lilikuwa ni bomu lisilo la nyuklia kuwahi kutengenezwa.

2012 - Ofisi za Ubalozi wa Mareani nchini Libya katika mji wa Benghazi zilichomwa moto na kupelekea vifo vya watu 4 akiwemo balozi wa Marekani nchini Libya, Christopher Stevens


KUZALIWA

1700 - Mshairi wa Scotland, James Thomson.

1877 - Mwanasayansi James Jeans.

1862 - Mwandishi wa Marekani O. Henry (William Sydney Porter) alizaliwa.

1939 - Charles M. Chuck Geschke muanzilishi wa Adobe System Inc.

1965 - Rais wa Syria Bashal al-Assad. Yupo madarakani tangu mwaka 2000.

1977 - Rapa Ludacris.
Rapa Ludacris alizaliwa mwaka 1977.


VIFO

1971 - Nikita Khrushchev moja kati ya viongozi wa kisoshalist alifariki akiwa na miaka 77 katika kipindi cha vita baridi.

NUKUU

"Kama mtu ameishi katika vita, umaskini na upendo, ameishi maisha kamili" - O. Henry.


KWA MSAADA WA MTANDAO.

MAPIGANO YAPAMBA MOTO SYRIA KUELEKEA SULUHU YA MGOGORO

Saa chache baada ya Marekani na Urusi kutangaza makubaliano ya kumaliza mgogoro wa kivita uliyodumu kwa miaka mitano nchini Syria, mapigano yemepamba moto upya. Karibu raia 100 wameuawa katika mashambulizi ya angani.


Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London,Uingereza, limeripoti siku ya Jumamosi kwamba raia wasiopungua 58 wameuawa katika mkoa unaodhibitiwa na waasi wa Idlib baada ya ndege za kivita kuliripua kwa mabomu soko kaskazini-magahribi mwa mji huo, saa kadhaa baada ya kutangazwa kwa masharti ya makubaliano ya kusitishwa mapigano nchini kote.

Mjini Aleppo, jeshi la Syria lilifanya mashambulizi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi katika jitihada za kuimarisha nafasi yake kuelekea usitishaji wa uhasama, unaoanza siku ya Jumatatu wakati wa siku kuu ya Eid al-Adha. "Mapigano yamepamba moto katika maeneo yote ya Aleppo," alisema kapteni Abdul Salam Abdul Razak, msemaji wa kundi la waasi la Brigedi za Nour al-Dine al Zinki , ambalo ni sehemu ya jeshi Huru la Syria (FSA). Watu wasiopungua 30 wameuawa katika mashambulizi hayo, kulingana na shirika la uangalizi wa haki za binaadamu.

Makubaliano kati ya Marekani na Urusi


Ongezeko hilo la machafuko linafuatia tangazo lililotolewa mapema Jumamosi juu ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na Urusi baada ya mazungumzo marefu mjini Geneva, Uswisi. Chini ya makubaliano hayo. Moscow itaushinikiza utawala wa Assad kukomesha kampeni yake ya kijeshi dhidi ya waasi wanaoungwa mkono na Marekani.


Mawaziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry, na wa Urusi Sergei Lavrov wakitangaza makubaliano ya kusitisha mapigano Syria.

Kwa Urusi kufanya hivyo, Marekani itaanzisha mashambulizi ya pamoja na Urusi dhidi ya kundi lililobadili jina la Jabhat Fatah al-Sham, zamani likijulikana kama Jabhatu Nusra wakati likiwa na mafungamano na mtandao wa Al-Qaeda, ikiwa makubaliano hayo yataheshiwa kwa muda usiyopungua siku saba.

"Hili linahitaji kusitisha mashambulizi, yakiwemo ya angani, na majaribio yoyote ya kutwaa ardhi zaidi kwa gharama ya pande zilizomo kwenye makubaliano ya usitishaji uhama. Inahitaji ufikishaji wa misaada usiyo na vikwazo vyovyote katika maeneo yote yaliozingirwa, ikiwemo Aleppo," alisema waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry.

Uidhinishwaji usiyo rasmi kutoka serikali ya Syria


Serikali ya rais Bashar al-Assad haijatoa tamko rasmi kuhusu makubaliano hayo. Badala yake, shirika la habari la serikali SANA limesema serikali inayakubali mapatano hayo, na kuongeza kuwa uhasama utaanza kusita katika mji wa kaskazini wa Aleppo kwa sababu za kibinaadamu. Halikusema ni lini vurugu zitamalizika, na kuongeza kuwa makubaliano hayo kati ya Marekani na Urusi yalifikiwa kwa idhini na taarifa ya serikali.

Basma Kodmani, kutoka muungano wa upinzani unaoungwa mkono na Saudi Arabia wa Kamati Kuu ya Majadiliano (HNC) alisema kundi linachukuwa tahadhari kwa makubaliano hayo, na kuongeza kuwa kunahitaji kuwepo na mifumo ya kuhakikisha utekelezaji wake.

Vurugu za Jumamosi zinaonyesha kuwa huenda ikawa vigumu kuyatekeleza makubaliano kati ya Marekani na Urusi kwa sabau mataifa hayo mawili yana ushawishi wenye mipaka kwa serikali na makundi ya waasi kuhusu kusitisha mashambulizi.

Makubaliano ya kusitisha uhasama yaliofikiwa na mataifa hayo mawili makubwa duniani mapema mwaka huu na kuanza kutekelezwa mwishoni mwa mwezi Februari yalishindwa muda mfupi baadae na yalifuatiwa na miezi miwili ya vurugu zilizouwa maelfu.


Waokozi wakitafuta maiti na manusura katika vifusi baada ya shambulizi la angani mkoani Idlib siku ya Jumamosi.

Muungaji mkono mkuu wa Assad


Urusi ndiyo muungaji mkono mkuu wa utawala wa Assad huku Marekani ikiyaunga mkono makundi ya waasi wanaotaka kum'ngoa madarakani. Vita vya Syria vilivyoigia mwaka wake wa tano, vimeendelea licha ya duru kadhaa za mazungumzo ya amani na majaribio ya jumuiya ya kimataifa kukomesha vurugu nchini humo. Watu wasiopungua robo milioni wameuwawa,na nusu ya wakazi wa nchi hiyo kabla ya vita wamekoseshwa makaazi.

Mashambulizi ya angani ya Jumamosi yalifanyika hasa katika miji ya Aleppo na Idlib. Aleppo imekuwa kituo cha vurugu nchini Syria katika miezi ya karibuni, ambapo watu karibu 2,200 wakiwemo raia 700 wameuwawa tangu mwezi Julai mwaka huu kwa mujibu wa shirika la uangalizi w ahaki za binaadamu, linalofuatilia vurugu hizon kupitia mtandao wa wanaharakati walioko ndani ya Syria.

Mgogoro wa Syria ulianza mnamo mwaka 2011, wakativikosi vya serikali vilipoanzisha ukandamizaji wa vurugu dhidi ya waandamanaji waliokuwa wanadai demokrasia, wakimtolea mwito Assad kuachia ngazi. Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 250,000 wameuawa, na zaidi ya nusu ya wakaazi jumla wamekosa makaazi.



Chanzo: DW

TETEMEKO LA ARDHI LIMEPITA MIKOA YA MWANZA NA KAGERA NA KUFANYA UHARIBIFU

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.7 limetikisa mkoa wa Mwanza likitokea mkoa wa Kagera umbali wa kilomita 44 karibu na ukingo wa magharibi wa Ziwa Victoria huku likijirudia kwa ukubwa zaidi ya ule wa awali. Tetemeko hilo lilipita umbali wa kilomita 10 kwenda chini limefanya uharibifu mkoani Kagera kama picha zinavyoonesha hapa chini. Pia kumeripotiwa vifo vya watu.












PICHA KWA HISANI YA JAMII FORUMS.