LIST OF UNDERGRADUATE APPLICANTS WITH MULTIPLE ADMISSIONS EXPECTING TO JOIN TUMAINI UNIVERSITY MAKUMIRA 2018/2019 (SECOND ROUND)


Names can be accessed by clicking HERE

LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN THE MWALIMU NYERERE MEMORIAL ACADEMY 2018/2019 ROUND 2


For the Names of those who have been selected after confirming their admission status, click HERE


Those selected after applying for the second round, names can be accessed by clicking HERE

KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA UDAHILI AWAMU YA TATU

tume ya Vyo Vikuu nchini (TCU)  imetoa tangazo kwa umma kuhusu zoezi la udahili awamu ya tatu. Dirisha la udahili liko wazi hadi Septemba 26, 2018. Maelezo zaidi bofya katika link hii HAPA

ORODHA YA WAOMBAJI WALIODAHILIWA NA CHUO ZAIDI YA KIMOJA DIRISHA LA PILI-MWAKA WA MASOMO 2018/2019


Kuangalia Orodha ya majina hayo bofya HAPA

LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

The following applicants have been selected to join various programmes offered by Tanzania Institute of Accountancy for the Academic year 2018/2019.

Selected candidates should report to their respective campuses on 29th OCTOBER 2018.

  1. Joining instructions and admission letters can be downloaded through our website www.tia.ac.tz
  2. The Institute has limited accommodation facilities for students. Those who wish to stay at the Institute’s Hostels should apply in advance to their respective campuses before commencement of an academic year.
  3. Applicants with status “PENDING FOR SELECTION’’ are advised to communicate with the institute through mobile numbers 062577774 OR O677777746 OR 0764777746. Applicants with ‘‘Prior admission status’’ in their accounts are advised to clear their prior admission status through filling TCU prior admission clearance formUnsuccessful applicants for the second round are advised to re-apply for third round applications by choosing other programme in which they are qualified as per our entry requirements communicated in TCU guidebook.
  4. Candidates with multiple admissions and have not yet confirmed are advised to continue with confirmation.
LIST OF SELECTED APPLICANTS CAN BE ACCESSED BY clicking HERE

    UCL: FAHAMU MACHACHE MECHI YA MAN CITY VS LYON

    Mechi itachezwa saa 4:00 usiku saa za Afrika Mashariki katika dimba la Man City Etihad. Mwamuzi wa mechi hii ni Muitalia Daniele Orsato. 

    Hii ni mechi ya kwanza baina ya timu hizi. Mpaka sasa hakuna klabu ya Ufaransa iliyowahi kushinda ugenini dhidi ya Man City zaidi ya kuambulia suluhu 1 na kupoteza michezo 2.

    Lyon imeshinda mechi 1 tu kati ya 8 ilizocheza na timu za Uingereza. Hii ilikua ni dhidi ya Liverpool katika dimba la Anfield Oktoba 2009.

    Hii ni mara ya 8 mfululizo kwa Man City kushiriki katika ligi ya mabingwa Ulaya. Hii ni rekodi ya juu kwa sasa katika timu za Uingereza kushiriki idadi hii ya Man City ambayo mara nyingi imekua ikiondolewa katika mechi ya 5 ya michuano hii hatua ya makundi.

    Katika mechi zao zote 42 walizocheza Man City hakuna mechi hata moja ambayo hawakufunga katika ligi hii.

    Hii ni mara ya 15 kwa Lyon kushiriki michuano hii. Hii inaifanya kuwa timu pekee kutoka nchini Ufaransa kushiriki mara nyingi zaidi. Wamekuwa wakiondolewa katika hatua ya mtoano kuanzia msimu wa 2003/2004 hadi 2011/2012 na hawajawahi tena kufikia hatua hiyo. 

    Lyon wameshinda mechi 3 tu kati ya mechi zao 13 za mwisho katika ligi hii pamoja na kusuluhu mechi 3 na kupoteza mechi 7.

    Lyon ilifunga magoli 5 tu katika mechi zao 5 za mwisho katika ligi hii. Magoli 2 yalifungwa nyumbani na magoli 3 ugenini. 

    Kocha wa Man City Pep Guardiola amewahi kufikisha timu zake katika hatua ya nusu fainali katika michuano 7 kati ya michuano 9 ya ligi hii aliyoshiriki kama kocha lakini hajatwaa ubingwa tangu alipotwaa mara ya mwisho 2011. Msimu huu atakua anawania kutwaa kombe hilo ili afikie rekodi ya Zinedine Zidane, Carlo Ancelotti na Bob Paisley ya kutwaa kombe hili mara 3.

    Raheem Sterling ameifungia klabu yake ya Man City magoli 8 wakiwa nyumbani na kuisaidia kufunga magoli 6 katika mechi 15 alizoichezea klabu hake hiyo. 

    Mshambuliaji wa Lyon Moussa Dembélé ameifungia klabu hiyo magoli 3 katika mechi 4 za mwanzo katika klabu hii katika UCL. Awali ya Lyon aliwahi kuichezea Celtic ambapo aliifungia klabu hii goli 1 katika mechi 6 kwenye michuano hii.

    Man City itaingia uwanjani bila wachezaji wake Benjamin Mendy, Danillo, Claudio Bravo, Kelvin De Bruyne, Sergio Kun Arguero, Eliaqim Mangala na Philippe Sandler ambao ni majeruhi. Kwa upande wa Lyon watakosekana Amine Gouiri na Fernando Marcal. 

    UCL: FAHAMU MACHACHE MECHI YA REAL MADRID VS ROMA

    Mechi itachezwa katika dimba la Santiago Bernabeu saa 4:00 usiku saa za Afrika Mashariki. Mwamuzi atakua ni Mfaransa Bjorn Kuipers. Madrid imeshinda mara 3 dhidi ya Roma katika mechi 3 zilizopita. 

    Timu hizi zimekutana mara 11 katika ligi hii ya mabingwa barani Ulaya wakati Madrid ikiwa na rekodi ya kushinda mara 6 katika mechi hizo ikisuluhu katika mechi 3 wakati Roma wamewahi kuifunga Madrid mara 1 tu. 

    Ni mechi 1 tu katika mechi 10 zilizopita ambayo Roma haikufungwa na Madrid na ilikuwa ni Oktoba 2002, ilishinda 1-0 katika dimba la Madrid Santiago Bernabeu goli lilifungwa na Fransesco Totti. 

    Msimu wa 2017/2018 Madrid ilikuwa timu ya kwanza kutwaa kombe hili mara 3 mfululizo ikilinganisha rekodi na Bayern Munich ya Ujerumani iliyowahi kushinda mara 3 katika mwaka 1974, 1975 na 1976.

    Madrid wanacheza michuano hii mara ya 22 mfululizo na kuwa timu yenye rekodi ya muda mrefu katika michuano hii. Katika michuano 8 iliyopita Madrid walifika hatua ya nusu fainali. 

    Madrid wameshinda mara 22 katika michezo 25 kwenye hatua ya makundi wakiwa nyumbani, walisuluhu mara 3 na bila kupoteza. Walifungwa mara ya mwisho na AC Milan magoli 3 dhidi ya magoli 2. Hii ilikua ni msimu wa Oktoba 2009.

    Madrid hawakufunga katika mechi 1 tu katika michezo 56 ya ligi hii ya mabingwa barani Ulaya katika hatua ya makundi na ilikua ni dhidi ya PSG, walitoka suluhu ya bila kufungana Oktoba 2015.

    Roma wanashiriki mara ya 11 sasa katika ligi hii (UCL), Juventus wameshiriki mara 19, AC Milan mara 17 na Inter Milan mara 12, hizi ndizo timu 3 zilizoshiriki mara nyingi zaidi katika ligi hii katika timu za nchini Italia. 

    Katika msimu uliyopita Roma ilifikia hatua ya nusu fainali ambayo ilikua ni mafanikio makubwa kwao katika ligi hii tangu walipopoteza katika finali ya ligi hii mwaka 1984. Wameshinda mechi 1 tu katika 15 walizocheza ugenini, walisuluhu 5 na kupoteza 9.

    Madrid wanashiriki bila Cristiano Ronaldo aliyejiunga na Juventus majira ya joto msimu uliopita baada ya michuano ya Kombe la Dunia. Mreno huyo amehusika kwa 50% katika magoli yote ya Madrid tangu msimu wa 2009/2010 hadi 2017/2018 katika ligi hii. Alifunga magoli 105 akisaidia magoli 27 yaliyofungwa.

    Edin Dzeko mshambuliaji wa klabu ya Roma amefunga katika kila mechi katika 5 alizocheza na klabu ya Roma katika ligi hii. 

    Jesús Vallejo wa Madrid na Javier Pastore watakosa kushiriki mechi ya leo kutokana na majeraha. 

    HAYA HAPA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018

    Kuona majina hayo bofya HAPA

    LIST OF UDSM UNDERGRADUATES WITH MULTIPLE ADMISSIONS 2018/2019


    To download the list of names click HERE

    LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE (SUA) AND THOSE WITH MULTIPLE ADMISSIONS 2018/2019


    FOR SELECTED STUDENTS
    Prospective Students are advised to observe the following:
    1. All candidates selected to join BSc. Environmental Science and ManagementBachelor of Tourism ManagementBachelor of Rural DevelopmentBSc. Agricultural Economics and AgribusinessBSc. Applied Agricultural ExtensionBSc. Range ManagementBSc. Informatics and all BSc. Education programs are supposed to report to Solomon Mahlangu Campus (SMC) – Mazimbu, whereas, students for other programs will report to the Main Campus (MC).
    2. All students are required to participate in a mandatory orientation programme planned to starts on 29th October, 2018
    3. Admitted students should download admission letters and invoice at www.suasis.sua.ac.tz  through their SUASIS (SUA Student Information System) account. SUASIS can be accessed using the username and password provided to you during application.
    4. Each student Must upload a recent and high quality passport size photo on their web page before arrival for official use. This must be of the same quality as those used for passports or Identity cards. 


    Sokoine University of Agriculturewishes to inform the following prospective students with multiple admissions to confirm their readiness to join SUA by using the special code sent to them by TCU through their mobile phone number used during application.  
    To confirm please log in into your SUA application account and enter your special code. 
    You are required to confirm by Wednesday 5th September, 2018 failure to confirm will lead to cancellation of your name from our list of potential candidates selected to join SUA in 2018/19 academic year.


    Issued by
    The Deputy Vice Chancellor (Academics), 
    Sokoine University of Agriculture,
    P. O. Box 3000,
    Inquiries should be sent to
    Directorate of Undergraduate Studies
    Sokoine University of Agriculture
    P. O. Box 3000, Chuo Kikuu, Morogoro
    Telephone No: 0744 555 448 OR 0692 862 360
    Email: admission@sua.ac.tz

    LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN MZUMBE UNIVERSITY (FIRST ROUND) 2018/2019


    Dear applicants, we congratulate all those who are selected to join various undergraduate programmes in this first round of selection. It is important to note that those who have multiple selections (that is, they have been selected in more than one University) they have to confirm to only one University. In order to confirm to Mzumbe University, please log in your respective account through this link http://admission.mzumbe.ac.tz/and go to the confirmation link, enter the secret CODE that was sent to your phone number that you used when applying to Mzumbe University and click confirm.
    Those who are not selected in the first round, please log in your respective accounts athttp://admission.mzumbe.ac.tz/  and you will find the reasons as to why you are not selected. Please, use the correct username and password as you entered when you were creating your account. First round selection was based on ranking of academic performance according to the three choices you made and the capacity of the programme (total number of the students in the particular programme). In that case, you can now log into your accounts and select same/new programmes depending on whether those programmes still have vacancies for selection. If you see any programme available for selection, then you can select it depending on your qualifications. Please, read carefully minimum qualifications for each specific programme before any selection.
    Those who did not meet minimum qualifications or they did not follow proper procedures during the first round of application, they are required to log into their respective accounts and re-start again their applications. You may change level from Bachelor to Diploma or from Diploma to Certificate depending on your academic qualifications. This will require you to pay once again application fee.
    The admissions’ office, Mzumbe University is ready to respond to your inquiries just in case you have any issue to inquire from us. Call our mobile phone numbers that are shown athttp://admission.mzumbe.ac.tz/.   
    Admission letters and joining instructions will be sent to selected candidates through their accounts that were created during application. See below the list of selected candidates (Bachelor, Diploma, Certificate programmes) who applied in our online application.
    You are welcome to Mzumbe University.

    LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN ST. AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA (SAUT) AND THOSE WITH MULTIPLE ADMISSIONS 2018/2019


    For Selected Students click HERE

    For those with multiple admissions click HERE

    It should be noted that studets with multiple admissions are supposed to conform one university/college of their choice. Don't confirm more than one university/college in order to be admitted in one college/university of your choice. 

    WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

    10. YUSUF MANJI

    Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini.

    9. FIDA RASHID

    Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine.

    8. GHALIB SAID MOHAMMED

    Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha na uuzaji wa bidhaa za rejareja, usafirishaji wa vifaa na bidhaa, huduma za kifedha, vyombo vya habari na mengine mengi. Vyanzo vyote hivi vinamfanya kua miongoni mwa matajiri wakubwa nchini. Kama mjasiriamali aliamua kujihusisha zaidi na mazao ya kilimo pamoja na baba yake jambo ambalo limewafanya kufikia walipo kwa sasa.

    7. SUBASH PATEL

    Patel ni mwanachama wa Taasisi ya Wahandisi wa Umeme na ana ubia na kampuni ya MMI Steels Resource Limited na Nyaza Road Works. Katika kipindi cha miaka 20 amefanikiwa kupanua biashara zake mpaka kufikia kuwa na kampuni inayoitwa Motsun Group. Kampuni hii imegawanyika katika makampuni mengine 11 ambazo zinahusika na bidhaa za chakula, madini, majengo na kusaidia makampuni mengine kitaalamu.

    6. SHEKHAR KANABAR

    Shekhar ni meneja katika kampuni ya Synarge Group. Hii ni kampuni inayohusika na bidhaa za magari. Kampuni hii pia inahusika na utengenezaji wa madini ya risasi. Licha ya kwamba kampuni hii ni mali ya familia, Shekhar anabainishwa kuwa miongoni mwa matajiri nchini kutokana na uongozi wake mzuri katika kampuni hiyo. Kampuni hii pia inahusika na usambazaji wa spea za magari nchini. Huwezi kuzungumzia Teknolojia hii ya magari bila kumzungumzia Shekhar. Synarge imekua ikifanya vema katika mauzo ya bidhaa za magari nchini.

    5. ALLY AWADH

    Awadh ni miongoni mwa watu wenye akili ya biashara. Amefanya uwekezaji katika sekta za mafuta na gesi, ni muwekezaji muhimu sana katika sekta hizi. Alifanya kazi kwa juhudi sana ili apewe kibali na serikali na baadaye alifanikiwa katika hilo na sasa ana kampuni yake ya Lake Oil Group inayohusika na kuingiza pamoja na kusambaza mafuta ya petroli na gesi nchini. Biashara ya mafuta inatajirisha kwa haraka sana lakini kwa Awadh haikua hivyo, amepitia changamoto nyingi pamoja na magumu mengi mpaka hapo alipofikia.

    4. REGINALD MENGI

    Mengi ni mmiliki na mkuu wa kampuni kubwa ya habari nchini IPP Media Group. Kampuni hii ina jumla ya vituo vya redio 11, vituo vya televisheni, magazeti na huduma za mtandao (Internet). Mengi pia ni mmiliki wa kampuni ya Kilimanjaro Spring Water na Bonite Bottlers. Ndoto yake na mapenzi katika tasnia ya habari vimemfanya kutimiza malengo yake ya kutangaza na kufikisha habari kwa Watanzania. Anamiliki utajiri unaokadiriwa kuwa dola milioni 560.

    3. SAID SALIM BAKHRESA

    Bakhresa aliacha masomo ya shule ya sekondari akiwa na umri wa miaka 14. Kwa kipindi hicho alikua akifanya biashara ya kuuza viazi na akafungua mgahawa wa kuuza chakula na kisha akafungua mashine ya kusaga nafaka. Bakhresa ameijenga biashara yake kwa muda wa miaka 30 iliyopita mpaka kufikia leo, pia ni miongoni mwa matajiri wakubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki. Kampuni yake ya Bakhresa Group of Companies ni maarufu kwa uzalishaji wa bidhaa za chakula, mafuta ya petroli, usafirishaji ndani ya bahari ya Hindi na usagaji wa nafaka. Pia ni mmiliki wa king'amuzi cha Azam TV ambacho kinatoa huduma kwa malipo katika ukanda wa Afrika Mashariki. Akiwa ameajiri zaidi ya watu 3000 katika ukanda huu wa Afrika Mashariki, akiwa na matawi ya kibiashara nchini Msumbiji, Malawi na Uganda, Bakhresa anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia dola milioni 650 za Marekani. Bakhresa amekuwa akitoa msaada wa kifedha kwa watu wenye uhitaji nchini.

    2. ROSTAM AZIZ

    Rostam anashikiria rekodi ya kuwa bilionea wa mwanzo nchini Tanzania. Anamiliki kampuni ya madini inayotwa Caspian Mining, kampuni hii inatoa huduma za kitaalamu kwa makampuni makubwa ya madini nchini kama vile Barrick Mining na BHP Billiton. Alinunua 17.2% ya hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania mwaka 2014. Anamiliki mali zisizohamishika nchini Tanzania, Lebanon, Dubai na Oman. Pia ni mdau mkubwa wa bandari ya Dar es Salaam. Utajiri wake unakadiriwa kuwa dola bilioni 1 za Marekani. Alikua ndiye bilionea wa kwanza nchini mpaka pale MO Dewji alipochukua nafasi hii. Ndiye tajiri wa kwanza kuwahi kufikia kada hii ya matajiri bilionea kutoka Tanzania.


    1. MOHAMMED DEWJI

    MO Dewji ni miongoni mwa matajari wenye umri wa miaka 40 barani Afrika. Anamiliki 75% ya hisa zote katika kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd (METL) ambayo inamiliki viwanda vingi nchini. Baada kupata umiliki wa viwanda vya nguo na mimea ya mafuta kutoka serikali ya Uganda utajiri wake ukaanza kukua kwa kasi. Ana utajiri uanaokadiriwa kufikia dola bilioni 1.3 za Marekani, hii inamfanya kuwa tajiri namba 1 kwa sasa nchini. MO alitajwa na Forbes kuwa tajiri namba 1 nchini mwanzoni mwa mwaka huu na bado ameendelea kushikilia namba hiyo. 


    Chanzo: Forbes Raking

    CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

    KUZALIWA 

    Celebrity wetu wa leo ni Shania Twain. Jina lake la kuzaliwa ni Eilleen Regina Edwards lakini umaarufu wake umetokana na jina lilizoeleka la Shania Twain. Wengine wanamuita Malkia wa Muziki wa Country.  Alizaliwa mnamo Agosti 28, 1965 leo anatimiza miaka 53 ya kuwepo duniani. Alizaliwa huko Windsor, Ontario, Canada akiwa ni mmoja kati ya mabinti 3 wa Clarence na Sharon (Morison) Edwards. Yeye ndiye mkubwa. Alipokua na miaka 6 mama yake aliolewa tena na Jerry Twain ambaye alimchukua kama mwanaye. Alianza kuimba katika vilabu vya pombe na alipokua na miaka 13 alionekana katika The Tommy Hunter Show. Alipokua na umri wa miaka 22 wazazi wake waliuawa katika ajali na hivyo akaacha sanaa muziki ili awalee wadogo zake Mark na Darryl pamoja na dada zake wawili aliozaliwa nao kwa baba yake na mama yake mzazi. Mwaka 1991 alibadilisha jina lake alilopewa na wazazi wake na kujiita Shania Twain na hapo ndipo jina hili lilipokua.  Mwaka huo huo pia alisaini mkataba na lebo ya muziki ya Mercury Nashville.
    Shania siku za hivi Karibuni.


    KUOLEWA

    Shania amewahi kufunga ndoa mbili ambapo ndoa ya kwanza alifunga na Robert John Lange Desemba 28, 1993 na ilidumu hadi Juni 9, 2010. Katika ndoa hii walifanikiwa kupata mtoto 1 kabla hawajaachana. Baadaye January 1, 2011 aliolewa na Frederic Nicolas Thiebaud ambaye yuko naye mpaka sasa. Hawajabahatika kupata mtoto. 

    TUZO


    Shania amewahi kushinda tuzo kadhaa na kutajwa katika nyingine:

    Mwaka 1996 alitajwa katika tuzo za Grammy kama msanii bora chipukizi lakini hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo.


    Mwaka 1997 aliteuliwa kuwania tuzo za Gemini katika kipengele cha mtumbuizaji bora katika vipindi mbalimbali vya television, huku pia hakufanikiwa kutwaa tuzo.

    Mwaka 1998 aliteuliwa kuwania tuzo za MTV kama Video Bora ya Msanii wa Kike: You're Still the One. Huku pia hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo. Mwaka huu alishinda tuzo ya Grammy na wimbo wake wa From this Moment on.

    Mwaka 1999 aliteuliwa kuwania tuzo ya Grammy kama Wimbo wa Mwaka: You're Still the One, pia hakufanikiwa kupata tuzo hiyo. 

    Mwaka 2004 alifanikiwa kutwaa tuzo ya Bambi katika kipengele cha Pop Kimataifa. 

    Mwaka 2005 Grammy walimchagua katika vipengele viwili; mtumbuizaji bora wa kike wa muziki wa country na kolabo bora ya country. Bado hakufanikiwa pia kutwaa tuzo. 

    Mwaka 2011 alitwaa tuzo kama Nyota wa tuzo za Walk of Fame. 
    Shania Twain katika video ya For evre and for always. 

    ALBUM ZAKE

    Shania Twain (1993)
    The Woman In Me (1995)
    Come Over (1998)
    Up (2003)
    Now (2017)

    MENGINE KUHUSU SHANIA TWAIN

    Anakula mboga za majani na alipendekezwa kua na mvuto kutokana na hili.

    Mwaka 1995 aliorodheshwa kama Mtu mwenye majibu Halisi anapoulizwa maswali katika jarida la People Weekly.

    Amewahi kukaa kwenye namba za juu za muziki duniani kwa wimbo wake You're Still the One ambayo ilishika namba 1 kwenye chati ya Billboard mara 7. Pia alishika namba 2 katika chati za Hot 100 kwa wimbo huo mwaka 1998.

    Wimbo wake "Love Gets Me Everytime" ulikua ni wimbo ulioshika nafasi ya juu zaidi ya Billboard kwa wiki 5 katika nyimbo za country tangu wimbo wa mwisho wa Dolly Parton "Here You Come Again" uliposhika nafasi hiyo mwaka 1997.

    Mwaka 1999 alitajwa kama mtumbuizaji bora wa muziki wa country na mwaka huo huo CMA walimtuza tuzo ya mwaka ya mafanikio katika muziki huo.

    Mwaka 1999 aliuza nakala milioni 19 za albam yake ya Come Over nchini Marekani peke yake.

    Mwaka 2003 aliwahi kushinda tuzo ya Juno ka Chaguo la Mashabiki.

    Album yake ya Come Over (mauzo na matamasha) viliingiza dola za Marekani milioni 40 nchini Australia pekee. Hii inaifanya kuwa miongoni mwa album zilizowahi kushika chati za juu za muda wote nchini humo.

    Alishika namba 39 katika orodha ya Jarida la Maxim kama mwanamke mwenye mvuto katika wanawake 100 waliotajwa katika orodha hiyo ya mwaka 2005.

    Album yake ya Up (2002) iliuza nakala milioni 2 nchini Marekani ndani ya mwezi 1 tangu ilipowekwa sokoni.

    Alipokua mdogo alikua na aibu na alikua Tom boy.

    Amekua katika familia maskini ambayo chakula tu ilikua ni tabu. Shania alikua akienda shule bila kula kutokana na hali ya maisha kifedha nyumbani kwao.

    Anapenda kushinda nyumbani na kupika. 
    Anaamini kwamba yeye ni kama watu wengine.

    Ni miongoni mwa wasanii wa 4 kutoka nchini Canada waliowahi kushika namba za juu katika chati ya Billboard tangu kuanzishwa kwake mwaka 1944. Wengine kutoka Canada ni Hank Snow, Anne Murray na Terry Klark.

    Aliwahi kusema kwamba anapendezwa na majukumu wanayofanya wanaume katika maisha ya kila siku.

    Shania anawasema kuwa anasikitika siku zote kwa kua ndoa yake ya awali alivunjika.

    Anao wafuasi 863K katika mtandao wa Instagram. Katika mtandao wa Twitter anao wafuasi 901K. Katika mtandao wa Facebook anao wafuasi zaidi ya milioni 5. Ukurasa wake wa YouTube umetazamwa na watu bilioni 1.2 huku akiwa na subscribers zaidi ya bilioni 1.1.

    Haya ni machache kati ya mengi niliyokuandalia kuhusu mwanamuziki Shania Twain. Kama una maoni usisite kuniandikia kupitia barua pepe: venancegilbert@gmail.com ama ujumbe Whatsapp 0712586027. Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG na karibu tena kwa mengine mengi. 

    LEO AGOSTI 6 KATIKA HISTORIA

    Leo ni Agosti 6, 2018 ikiwa ni siku ya 218 katika mwaka 2018. Zimesalia siku 147 katika mwaka huu. Nakukaribisha tena katika muendelezo ya Leo Katika Historia. Kwa leo nimekuletea matukio kadhaa yaliyopata kutokea katika historia ya dunia, na tuanze kuyahesabu matukio hayo:

    MATUKIO

    1787 - Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Marekani ilianza kujadiliwa huko Philadelphia.

    1890 - Hukumu ya kuuawa kwa kiti cha umeme ilianza kutekelezwa katika gereza la Auburn huko New York, Marekani ambapo William Kemmier alihukumiwa kifo katika kiti cha umeme kwa kumuua mpenzi wake Matilda Ziegler kwa shoka. Adhabu hii ya kifo ilipendekezwa mwaka 1881 na Dk. Albert Southwick baada kushuhudia mlevi akiuawa kwa shoti ya umeme. Katika kutekeleza adhabu hii zilitumika volti 700 za umeme na katika sekunde 17 umeme ulifeli kabla Kemmier hajafariki na baadaye waliongeza umeme hadi volti 1,030 ndani ya dakika 2 na ndipo Kemmier alifariki.
    Kiti cha Umeme kilichotumika kutekeleza adhabu ya kifo kwa Kemmier.

    1904 - Jeshi la Japan lililokua nchini Korea lilizunguka Jeshi la Urusi ambalo lilizidiwa nguvu na kuamua kurudi nyuma katika jimbo la Manchuria.

    1945 - Ndege ya Marekani B-29 ikiongozwa na rubani Paul Tibbets ilidondosha bomu la nyuklia katika jimbo la Hiroshima. Bomu hilo liliua watu waliofikia 80,000 na pia watu 35,000 walijeruhiwa na inakadiriwa kua baadaye mwishoni mwa mwaka huo watu wengine 60,000 walifariki kwa madhara ya bomu hilo. Kulikua na majengo 90,000 katika mji wa Hiroshima lakini baada ya bomu kulipuka yalibaki majengo 28,000 tu, madakatari walikua 200 lakini waliosalia walikua 20 tu, manesi walikua 1,754 lakini walisalia 150 tu.
    Ndege aina ya B-29 iliyodondosha bomu la nyuklia huko Hiroshima.
    Baada ya bomu kudondoshwa hali ilikua hivi. 

    Hivi ndiyo Hiroshima ilivyojengwa kwa sasa. 

    1962 - Jamaica ilipata Uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza baada ya kutawaliwa kwa miaka 300.

    1973 - Mwanamuziki wa Marekani Steve Wonder alipata ajali ya gari iliyopelekea kupoteza fahamu kwa siku 4.

    1993 - Papa John Paul II alichapisha makala iliyohusu Umuhimu wa Kanisa Katoliki katika kufundisha maadili.

    KUZALIWA

    1809 - Mtunzi wa mashairi wa Uingereza Alfred Lord Tennyson alizaliwa. Moja kati ya mashairi yake maarufu ni "The Charge of the Light Bregade" la mwaka 1850.

    1881 - Alexander Flemming mgunduzi wa dawa aina ya Penicillin mwaka 1928 alizaliwa.

    1911 - Muigizaji na mchekeshaji wa Marekani Lucille Ball alizaliwa. 

    1934 - Piers Anthony Dillingham Jacob mwandishi wa riwaya za kisayansi na matukio ya ajabu na ya kusimumua alizaliwa.