Skip to main content

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

tanzania flagLeo nakufahamisha baadhi ya mambo ambayo huenda hukuyafahamu ama ulichukulia kawaida tu. Mambo hayo ni hapahapa Tanzania.  Tanzania ina eneo la kilomita za mraba 945,087. Ina jumla mikoa 31 kote bara na visiwani. Mpaka kufikia mwaka 2017 idadi ya watu nchini ilikadiriwa kuwa milioni 52.554 kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya takwimu. Twende sasa tuanze kuhesabu moja baada ya jingine


#1. Wimbo wa taifa "Mungu Ibariki Tanzania" ni wimbo unaofanana na nyimbo za mataifa ya Afrika Kusini na Zambia. Wimbo huu ulitungwa na Enock Sontonga kwa lugha ya Xhosa "Nkosi Sikelel iAfrika". Wimbo huu pia uliwahi kutumiwa na nchi za Zimbabwe na Namibia.
Image result for enoch sontonga
Enock Sontonga mtunzi wa wimbo Mungu Ibariki Afrika


#2. Ni Tanzania pakee ambako kunapatikana Simba wenye uwezo wa kupanda juu ya miti. Simba hawa wanapatikana katika hifadhi ya taifa ya Ziwa Manyara.
bwindi-and-serengeti-safari_18889423181_o
Simba wenye uwezo wa kupanda miti hifadhi ya Ziwa Manyara.


#3. Tanzania ni nchi ambako fuvu la mtu wa kale zaidi liligunguliwa. Fuvu hili liligunguliwa katika bonde la Olduvai mwaka 1959 na Dr. Louis Leakey.
Olduvai Gorge


#4. Tanzania in Mlima Kilimanjaro ambao ni Mlima mrefu kuliko yote barani Afrika. Mlima huu una urefu wa mita 5895.
Related image



#5. Pamoja na kwamba Kiswahili ni lugha ya taifa, Tanzania inayo makabila 120 ambayo yana mila, desturi na tamaduni tofauti tofauti. Makabila haya yanaishi vyema na kuelewana chini ya mwamvuli wa Utanzania na lugha ya taifa ya Kiswahili.
Related image
Ramani ya Tanzania ikionesha Makabila

#6. Uwepo wa Ziwa Tanganyika ambalo ni ziwa lenye kina kirefu kuliko yote barani Afrika. Ziwa hili lina kina cha futi 4823 ambazo ni sawa na mita 1470. Ziwa hili pia lipo katika nchi za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na Zambia. Ziwa hili pia ni la pili duniani kwa kuwa na kina kirefu zaidi baada ya ziwa Baikal likifuatiwa na Caspian.
Related image
Ziwa Tanganyika

#7. Tanzania ina zaidi ya wanyama pori milioni 4 ambao wamegawanyia katika makundi 430 tofauti ya wanyama.



#8. Hifadhi ya taifa ya Serengeti ni hifadhi maarufu kwa kuwa na mimea na wanyama wa aina tofauti tofauti. Pia ni mbuga inayoongoza kwa kuwa na makundi makubwa ya wanyama wanaohama kila mwaka kundi kubwa likiwa ni kundi la nyumbu. Mwaka 1981 hifadhi hii ilitajwa na UNESCO kama sehemu ya urithi wa kujivunia duniani.
Image result for ngorongoro
Hifadhi ya Serengeti.


#9. Tanznaia ina hifadhi ya taifa ya Ngorongoro ambayo ni maarufu kwa kuwa na ziwa ambalo limetokana na mlipuko wa Volkano; Ziwa Magadi ziwa hili lina kilomita za mraba 264 na maarufu kwa kuwa na ndege wengi aina ya flamingo. Eneo hili la Ngorongoro lina aina mbalimbali za wanyama kama vile tembo, faru, kiboko, pundamilia, nyati n.k. Katika eneo hili jamii ya Wamasai hufanya shughuli zao za ufugaji. Hifadhi hii ilitajwa kama eneo la urithi wa kujivunia wa dunia mwaka 1979.
ngorongoro conservation area
Hifadhi ya Ngorongoro

Ngorongoro-Crater
Ziwa Magadi linalopatikana hifadhi ya Ngorongoro


#10. Tanzania ina mji eneo maarufu kwa kivutio cha utalii ambacho huitwa mji mongwe. Eneo hili lipo Unguja-Zanzibar. Kitovu cha historia yake ni Mji Mkongwe (Stone Town) ulioandikishwa katika orodha ya UNESCO ya “Urithi wa Dunia” (World Heritage). Nyumba za Mji Mkongwe zilijengwa tangu mwaka 1830 wakati Sultani Sayyid Said alipohamisha mji mkuu wake kutoka Omani kuja Unguja.
Image result for mji mkongwe wa zanzibar
Mji Mkongwe uliojengwa tokea enzi za utawala wa Waarabu wa Omani

#11. Uwepo wa daraja la Nyerere linalounganisha wilaya ya Kigamboni kupitia Kurasini. Ujenzi wa daraja hili ulianza Februari 2012 na kukamilika April 2016. Daraja hili lina urefu wa mita 680.
Image result for kigamboni bridge
Daraja la Nyerere linalounganisha wilaya ya Kigamboni na kata ya Kurasini kupitia mkondo bahari wa Kurasini


#12. Ziwa kubwa kulio yote Afrika na Ziwa la tatu kwa ukubwa duniani; Ziwa Victoria lipo Tanzania kwa kiasi kikubwa likipakana na nchi za Uganda na Kenya. Ziwa hili lina ukubwa wa eneo la mraba 68,870 likiwa na urefu wa kilomita 332 na kina cha mita 84 sawa na futi 276.
Related image
Ziwa Victoria

#13. Pengine kuna hili hukulifahamu. Tanzania ina majiji 6 kwa sasa Dar es Salaam likiwa ni jiji kubwa kuliko yote, likifuatia jiji la Mwanza, Arusha na majiji ya Mbeya, Tanga na jiji pipya la Dodoma ambalo limepata hadhi ya jiji April 26, 2018 siku ya kumbukumbu ya maandhimisho Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 19964.
Ramani ya Tanzania ikionesha mikoa yake (mikoa michache haijaoneshwa katika ramani hii)


#14. Kuna fukwe (beach) nzuri na za kuvutia pindi unapohitaji sehemu ya kupunga upepo baharini. Coco beach, Landmark, Ocean view, Lamada, Nungwi, Sea cliff, Zanzi Resort, Tanga beach, Mbezi beach, Malaika Beach Resort n.k. ni baadhi ya fukwe maarufu nchini
tanzania beach



#15. Tanzania inapakana na nchi 8 ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi, Zambia na Msumbiji.
Image result for tanzania map with lakes



#16. Tanzania ilisaidia nchi nyingi za Kusini mwa Afrika kupata uhuru wake kutoka kwa wakoloni; nchi hizo ni Jamhuri za Afrika ya Kusini, Angola, Namibia, Msumbiji na Zimbabwe. Mwalimu Nyerere aliwasaidia wapigani uhuru wa vyama vya ANC, MPLA, SWAPO, FRELIMO na ZANU. 
Related image


#17. Tanzania ina kisiwa kikubwa katika visiwa vyote vilivyo ndani ya maziwa ya bara la Afrika; Kisiwa cha Ukerewe ambacho kina eneo la kilomita za mraba 530. Kisiwa hiki kinapatikana ndani ya Ziwa Victoria. Huenda hukuifahamu hii, basi nimekufahamisha.
Image result for ukerewe map
Kisiwa cha Ukerewe kama jinsi ramani inavyoonekana kwa juu.
Image result for ukerewe map
Kisiwa cha Ukerewe (rangi nyekundu)
#18. Tanzania kuna mawe ambayo ni kuvutio kikubwa cha utalii nchini. Mawe haya yamebebana bila kudondoka kwa miaka mingi sasa. Ni maarufu kama Bismarck rock. Yapo jijini Mwanza na yamewekwa katika noti ya Tsh. 1,000/=
Image result for bismarck rock
Mawe ya Bismarck ambayo ni maarufu sana nchini

#19. Uwepo wa banadari ya Dar es Salaam ambayo inakuza uchumi na pato la taifa kwa kuingiza na kusafirisha bidhaa ndani na nje ya nchi. Bandari hii inasaidia pia nchi za Congo DR, Rwanda, Zambia, Burundi na Malawi.
An aerial view of a section of the port. Credit: Tanzania Ports Authority
Picha ya Bandari ya Dar es Salaam kama ilivyopigwa kutoka juu.

#20. Tanzania ina maeneno 7 ambayo yalitangazwa kuwa ni maeneo ya urithi wa kujivunia duniani. Maamuzi hayo yalitajwa kwa nyakati miaka tofauti na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia elimu, sayansi na utamaduni (UNESCO). Maeneo hayo ni haya yafuatavyo:
  • Hifadhi ya Taifa ya Serengeti
  • Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro
  • Mlima Kilimanjaro
  • Magofu ya kale ya Kilwa na Songa Mnara
  • Michoro ya Mapangoni ya Kondoa
  • Hifadhi ya Wanyama ya Selous
  • Mji Mkongwe Unguja.


Picha zote kwa msaada wa mtandao. Picha hizi si miliki ya blogu hii, kila picha ina mmliki wake.
Unaweza kuacha maoni yako chini ya chapisho hili ama kutuma barua pepe kupitia venancegilbert@gmail.com kama una lolote la kusema ama kuwasiliana nami kwa WhatsApp namba +255712586027 ama kunipigia kwa namba +255753400208.

Comments

Popular posts from this blog

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

VITAMBULISHO VYA URAIA KUVUKIA MIPAKA KENYA, RWANDA NA UGANDA

Wananchi wa mataifa ya Rwanda, Uganda na Kenya wamepokea kwa shangwe kuanza kwa mpango wa kutumiwa kwa vitambulisho vya uraia kama cheti cha kuwaruhusu kuvuka mpaka na kuingia moja wapo wa nchi hizo.Mpango huu wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kusafiria katika nchi hizo tatu umeanza kutumiwa rasmi tarahe Mosi Januari 2014, kufuatia makubaliano kati ya viongozi wa mataifa hayo.Mpango wenyewe unatokana na makubaliano kati ya viongozi wa nchi tatu waliofikia wakati wa mkutano uliofanyika nchini Uganda mwezi Juni mwaka jana.Pia mpango huu unalenga kurahisisha usafiri wa watu wa jumuiya katika mataifa wanachama kama awamu ya pili ya ushirikiano kati ya mataifa wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.Hata hivyo siku moja tu baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kuwaruhusu raia wa nchini tatu, Uganda, Kenya na Rwanda kuvuka mpaka na kuingia mojawapo ya nchi hizo sasa inaonekana mpango huo huenda ukawanufaisha watu wachache peke yake.Sio ...

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

10. YUSUF MANJI Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini. 9. FIDA RASHID Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine. 8. GHALIB SAID MOHAMMED Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

MADAGASCAR YAPATA RAIS MPYA

Maafisa nchini Madagascar wanasema kuwa matokeo ya mwanzo mwanzo ya duru ya pili ya uchaguzi wa Rais uliofanyika mwezi Disemba, yanaonyesha mshindi kuwa waziri wa zamani wa fedha Hery Rajaonarimampianina.Tume ya uchaguzi ya nchi hiyo inasema kuwa bwana Hery Rajaonarimampianina alishinda asilimia hamsini na tatu (53%) ya kura zilizopigwa.Mshindani wake, Jean Louis Robinson anasema kuwa uchaguzi ulikumbwa na wizi wa kura na sasa anasema sharti shughuli ya kuhesabu kura irejelewe.Uchaguzi huo ulikuwa mpango wa kurejesha utulivu kwa nchi hiyo baada ya mapinduzi ya kijeshi kufanyika miaka minne iliyopita.Bwana Rajaonarimampianina alikuwa mgombea aliyeungwa mkono na kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi, Rais wa zamani Andry Rajoelina. Chanzo: BBC Swahili