NDEGE YA MAREKANI YAZUILIWA NA NDEGE ZA CHINA

Ndege za China zaizuia ndege ya MarekaniNdege mbili za kijeshi za China zimeizuia 'vibaya' ndege ya Marekani kulingana na jeshi la Marekani.

Ndege hiyo inayohusika na kufanya uchunguzi, ilikuwa katika safari yake ya kutaka kugundua mionzi katika anga ya kimataifa iliopo mashariki mwa bahari ya China.
Ndege hiyo ilikuwa imetumiwa kugundua ushahidi kuhusu majaribio ya kinyuklia ya Korea Kaskazini. 

China imekuwa ikituhumu vitendo vya Marekani karibu na maji hayo yenye utajiri mkubwa yaliopo katika pwani yake ,hatua ambayo imesababisha wasiwasi kati ya mataifa hayo mawili.
''Swala hilo linaangaziwa na China kupitia njia mwafaka ya kidiplomasia mbali na zile za kijeshi'', msemaji wa jeshi la angani la Marekani Luteni kanali Lori Hodge amesema.
''Uzuizi huo haukufanywa kwa njia ya ''utaalamu'' kutokana na hali ya rubani wa ndege hiyo ya China ikiwemo kasi ya ndege zote mbili'', aliongezea akisema uchungzi wa kijeshi unaendelea.
Bahari hiyo ya kusini mwa China
Bahari ya Kusini mwa China
Mnamo mwezi Februari , ndege moja ya Marekani ilianza kile Washington ilielezea kuwa doria yake ya kawaida kusini mwa bahari ya China ikiandamana na idadi fulani ya meli za kijeshi.
Ndege na meli hizo zilielekea katika eneo hilo licha ya onyo kutoka China dhidi ya kutoa changamoto yoyote kwa uhuru wa China katika eneo hilo.

Kwa nini bahari hiyo ya kusini mwa China inazozaniwa?
Mnamo mwezi Mei 2016 ndege mbili za kijeshi za China zilizuia ndege nyengine ya Marekani iliokuwa katika anga ya kusini mwa bahari ya China.

Wakati huo, jeshi la Marekani lilisema kuwa ilikuwa ikipiga doria ya kawaida katika eneo hilo.

Chanzo: BBC

MABOMU YASABABISHA WATU ZAIDI YA ELFU 50 KUHAMA UJERUMANI

Mabomu kutoka vita vya pili vya dunia bado yako Hannover

Operesheni kubwa ya kuwaondoa wakaazi wengi wa mji wa Hanover ulioko kaskazini mwa Ujerumani, inaendelea, ya kuwahamisha zaidi ya watu elfu 50 baada ya mabomu makubwa ya wakati wa vita vya dunia, kupatikana kama hayajalipuka.
Wakaazi hao wanatarajiwa kuondoka majumbani mwao baadaye leo, ili kuwapa nafasi wataalamu wa kutegua mabomu, kuhamishia mahala salama mabomu hayo ambayo yanakisiwa kuwa matano.

Operesheni hiyo itachukua siku nzima, na hata zaidi ikiwa mabomu mengineyatapatikana.
Washambuliaji walivamia mji wa Hanover mara 125 kwa mabomu, wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia.
Wataalamu wanaamini kuwa mabomu ambayo hayakulipuka huenda yako chini ya jengo hiliHaki miliki ya picha Getty Images.    Wataalamu wanaamini kuwa mabomu ambayo hayakulipuka huenda yako chini ya jengo hili                
Zaidi ya asilimia 20 ya mabomu yaliyoangushwa mjini humo hayakulipuka.
Baadhi ya mabomu mengine yalikuwa na vifaa vinavyochukua muda mrefu kulipuka, na ambayo kwa sasa yameanza kuoza, na kusababisha hatari kubwa.


Chanzo: BBC

WAPIGANAJI WA HAMAS WAPATA KIONGOZI MPYA

Ismael Haniyeh ndio kiongozi mpya wa kundi la Hamas
Ismael Haniyeh ndio kiongozi mpya wa kundi la Hamas
Wapiganaji wa Palestina Hamas wamepata kiongozi mpya.
Kiongozi huyo ni Ismail Haniyeh ambaye hadi hivi karibuni alikuwa ndio kiongozi wa kundi hilo katika ukanda wa Gaza.
Akijulikana kama kiongozi anayetumia akili nyingi wakati wa kutatua maswala, anachukua mahala pake Khaled Meshaal ambaye ameliongoza kundi hilo akiwa ughaibuni kwa miongo miwili.
Uchaguzi wa kiongozi mpya ulifanyika kupitia njia ya Video Link kati ya wajumbe waliopo katika ukanda wa Gaza na wale waliopo nchini Qatar ambako Meshaal ana makao yake.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa bwana Meshaal anaachia ngazi wakati ambapo Hamas limeanza kulegeza msimamo wa kisiasa.
Kwa mara ya kwanza wiki iliopita katika sera mpya kundi hilo liliwachilia wito wake wa kuiharibu Israel.
Hamas bado lina wapiganaji wake katika eneo la Gaza na bado linaaminika kuwa kundi la kigaidi na Israel Marekani na mataifa ya bara Ulaya.

Chanzo: BBC

MANCHESTER CITY YAIBURUZA VIBAYA CRYSTAL PALACE

Tokeo la picha la Machester City
Klabu ya Manchester City imerudi katika nafasi yake ya tatu katika ligi ya Uingereza baada ya kupata ushindi mkubwa dhidi ya Crystal Palace ambayo imeshindwa kwa mara ya tatu mfululizo.
City ilihitaji dakika mbili pekee kupata bao la kwanza baada ya David Silva kufunga baada ya kurudi kutoka kuuguza jereha.
Wenyeji waliongeza bao la pili dakika tatu katika kipindi cha pili wakati Vincent Kompany alipopiga mkwaju ulioingia katika kona ya ya juu ya goli na baadaye Kevin De Bruyne akafunga bao la tatu.
Ndoto ya Palace ilithibitishwa baada ya Raheem Sterling kufunga bao la nne kabla ya beki Otamendi kufunga bao la tano katika dakika za lala salama.
Kikosi hicho cha Sam Allardyce kiko pointi tano juu ya eneo la kushushwa daraja na kinaweza kuwa hatarini iwapo klabu za Hull City na Swansea zitaibuka washindi siku ya Jumamosi.

RAIS MAGUFULI AMETUMA SALAMU ZA POLE KWA WAFIWA WA AJALI ARUSHA

Tokeo la picha la magufuli
Hii hapa chini ni taarifa kama ilivyoandikwa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko mkubwa taarifa ya vifo vya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu 2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha vilivyotokea leo saa 3 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika eneo la Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.
Wanafunzi na walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni ambako limesababisha vifo hivyo na majeruhi watatu.
Kufuatia ajali hiyo, Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo na kueleza kuwa ajali hiyo imezima ndoto za watoto waliokuwa wakijiandaa kulitumikia Taifa na imesababisha uchungu, huzuni na masikitiko makubwa kwa familia za marehemu na taifa kwa ujumla.
"Ndugu Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo naomba unifikishie pole nyingi kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wote wa wanafunzi, walimu na dereva waliopoteza maisha, hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na uwaambie naungana nao katika majonzi na maombi.
"Muhimu kwa sasa tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema, majeruhi wapone haraka na wote walioguswa na msiba huu wawe na moyo wa subira, ustahimilivu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu" Amesema Rais Magufuli.

KANYE WEST AMEFUTA AKAUNTI ZAKE KATIKA MITANDAO YA KIJAMII


Msanii wa muziki wa Rap nchini Marekani Kanye West amefuta akaunti zake za Twitter na zile za Instagram ambazo zilikuwa na makumi ya mamilioni ya wafuasi.
Sababu hazijulikani lakini mwezi Novemba mwaka jana alimaliza ziara yake mapema.
Alimshtumu mwanamuziki mwenza Jay Z kwa kujaribu kumuua na kuondoka katika jukwaa baada ya kutangaza kwamba atampigia kura rais wa Marekani Donald Trump wakati wa uchaguzi wa taifa hilo.
Mkewe nyota wa Raality TV Kim Kardashian amesalia katika mtandao wa Twitter na ana wafuasi milioni 51.
Hivi ndivyo ilivyokuwa wakati mashabiki walipojaribu kuwasiliana na msanii huyoHaki miliki ya pichaTWITTER
Image captionHivi ndivyo ilivyokuwa wakati mashabiki walipojaribu kuwasiliana na msanii huyo
Amekuwa akijikuza pamoja na kampuni ya kuuza nguo ya mumewe.
Muda mfupi baada ya akaunti zake za mitandao kufungwa mkewe alichapisha ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kwamba amechora nembo ya kampuni hiyo katika mkono wake.
Mashabiki walimsihi Kardashian amwambie mumewe arudi katika mtandao.
Hivi ndivyo ilivyokuwa katika mtandaoo wa Twitter wa mkewe Kim KardashianHaki miliki ya pichaTWITTER
Image captionHivi ndivyo ilivyokuwa katika mtandaoo wa Twitter wa mkewe Kim Kardashian
West alikuwa ameanza kuishi maisha ya ukimya katika mitandao ya kijamii mapema mwaka huu na alidaiwa kufuta ujumbe wake uliokuwa ukimuunga mkono rais Donald Trump.
Hatua yake pia ilijiri baada ya mkewe kuibiwa vito vyenye thamani ya dola milioni 10.5 mjini Paris mwezi Oktoba.

MFAHAMU KARL MARX KWA UFUPI: DUNIA INAMKUMBUKA LEO

Karl Mark alikuwa ni mwanafalsafa na mwanamapinduzi wa Ujerumani aliyeandika vitabu vya The Communist Manifesto na Das Capital vitabu ambavyo vilikuwa vikipingana na mfumo wa kibepari na kuunda mfumo wa Ukomunisti ama Ujamaa kama alivyoutafsiri hayati Mwalimu JK Nyerere.

Karl Marx alizaliwa Mei 5, 1818. Alianza kuchunguza nadharia za kijamii alipokuwa Chuo Kikuu na wenzie waliounda kikundi chao kilichoitwa Young Hegelians. Hiki kilikuwa ni kikundi kilichokuwa kinaamini katika falsafa za mwalimu wao aliyeitwa Hegel. Marx alikuwa mwandishi wa habari na machapisho yake kuhusu Ukomunisti vilipelekea yeye kufukuzwa Ujerumani na Ufaransa. Mwaka 1848 alichapisha kitabu chake cha The Communist Manifesto akiwa na Friedrich Engels ambacho kilipelekea kufukuzwa Ujerumani na kukimbilia London, Uingereza, huko pia aliandika kitabu cha Das Kapital ambako ndiko alikoishi mpaka alipoiaga dunia.

Karl Marx alikuwa ni miongoni mwa watoto 9 wa Heinrich Marx na Henrietta Marx huko Trier Prussia ya zamani (kwa sasa Ujerumani) Baba yake alikuwa mwanasheria aliyefanikiwa sana na alikuwa mwanaharakati aliyependa mabadiliko nchini Prussia. Japokuwa wazazi wake walikuwa na asili ya Kiyahudi, baba yake Marx alihamia katika Ukristu mwaka 1816 alipokuwa na umri wa miaka 3.

Marx alikuwa ni mwanafunzi wa kawaida. Alisomea nyumbani hadi alipokuwa na umri wa miaka 12 na kisha alipelekwa Jesuit High School alikosoma kwa muda wa miaka 5 kuanzia 1830 hadi 1835.

Mwaka 1835 Marx alijiunga na Chuo Kikuu cha Bonn. Chuo hiki kilikuwa na Itikadi za kuipinga serikali. Marx alijiunga na maisha ya uanafunzi katika chuo hiki. Katika semista mbili chuoni hapo, alifungwa kwa ulevi na kuvuruga amani chuoni hapo, kuwa na madeni lakini pia kushiriki katika falsafa zilizokinzana na chuo. Mwisho wa mwaka baba yake Marx alimsisitiza kuwa serious na masomo katika Chuo Kikuu cha Berlin.

Katika Chuo Kikuu Berlin alisomea fani ya sheria na falsafa ambako alikutana na falsafa za mwalimu wake George Hegel ambaye alikuwa profesa katika chuo hicho mpaka alipofariki mwaka 1895. Baadaye Marx alijiunga na kikundi cha Young Hegelians ambacho pia kulikuwa na Bruno Bauer na Ludwig Feuerbach ambao walikosoa kuanzishwa kwa siku za kisiasa na kidini nchini humo. Kuna mengi yalijiri Marx alipokuwa Berlin.
Tokeo la picha la marx and bruno bauer
Bruno Bauer
Marx hakutulia wala kuishia hapo. Mwaka 1841 alitunukiwa Shahada yake ya Uzamivu ya Chuo Kikuu cha Jena lakini harakati zake za kisiasa zilipelekea yeye kutokuaminiwa na kuwa mwalimu katika chuo chochote nchini Ujerumani. Alianza kufanya kazi kama mwandishi wa habari na mwaka 1842 alikuwa Mhariri wa Rheinische Zeitung ambalo lilikuwa ni gazeti la wanaharakati wa usawa huko Cologne, Ujerumani. Mwaka mmoja baadaye serikali ililifuta gazeti hilo kuanzia April 1, 1843. Marx aliacha kazi hapo Machi 18. Miezi mitatu baadaye alimuoa Jenny von Westephalen  na Oktoba walihamia Paris, Ufaransa.
Tokeo la picha la karl marx and his family
Marx akiwa na mkewe Jenny von Westephalen
Mji wa Paris ulikuwa ni kitovu cha harakati za kisiasa barani Ulaya mwaka 1843. Huko Marx akiwa na Arnold Ruge, walianzisha gazeti la uchambuzi wa kisiasa lilioitwa Deutsch-Franzosische Jahrbucher (German-French Annals) jambo moja tu ndilo lilikuwa likichapishwa katika gazeti hili kabla Marx na Ruge hawajatofautiana kiitikadi hadi kupelekea gazeti hilo kupotea kwenye ramani lakini Agosti 1844, gazeti hilo liliwaleta pamoja Marx na Friedrich Engels kama mwandishi mshiriki ambaye alikuwa msaidizi wake na rafiki yake hadi kifo. Pamoja, wawili hao walianza kuandika makala za kukosoa mawazo ya Bruno Bauer ambaye alikuwa ni mshiriki katika kikundi cha Young Hegelians. Mwaka 1845 Marx na Engels walichapisha makala yao iliyojulikana kama The Holy Family.


Baadaye katika mwaka huo, Marx alihamia Ubeligiji baada ya kufukuzwa nchini Ufaransa ambako aliandika katika gazeti la Vorwarts! ambalo lilikuwa na itikadi ambazo baadaye zingepelekea kuanzishwa kwa Jumuiya ya Kikomunisti. Alipokuwa Ubeligiji, Marx alipokelewa na Moses Hess, na baadaye aliachana kabisa na siasa za Young Hegelians. Alipokuwa nchini humo aliandika The German Ideology ambako ndiko alipoandika nadharia yake inayojulikana kama Historical Materialism. Marx hakupata mtu wa kuruhusu kuchapisha makala yake. The German Ideology na Theses on Feuerbach hayakuchapisha makala hiyo hadi alipofariki. Nadharia hii inawataka watu kushiriki kwa vitendo kupinga uonevu.


Tokeo la picha la Karl marx and engels
Karl Marx & Friedrich Engels
Mwanzoni mwa mwaka 1846, Mark alianzisha Communist Correspondence Committee katika juhudi zake za kuunganisha ukomunisti barani Ulaya. Waingereza walivutiwa na sera zake na kuitisha mkutano na kuunda shirikisho lao Communist League na mwaka 1847 katika mkutano wao mkuu uliofanyika London, shirikisho hilo liliwaomba Marx na Engels kuandika Manifest der Kommunistischen Partei (Manifesto of the Communist Party)

The Communist Manifesto ni miongoni mwa kazi maarufu za Marx ambayo ilichapishwa mwaka 1848 na baadaye mwaka 1849 Marx alifukuzwa nchini Ubeligiji. Alikwenda Ufaransa ambako alianzisha vuguvugu la Mapinduzi nchini humo ambako pia alifukuzwa. Prussia ilikataa kumpokea Marx na hivyo alihamia London japokuwa Uingerza ilikataa kumpa uraia nchini humo hadi kifo chake.

Marx alipokuwa London alisaidia kuundwa kwa shirikisho la wanataaluma wa Ujerumani German Workers' Educational Society lakini pia Shirikisho la Kikomunisti The Communist League. Aliendelea kufanya kazi kama mwandishi japokuwa safari hii alizuiwa na baadhi ya itikadi zake. Alifanya kazi katika The New York Daily Tribune kwa miaka 10 kuanzia 1852-1862 lakini hakulipwa , aliishi kwa kusaidiwa na rafiki yake Engels.

Marx aliutazama mfumo wa kibepari zaidi na mwaka 1867 alichapisha toleo la kwanza la kitabu chake Das Kapital. Baadaye alitumia muda wake kupitia chapisho hilo na akawa akilifanyia masahihisho na kuongeza baadhi ya vitu. Matoleo mawili yaliyofuata baadaye ambayo hata hakuyakamilisha yaliunganishwa na kuchapishwa na Engels.

Marx alifariki kwa ugonjwa wa mapafu unaojulikana kitaalamu kama pleurisy alipokuwa London Machi 14, 1883. Katika kaburi lake kuna maandishi ya kitabu chake The Communist Manifesto yenye maana wafanyakazi wote waungane.



MAKALA HII IMEANDALIWA KWA MSAADA WA MTANDAO INAWEZA KUFANYIWA MAREKEBISHO MUDA WOWOTE PANAPOHITAJIKA.

AUDIO | DARASSA-HASARA ROHO | DOWNLOAD

MECHI YA ATLETICO & REAL MADRID KULINDWA NA POLISI 2,000

Polisi wa kukabiliana na fujo walikabiliana na mashabiki wa Bayern Munich mnamo 18 Aprili
Polisi wa kukabiliana na fujo walikabiliana na mashabiki wa Bayern Munich mnamo 18 Aprili
Walinzi zaidi ya 2,000 watatumiwa kudumisha usalama na kudhibiti mashabiki wakati wa mechi ya nusufainali ya mkondo wa kwanza kati ya Real Madrid na Atletico Madrid katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Mechi hiyo itakayochezewa Santiago Bernabeu siku ya Jumanne imeorodheshwa kama yenye "hatari kubwa" na usalama "utaimarishwa", maafisa wasimamizi wa jiji la Madrid walisema Ijumaa.

UEFA wameamrisha usalama katika mechi za klabu Ulaya uimarishwe baada ya shambulio kwenye basi la timu ya Borussia Dortmund mnamo 11 Aprili.

Atletico watakuwa na mashabiki 4,000 katika uwanja huo wa Real unaotoshea mashabiki 80,000.
Kawaida ni mashabiki wachache sana husafiri kuhudhuria mechi za ugenini Uhispania.

Idadi ya walinzi tarehe 2 Mei itakuwa ya juu zaidi ya waliokuwepo wakati wa mechi iliyopita ya Real Ulaya dhidi ya Bayern Munich polisi wa kukabiliana na fujo walipokabiliana na mashabiki wageni wakati wa mapumziko.

Kulikuwa pia na fujo mechi ya robofainali ya Atletico nyumbani, polisi wakikabiliana na mashabiki wa Leicester City.

Chanzo: BBC

WAFAHAMU MARAIS 10 WA AFRIKA WALIOFARIKI WAKIWA MADARAKANI

Leo nimekuandikia orodha ya marais 10 waliofariki wakiwa madarakani. Tuanze kuhesabu sasa:

Lansana Conté, President of Guinea 
10. Lansana Conte, Rais wa Guinea
Baada ya miaka 24 Lansana Conte alifariki na ugonjwa usiojulikana akiwa na umri wa miaka 74. Alipambana na matatizo ya kisukari na maradhi ya moyo. Kuanzia Aprili 1984 mpaka kifo chake Desemba 2008 alikuwa ni rais wa pili kushika madaraka nchini Guinea. Mbali na matatizo ya afya aliyokuwa nayo aliweza kushinda uchaguzi.


Flash - Galerie Verstorbene Persönlichkeiten 2009 Omar Bongo (AP) 

9. Omar Bongo, Rais wa Gabon

Saratani ya tumbo iliosambaa ndio iliyosababisha kifo cha Rais Omar Bongo June 2009 mjini Barcelona, Uhispania, baada ya kuwa rais kwa miaka 42 mfululizo. Alifariki akiwa na umri wa miaka 72 na pia alikuwa ni kiongozi aliyekaa madarakani kwa muda mrefu katika historia na alikuwa akiongoza katika mambo ya rushwa. Bongo alijikusanyia utajiri mkubwa huku akiiacha nchi yake katika hali ya umasikini. 


João Bernardo Vieira, President of Guinea-Bissau 

8. Joao Bernardo Vieira, Rais wa Guinea-Bissau

Joao Bernardo Vieira rais wa Guinea-Bissau aliuwawa nchi mwake Machi 2009, akiwa na umri wa miaka 69. Alikuwa kiongozi wa nchi kwa muda wa miaka 31. 1978 alikuwa waziri mkuu na kuchukua madaraka 1980 na alitawala kwa miaka 19. Alibadilika na kuwa kiongozi wa umma na aliongoza miaka minne mingine zaidi. 2005 alishinda tena uchaguzi wa uraisi. 


Umaru Musa Yar’Adua, President of Nigeria  

7. Umaru Musa Yar’Adua, Rais wa Nigeria

Umaru Musa Yar’Adua, alifariki akiwa na umri wa miaka 58 mwaka 2011 akisumbuliwa na matatizo ya moyo nchini Nigeria. Alikuwa madarakani kwa miaka mitatu pekee. Alikosekana katika kampeni za uchaguzi kwa sababu za kiafya. Baada ya kuchaguliwa kwake 2007, afya yake ilidhoofika kwa haraka. 


Muammar Gaddafi, Brotherly Leader and Guide to the Revolution of Libya  

6. Muammar Gadhafi, kiongozi na mwana mapinduzi wa Libya

Mwathirika wa mauaji, Muammar Gadhafi aliuawa akiwa na umri wa miaka 69 na vikosi vya waasi katika mazingira yasiyoeleweka nchini Libya, baada ya kuwa kiongozi wa taifa hilo kwa muda wa miaka 42. Aliuondoa uongozi wa kifalme bila ya kumwaga damu wakati wa mapinduzi ya kijeshi ya mwaka 1969 lakini utawala wake ulifikia kikomo baada ya matokeo ya vuguvugu la mapinduzi ya uarabuni. 


Malam Bacai Sanhá, President of Guinea Bissau 

5. Malam Bacai Sanha, Rais wa Guinea-Bissau

Kiongozi wa nne kufariki mwaka 2012 alikuwa ni Malam Bacai Sanha rais wa Guinea-Bissau. Aliugua ugonjwa wa kisukari na alifariki mjini Paris baada ya miaka minne kama rais akiwa na umri wa miaka 64. Katika kipindi chote cha utawala wake alisumbuliwa na matatizo kadhaa ya kiafya yalosababisha kwenda hospitali mara nyingi.

Bingu wa Mutharika, President of Malawi  

4. Bingu wa Mutharika, Rais wa Malawi

Rais mwingine aliyefariki mwaka 2012 ni Bingu wa Mutharika, rais wa Malawi. Alipata mshutuko wa moyo mwezi Aprili na kufariki siku mbili baadae akiwa na umri wa miaka 78. Uongozi wake ulikuwa ni wa miaka nane na alipata mafanikio makubwa katika sera zake za kilimo na chakula. Sifa yake iliharibika kufuatia maandamano makubwa yalopinga ununuzi wa ndege ya rais iliyogharimu Dola milioni 14


John Atta Mills, President of Ghana 

3. John Atta Mills, Rais wa Ghana

Pia mwaka 2012, John Atta Mills, rais wa Ghana alifariki akiwa nyumbani kwake kwa mshutuko wa moyo na saratani ya koo akiwa na umri wa miaka 68. Alishinda uchaguzi wa rais wa 2008 alishika madaraka kwa miaka mitatu pekee. Alianzisha mikakati mingi ya kiuchumi na mageuzi ya kiuchumi yalomletea sifa kutoka ndani na nje ya nchi. 

Meles Zenawi, Prime Minister of Ethiopia 

2. Meles Zenawi, Waziri Mkuu wa Ethiopia

Meles Zenawi alifariki Agosti 2012 nchini Ubelgiji akiwa na umri wa miaka 57 kwa maambukizi yasiyojulikana. Ameiongoza Ethiopia kwa miaka 5 kama rais kuanzia mwaka 1991 hadi 1995 na kama Waziri Mkuu kwa miaka 17 kuanzia 1995 hadi 2012. Anajulikana kwa kuanzisha mfumo wa siasa wa vyama vingi, lakini pia kwa ukandamizaji wa maandamano halali ya watu wa Oromia wa kaskazini mwa Ethiopia. 

Michael Sata, President of Zambia 

1. Michael Sata, Rais wa Zambia

Michael Sata ni kiongozi wa hivi karibuni aliyefariki madarakani akiwa na umri wa miaka 77 kwa maradhi ambayo hayakuwekwa wazi Oktoba 28 2014, nchini Uingereza. Baada ya uchaguzi wa 2011, uvumi juu ya afya yake ulisambaa nchini Zambia. Kukosekana kwake katika shughuli kubwa za kitaifa kuliibua wasiwasi wa afya yake ingawa msemaji wake alisema alikuwa katika afya nzuri.




Chanzo: DW Idhaa ya Kiswahili.

THE WHEEL A POEM BY VENANCE GILBERT

Venance on the sitting benches of Vikenge Hostels, Mzumbe University Main Campus Morogoro

Poet: Venance Gilbert
Poem: The Wheel
Composition: October 18, 2016
Publication: April 20, 2017
Copyright: Venance Gilbert  2016



The wheel was moving
But I never noticed
second counted, minutes gone,
hours died, days were numbered
weeks moved, months and years passed
I noticed it as the matter of living.

Mental pictures remind me
those days when the moments existed
Sometimes I wish to restore and start
I find the wheel moving fast following the line
Like the train on its pathway
Happy birthday takes back to those moments.

Today I am youth
Full capable to place the mind on motion
I often regret when I remember the moment
The moment when I was the driver of the wheel
But now the wheel drives, how possible?
I never drove it well and careful at the moment,
Drive the wheel careful before it drive you on its pathway.

DOWNLOAD JAY2 THE HUSTLER X CAST BEEZY-TIME IS NOW


Hii ni mpya kutoka kwa Jay2 th hustler & Cast beezy-Time is Now.

DOWNLOAD HARMONIZE & RICH MAVOKO-SHOW ME NEW SONG

Tokeo la picha la harmonize & mavoko show me 
Brand new track kutoka WCB. Harmonize & Rich Mavoko wametuletea hii, Show Me

DOWNLOAD

WANASAYANSI WAGUNDUA UHAI KATIKA SAYARI YA SATURN

Sayari ya Saturn
Sayari ya Sarateni "Saturn"

Mwezi wa Enceladus ambao uko kwenye sayari ya Saturn huenda ukawa mahali bora zaidi pa kwenda kutafuta maisha nje ya dunia.

Tathmini hii inatokea kufuatia uchunguzi katika sayari hiyo yenye kilomita 500 uliofanywa na Cassini.

Uchambuzi wa kemia wa Cassini unaonyesha matundu ya maji moto kwenye sakafu ya bahari ya Enceladus, maeneo ambayo yanahusishwa na kuwepo kwa maisha, hapa duniani.

Kuwepo kwa maji haya sio thibitisho kamili kwamba vitu vilivyo na uhai vinaishi katika mwezi huo mdogo lakini teknolojia zinaweza kutumika kupima maji hayo na kutoa ushahidi zaidi.

"Tuna uhakika kuwa kitu chenye uhai kinaweza kuishi kwenye bahari ya Enceladus lakini lazima tufanye utafiti zaidi," alisema mwanasayansi wa Cassini kutoka Taasisi ya Utafiti ya Southwest, San Antonio, Dkt. Hunter Waite.

"Iwapo hakuna maisha huko, ni sawa, lakini ikiwa maisha yapo itakuwa bora zaidi," alieleza BBC.
Bahari iliyopo kwenye Enceladus inakisiwa kuwa na kina kirefusana sana na yapo majimaji kwa sababu ya joto linalotokana na mvuto wa mara kwa mara kutoka kwenye sayari ya Saturn.

Cassini tayari amedhibitisha kwamba maji hayo yanashikana na sakafu ya bahari kutokana na aina ya chumvi na silika ambayo pia imeonekana katika mashimo.
 
Lakini wanachotaka kujua sana wanasayansi ni ikiwa maswala fulani yanayotendeka duniani pia yanaweza kufanyika katika Enceladus - kitu kinachoitwa serpentinisation, ambayo hutengeneza gesi ya hidrojeni.

"Kwa viumbe hai, hidrojeni huwa ni kama kama pipi - ni chakula wanachokienzi," alieleza Dkt Chris McKay, mwanabiolojia wa maswala ya anga wa shirika la Nasa.

"Ni nzuri sana kwa kuvipa nguvu, na inaweza kusaidia viumbe vidogo sana. Kupata hidrojeni itakuwa vizuri sana na itakuwa moja ya ushahidi utakaoonyesha uwezekano wa kuwepo na uhai."

Viumbe hai anavyozungumzia Dkt McKay vinaitwa methanojeni kwa sababu vinatengeneza gesi ya metheni vinapogusana na hidrojeni na gesi ya kaboni .

Nasa, ambayo inaongoza ujumbe wa Cassini , ilitakikana kufanya tangazo la hidrojeni miezi michache baada ya uchunguzi wa mwisho waroketi ya mwezini, Oktoba mwaka wa 2015.

Ziara ya Cassini sasa inakamilika . Baada ya kuizunguka Saturn kwa muda wa miaka 12, inaendelea kuishiwa na mafuta na sasa itawachiliwa kuingia kwenye anga ya dunia hiyo ya Saturn mwezi Septemba, kuhakikisha kuwa haiwezi kugongana na Enceladus na kusababisha kuchafuka kwake.


Chanzo: BBC

DOWNLOAD ACHA NIKAE KIMYA DOWNLOAD PLATNUMZ NEW SONG

Huu ni wimbo mpya kuhusu hali inayoendelea nchini hivi sasa. Diamond pia ameamua kuzungumza kwa namna yake.