Skip to main content

WABUNGE: "BILA KILIMO KWANZA HAKUNA SERIKALI YA VIWANDA"

 
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wamesema bila kuwekeza katika kilimo, azima ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda haitatimia.

Kadhalika, wameipongeza Serikali kwa kuondoa tozo 108 zilizokuwa kero kwa wakulima na kuitaka Serikali kuhakikisha tozo zilizoondolewa zinawanufaisha zaidi wakulima na Watanzania, badala ya kuwanufaisha wafanyabiashara pekee. Waliyasema hayo jana kwa nyakati tofauti bungeni Dodoma wakati wakichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Mwaka wa Fedha 2017/18.

Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Ditopile (CCM), alisema kama Tanzania inataka kuwa ya viwanda, haina budi kuwekeza katika utafiti kwa ajili ya sekta ya kilimo ili kubaini namna bora zaidi za kutumia rasilimali na fursa zilizopo ili kuimarisha kilimo na hivyo kusaidia kufikia haraka azima ya kujenga Tanzania ya viwanda. Alisema tayari fursa za kuinua kilimo na kukifanya uti wa mgongo nchini zimeanza kuonekana kwani kwa sasa Tanzania ndiyo inayouza vyakula na bidhaa za biashara katika nchi mbalimbali duniani zikiwemo nchi za Sudan, Kenya na Uganda wanaonunua mazao ya chakula kama mahindi.

“Nchi kama India inanunua kwetu korosho, choroko na tumbaku. Kwa sasa mipango ni kuipeleka nchi kwenye viwanda ni wakati muafaka wa kuwekeza kwenye kilimo kwa kufanya utafiti za kisayansi za namna bora ya kuendeleza kilimo chetu kwa sababu kilimo ndio ajira, chakula na fedha,” alisisitiza. Alisema Tanzania inasifika kwa kufanya utafiti, lakini pamoja na kuwa na uwezo huo bado haujatumika vizuri kuendeleza mambo ya msingi yakiwamo maeneo ya kilimo, mifugo na uvuvi.

“Kwa mfano sisi ndio wenye eneo kubwa katika Ziwa Victoria, lakini takwimu za kidunia zinaonesha Uganda yenye sehemu ndogo katika ziwa hilo ndiyo inayoshika nafasi ya juu; ya sita duniani kwa uvuvi huku sisi Tanzania tukishika nafasi ya nane,” alisema. Mbunge wa Mbinga Mjini, Sixtus Mapunda (CCM) aliitaka serikali iwekeze kwenye utafiti wa kilimo ili kuyabaini maeneo ya kijiografia na kisayansi yanayoweza kuikuza kwa kasi sekta hiyo ya kilimo inayokwenda sambamba na sekta ya viwanda.

“Kwa mfano Morogoro ina udongo wenye rutuba na mito inayotiririsha maji kwa mwaka mzima, utafiti ukifanyika wa namna bora ya kutumia rasilimali hizo, ni wazi kuwa Morogoro pekee inaweza kulisha Tanzania nzima,” alisema. Pamoja na hayo mbunge huyo alisema si kweli utitiri wa kodi zilizofutwa na serikali umewalenga zaidi wafanyabiashara na wenye kampuni na si wakulima kwa kuwa wafanyabiashara na kampuni hizo kutokana na kufutwa kwa tozo hizo kuanzia sasa watanunua mazao na bidhaa hiyo kwa bei inayostahili.

Kwa upande wake Mbunge wa Hanang, Mary Nagu (CCM), alisema serikali haina budi kuzingatia kuwa kilimo ndicho kinachochangia ajira kwa Watanzania takribani asilimia 65, kinachozalisha chakula kwa Watanzania kwa asilimia 100 na kuingiza asilimia 28 katika pato la taifa. “Hii ni sekta muhimu sana, ni vema Serikali ione umuhimu wa kuifanyia mageuzi sekta ya kilimo na kuongeza bajeti ya wizara ya kilimo kwani hali ilivyo sasa badala ya kilimo kukua, kinashuka kwa kasi,”alisema.

Alisema takwimu zinaonesha kuwa, mwaka 2011 kilimo kilikuwa kwa wastani wa asilimia 3.5 lakini miaka sita baadaye yaani mwaka2016 kilimo hicho kilishuka na ukuaji wake kufikia asilimia 1.7 hali inayozidisha umasikini kwa Watanzania,” alisema Dk Nagu. Alisema pamoja na ukuaji wa kilimo pia bajeti ya Wizara ya Kilimo imekuwa ilishuka badala ya kupanda kila mwaka kwani mwaka 2011 bajeti ya Wizara hiyo ilikuwa asilimia 7.8 ya bajeti nzima ya Serikali, lakini katika bajeti ya mwaka 2016, bajeti ya Wizara hiyo ilishuka na kufikia asilimia 4.9.

Nagu aliyewahi kuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji katika Serikali ya Awamu ya Nne, kupongeza hatua ya Serikali kuondoa utitiri wa kodi zenye kero kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi, aliitaka Serikali ihakikishe kuwa hatua hiyo inawanufaisha zaidi wakulima, wafugaji na wavuvi na si kwa wafanyabiashara.

Kwa upande wake mbunge wa Malindi, Ally Saleh (CUF) aliishauri serikali iwekeze zaidi kwenye fikra za kuleta mabadiliko ya kilimo, mifugo na uvuvi kutokana na ukweli kuwa Tanzania imebarikiwa rasilimali kama vile maziwa, mito, bahari na mikoa yenye rutuba ambayo endapo itatumiwa vema itakuza sekta hizo.
“Sasa hivi tuna tatizo gani, badala ya kilimo kwenda mbele kinashuka. Leo hii haiwezekani sisi tunaongoza kwa kuwa na ng’ombe wengi kuliko Kenya, lakini wao wanatuzidi kwa kuzalisha maziwa. Tunahitaji fikra mpya,” alisema. Alisema Tanzania kuna hekta takribani milioni 13.5 zinazolimika na hekta milioni 1.5 za mikoko, pia ni nchi ya tatu Afrika lakini pia nchi ya 11 duniani kwa kuwa na wingi wa mifugo, lakini bado rasilimali hizo haijatumiwa vizuri.

Mbunge wa Momba, David Silinde (Chadema), aliishauri Serikali iwekeze zaidi katika kilimo kupitia mbolea ya uhakika, dawa za mimea, masoko na miundombinu bora kwa kuwa huo ndio usalama wa watanzania katika chakula.


Chanzo: Habari Leo

Comments

Popular posts from this blog

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

PREMIER: A POEM BY VENANCE GILBERT FOR CELEBRATING THE WORLD MOTHERS' DAY 2018

Venance Gilbert: A composer of this poem. Today is a very special day to all Mothers in the World. It is called World Mothers' Day . As one among the people who were raised by a mother, I found an interest in holding a pen and a piece of paper at least to write the few from the collection of what I did as I was growing up and my mother was there for me to make sure that I grow up wisely and intelligently. On March 28, 2017 I completed the long lasting composition of this poem. IT IS VERY SPECIAL FOR MY DEAR MAMA FLORENTINA AND ALL MOTHERS' IN THE WORLD. May be your mother has passed away (sorry for the loss) but due to spiritual faith, we believe that the resting mothers in heaven can hear our voices, so you can also recite the poem for your mom and she will hear you in one way or another. The poem is called Premier. I welcome you once again to this field of language use. I have hired a very simple language in composing this poem, it is very understood and straightforw...

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD  

RIHANNA - DIAMONDS SONG LYRICS

Shine bright like a diamond Shine bright like a diamond Find light in the beautiful sea, I choose to be happy You and I, you and I, we're like diamonds in the sky You're a shooting star I see, a vision of ecstasy When you hold me, I'm alive, we're like diamonds in the sky I knew that we'd become one right away Oh, right away At first sight I felt the energy of sun rays I saw the life inside your eyes So shine bright, tonight, you and I We're beautiful like diamonds in the sky Eye to eye, so alive We're beautiful like diamonds in the sky Shine bright like a diamond (whoa) Shine bright like a diamond (whoa) Shining bright like a diamond We're beautiful like diamonds in the sky Shine bright like a diamond (whoa) Shine bright like a diamond (whoa) Shining bright like a diamond We're beautiful like diamonds in the sky Palms rise to the universe as we moonshine and molly Feel the warmth, we'll never die, we're like diamonds in the sky You're a ...

TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA

Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz . Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika. Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya  HAPA  ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya  HAPA  ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa: 1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3) SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno ku...