Skip to main content

UMOJA WA MATAIFA WAOMBA MSAADA KWA AJILI YA SYRIA

Umoja wa Mataifa umeomba kiasi cha Dola bilioni 8.4 kwa ajili ya kutoa msaada wa dharura wa kibinaadamu kwa takribani watu milioni 18 wa Syria na kuzunguka ukanda huo unaokumbwa na mzozo.
Ombi hilo limetolewa jana na maafisa wa Umoja wa Mataifa mjini Berlin, Ujerumani kwenye mkutano wa wafadhili na wamesema msaada huo unahitajika haraka nchini Syria, na katika nchi na jamii zinazopambana kuwahifadhi wakimbizi wa Syria.
Kwa mara ya kwanza ombi hilo la Umoja wa Mataifa, linahusisha msaada wa chakula cha kuwapa nguvu na kurudisha afya, malazi, msaada mwingine wa kibinaadamu pamoja na msaada wa maendeleo.
Maafisa wa umoja huo wamesema Dola bilioni 2.9 zinahitajika ili kuwasaidia watu milioni 12.2 walioko ndani ya Syria kwa mwaka 2015, na Dola bilioni 5.5 zinahitajika kwa ajili ya Wasyria walioomba hifadhi ya ukimbizi kwenye nchi jirani na zaidi ya watu milioni moja katika jamii zinazowahudumia.
Kiasi hicho cha fedha kilichoombwa mjini Berlin, ni kikubwa zaidi ya kile kilichoombwa mjini Geneva, mwanzoni mwa mwezi huu, msaada ambao haukujumuisha fedha kwa ajili ya nchi jirani. Hata hivyo, umoja huo umeshapata nusu tu ya kiwango kilichoombwa mwaka huu 2014.
Mahitaji ya kibinaadamu yanaongezeka
Kamishna Mkuu wa Shirika linalowahudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa-UNHCR, Antonio Gutteres ameonya kuwa wakimbizi na watu wasio na makaazi ndani ya Syria hawana akiba na nchi zinazowahifadhi ziko katika wakati mgumu, hivyo utaratibu mpya wa misaada unahitajika.
''Mahitaji ya kibinaadamu duniani yanaongezeka, na yanaongezeka kwa kasi. Na ni wazi kwamba fedha zilizopo kwa ajili ya kutimiza mahitaji hayo, haziongezeki kulingana na kukua kwa kasi ya mahitaji,'' alisema Gutteres.
Naye Mkuu wa shughuli za kibinadamu na misaada ya dharura ya Umoja wa Mataifa, Valerie Amos amesema Syria imetoka katika taifa la watu wenye kipato cha kati na kutumbukia kwenye nchi inayopambana na umaskini mkubwa. Amesema watu walioathirika na mzozo wanahitaji chakula, malazi, maji, dawa na ulinzi, lakini pia wanahitaji msaada wa kujenga upya maisha yao, kupata elimu na huduma za afya.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier amesema mzozo wa kibinaadamu nchini Syria na kwenye nchi jirani unatoa kitisho kwa utulivu wa ukanda wote. Amesema huo ni mwito wa mshikamano kwa mataifa yote na nchi yake iko tayari kutoa sehemu yake.
Mwezi Oktoba, Ujerumani ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa kuhusu Syria, ambapo wajumbe waliahidi kuongeza msaada wa kifedha wa muda mrefu katika nchi kama vile Lebanon na Jordan, ambazo zinakabiliana na mamilioni ya wakimbizi wa Syria wanaoingia kwa kasi kwenye nchi hizo.
Kiasi watu 200,000 wamekufa na karibu nusu ya idadi ya wakaazi wa Syria hawana makaazi kutokana na mgogoro ulioanza kwa maandamano ya kuipinga serikali ya Rais Bashar al-Assad mwaka 2011 na kugeuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.




Chanzo: Deustche Welle (DW)












WASILIANA NAMI: 
Facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: venancegilbert

Comments

Popular posts from this blog

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

PREMIER: A POEM BY VENANCE GILBERT FOR CELEBRATING THE WORLD MOTHERS' DAY 2018

Venance Gilbert: A composer of this poem. Today is a very special day to all Mothers in the World. It is called World Mothers' Day . As one among the people who were raised by a mother, I found an interest in holding a pen and a piece of paper at least to write the few from the collection of what I did as I was growing up and my mother was there for me to make sure that I grow up wisely and intelligently. On March 28, 2017 I completed the long lasting composition of this poem. IT IS VERY SPECIAL FOR MY DEAR MAMA FLORENTINA AND ALL MOTHERS' IN THE WORLD. May be your mother has passed away (sorry for the loss) but due to spiritual faith, we believe that the resting mothers in heaven can hear our voices, so you can also recite the poem for your mom and she will hear you in one way or another. The poem is called Premier. I welcome you once again to this field of language use. I have hired a very simple language in composing this poem, it is very understood and straightforw...

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD  

RIHANNA - DIAMONDS SONG LYRICS

Shine bright like a diamond Shine bright like a diamond Find light in the beautiful sea, I choose to be happy You and I, you and I, we're like diamonds in the sky You're a shooting star I see, a vision of ecstasy When you hold me, I'm alive, we're like diamonds in the sky I knew that we'd become one right away Oh, right away At first sight I felt the energy of sun rays I saw the life inside your eyes So shine bright, tonight, you and I We're beautiful like diamonds in the sky Eye to eye, so alive We're beautiful like diamonds in the sky Shine bright like a diamond (whoa) Shine bright like a diamond (whoa) Shining bright like a diamond We're beautiful like diamonds in the sky Shine bright like a diamond (whoa) Shine bright like a diamond (whoa) Shining bright like a diamond We're beautiful like diamonds in the sky Palms rise to the universe as we moonshine and molly Feel the warmth, we'll never die, we're like diamonds in the sky You're a ...

TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA

Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz . Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika. Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya  HAPA  ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya  HAPA  ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa: 1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3) SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno ku...