AUDIO | DARASSA-HASARA ROHO | DOWNLOAD

MECHI YA ATLETICO & REAL MADRID KULINDWA NA POLISI 2,000

Polisi wa kukabiliana na fujo walikabiliana na mashabiki wa Bayern Munich mnamo 18 Aprili
Polisi wa kukabiliana na fujo walikabiliana na mashabiki wa Bayern Munich mnamo 18 Aprili
Walinzi zaidi ya 2,000 watatumiwa kudumisha usalama na kudhibiti mashabiki wakati wa mechi ya nusufainali ya mkondo wa kwanza kati ya Real Madrid na Atletico Madrid katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Mechi hiyo itakayochezewa Santiago Bernabeu siku ya Jumanne imeorodheshwa kama yenye "hatari kubwa" na usalama "utaimarishwa", maafisa wasimamizi wa jiji la Madrid walisema Ijumaa.

UEFA wameamrisha usalama katika mechi za klabu Ulaya uimarishwe baada ya shambulio kwenye basi la timu ya Borussia Dortmund mnamo 11 Aprili.

Atletico watakuwa na mashabiki 4,000 katika uwanja huo wa Real unaotoshea mashabiki 80,000.
Kawaida ni mashabiki wachache sana husafiri kuhudhuria mechi za ugenini Uhispania.

Idadi ya walinzi tarehe 2 Mei itakuwa ya juu zaidi ya waliokuwepo wakati wa mechi iliyopita ya Real Ulaya dhidi ya Bayern Munich polisi wa kukabiliana na fujo walipokabiliana na mashabiki wageni wakati wa mapumziko.

Kulikuwa pia na fujo mechi ya robofainali ya Atletico nyumbani, polisi wakikabiliana na mashabiki wa Leicester City.

Chanzo: BBC

WAFAHAMU MARAIS 10 WA AFRIKA WALIOFARIKI WAKIWA MADARAKANI

Leo nimekuandikia orodha ya marais 10 waliofariki wakiwa madarakani. Tuanze kuhesabu sasa:

Lansana Conté, President of Guinea 
10. Lansana Conte, Rais wa Guinea
Baada ya miaka 24 Lansana Conte alifariki na ugonjwa usiojulikana akiwa na umri wa miaka 74. Alipambana na matatizo ya kisukari na maradhi ya moyo. Kuanzia Aprili 1984 mpaka kifo chake Desemba 2008 alikuwa ni rais wa pili kushika madaraka nchini Guinea. Mbali na matatizo ya afya aliyokuwa nayo aliweza kushinda uchaguzi.


Flash - Galerie Verstorbene Persönlichkeiten 2009 Omar Bongo (AP) 

9. Omar Bongo, Rais wa Gabon

Saratani ya tumbo iliosambaa ndio iliyosababisha kifo cha Rais Omar Bongo June 2009 mjini Barcelona, Uhispania, baada ya kuwa rais kwa miaka 42 mfululizo. Alifariki akiwa na umri wa miaka 72 na pia alikuwa ni kiongozi aliyekaa madarakani kwa muda mrefu katika historia na alikuwa akiongoza katika mambo ya rushwa. Bongo alijikusanyia utajiri mkubwa huku akiiacha nchi yake katika hali ya umasikini. 


João Bernardo Vieira, President of Guinea-Bissau 

8. Joao Bernardo Vieira, Rais wa Guinea-Bissau

Joao Bernardo Vieira rais wa Guinea-Bissau aliuwawa nchi mwake Machi 2009, akiwa na umri wa miaka 69. Alikuwa kiongozi wa nchi kwa muda wa miaka 31. 1978 alikuwa waziri mkuu na kuchukua madaraka 1980 na alitawala kwa miaka 19. Alibadilika na kuwa kiongozi wa umma na aliongoza miaka minne mingine zaidi. 2005 alishinda tena uchaguzi wa uraisi. 


Umaru Musa Yar’Adua, President of Nigeria  

7. Umaru Musa Yar’Adua, Rais wa Nigeria

Umaru Musa Yar’Adua, alifariki akiwa na umri wa miaka 58 mwaka 2011 akisumbuliwa na matatizo ya moyo nchini Nigeria. Alikuwa madarakani kwa miaka mitatu pekee. Alikosekana katika kampeni za uchaguzi kwa sababu za kiafya. Baada ya kuchaguliwa kwake 2007, afya yake ilidhoofika kwa haraka. 


Muammar Gaddafi, Brotherly Leader and Guide to the Revolution of Libya  

6. Muammar Gadhafi, kiongozi na mwana mapinduzi wa Libya

Mwathirika wa mauaji, Muammar Gadhafi aliuawa akiwa na umri wa miaka 69 na vikosi vya waasi katika mazingira yasiyoeleweka nchini Libya, baada ya kuwa kiongozi wa taifa hilo kwa muda wa miaka 42. Aliuondoa uongozi wa kifalme bila ya kumwaga damu wakati wa mapinduzi ya kijeshi ya mwaka 1969 lakini utawala wake ulifikia kikomo baada ya matokeo ya vuguvugu la mapinduzi ya uarabuni. 


Malam Bacai Sanhá, President of Guinea Bissau 

5. Malam Bacai Sanha, Rais wa Guinea-Bissau

Kiongozi wa nne kufariki mwaka 2012 alikuwa ni Malam Bacai Sanha rais wa Guinea-Bissau. Aliugua ugonjwa wa kisukari na alifariki mjini Paris baada ya miaka minne kama rais akiwa na umri wa miaka 64. Katika kipindi chote cha utawala wake alisumbuliwa na matatizo kadhaa ya kiafya yalosababisha kwenda hospitali mara nyingi.

Bingu wa Mutharika, President of Malawi  

4. Bingu wa Mutharika, Rais wa Malawi

Rais mwingine aliyefariki mwaka 2012 ni Bingu wa Mutharika, rais wa Malawi. Alipata mshutuko wa moyo mwezi Aprili na kufariki siku mbili baadae akiwa na umri wa miaka 78. Uongozi wake ulikuwa ni wa miaka nane na alipata mafanikio makubwa katika sera zake za kilimo na chakula. Sifa yake iliharibika kufuatia maandamano makubwa yalopinga ununuzi wa ndege ya rais iliyogharimu Dola milioni 14


John Atta Mills, President of Ghana 

3. John Atta Mills, Rais wa Ghana

Pia mwaka 2012, John Atta Mills, rais wa Ghana alifariki akiwa nyumbani kwake kwa mshutuko wa moyo na saratani ya koo akiwa na umri wa miaka 68. Alishinda uchaguzi wa rais wa 2008 alishika madaraka kwa miaka mitatu pekee. Alianzisha mikakati mingi ya kiuchumi na mageuzi ya kiuchumi yalomletea sifa kutoka ndani na nje ya nchi. 

Meles Zenawi, Prime Minister of Ethiopia 

2. Meles Zenawi, Waziri Mkuu wa Ethiopia

Meles Zenawi alifariki Agosti 2012 nchini Ubelgiji akiwa na umri wa miaka 57 kwa maambukizi yasiyojulikana. Ameiongoza Ethiopia kwa miaka 5 kama rais kuanzia mwaka 1991 hadi 1995 na kama Waziri Mkuu kwa miaka 17 kuanzia 1995 hadi 2012. Anajulikana kwa kuanzisha mfumo wa siasa wa vyama vingi, lakini pia kwa ukandamizaji wa maandamano halali ya watu wa Oromia wa kaskazini mwa Ethiopia. 

Michael Sata, President of Zambia 

1. Michael Sata, Rais wa Zambia

Michael Sata ni kiongozi wa hivi karibuni aliyefariki madarakani akiwa na umri wa miaka 77 kwa maradhi ambayo hayakuwekwa wazi Oktoba 28 2014, nchini Uingereza. Baada ya uchaguzi wa 2011, uvumi juu ya afya yake ulisambaa nchini Zambia. Kukosekana kwake katika shughuli kubwa za kitaifa kuliibua wasiwasi wa afya yake ingawa msemaji wake alisema alikuwa katika afya nzuri.




Chanzo: DW Idhaa ya Kiswahili.

THE WHEEL A POEM BY VENANCE GILBERT

Venance on the sitting benches of Vikenge Hostels, Mzumbe University Main Campus Morogoro

Poet: Venance Gilbert
Poem: The Wheel
Composition: October 18, 2016
Publication: April 20, 2017
Copyright: Venance Gilbert  2016



The wheel was moving
But I never noticed
second counted, minutes gone,
hours died, days were numbered
weeks moved, months and years passed
I noticed it as the matter of living.

Mental pictures remind me
those days when the moments existed
Sometimes I wish to restore and start
I find the wheel moving fast following the line
Like the train on its pathway
Happy birthday takes back to those moments.

Today I am youth
Full capable to place the mind on motion
I often regret when I remember the moment
The moment when I was the driver of the wheel
But now the wheel drives, how possible?
I never drove it well and careful at the moment,
Drive the wheel careful before it drive you on its pathway.

DOWNLOAD JAY2 THE HUSTLER X CAST BEEZY-TIME IS NOW


Hii ni mpya kutoka kwa Jay2 th hustler & Cast beezy-Time is Now.

DOWNLOAD HARMONIZE & RICH MAVOKO-SHOW ME NEW SONG

Tokeo la picha la harmonize & mavoko show me 
Brand new track kutoka WCB. Harmonize & Rich Mavoko wametuletea hii, Show Me

DOWNLOAD

WANASAYANSI WAGUNDUA UHAI KATIKA SAYARI YA SATURN

Sayari ya Saturn
Sayari ya Sarateni "Saturn"

Mwezi wa Enceladus ambao uko kwenye sayari ya Saturn huenda ukawa mahali bora zaidi pa kwenda kutafuta maisha nje ya dunia.

Tathmini hii inatokea kufuatia uchunguzi katika sayari hiyo yenye kilomita 500 uliofanywa na Cassini.

Uchambuzi wa kemia wa Cassini unaonyesha matundu ya maji moto kwenye sakafu ya bahari ya Enceladus, maeneo ambayo yanahusishwa na kuwepo kwa maisha, hapa duniani.

Kuwepo kwa maji haya sio thibitisho kamili kwamba vitu vilivyo na uhai vinaishi katika mwezi huo mdogo lakini teknolojia zinaweza kutumika kupima maji hayo na kutoa ushahidi zaidi.

"Tuna uhakika kuwa kitu chenye uhai kinaweza kuishi kwenye bahari ya Enceladus lakini lazima tufanye utafiti zaidi," alisema mwanasayansi wa Cassini kutoka Taasisi ya Utafiti ya Southwest, San Antonio, Dkt. Hunter Waite.

"Iwapo hakuna maisha huko, ni sawa, lakini ikiwa maisha yapo itakuwa bora zaidi," alieleza BBC.
Bahari iliyopo kwenye Enceladus inakisiwa kuwa na kina kirefusana sana na yapo majimaji kwa sababu ya joto linalotokana na mvuto wa mara kwa mara kutoka kwenye sayari ya Saturn.

Cassini tayari amedhibitisha kwamba maji hayo yanashikana na sakafu ya bahari kutokana na aina ya chumvi na silika ambayo pia imeonekana katika mashimo.
 
Lakini wanachotaka kujua sana wanasayansi ni ikiwa maswala fulani yanayotendeka duniani pia yanaweza kufanyika katika Enceladus - kitu kinachoitwa serpentinisation, ambayo hutengeneza gesi ya hidrojeni.

"Kwa viumbe hai, hidrojeni huwa ni kama kama pipi - ni chakula wanachokienzi," alieleza Dkt Chris McKay, mwanabiolojia wa maswala ya anga wa shirika la Nasa.

"Ni nzuri sana kwa kuvipa nguvu, na inaweza kusaidia viumbe vidogo sana. Kupata hidrojeni itakuwa vizuri sana na itakuwa moja ya ushahidi utakaoonyesha uwezekano wa kuwepo na uhai."

Viumbe hai anavyozungumzia Dkt McKay vinaitwa methanojeni kwa sababu vinatengeneza gesi ya metheni vinapogusana na hidrojeni na gesi ya kaboni .

Nasa, ambayo inaongoza ujumbe wa Cassini , ilitakikana kufanya tangazo la hidrojeni miezi michache baada ya uchunguzi wa mwisho waroketi ya mwezini, Oktoba mwaka wa 2015.

Ziara ya Cassini sasa inakamilika . Baada ya kuizunguka Saturn kwa muda wa miaka 12, inaendelea kuishiwa na mafuta na sasa itawachiliwa kuingia kwenye anga ya dunia hiyo ya Saturn mwezi Septemba, kuhakikisha kuwa haiwezi kugongana na Enceladus na kusababisha kuchafuka kwake.


Chanzo: BBC

DOWNLOAD ACHA NIKAE KIMYA DOWNLOAD PLATNUMZ NEW SONG

Huu ni wimbo mpya kuhusu hali inayoendelea nchini hivi sasa. Diamond pia ameamua kuzungumza kwa namna yake.

WELCOME ON BOARD: A POEM BY VENANCE GILBERT


Poem: Welcome on Board
Date composed: January 3, 2017.
Copyright: Venance Gilbert.


If it would be changing
Possibly this might be like pressing next
Particularly on a DVD player
But this does not let us press
Welcome on board; you are now part of us.

If be it swotting
Feasibly this may be pacing another course
Chiefly at school, college or varsity
But this does not rest on on papers
Welcome on board; you are now part of us.

If it would be moving
Positively this would be rambling
Definitely to beings
But this does not hinge on our feet strength
Welcome on board; you are now part of us.

If be it breathing
Certainly this would be breathing in
Specifically in all the livings
But this does not need breathing structures
Welcome on board; you are now part of us.

We have now trodden on another numeral
Each of us has to go through nippy revolution
Or reasonably style headway
Never welcome him on board as part of us
Let us welcome him with fresh hallucinations
Welcome on board; you are now part of us.

KUTOKA OMBA OMBA MPAKA KUWA MWANDISHI NA MUUZAJI BORA WA RIWAYA

Jean-Marie Roughol 
Kwa takribani miongo 3 (miaka 30) , Jean-Marie Roughol aliishi maisha ya dhiki sana kama omba omba huko Arc de Triomphe, Paris Ufaransa. Ni miongoni mwa wamafamilia waliokuwa wakimiliki utajiri na maduka makubwa ya nguo na sehemu za starehe.

Wapo waliomdharau kama ilivyokawaida kwa omba omba yeyete, wapo waliomrushia sarafu walipokuwa wakitembea wapo waliompatia note nakadhalika lakini wapo pia ambao waliompa kipande cha kutembea tembea kwenye muvi zao.

Baada ya kukutana na aliyekuwa Waziri serikalini ambaye alimsidia kuchapisha kitabu kuhusu maisha ya dhiki aliyokuwa akiishi, maisha ya Roughol yamekuwa ni kile anchoita yeye "muujiza".

Matajiri walionunua kitabu chake ambacho kimeuza karinu nakala elfu 50 na kitabu cha tatu katikaa orodha ya vitabu vya Jamii ya Kifaransa, "French Society" muuzaji huyu (Roughol) kwa sasa anamiliki nyumba yake, anatafuta kazi lakini pia yupo katika maandalizia ya kuandaa kitabu ambaco kitakuwa ni muendelezo wa kitabu chake hicho cha sasa.


"Nimepewa nafasi katika maisha. Ni muujiza kwangu na sitamani tena kurudi mtaaniSitaki kuwakatisha tamaa watu walionisaidia nna kuwa na imani na mimi" Roughol alizungumza hayo katika mahojiano na The Observer. "sasa nakwenda kutafuta kazi hata kama ni kuosha vyombo mgahawani. Sasas ni zamu yangu kuwasaidia watu mtaani.Mtu yeyote anaweza kuwaona mtaani. Unaweza kua kiongozi na ukapoteza kazi, au ukawa katika janga la moto au ukawa na malipo kidogo ya uzeeni ambayo hata hayatoshi kukidhi maisha yako lakini bado upo hapo ulipo. Na wale wasiokuwa mtaani wanatakiwa kuwa na mshikamano kwa sababu inawezekana wakawa wao"

"Sihisi kama nimeona zaidi ya umaskini" George Orwell aliandika katika Down and Out in Paris zaidi ya miaka 80 iliyopita. 'Bado naweza kuchagua kitu kimoja ama viwili nilivyojifunza katika maisha ya dhiki, sitafikiri tena kua omba omba wote ni waongo ama kudhani uwa omba omba anaweza kutoka katika umasikini huo kwa kumpa kalamu. ama kushangazwa na mtu aliyeishiwa nguvu bila kufanya kazi au hata labda kujisogeza karibu na jeshi la Wokovu ama kufurshia chakula kizuri katika mgahawa nadhifu. Huu ni mwanzo"

"Sikuwahi kufikiria kama maisha yangu yangekuwa ya kuomba omba katika mitaa ya Paris ili niweze kuishi" Roughol anaandika "sikuwahi kufikiri pia kama nitakuja ulala mitaani usiku... hakika ninawajibka kwa yaliyotokea katika maisha yangu, lakini maisha yangu hayakuanza vizuri: huu sio utani: ni kweli"

Roughol alizaliwa mwaka 1968, mama yake alimtelekeza na baba yake alimtuma akatafute wazazi kokote kule nchini Ufaransa. Akiwa kwenye treni aliandika "Nilikuwa na furaha, nilishawishiwa nitawaona tembo. Nilikuwa nikiangalia nje ya dirisha kuwaona tembo hao".

Mama yake wa hiari alikuwa mkali sana, alikuwa akimpa vyakula vilivyooza na maji ambayo si safi na salama na pia alikuwa akimfungia kwenye sehemu kama banda. Anasema, "hakukuwa na chochote, hakukuwa na upendo, nakukuwa na chakula; watu hawa walilipwa kwa kulea watoto hivyo mimi nilikuwa kipato kwao"

Anakumbuka pia jinsi alivyowahi kulala na panya waliokuwa na ukubwa sawa na paka.

Maisha yake yalianza kubadilika alipoamua kuchunga baiskeli ya Jean-Louis Debre, 72, aliyewahi kuwa Waziri katika serikali ya Ufaransa baada ya hapo Waziri huyo alimshawishi Roughol kuandika kuhusu maisha yake.

"Nilimwambia mengine hayana umuhimu na nilitaka kujua kuhusu maisha yake, kwa nini alikuwa omba omba" Debre anaeleza katika Dibaji ya kitabu. "ni kwa nini watu mashuhuri tu, au wale wanaotaka kuwa wanasiasa, nyota wa TV, radio, sinema wanaruhusiwa kuelezea maisha yao ya awali? Je wale wasiofahamika hawana chochote cha kusema kuhusu maisha yao ya awali? Roughol amenifundisha zaidi ya kile nilichomfanyia."

Kitabu hicho "Je tape la manche" (I’m begging) kilichapishwa mwaka juzi 2015 lakini hakikuwa maarufu sana hadi kufikia miezi kadhaa alipopokea cheki kutoka kwa wasambazaji wa kitabu chake hicho, cheki hiyo ilimruhusu Roughol kuanza maisha mapya.




Jean-Louis Debré with Jean-Marie Roughol
Roughol (kulia) na aliyemsaidia Debre (kushoto) aliyewahi kuwa Waziri katika serikali ya Ufaransa.


Leo, Roughol anamheshimu sana Debre kama mkombozi wa maisha yake. "miaka miwili iliyopita, sikuweza kufikiri kuwa hapa nilipo sasa. Jean-Louis ni baba ambaye sikutarajia kwa naye. Bado yuko pamoja nami na hajaniacha. Anasema maisha yangu yameanza kuimarika na sasa nina jukumu la kuhakikisha naendelea kutembea mwenyewe. Yuko sahihi" anasema Ruoughol.




MAKALA HII IMETAFSIRIWA KUTOKA THE GUARDIAN.


UNGANA NA VENANCE BLOG MITANDAONI
Facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venancegilbert
email: venancegilbert@gmail.com & venanceblog@gmail.com

FAHAMU WATU AU MAMBO YALIYOTAFUTWA SANA GOOGLE MWAKA 2016


Kila mwisho wa mwaka Mtandao wa Google hutoa orodha ya yale yaliyotafutwa kupitia mtandao huo. Tutaangalia katika nyanja za kiujumla, habari za dunia, watu, bidhaa za kiteknolojia, habari za michezo duniani, vifo, muvi/sinema, wasanii na vipindi vya runinga. Katika kila nyanja tutaangalia mambo au watu 10. Tuanze kuangalia trends hizo:

KIUJUMLA 

1. Pokeman Go
2. iPhone 7
3. Donald Trump
4. Prince
5. Powerball
6. David Bowie
7. Deadpool
8. Olympics
9. Slither.io
10. Sucide Squad


HABARI ZA DUNIA

1. Uchaguzi wa Marekani (US Election)
2. Olympics
3. Brexit
4. Mauaji ya Orlando (Orlando Shooting)
5. Virusi vya Zika
6. Panama Papers
7. Nice
8. Brussels
9. Mauaji ya Dallas (Dallas Shooting)
10. Tetemeko la ardhi Kumamoto (Kumamoto Earthquake)

WATU

1. Donald Trump
2. Hillary Clinton
3. Michael Phelps
4. Melania Trump
5. Simone Biles
6. Bernie Sanders
7. Steven Avery
8. Celine Dion
9. Ryan Lochte
10. Tom Hiddleston


BIDHAA

1. iPhone 7
2. Freedom 251
3. iPhone SE
4. iPhone 6S
5. Google Pixel
6. Samsung Galaxy S7
7. iPhone 7 Plus
8. Note 7
9. Nintendo Switch
10. Samsung J7

HABARI ZA MICHEZO KIDUNIA

1. Rio Olympics
2. World Series
3. Tour de France
4. Wimbledon
5. Australian Open
6. EK 2016
7. T20 World Cup
8. Copa América
9. Royal Rumble
10. Ryder Cup


VIFO

1. Prince
2. David Bowie
3. Christina Grimmie
4. Alan Rickman
5. Muhammad Ali
6. Leonard Cohen
7. Juan Gabriel
8. Kimbo Slice
9. Gene Wilder
10. José Fernández 
 

MUVI

1. Deadpool
2. Suicide Squad
3. The Revenant
4. Captain America Civil War
5. Batman v Superman
6. Doctor Strange
7. Finding Dory
8. Zootopia
9' The Conjuring 2
10. Hacksaw Ridge 
 

WANAMUZIKI


1. Céline Dion
 

VIPINDI VYA RUNINGA 

 

1. Stranger Things
2. Westworld
3. Luke Cage
4. Game of Thrones
5. Black Mirror
6. Fuller House
7. The Crown
8. The Night Of
9. Descendants of the Sun
10. Soy Luna 
 
 
 

TAARIFA HII IMEANDALIWA KWA MSAADA KUTOKA GOOGLE.

Sogea karibu na VENANCE BLOG  kwenye mitandao ya kijamii
facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venancegilbert
Barua pepe (e-mails): venancegilbert@gmail.com & venanceblog@gmail.com

KUELEKEA MWISHONI 2016 LADY JAY DEE KAYAANDIKA HAYA INSTAGRAM



Kuelekea mwisho wa mwaka 2016 msanii mkongwe Lady Jay Dee ameyaandika haya katika mtandao wa Instagram:

"Kiukweli comeback yangu ya 2016 ilikuwa kubwa sana kuliko watu wengi walivyoitegemea mbali na changamoto ngumu na nyingi nilizowahi kupitia na ninazoendelea kuzipitia kuliko msanii yeyote yule wa kike wala wa kiume Tanzania nadiriki kusema bado nimesimama Imara *Kejeli *Dhihaka *Mabezo *Kutengwa *Story za kusingiziwa ikiwemo kuambiwa nyumba yangu inauzwa sijui inapigwa mnada na mengine yote mnayoyajua ni vitu vinavyovunja moyo sana. Ila Wa Tanzania ninawaheshimu sana linapokuja swala la kupigania kitu mnachokipenda. Hivi bila nyie si ningekuwa marehemu??? Bila fans JayDee ni nani??? Ninawashukuru kwa kuniamsha. Ninawashukuru kwa kuniamini. Ninawashukuru kwa kunipa nguvu na jeuri. Kuanzia Ndindindi mpaka Together *Mliijaza Mlimani City *Mkajaza mikoa niliyopita. Nawaomba muendelee kujaa 2017. Ili kuwadhihirishia wanadamu kuwa Mungu huwa ni mmoja tu. Happy new year to my fans all around the world. Nawapenda hata nikinuna. Kaeni tayari kwa album ya WOMAN 2017."

Hiyo ilikuwa ni sehemu ya kwanza, aliyoiandika jana na hii hapa chini ni sehemu ya pili:

"Kama nilivyoeleza hapo awali mwaka 2015 vitu vingi  vilisimama ili nijpange upya. Na 2016 vitu vingi vilianza kurudi Ikiwemo kuendelea kuperform na Band yangu THE BAND ambayo niliondoa jina la MACHOZI BAND na tulizunguka sehemu nyingi nchini. Mwaka 2017 nitarudisha kitu kingine ambacho kimekuwa kikiulizwa na watu wengi sana kutokana na kutokuwepo hewani kwa takribani mwaka na nusu. DIARY YA LADY JAYDEE Itarudi tena kwa mfumo na muonekano wa tofauti na wa mwanzo ukizingatia maisha yangu pia yamebadilika Hivyo naomba sponsor kujitokeza kwa wingi pia kwani mambo yakuwa ni moto sana. Itakuwa ni kuhusu misha yangu binafsi ya kimuziki, kibiashara, mapenzi na kila kinachonizunguka. Kaeni tayari kwa Msimu mpya wa Diary ya Lady JayDee yenye production bora zaidi ya jana. Diary ya Lady JayDee pia itapatikana kwenye YouTube channel yangu fanya kusubscribe"

Hii ni sehemu ya pili aliyoiandika katika mtandao wa Instagram. Kama kuna lolote usikose kutembelea VENANCE BLOG kwa mengine zaidi. Jay Dee anapatikana Instagram @jidejaydee





 Unaweza kulike VENANCE BLOG facebook kwa kubofya HAPA
Nifolo kwenye Twitter @Venancetz au bofya HAPA
Nipo Instagram pia @venancegilbert au bofya HAPA

TATHIMINI KWA UFUPI CHELSEA vs EVERTON KABLA YA MECHI SAA 2:30 EAT

Timu hizi mbili zimekutana katika michezo 49 ambapo Chelsea imeshinda mechi 22 na Everton imeshinda mechi 10 na kudroo mechi 17. Chelsea imeshinda nyumbani mechi 13 wakati Everton imeshinda mechi 9. Nje, Chelsea imeshinda mechi 9 wakati Everton imeshinda 2.

Katika mechi 3 zilizopita Chelsea ilifungwa na Everton magoli 2 kwa nunge, hii ilikuwa mechi ya Machi 12, 2016. Lakini pia mechi ya Januari 16, 2016 timu hizi zilitoka sare ya magoli 3. Na ile ya Septemba 12, 2015 Chelsea alipigwa magoli 3 kwa 1.

Katika msomu huu Chelsea ipo katika nafasi ya 4 wakati Everton ipo nafasi ya 6 kwenye msimamo wa Ligi. Chelsea imeshinda 70% ya mechi ilizocheza huku Everton ikishinda 50%. Mechi za nyumbani Chelsea ina asilimia 80% dhidi ya mpinzani wake Everton 50% huku mechi zilizopigwa nje Chelsea ana 60% na Everton 40%. Chelsea ina wastani wa 2.1 katika magoli iloshinda wakati Everton ana wastani wa 1.5 Lakini pia Chelsea imefungwa wastani wa 0.9 wakati Everton ina 0.8.