Skip to main content

KUTOKA OMBA OMBA MPAKA KUWA MWANDISHI NA MUUZAJI BORA WA RIWAYA

Jean-Marie Roughol 
Kwa takribani miongo 3 (miaka 30) , Jean-Marie Roughol aliishi maisha ya dhiki sana kama omba omba huko Arc de Triomphe, Paris Ufaransa. Ni miongoni mwa wamafamilia waliokuwa wakimiliki utajiri na maduka makubwa ya nguo na sehemu za starehe.

Wapo waliomdharau kama ilivyokawaida kwa omba omba yeyete, wapo waliomrushia sarafu walipokuwa wakitembea wapo waliompatia note nakadhalika lakini wapo pia ambao waliompa kipande cha kutembea tembea kwenye muvi zao.

Baada ya kukutana na aliyekuwa Waziri serikalini ambaye alimsidia kuchapisha kitabu kuhusu maisha ya dhiki aliyokuwa akiishi, maisha ya Roughol yamekuwa ni kile anchoita yeye "muujiza".

Matajiri walionunua kitabu chake ambacho kimeuza karinu nakala elfu 50 na kitabu cha tatu katikaa orodha ya vitabu vya Jamii ya Kifaransa, "French Society" muuzaji huyu (Roughol) kwa sasa anamiliki nyumba yake, anatafuta kazi lakini pia yupo katika maandalizia ya kuandaa kitabu ambaco kitakuwa ni muendelezo wa kitabu chake hicho cha sasa.


"Nimepewa nafasi katika maisha. Ni muujiza kwangu na sitamani tena kurudi mtaaniSitaki kuwakatisha tamaa watu walionisaidia nna kuwa na imani na mimi" Roughol alizungumza hayo katika mahojiano na The Observer. "sasa nakwenda kutafuta kazi hata kama ni kuosha vyombo mgahawani. Sasas ni zamu yangu kuwasaidia watu mtaani.Mtu yeyote anaweza kuwaona mtaani. Unaweza kua kiongozi na ukapoteza kazi, au ukawa katika janga la moto au ukawa na malipo kidogo ya uzeeni ambayo hata hayatoshi kukidhi maisha yako lakini bado upo hapo ulipo. Na wale wasiokuwa mtaani wanatakiwa kuwa na mshikamano kwa sababu inawezekana wakawa wao"

"Sihisi kama nimeona zaidi ya umaskini" George Orwell aliandika katika Down and Out in Paris zaidi ya miaka 80 iliyopita. 'Bado naweza kuchagua kitu kimoja ama viwili nilivyojifunza katika maisha ya dhiki, sitafikiri tena kua omba omba wote ni waongo ama kudhani uwa omba omba anaweza kutoka katika umasikini huo kwa kumpa kalamu. ama kushangazwa na mtu aliyeishiwa nguvu bila kufanya kazi au hata labda kujisogeza karibu na jeshi la Wokovu ama kufurshia chakula kizuri katika mgahawa nadhifu. Huu ni mwanzo"

"Sikuwahi kufikiria kama maisha yangu yangekuwa ya kuomba omba katika mitaa ya Paris ili niweze kuishi" Roughol anaandika "sikuwahi kufikiri pia kama nitakuja ulala mitaani usiku... hakika ninawajibka kwa yaliyotokea katika maisha yangu, lakini maisha yangu hayakuanza vizuri: huu sio utani: ni kweli"

Roughol alizaliwa mwaka 1968, mama yake alimtelekeza na baba yake alimtuma akatafute wazazi kokote kule nchini Ufaransa. Akiwa kwenye treni aliandika "Nilikuwa na furaha, nilishawishiwa nitawaona tembo. Nilikuwa nikiangalia nje ya dirisha kuwaona tembo hao".

Mama yake wa hiari alikuwa mkali sana, alikuwa akimpa vyakula vilivyooza na maji ambayo si safi na salama na pia alikuwa akimfungia kwenye sehemu kama banda. Anasema, "hakukuwa na chochote, hakukuwa na upendo, nakukuwa na chakula; watu hawa walilipwa kwa kulea watoto hivyo mimi nilikuwa kipato kwao"

Anakumbuka pia jinsi alivyowahi kulala na panya waliokuwa na ukubwa sawa na paka.

Maisha yake yalianza kubadilika alipoamua kuchunga baiskeli ya Jean-Louis Debre, 72, aliyewahi kuwa Waziri katika serikali ya Ufaransa baada ya hapo Waziri huyo alimshawishi Roughol kuandika kuhusu maisha yake.

"Nilimwambia mengine hayana umuhimu na nilitaka kujua kuhusu maisha yake, kwa nini alikuwa omba omba" Debre anaeleza katika Dibaji ya kitabu. "ni kwa nini watu mashuhuri tu, au wale wanaotaka kuwa wanasiasa, nyota wa TV, radio, sinema wanaruhusiwa kuelezea maisha yao ya awali? Je wale wasiofahamika hawana chochote cha kusema kuhusu maisha yao ya awali? Roughol amenifundisha zaidi ya kile nilichomfanyia."

Kitabu hicho "Je tape la manche" (I’m begging) kilichapishwa mwaka juzi 2015 lakini hakikuwa maarufu sana hadi kufikia miezi kadhaa alipopokea cheki kutoka kwa wasambazaji wa kitabu chake hicho, cheki hiyo ilimruhusu Roughol kuanza maisha mapya.




Jean-Louis Debré with Jean-Marie Roughol
Roughol (kulia) na aliyemsaidia Debre (kushoto) aliyewahi kuwa Waziri katika serikali ya Ufaransa.


Leo, Roughol anamheshimu sana Debre kama mkombozi wa maisha yake. "miaka miwili iliyopita, sikuweza kufikiri kuwa hapa nilipo sasa. Jean-Louis ni baba ambaye sikutarajia kwa naye. Bado yuko pamoja nami na hajaniacha. Anasema maisha yangu yameanza kuimarika na sasa nina jukumu la kuhakikisha naendelea kutembea mwenyewe. Yuko sahihi" anasema Ruoughol.




MAKALA HII IMETAFSIRIWA KUTOKA THE GUARDIAN.


UNGANA NA VENANCE BLOG MITANDAONI
Facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venancegilbert
email: venancegilbert@gmail.com & venanceblog@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

10. YUSUF MANJI Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini. 9. FIDA RASHID Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine. 8. GHALIB SAID MOHAMMED Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

MFAHAMU KARL MARX KWA UFUPI: DUNIA INAMKUMBUKA LEO

Karl Mark alikuwa ni mwanafalsafa na mwanamapinduzi wa Ujerumani aliyeandika vitabu vya The Communist Manifesto na  Das Capital vitabu ambavyo vilikuwa vikipingana na mfumo wa kibepari na kuunda mfumo wa Ukomunisti ama Ujamaa kama alivyoutafsiri hayati Mwalimu JK Nyerere. Karl Marx alizaliwa Mei 5, 1818. Alianza kuchunguza nadharia za kijamii alipokuwa Chuo Kikuu na wenzie waliounda kikundi chao kilichoitwa Young Hegelians. Hiki kilikuwa ni kikundi kilichokuwa kinaamini katika falsafa za mwalimu wao aliyeitwa Hegel. Marx alikuwa mwandishi wa habari na machapisho yake kuhusu Ukomunisti vilipelekea yeye kufukuzwa Ujerumani na Ufaransa. Mwaka 1848 alichapisha kitabu chake cha The Communist Manifesto akiwa na Friedrich Engels ambacho kilipelekea kufukuzwa Ujerumani na kukimbilia London, Uingereza, huko pia aliandika kitabu cha Das Kapital ambako ndiko alikoishi mpaka alipoiaga dunia. Karl Marx alikuwa ni miongoni mwa watoto 9 wa Heinrich Marx na Henrietta Marx huko Tr...

HEZBOLLAH YATAJA SABABU YA KUUAWA KIONGOZI WAO

 Kundi la Waislamu wa madhehebu ya Kishia la Hezbollah nchini Lebanon limetaja sababu ya kifo cha kiongozi wake wa ngazi ya juu wa kijeshi, Mustafa Badreddine kuwa kimetokana na makombora ya mizinga liliofanyika karibu na uwanja wa ndege wa Damascus nchini Syria.  Hezbollah lilitangaza  kifo cha Badreddine hapo jana na alifanyiwa mazishi ya kijeshi siku hiyo hiyo katika eneo la ngome la kundi hilo huko kusini mwa Beirut. Taarifa ya kundi hilo imesema mashambulizi hayo yamefanywa na kundi linaloitwa Takfiri. Takfiri ni neno linalotumiwa na kundi hilo la Kisunni kwa kuonesha msimamo mkali, kundi lenye kujihami na silaha, lililo na itikadi kali. Badreddine alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa kundi la Hezbollah walioshutumiwa mwaka 2005 kuhusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanon Rafik Hariri. Chanzo: Deutsche Welle (DW)