Skip to main content

KUTOKA OMBA OMBA MPAKA KUWA MWANDISHI NA MUUZAJI BORA WA RIWAYA

Jean-Marie Roughol 
Kwa takribani miongo 3 (miaka 30) , Jean-Marie Roughol aliishi maisha ya dhiki sana kama omba omba huko Arc de Triomphe, Paris Ufaransa. Ni miongoni mwa wamafamilia waliokuwa wakimiliki utajiri na maduka makubwa ya nguo na sehemu za starehe.

Wapo waliomdharau kama ilivyokawaida kwa omba omba yeyete, wapo waliomrushia sarafu walipokuwa wakitembea wapo waliompatia note nakadhalika lakini wapo pia ambao waliompa kipande cha kutembea tembea kwenye muvi zao.

Baada ya kukutana na aliyekuwa Waziri serikalini ambaye alimsidia kuchapisha kitabu kuhusu maisha ya dhiki aliyokuwa akiishi, maisha ya Roughol yamekuwa ni kile anchoita yeye "muujiza".

Matajiri walionunua kitabu chake ambacho kimeuza karinu nakala elfu 50 na kitabu cha tatu katikaa orodha ya vitabu vya Jamii ya Kifaransa, "French Society" muuzaji huyu (Roughol) kwa sasa anamiliki nyumba yake, anatafuta kazi lakini pia yupo katika maandalizia ya kuandaa kitabu ambaco kitakuwa ni muendelezo wa kitabu chake hicho cha sasa.


"Nimepewa nafasi katika maisha. Ni muujiza kwangu na sitamani tena kurudi mtaaniSitaki kuwakatisha tamaa watu walionisaidia nna kuwa na imani na mimi" Roughol alizungumza hayo katika mahojiano na The Observer. "sasa nakwenda kutafuta kazi hata kama ni kuosha vyombo mgahawani. Sasas ni zamu yangu kuwasaidia watu mtaani.Mtu yeyote anaweza kuwaona mtaani. Unaweza kua kiongozi na ukapoteza kazi, au ukawa katika janga la moto au ukawa na malipo kidogo ya uzeeni ambayo hata hayatoshi kukidhi maisha yako lakini bado upo hapo ulipo. Na wale wasiokuwa mtaani wanatakiwa kuwa na mshikamano kwa sababu inawezekana wakawa wao"

"Sihisi kama nimeona zaidi ya umaskini" George Orwell aliandika katika Down and Out in Paris zaidi ya miaka 80 iliyopita. 'Bado naweza kuchagua kitu kimoja ama viwili nilivyojifunza katika maisha ya dhiki, sitafikiri tena kua omba omba wote ni waongo ama kudhani uwa omba omba anaweza kutoka katika umasikini huo kwa kumpa kalamu. ama kushangazwa na mtu aliyeishiwa nguvu bila kufanya kazi au hata labda kujisogeza karibu na jeshi la Wokovu ama kufurshia chakula kizuri katika mgahawa nadhifu. Huu ni mwanzo"

"Sikuwahi kufikiria kama maisha yangu yangekuwa ya kuomba omba katika mitaa ya Paris ili niweze kuishi" Roughol anaandika "sikuwahi kufikiri pia kama nitakuja ulala mitaani usiku... hakika ninawajibka kwa yaliyotokea katika maisha yangu, lakini maisha yangu hayakuanza vizuri: huu sio utani: ni kweli"

Roughol alizaliwa mwaka 1968, mama yake alimtelekeza na baba yake alimtuma akatafute wazazi kokote kule nchini Ufaransa. Akiwa kwenye treni aliandika "Nilikuwa na furaha, nilishawishiwa nitawaona tembo. Nilikuwa nikiangalia nje ya dirisha kuwaona tembo hao".

Mama yake wa hiari alikuwa mkali sana, alikuwa akimpa vyakula vilivyooza na maji ambayo si safi na salama na pia alikuwa akimfungia kwenye sehemu kama banda. Anasema, "hakukuwa na chochote, hakukuwa na upendo, nakukuwa na chakula; watu hawa walilipwa kwa kulea watoto hivyo mimi nilikuwa kipato kwao"

Anakumbuka pia jinsi alivyowahi kulala na panya waliokuwa na ukubwa sawa na paka.

Maisha yake yalianza kubadilika alipoamua kuchunga baiskeli ya Jean-Louis Debre, 72, aliyewahi kuwa Waziri katika serikali ya Ufaransa baada ya hapo Waziri huyo alimshawishi Roughol kuandika kuhusu maisha yake.

"Nilimwambia mengine hayana umuhimu na nilitaka kujua kuhusu maisha yake, kwa nini alikuwa omba omba" Debre anaeleza katika Dibaji ya kitabu. "ni kwa nini watu mashuhuri tu, au wale wanaotaka kuwa wanasiasa, nyota wa TV, radio, sinema wanaruhusiwa kuelezea maisha yao ya awali? Je wale wasiofahamika hawana chochote cha kusema kuhusu maisha yao ya awali? Roughol amenifundisha zaidi ya kile nilichomfanyia."

Kitabu hicho "Je tape la manche" (I’m begging) kilichapishwa mwaka juzi 2015 lakini hakikuwa maarufu sana hadi kufikia miezi kadhaa alipopokea cheki kutoka kwa wasambazaji wa kitabu chake hicho, cheki hiyo ilimruhusu Roughol kuanza maisha mapya.




Jean-Louis Debré with Jean-Marie Roughol
Roughol (kulia) na aliyemsaidia Debre (kushoto) aliyewahi kuwa Waziri katika serikali ya Ufaransa.


Leo, Roughol anamheshimu sana Debre kama mkombozi wa maisha yake. "miaka miwili iliyopita, sikuweza kufikiri kuwa hapa nilipo sasa. Jean-Louis ni baba ambaye sikutarajia kwa naye. Bado yuko pamoja nami na hajaniacha. Anasema maisha yangu yameanza kuimarika na sasa nina jukumu la kuhakikisha naendelea kutembea mwenyewe. Yuko sahihi" anasema Ruoughol.




MAKALA HII IMETAFSIRIWA KUTOKA THE GUARDIAN.


UNGANA NA VENANCE BLOG MITANDAONI
Facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venancegilbert
email: venancegilbert@gmail.com & venanceblog@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

MAANDALIZI MEMA YA SIKUKUU YA KRISMAS

Kwanza namshukuru Mungu toka tukiwa wadogo mpaka sasa anaendelea kutulinda. Uongozi mzima wa Venance Blog tunawatakieni maandalizi mema ya Krismas hapo kesho, wale wa kanisani tukafurahi kwani bwana atazaliwa. Msali salama katika misa za mkesha kubwa zaidi kudumisha amani na usalama kuanzia leo mpaka sikuku itakapoisha. MAANDALIZI MEMA YA KRISMAS!!!

AJALI: BASI LAUA WATU 12 PAPO HAPO

Watu 12 wamekufa papo hapo na wengine zaidi ya 90 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Korogwe, Tanga kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka. Ajali hiyo ilitokea jana saa 1.30 asubuhi kwenye barabara kuu ya Segera-Chalinze katika kijiji cha Kwalaguru kata ya Kwedizinga wilayani hapa. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alithibitisha jana kutokea kwa ajali hiyo ya basi la Burudani namba T 610 ATR aina ya Nissan. Majeruhi walipelekwa katika hospitali ya wilaya ya Korogwe ya Magunga, kwa matibabu ya awali na miili ya marehemu, akiwamo dereva wa gari hilo, Luta Mpenda (35) imehifadhiwa hospitalini hapo.  “Tukiwa tunakaribia kwenye kona ile, tulipishana na lori hilo likiwa kasi upande wetu, dereva wetu akajitahidi kulikwepa lakini kutokana na ile kona kuwa kali, gari lilimshinda na kupinduka,” alisema Bendera. Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo walisema walisikia kishindo kutoka eneo hilo wakaenda na kukuta gari limepinduka na baadh...

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

Leo nakufahamisha baadhi ya mambo ambayo huenda hukuyafahamu ama ulichukulia kawaida tu. Mambo hayo ni hapahapa Tanzania.  Tanzania ina eneo la kilomita za mraba 945,087. Ina jumla mikoa 31 kote bara na visiwani. Mpaka kufikia mwaka 2017 idadi ya watu nchini ilikadiriwa kuwa milioni 52.554 kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya takwimu. Twende sasa tuanze kuhesabu moja baada ya jingine #1 . Wimbo wa taifa "Mungu Ibariki Tanzania"  ni wimbo unaofanana na nyimbo za mataifa ya Afrika Kusini na Zambia. Wimbo huu ulitungwa na Enock Sontonga kwa lugha ya Xhosa "Nkosi Sikelel iAfrika" . Wimbo huu pia uliwahi kutumiwa na nchi za Zimbabwe na Namibia. Enock Sontonga mtunzi wa wimbo Mungu Ibariki Afrika #2. Ni Tanzania pakee ambako kunapatikana Simba wenye uwezo wa kupanda juu ya miti. Simba hawa wanapatikana katika hifadhi ya taifa ya Ziwa Manyara. Simba wenye uwezo wa kupanda miti hifadhi ya Ziwa Manyara. #3. Tanzania ni nchi ambako fuvu la mtu wa kale z...

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: FIFA IMESEMA ITAZIPA DOLA MILIONI 2 NCHI ZA AFRIKA ZINAZOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA

FIFA itatoa zawadi ya dola milioni mbili kwa kila mojawapo ya timu tano za Afrika zilizofuzu kucheza kombe la dunia kuzisaidia katika maandalizi, amesema rais wa shirikisho la kandanda barani Afrika CAF. Misri, Morocco, Nigeria, Senegal na Tunisia, zimefuzu kushiriki katika michuano ya kombe la dunia itakayofanyika nchini Urusi, na rais wa shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF, Ahmad Ahmad, alismea katika taarifa kwamba fedha hizo zitatumika "kushughulikia mapema, suala la bonasi za wachezaji." "Migogoro juu ya malipo katika michuano iliyopita ilipelekea kuwepo na hali zilizoathiri vibaya taswira ya soka barani Afrika, ikiwa ni pamoja na kuathiri kwa kiwango kikubwa utendaji wa timu viwanjani," aliongeza. Mwaka uliopita, shirikisho la kandanda la Nigeria (NFF) lilisaini makubaliano na wachezaji wake wakiahidi kujiepusha na migogoro ya bonasi na malipo ambayo imeharibu kampeni zao za nyuma za kombe la dunia. Wachezaji wa timu ya Nigeria, Sup...