Skip to main content

RAIS MAGUFULI AAHIDI KUENDELEA KUTOA MIKOPO 2016/2017 KWA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU NA KUTOA RAI SUALA HILO KUSHUGHULIKIWA

Tokeo la picha la magufuli udsm leo oktoba 21

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo kwa nafsi yake ametoa matumaini kwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali nchini kuhusu hatima yao ya mkopo wa Elimu ya Juu alipokuwa akihudhuria sherehe ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Rais Magufuli amebainisha haya, namnukuu;

"Tunapopitia katika challenge hii muivumilie serikali kutengeneza utaratibu ulio mzuri, ninafahamu, katika bajeti ya mwaka 2015/2016, fedha iliyotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa sababu Mh. Waziri umezungumza hapa zilikuwa bilioni 340 ambazo  zilikjuwa zinatosha karibu wanafunzi tisini elfu (90,000)  baada ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani  ili kutimiza yale tuliyokuwa tumeahidi tuliongeza fedha hizo za mkopo hadi kfikia bilioni 473 bajeti ilikuwa ya bilioni 340 tukaongeza zikafika bilioni 473 kutokana na makusanyo na tukaweza kutoa mikopo kwa wanafunzi 124,358 mwaka huu ameeleza ni zaidi ya bilioni 483 zimepitishwa katika bajeti  kwa hiyo wanafunzi wengi zaidi watapata mkopo ninafahamu kwa mfano wanafunzi wanaoendelea ambao wako karibu 93,000 wote wamekuwa accommodated kwenye mkopo pamoja na wanafunzi wapya ambao nafikiri ni zaidi ya 25,000 lakini ni lazima kweli nikiri hapakuwepo na coordination palitakiwa kwanza vyuo vyote vya elinu ya juu viwe na tarehe moja ya kufungua kwa sababu wapo wengine walifungua mwezi mzima uliopita wako wengine wamefungua jana wako wengine watafungua keshokutwa ukishafungua haraka haraka wanafunzi wakakaa pale kwa mwezi mmoja halafu unawambia kufanya registration lazima walipe wakati Bodi ya Mikopo haijatoa orodha ya majina ya vijana ambao watakaokopeshwa ni contradiction.

Palikuwa pawepo na communication kati ya Bodi ya Mikopo sijui ni TCUsijui ni nani, Wizara ya Elimu na Wizara ya Fedha kwamba katika orodha ya wanafunzi watakaopata mikopo ni hawa hapa majina yao ni haya hapa mnapeleka majina hayo na orodha, amount ya fedha zinazotakiwa Wizara ya Fedha, Wizara ya Fedha nao wanaprocess zao fedha hizi tunazitoa baadaye zikishapelekwa kwenye benki kwenye hizo akaunti za wanafunzi, mngeweza mkafungua vyuo hapakuwa na sababu ya kufungua mwezi mzima kabla wanafunzi wanakaa pale hajui kama atapata mkopo au hatapata mkopo halafu unamwambia hakuna registration  kwa sababu hujapata mkopo inaleta usumbufu wa ajabu, na hilo.

Nitoe wito kwa Wizara ya Elimu na hili nasema kwa dhati lengo la serikali si kuleta usumbufu kwa wanfunzi  lakini ni ukweli pia kwamba haitatoa mikopo kwa wanafunzi ambao wenye uwezo unamkuta mtoto wa Profesa Rwekaza na wewe upate mkopo mtoto wa Ndalichako naye apate mkopo mtoto wa Katibu Mkuu Kijazi naye apate mkopo haiwezekani mkopo huu umelenga kwa ajili ya kutoa watoto masikini lakini nafahamu na ninasikia hata katika Bodi ya Mikopo kule kuna upendeleo upendeleo wa aina fulani katika kutoa mkopo hata ambao hawastahili wanapewa mikopo na ambao hawastahili wananyimwa mkopo sasa hili Waziri na Bodi zinazohusika mulisimamie sitaki siku moja nije huko kwenye Bodi ya mikopo nichukue orodha ya wanafunzi wote niangalie shule walizosoma na particulars walizozijaza halafu nije nipewe majina ya watu ambao hawakustahili kupewa mkopo wanafunzi 25 wa mwaka huu siwezi kushindwa kusoma kwa siku 1 ntapekua page by page 25,000 ukigawa kwa masaa 12 ambayo naweza nikajifungia kila jina naweza nikalisoma kwa sekunde ngapi ninajua naweza, sasa tusifikie huko.

Ninashukuru Waziri baada ya kuona hii changamoto ukawa umelileta hili suala haraka haraka na tukatoa instruction Wizara ya Fedha watoe bilioni 80 za mwanzo haraka haraka na nimeambiwa zimeshatolewa, sasa niwaombe wanafunzi msiwe na haraka haraka kwa sababu katika changamoto hizi ambazo zinapita ndani ya serikali wanafunzi hewa, mikopo hewa, mishahara hewa hatutaki hela yetu ipotee ovyo pameshatokea changamoto na najua haitatokea tena vyuo vikuu vitakuwa vinafunguliwa siku ambapo wana uhakika na fedha zitakuwa zimeshapelekwa kwenye wanafunzi.

Lakini pia pamekuwa na utitiri mwingi mno wa vyuo vikuu unakuta shule ilikuwa inaitwa sekondari leo ukisoma kwenye orodha nayo inaitwa Chuo Kikuu na saa nyingine inafikia wanafunzi unaanza kuwagombania, Chuo Kikuu kwa mfano cha Dodoma kina capacity ya kuweka wanafunzi mpaka 45,000 waliopo ni 30,000 lakini unakuta kinafunguliwa chuo kingine Bagamoyo kina wanafunzi 20 mabweni hayapo maabara hayapo natoa mfano tu labda nimesema Bagamoyo kingine kinafunguliwa Chato.

Sasa ninachotaka kutoa wito kwa Bodi, TCU, Wizara hebu mpitie vizuri hivi vyuo mnatoa vibali mnatoa vibali mno vya kuanzisha chuo kikuu kila mahali wakati vyuo vilivyopo havijajaa watu na mnawachanganya saa nyingine hawa watoto kwa sababu mnakuwa mnawagombania, na vyuo vikuu vingine havina walimu unakuta mwalimu leo yuko  Dar es Salaam kesho yuko Mbeya keshokutwa yuko Iringa keshokutwa Moshi ataconcentrate namna gani kufundisha kwa hiyo matatizo haya mengine yameletelezwa na nyinyi mnnaopendwa kuitwa maVice Chancellors wenye vyuo vilivyopo sijasema wewe (akimaanisha Prof. Rwekaza, VC wa UDSM) kwa hiyo nikuombe Waziri simamia hili, kwanu kuna ubaya gani tukiwa hata na vyuo vikuu vinne tu kila chuo kina watu milioni moja moja watu wako palepale wanalipwa mshahara mzuri na wanaconcentrate vizuri."


KWA MSAADA KUTOKA KWA MWANAFUNZI ALIYEFATILIA SPEECH HII CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM NA KUSAMBAZA KWA WATANZANIA.

Comments

Popular posts from this blog

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

MAMBO YA MUHIMU KUFAHAMU NA KUZINGATIA KABLA YA KUCHAGUA KOZI (TAALUMA) CHUO KIKUU

Picha kwa hisani ya Debt.org 1.0 UTANGULIZI Nilipokuwa mwanafunzi wa chuo kikuu nilisikia manung'uniko miongoni mwa wanafunzi wenzangu wengi wa vyuo vikuu ambayo yalitokana na taaluma wanazosoma. Kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea manung'uniko hayo miongoni mwa wasomi hawa tukiachilia mbali suala la ucheleweshwaji wa mikopo miongoni mwa wasomi hawa (kwa sasa changamoto hii inapungua kadiri siku zinavyosonga). Tatizo lingine ambalo linawasumbua wasomi hawa ni suala la uchaguzi wa taaluma gani akaisome Chuo Kikuu. Uchaguzi wa taaluma (career choice) ni jambo nyeti sana na la kuzingatia kwa muhitimu yeyote wa elimu ya kuanzia kidato cha nne. Jamii yetu ya Tanzania haifahamu kwa undani kuhusu umuhimu wajambo hili lakini huku ndiko msingi hundaliwa. Mtu anapohitimu kidato cha nne na kupata ufaulu wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ama ngazi ya astashahada (certificate) na stashahada (diploma) hapo ndipo uchanguzi wa taaluma huanza. Kwa kuandika makala haya ninakusudia ...

JAY Z FT. MR. HUDSON-YOUNG FOREVER SONG LYRICS

Let's dance in style, let's dance for a while Heaven can wait, we're only watching the skies Hoping for the best but expecting the worst Are you gonna drop the bomb or not? Let us die young or let us live forever We don't have the power but we never say never Sitting in a sandpit, life is a short trip The music's for the sad man Forever young, I wanna be forever young Do you really want to live forever, forever, and ever? Forever young (young) I wanna be (Aye, may the best of your todays) Forever young (Be the worst of your tomorrows) Do you really want to live forever (But we ain't even thinking that far) Forever (ya know what I mean?) Forever young So we're living life like a video (video) Where the sun is always out and you never get old And the champagne's always cold and the music's always good And the pretty girls just happen to stop by in the hood And they hop their pretty ass up on the hood of that pretty ass car Without a wrinkle in today, ...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 12.10.2017

Viunganis Image caption Phillipe Coutinho Afisa mkuu mtendaji wa klabu ya Bercelona Oscar Grau anasema kuwa klabu hiyo itajaribu tena kumsajili kiungo wa kati wa Brazil Philippe Coutinho, 25, wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa mwezi Januari. (Guardian) Liverpool itaendelea kukataa kuingia katika makubaliano ya kumuuza Coutinho Barcelona (Independent) Vilevile , Liverpool imekubali kumkubali Coutinho kuelekea Nou Camp mnmao mwezi Januari katika makubaliano yenye thamani ya £98.6m. (Mundo Deportivo via Daily Mail) Image caption Mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho Meneja Jose Mourinho yuko tayari kutia saini kandarasi ya miaka mitano na klabu ya Manchester United itakayokuwa na thamani ya £65m (Sun) Mchezaji wa Manchester United Juan Mata, 29, amekataa fursa ya kuhamia katika ligi ya China(Daily Mirror) Kiungo wa kati wa Uingereza Jack Wilshere, 25, anaaminika kutaka kuondoka Arsenal mwezi Januari ili kuimarisha uwezo wake wa kujumuishwa...