Skip to main content

YAFAHAMU HAYA KUTOKA BODI YA MIKOPO (HESLB)

Jana katika kipindi cha Dakika 45 ambacho hurushwa kila Jumatatu saa 3 usiku kupitia ITV/Radio One, Sam Mahela mtangazaji wa kipindi hicho alipata nafasi ya kufanya mahojiano na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo, Mh. Abdul Razaq Badru ambaye ameteuliwa na Waziri wa Elimu Prof. Ndalichako kufahamu mambo fulani kuhusu HESLB.

Mkurugenzi huyo alianza kwa kubainisha kuwa tangu kuanzishwa kwake HESLB imekopesha watu laki tatu na ishirini na nne (300,024). Aliongeza kuwa makato ya fedha kwa wale ambao walinufaika na mikopo ya elimu ya juu yanaendelea. Pia alibainisha kwamba kumekuwepo na dosari katika kuwakata watu 200 ambao hawakuwahi kunufaika na mikopo ya elimu ya juu na kusisitiza kwamba kama kuna mtu anakatwa na hakukopeshwa na bodi hiyo atoe taarifa katika Ofisi zilizojirani naye. Lakino pia alidai kuwa waliokatwa kimakosa watarudishiwa fedha zao.

Mkurugenzi aliongeza kuwa Bodi imekopesha jumla ya Tsh. Trilioni 2.4 (waliowahi kukopeshwa na wanaondelea na masomo kwa mwaka 2015/2016) na kwamba kiasi kilichorejeshwa ni Tsh Bilioni 284 na zilizokusanywa ni kiasi cha Tsh Bilioni 105. Mkurugenzi alibainisha kuwa kwa mwaka wa masomo/fedha 2015/2016 ilitakiwa mkopo jumla utolewe Tsh Bilioni 400 na kiasi kadhaa lakini Rais Magufuli alipoingia madarakani aliongeza kiasi cha Tsh Bilioni 132. Ikumbukwe kwamba fedha hizi ni zile za kujikimu, vitabu na maktaba, ada ya chuo pamoja na gharama ya mafunzo kwa vitendo.

Kuhusu kukatwa fedha kwa wafanyakazi walioajiriwa katika taasisi binafsi Mkurugenzi alidai kuwa elimu inatolewa kwa waajiri kuhusu kukata fedha hiyo kwa mujibu wa sheria. Aidha Mkurugenzi aliongeza kwamba muda wa kurejesha mkopo huo ni baada ya miaka 10 toka mnufaika amalize masomo yake bila kujali ameajiriwa au la! Aliongeza kuwa inapopita miaka 10 bila mnufaika kujeresha kiasi hicho, kunakuwa na faini ya 6% kwa mwaka kwa jumla ya miaka yote ambayo mnufaika atakuwa amechelewa kurejesha mkopo.
Kuhusu mwaka wa masomo 2016/2017, Mkurugenzi alidai kuwa wanafunzi elfu themanini na nane 88,000 ndiyo wameomba kunufaika na mikopo hiyo na kwamba zoezi la kupitia wenye sifa za kukopeshwa bado linaendelea.

Lakini pia Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa mpaka sasa Vyuo vimerejesha kiasi cha Tsh Bilioni 1 na laki 2 (1,000,200,000/=) kati ya Tsh Bilioni 2 na laki 7 (2,000,700,000/=) fedha ambazo zilitumika kwa wanafunzi hewa. Hili alilibainisha alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Sam Mahela kuhusu kiasi cha Tsh Bilioni 14 (14,000,000,000) kutumika kuwalipa wanafunzi hewa.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema kwamba kuhusu utoaji wa mikopo unafata vigezo kama muombaji anafaa. Hili alilibainisha wakati akijibu swali kuhusu kushuka kwa udahili wa waliosoma Diploma kutoka GPA ya 3.5 hadi 3.0 kama wanaweza kunufaika na mkopo kutoka HESLB. Mkurigenzi alibainisha kuwa watu wenye mahitaji mkubwa kama vile Yatima, Walemavu na Wale wanaotoka katika hali duni pamoja na Watakaosoma kozi za uhandisi, uhandisi wa mafuta na gesi, Ualimu wa Sayansi na Hisabati pamoja na Udaktari hao watapakuwa na kipaumbele kunufaika na mkopo wa Elimu ya Juu.

Mkurugenzi alipoulizwa kuhusu wanafunzi waliokuwa wakisoma Diploma maalum ya Ualimu katika Chuo Kikuu cha Dodoma na kuhamishiwa katika vyuo vingine kama wanaweza kunufaika tena mikopo, alidai kuwa utaratibu maalumu utatolewa na Serikali panapostahili.

Mkurugenzi pia alibainisha kuwa Bodi ya Mikopo (HESLB) inafanya kazi kwa ushirikiano kabisa na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) na kwamba ili mwanafunzi apatiwa mkopo sharti adailiwe kupitia TCU kama kigezo cha kwanza kupata mkopo wa Elimu ya Juu na kuwatoa hofu wanafunzi, wazazi na wadau wa Elimu kuhusu kuwepo awamu mbalimbali za Udahili TCU kuwa hakutokwamisha suala la ukopeshwaji kwa wenye sifa stahiki.

Pia alibainisha kuwa kiasi cha fedha Tsh Bilioni Mia tano (500,000,000,000) zimetengwa na Wizara kuhudumia mikopo ya Wanafunzi wa elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

MAANDALIZI MEMA YA SIKUKUU YA KRISMAS

Kwanza namshukuru Mungu toka tukiwa wadogo mpaka sasa anaendelea kutulinda. Uongozi mzima wa Venance Blog tunawatakieni maandalizi mema ya Krismas hapo kesho, wale wa kanisani tukafurahi kwani bwana atazaliwa. Msali salama katika misa za mkesha kubwa zaidi kudumisha amani na usalama kuanzia leo mpaka sikuku itakapoisha. MAANDALIZI MEMA YA KRISMAS!!!

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

AJALI: BASI LAUA WATU 12 PAPO HAPO

Watu 12 wamekufa papo hapo na wengine zaidi ya 90 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Korogwe, Tanga kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka. Ajali hiyo ilitokea jana saa 1.30 asubuhi kwenye barabara kuu ya Segera-Chalinze katika kijiji cha Kwalaguru kata ya Kwedizinga wilayani hapa. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alithibitisha jana kutokea kwa ajali hiyo ya basi la Burudani namba T 610 ATR aina ya Nissan. Majeruhi walipelekwa katika hospitali ya wilaya ya Korogwe ya Magunga, kwa matibabu ya awali na miili ya marehemu, akiwamo dereva wa gari hilo, Luta Mpenda (35) imehifadhiwa hospitalini hapo.  “Tukiwa tunakaribia kwenye kona ile, tulipishana na lori hilo likiwa kasi upande wetu, dereva wetu akajitahidi kulikwepa lakini kutokana na ile kona kuwa kali, gari lilimshinda na kupinduka,” alisema Bendera. Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo walisema walisikia kishindo kutoka eneo hilo wakaenda na kukuta gari limepinduka na baadh...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

TCU IMEFUNGUA DIRISHA LA UDAHILI KWA AWAMU YA PILI

Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imefungua tena dirisha la udahiri kwa Wanafunzi wanaoomba kuchaguliwa katika kozi mbalimbali za Shahada ya Kwanza mwaka huu wa masomo 2016/2017. Linasomeka hivi: TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA (TCU) TAARIFA KWA UMMA Tunapenda kuutangazia Umma kuwa tulifunga mfumo wa pamoja wa udahili tarehe 31/08/2016 saa sita usiku ili kuchakata maombi ya waombaji waliofanikiwa kuomba udahili kwa mwaka wa masomo 2016/2017. Hata hivyo kutokana na wengine kushindwa kufanikiwa kutokana na sababu mbali mbali, Tume inatangaza kuwa itafungua maombi kwa awamu ya pili kuanzia tarehe 12 hadi 23 Septemba 2016 ili kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili. • Waombaji watakaokuwa wamekosa nafasi kwenye awamu ya kwanza • Waombaji wa kidato cha Sita walioshindwa kuomba katika awamu ya kwanza • Waombaji wenye vigezo vya Stashahada ambao walishindwa kuomba kutokana na matokeo yao kuchelewa kufika NACTE kwa wakati, • Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya “Cambridge” mwaka...

CCM WALIPOKUJA KUKAGUA UJENZI MWAKALELI

Kinana akishirili katika ujenzi Mwakaleli Dr. Asha Rose Migiro na Nape wakishiriki ketika ujenzi Dr. Asha Rose Migiro akizungumza na wanafunzi wa Mwakaleli Katibu mwenezi wa CCM akizungumza na wanafunzi wa Mwakaleli Prof. David Mwakyusa akizungumza na wanafunzi wa Mwakaleli, akiwaasa kusoma kwa bidna kuepukana na mahusiano kwani UKIMWI unaua. Wanafunzi wa kidato cha sita Mwakaleli wakiwa na Dr. Asha Rose Migiro nambunge wa vuti maalumu Mbeya Dr. Mary Mwanjelwa kwtika picha. SOURCE: CCM BLOG