Skip to main content

MFAHAMU HILLARY CLINTON KWA MAMBO HAYA 15

Tokeo la picha la hillary clinton
Jina Kamili: Hillary Diane Rodham Clinton
Kuzaliwa: Oktoba 26, 1947
Alikozaliwa: Chicago, Illinois

Kwa Ufupi

Alipochaguliwa kuwa Seneta mwaka 2001 alikuwa mwanamke wa kwanza First Lady kuwa mtumishi wa serikali. Baadaye alikuwa Katibu Mkuu wa Ikulu ya Marekani mwaka 2009 akitumikia wadhifa huo hadi mwaka 2013 katika utawala wa Rais Barrack Obama. Mwaka huu (2016), amekuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kugombea Urais kwa tiketi ya chama cha The Democratics.

Tokeo la picha la hillary clinton
Hillary alizaliwa  Oktoba 26, 1947 huko Chicago, Illinois. Alipata Shahada yake ya Sheria kutoka Yale University. Alifunga ndoa na mwanafunzi mwenziye aliyekuwa akisoma sheria Bill Clinton mwaka 1975. Baadaye alitumikia taifa la Marekani kama First lady  mwaka 1993 hadi 2001, na baadaye akiwa Seneta mwaka 2001 hadi 2009. Mapema mwaka 2007 Clinton alitangaza kugombea Urais nchini Marekani. Katika kura za maoni mwaka 2008 alichuana na Barrack Obama lakini kura hazikumruhusu kugombea Urais kwa ticket ya Democratic. Rais Obama alipoingia madarakani alimchagua kuwa Katibu Mkuu mwaka 2009 hadi 2013.

HillaryRodham ni mtoto  mkubwa katika familia ya Hugh Rodham na Dorothy Emma Howell Rodham. Ana wadogo zake wawili wanaume; Hugh Jr. aliyezaliwa 1950 na Anthony aliyezliwa 1954.

Kama kijana Hillary aliingia katika siasa na kumfanyia kampeni mgombea wa chama cha Republican Barry Goldwater mwak 1954. Alivutiwa kufanya kazi za umma baada ya kusikia hotuba ya Martin Luther King Jr. huko Chicago na hapo alijiunga na chama cha Democratic mwaka 1968.

Elimu

Tokeo la picha la hillary clinton at yale
Hillary enzi za Yale
Hillary alisoma Wellesley College ambapo alikuwa akishiriki katika masuala ya siasa shuleni na alichaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa darasa lake kabla hajahitimu mwaka 1959. Baadaye alijiunga na Shule ya Sheria Yale ambako alikutana na Bill Clinton. Alitunukiwa Shahada ya Heshima katika sheria mwaka 1973 na aliendelea na alijiunga na Kituo cha masomo ya watoto Yale ambako alisoma kozi za masomo ya watoto na madawa nakwa mwaka mmoja.

Ndoa

Tokeo la picha la hillary clinton and bill wedding
Hillary na Bill Clinton siku ya harusi yao 1975

Alifunga ndoa na Bill Clinton mwaka 1975 na wana mtoto mmoja anayeitwa Chelsea. Ndoa hii ipo katika orodha ya watu maarufu duniani ambao wameanza mahusiano tokea wakiwa masomoni. Hillary alipomaliza chuo kwa wakti ule alikaa mwaka mzima chuoni hapo akimsubiri mpenzi wake Bill Clinton ahitimu masomo yake.

Vitabu alivyoandika

1996- It Takes a Village
1997- The Unuque Voice of Hillary Clinton
1998- Dear Socks, Dear Buddy
 2000- An Invitation to the White House
2003- Living History
2014- Hard Choices
2015- Solutions: American Leaders Speak Out on Criminal Justice
2016- Stronger Together

First Lady wa Marekani

Tokeo la picha la the clintons during bill inauguration
Siku ya kiapo, Bill Clinton kama Rais akiwa na mkewe Hillary na binti yao Chelsea

Katika Uchaguzi wa mwaka 1992 Hillary alishiriki vyema katika kuaslimia wapiga kura, kuhutubia na kuwa miongoni mwa washauri wakuu wa Bill Clinton.


MAMBO 15 UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU HILLARY CLINTON

15. Ameshinda tuzo ya Grammy mwaka 1997 lakini sio tuzo ya muziki. Ni kuhusu kitabu chake cha It Takes a Village lakini sio pekee aliyeshinda tuzo hizo, Obama pia alishachukua tuzo hii katika kitabu chake pia.

14. Hillary hajaendesha gari toka mwak 1996 alilisema hili mwaka 2012.

13.  Mama yake Bill Clinton (mama mkwe wa Hillary) hakufikiria kwamba Hillary ni mzuri sana kuwa na mwanaye kuwa hana mvuto.

12. Moja kati ya kesi za awali za Hillary kama mwanasheria ilikuwa inahusisha Panya.

11. Hillary Clinton mwanzoni alikuwa mfuasi wa chama cha Republican kabla ya kuhamia Democratic mwaka 1968 baada ya kuvutiwa na moja kati ya hotuba za Martin Luther King Jr.

10.Katika utawala waRais Bill Clinton FBI walichukua picha za viganja (fingerprints) vya Bill na Hillary kuona kama wawili hao waliweza kuangalia nyaraka za FBI.Ilibainika kwamba hawakuhusika kuangalia nyaraka hizo lakini miaka miwili baadaye zilikutwa nyumbani kwa Hillary zikiwa na alama za viganja vyake.

9. Utambulisho wake wa Huduma za Siri ni "Evergreen" na alipewa utambulisho huu akiwa First lady na Huduma za Siri.Amekua akitumia utambulisho huu hata katika kampeni zake za Urais. Katika kipindi cha 2008 alipokuwa akigombea utambulisho huu ulirejeshwa tena. Bill Clinton pia amekuwa akitumia utambulisho wa "Eagle" katika kipindi cha harakati za mkewe kuelekea Ikulu .

8. Ni First lady pekee ambaye amegombea Useneta na kushinda kiti hicho akiwa pia ni First lady. Alikuwa Seneta wa New York mwaka 2001 na kukabidhiwa Ofisi Januari 3 mwaka huo.

7. Jarida la Sheria la Marekani 'The National Law Journal' lilimtaja Hillary kuwa miongoni mwa wanasheria 100 wenye ushawishi nchini humo mwaka 1988 na 1991. Umahiri wake katik sheria ulimfanya awe na pesa nyingi hata kumshinda mumewe Bill aliyekuwa Gavana wa Arkansas kwa wakati huo. Umahili wa Clinton ktik sheria ulichangia pia kwa kiasi kikubwa kumfanya Bill awe Rais wa nchi hiyo kwa kipindi hicho.

6. Ni Katibu Mkuu aliyesafiri kuliko makatibu wengine katika Historia katika kipindi chake cha miaka 4. Alizuru nchi 112 na kusafiri kwa ndege maili milioni 1 na kutumia 25% ya kipindi chake katika safari.

5. Amekuwa akituhumiwa kujihusisha na Usagaji "mapenzi ya jinsia moja". Baadhi ya watu wamekuwa wakithibitisha hili kwa mfano Edward Klein ambaye ameandika ktika kitabu chake The Truth About Hillary kuwa amekuwa akishiriki usagaji na msaidizi wake Huma Abedin na wasagaji wengine.

4. Hillary na mumewe Bill waliwahi kuitwa Mahakamani kutoa ushahidi kuhusika katik scandal ya Whitewater Development. Hata hivyo baadaye hawakukutwa na hatia ya kufanya mabaya katika scandal hiyo.

3. Hillary aliamua kutumia jina la Clinton baada ya kushawishiwa na wapiga kura wa Arkansas. Baada ya ndoa yao Hillary aliendelea kutumia jina lake la Hillary Rodham, Wapiga kura hao walitaka kujua kama ndoa yao ni ndoa kweli ama fasheni tu hivyo Hillary akaamua kutumia jina la Hillary Rodham Clinton. Kwa hiyo ili kufanya mumewe ashinde katika Uchaguzi kuwa Gavana wa jimbo la Arkansas aliamua kujiita Hillary Rodham Clinton.

2. Alishiriki katika jopo la wanasheria 43 kumtia hatiani Rais Richard Nixon. Wanajopo wenzie walimtuhumu kama muongo na kutofuata maadili ya kumtia hatiani Rais Nixon. Bosi wa Hillary alisema mara kwa mara Hillary alikuwa akikosea katik kuuliza maswali lakini hakuwa na uwezo wa kumfukuza Hillary kazi.

1. Japokuwa alipmba kurasa za jarida la The Vogue mwaka 1998, alikataa kuonekana katika Jarida hilo mwaka 2007 kwa kuhofia kuwa mfeministi sana kitu ambacho kingeleta shida katika mbio zake za uchaguzi wa Urais mwaka 2008.








Tokeo la picha la hillary clinton
 Tokeo la picha la hillary clinton

MAKALA HII IMEHARIRIWA KWA HISANI YA MTANDAO.

Comments

Popular posts from this blog

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

EYMAEL: NIPENI YANGA NIIUE AL-AHLY

KOCHA Luc Eymael ambaye tayari ameshafanya mazungumzo ya awali na viongozi wa Yanga, ameuambia uongozi wa klabu hiyo kuwa anaijua vizuri Klabu ya Al-Ahly ya Misri na endapo watampatia kibarua hicho, atawasaidia kuwang’oa katika Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Akizungumza na Mwanaspoti kwa njia ya mtandao, Eymael ambaye ni raia wa Ubelgiji, alisema amefanya mazungumzo ya awali na mmoja wa viongozi wa Yanga kupitia barua pepe, ambapo alisema kama klabu hiyo itampatia ajira hiyo hana wasiwasi na uwezo wake katika kuwang’oa Al-Ahly ambao Yanga inatarajia kukutana nao raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Yanga itaanza michuano hiyo dhidi ya timu ya Comoronize ya Visiwa vya Comoro inayotajwa kuwa ni dhaifu na baada ya hapo itakuwa na kibarua kizito dhidi ya wababe hao wa Misri. Eymael aliyezaliwa miaka 54 iliyopita katika mji mdogo wa Tongeren, Ubelgiji alisema hajajua Yanga inaundwa na nyota wenye uwezo kiasi gani lakini anachoweza kuwaambia viongozi wa klabu hiyo ni k...

DIRISHA LA UFADHILI WA MASOMO "SAMIA SCHOLARSHIP" 2023/2014 LIMEFUNGULIWA

TANGAZO LA SAMIA SCHOLARSHIP MWAKA 2023/2024 UFADHILI KUPITIA SAMIA SCHOLARSHIP KWA WAHITIMU WENYE UFAULU WA JUU KATIKA MITIHANI YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2023 KATIKA TAHASUSI ZA SAYANSI 1.0 UTANGULIZI Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatangaza programu ya Ufadhili iitwayo SAMIA SCHOLARSHIP kwa masomo ya shahada ya kwanza kwa wanafunzi waliopata ufaulu wa juu katika mitihani ya Kidato cha Sita mwaka 2023 iliyoendeshwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) katika Tahasusi za Sayansi (PCB, PCM, PGM, CBG, CBA, PMC na CBN).  SAMIA SCHOLARSHIP itagharamia kwa asilimia mia moja (100%) masomo ya Elimu ya Juu kwa wanafunzi hao ambao wamepata udahili katika fani za Teknolojia, Uhandisi, Hisabati na Tiba. 2.0 SIFA ZA KUPATA UFADHILI Ufadhili huu utatolewa kwa wahitimu wa kidato cha sita wenye sifa zifuatazo: 1. Awe Mtanzania; 2. Awe na ufaulu wa juu kwenye mitihani ya taifa ya kidato cha sita mwaka 2023 iliyoendeshwa na NECTA katika tahasusi za sayansi; 3. Awe amepata ...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA

Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz . Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika. Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya  HAPA  ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya  HAPA  ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa: 1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3) SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno ku...

MGAHAWA WAKUMBWA NA KASHFA YA KUUZA NYAMA YA BINADAMU

Mgahawa mmoja mjini London umekumbwa na habari bandia za kuuza nyama ya mtu. Wafanyikazi katika mkahawa wa Karri Twist katika eneo la New Cross nchini Uingereza wamehangaishwa kwa kupigiwa simu kutoka kwa wateja wanaosema ''Kwa nini hamujafunga''?. Mkahawa huo wa chakula cha jioni ni mwathiriwa wa habari za mzaha zilizodai kwamba mmiliki wake alikamatwa kwa kuweka nyama ya binadamu katika chakula na kwamba miili 9 ilipatikana katika jokovu la mkahawa huo. Na watu wengine waliamini mzaha huo. Habari hiyo ilichapishwa katika chombo cha habari cha channel23news.com, mtandao ambao wateja wake wanaweza kuchapisha habari za uwongo ili kuwafanyia mzaha rafiki zao kwa kuchapisha moja kwa moja katika mtandao wa fecbook. Shinra Begum ambaye ndio mmiliki wake aliambia Newsbeat kwamba biashara hiyo ya familia imekumbwa na wakati mgumu tangu habari hiyo ilipochapishwa siku ya Alhamisi. ''Wakati watu walipoanza kunipigia simu na kuuliza iwapo tulikuw...

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI: TRUMP NA RUBIO WATOFAUTIANA KUHUSU UISLAM

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Marco Rubio amemshtumu Donald Trump kwa kusema kuwa Uislamu unachukia Marekani katika mjadala uliokuwa moja kwa moja runingani. Bwana Rubio ambaye anakabiliwa na ushindani wa maisha yake katika jimbo la Florida siku ya Jumanne amesema kuwa Uislamu una tatizo la itikadi kali lakini akaongezea kuwa Waislamu wengi wanapenda Wamerekani. ''Marais hawawezi kusema kile wanachotaka ,kuna madhara'',alisema huku raia wakimpigia makofi. Wagombea hao wanne wa chama cha Republican walisikia maombi kutoka kwa viongozi wa chama hicho kuwa na mjadala wa amani. Ikilinganishwa na mjadala uliopita ambao ulikabiliwa na na matusi ya kibinafsi mjadala huu ulikuwa na muongozo mzuri huku wagombea wote wakitoa malengo ya sera zao. ''Kufikia sasa siamini vile tumekuwa watulivu hapa'',bwana Trump alinukuliwa akisema. Lakini katika swala la Uislamu,kulikuwa na tofauti kubwa kati ya Trump na wagombea wengine huku wen...

FACEBOOK KUANZISHA PROGRAMU YA KUWAPATANISHA WAPENDANAO HUKU IKIIMARISHA KIWANGO CHA FARAGHA

Mark Zuckerberg mmiliki wa mtandao wa Facebook Kampuni ya Facebook  inaongeza faragha kwa watumiaji wake kwa kuweka sehemu ya kufuta historia ya ulichokitafuta katika mtandao huo wa kijamii. Aidha amesema kwamba programu hiyo itaangazia uhusiano wa muda mrefu na sio urafiki wa muda mfupi na itawatenganisha marafiki na watu wanaotarajiwa kuwa na uhusiano. ''Programu hii itakuwa na kiwango cha juu cha siri na usalama kutoka mwanzo'', aliongeza. Hivi karibuni kampuni hiyo ilikumbwa na kashfa ya kutothamini faragha za watumiaje wake huku watumiaji zaidi ya millioni hamsini walidukuliwa katika kipindi cha uchaguzi wa Marekani. Facebook imekua katika sakata la faragha ya watumiaje hivi karibuni, mamilioni ya taarifa za watumiaji zilichukuliwa bila ridhaa na kampuni ya Cambridge Analytica kwa matumizi ya wanasiasa.  Mark Zuckerberg amesema kuwa atahakikisha suala kama hilo halitajitokeza tena, kwa kutengeneza ulinzi zaidi wa mtandao huo. Kitendo hicho kilishusha...