Skip to main content

MFAHAMU HILLARY CLINTON KWA MAMBO HAYA 15

Tokeo la picha la hillary clinton
Jina Kamili: Hillary Diane Rodham Clinton
Kuzaliwa: Oktoba 26, 1947
Alikozaliwa: Chicago, Illinois

Kwa Ufupi

Alipochaguliwa kuwa Seneta mwaka 2001 alikuwa mwanamke wa kwanza First Lady kuwa mtumishi wa serikali. Baadaye alikuwa Katibu Mkuu wa Ikulu ya Marekani mwaka 2009 akitumikia wadhifa huo hadi mwaka 2013 katika utawala wa Rais Barrack Obama. Mwaka huu (2016), amekuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kugombea Urais kwa tiketi ya chama cha The Democratics.

Tokeo la picha la hillary clinton
Hillary alizaliwa  Oktoba 26, 1947 huko Chicago, Illinois. Alipata Shahada yake ya Sheria kutoka Yale University. Alifunga ndoa na mwanafunzi mwenziye aliyekuwa akisoma sheria Bill Clinton mwaka 1975. Baadaye alitumikia taifa la Marekani kama First lady  mwaka 1993 hadi 2001, na baadaye akiwa Seneta mwaka 2001 hadi 2009. Mapema mwaka 2007 Clinton alitangaza kugombea Urais nchini Marekani. Katika kura za maoni mwaka 2008 alichuana na Barrack Obama lakini kura hazikumruhusu kugombea Urais kwa ticket ya Democratic. Rais Obama alipoingia madarakani alimchagua kuwa Katibu Mkuu mwaka 2009 hadi 2013.

HillaryRodham ni mtoto  mkubwa katika familia ya Hugh Rodham na Dorothy Emma Howell Rodham. Ana wadogo zake wawili wanaume; Hugh Jr. aliyezaliwa 1950 na Anthony aliyezliwa 1954.

Kama kijana Hillary aliingia katika siasa na kumfanyia kampeni mgombea wa chama cha Republican Barry Goldwater mwak 1954. Alivutiwa kufanya kazi za umma baada ya kusikia hotuba ya Martin Luther King Jr. huko Chicago na hapo alijiunga na chama cha Democratic mwaka 1968.

Elimu

Tokeo la picha la hillary clinton at yale
Hillary enzi za Yale
Hillary alisoma Wellesley College ambapo alikuwa akishiriki katika masuala ya siasa shuleni na alichaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa darasa lake kabla hajahitimu mwaka 1959. Baadaye alijiunga na Shule ya Sheria Yale ambako alikutana na Bill Clinton. Alitunukiwa Shahada ya Heshima katika sheria mwaka 1973 na aliendelea na alijiunga na Kituo cha masomo ya watoto Yale ambako alisoma kozi za masomo ya watoto na madawa nakwa mwaka mmoja.

Ndoa

Tokeo la picha la hillary clinton and bill wedding
Hillary na Bill Clinton siku ya harusi yao 1975

Alifunga ndoa na Bill Clinton mwaka 1975 na wana mtoto mmoja anayeitwa Chelsea. Ndoa hii ipo katika orodha ya watu maarufu duniani ambao wameanza mahusiano tokea wakiwa masomoni. Hillary alipomaliza chuo kwa wakti ule alikaa mwaka mzima chuoni hapo akimsubiri mpenzi wake Bill Clinton ahitimu masomo yake.

Vitabu alivyoandika

1996- It Takes a Village
1997- The Unuque Voice of Hillary Clinton
1998- Dear Socks, Dear Buddy
 2000- An Invitation to the White House
2003- Living History
2014- Hard Choices
2015- Solutions: American Leaders Speak Out on Criminal Justice
2016- Stronger Together

First Lady wa Marekani

Tokeo la picha la the clintons during bill inauguration
Siku ya kiapo, Bill Clinton kama Rais akiwa na mkewe Hillary na binti yao Chelsea

Katika Uchaguzi wa mwaka 1992 Hillary alishiriki vyema katika kuaslimia wapiga kura, kuhutubia na kuwa miongoni mwa washauri wakuu wa Bill Clinton.


MAMBO 15 UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU HILLARY CLINTON

15. Ameshinda tuzo ya Grammy mwaka 1997 lakini sio tuzo ya muziki. Ni kuhusu kitabu chake cha It Takes a Village lakini sio pekee aliyeshinda tuzo hizo, Obama pia alishachukua tuzo hii katika kitabu chake pia.

14. Hillary hajaendesha gari toka mwak 1996 alilisema hili mwaka 2012.

13.  Mama yake Bill Clinton (mama mkwe wa Hillary) hakufikiria kwamba Hillary ni mzuri sana kuwa na mwanaye kuwa hana mvuto.

12. Moja kati ya kesi za awali za Hillary kama mwanasheria ilikuwa inahusisha Panya.

11. Hillary Clinton mwanzoni alikuwa mfuasi wa chama cha Republican kabla ya kuhamia Democratic mwaka 1968 baada ya kuvutiwa na moja kati ya hotuba za Martin Luther King Jr.

10.Katika utawala waRais Bill Clinton FBI walichukua picha za viganja (fingerprints) vya Bill na Hillary kuona kama wawili hao waliweza kuangalia nyaraka za FBI.Ilibainika kwamba hawakuhusika kuangalia nyaraka hizo lakini miaka miwili baadaye zilikutwa nyumbani kwa Hillary zikiwa na alama za viganja vyake.

9. Utambulisho wake wa Huduma za Siri ni "Evergreen" na alipewa utambulisho huu akiwa First lady na Huduma za Siri.Amekua akitumia utambulisho huu hata katika kampeni zake za Urais. Katika kipindi cha 2008 alipokuwa akigombea utambulisho huu ulirejeshwa tena. Bill Clinton pia amekuwa akitumia utambulisho wa "Eagle" katika kipindi cha harakati za mkewe kuelekea Ikulu .

8. Ni First lady pekee ambaye amegombea Useneta na kushinda kiti hicho akiwa pia ni First lady. Alikuwa Seneta wa New York mwaka 2001 na kukabidhiwa Ofisi Januari 3 mwaka huo.

7. Jarida la Sheria la Marekani 'The National Law Journal' lilimtaja Hillary kuwa miongoni mwa wanasheria 100 wenye ushawishi nchini humo mwaka 1988 na 1991. Umahiri wake katik sheria ulimfanya awe na pesa nyingi hata kumshinda mumewe Bill aliyekuwa Gavana wa Arkansas kwa wakati huo. Umahili wa Clinton ktik sheria ulichangia pia kwa kiasi kikubwa kumfanya Bill awe Rais wa nchi hiyo kwa kipindi hicho.

6. Ni Katibu Mkuu aliyesafiri kuliko makatibu wengine katika Historia katika kipindi chake cha miaka 4. Alizuru nchi 112 na kusafiri kwa ndege maili milioni 1 na kutumia 25% ya kipindi chake katika safari.

5. Amekuwa akituhumiwa kujihusisha na Usagaji "mapenzi ya jinsia moja". Baadhi ya watu wamekuwa wakithibitisha hili kwa mfano Edward Klein ambaye ameandika ktika kitabu chake The Truth About Hillary kuwa amekuwa akishiriki usagaji na msaidizi wake Huma Abedin na wasagaji wengine.

4. Hillary na mumewe Bill waliwahi kuitwa Mahakamani kutoa ushahidi kuhusika katik scandal ya Whitewater Development. Hata hivyo baadaye hawakukutwa na hatia ya kufanya mabaya katika scandal hiyo.

3. Hillary aliamua kutumia jina la Clinton baada ya kushawishiwa na wapiga kura wa Arkansas. Baada ya ndoa yao Hillary aliendelea kutumia jina lake la Hillary Rodham, Wapiga kura hao walitaka kujua kama ndoa yao ni ndoa kweli ama fasheni tu hivyo Hillary akaamua kutumia jina la Hillary Rodham Clinton. Kwa hiyo ili kufanya mumewe ashinde katika Uchaguzi kuwa Gavana wa jimbo la Arkansas aliamua kujiita Hillary Rodham Clinton.

2. Alishiriki katika jopo la wanasheria 43 kumtia hatiani Rais Richard Nixon. Wanajopo wenzie walimtuhumu kama muongo na kutofuata maadili ya kumtia hatiani Rais Nixon. Bosi wa Hillary alisema mara kwa mara Hillary alikuwa akikosea katik kuuliza maswali lakini hakuwa na uwezo wa kumfukuza Hillary kazi.

1. Japokuwa alipmba kurasa za jarida la The Vogue mwaka 1998, alikataa kuonekana katika Jarida hilo mwaka 2007 kwa kuhofia kuwa mfeministi sana kitu ambacho kingeleta shida katika mbio zake za uchaguzi wa Urais mwaka 2008.








Tokeo la picha la hillary clinton
 Tokeo la picha la hillary clinton

MAKALA HII IMEHARIRIWA KWA HISANI YA MTANDAO.

Comments

Popular posts from this blog

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

RIHANNA - DIAMONDS SONG LYRICS

Shine bright like a diamond Shine bright like a diamond Find light in the beautiful sea, I choose to be happy You and I, you and I, we're like diamonds in the sky You're a shooting star I see, a vision of ecstasy When you hold me, I'm alive, we're like diamonds in the sky I knew that we'd become one right away Oh, right away At first sight I felt the energy of sun rays I saw the life inside your eyes So shine bright, tonight, you and I We're beautiful like diamonds in the sky Eye to eye, so alive We're beautiful like diamonds in the sky Shine bright like a diamond (whoa) Shine bright like a diamond (whoa) Shining bright like a diamond We're beautiful like diamonds in the sky Shine bright like a diamond (whoa) Shine bright like a diamond (whoa) Shining bright like a diamond We're beautiful like diamonds in the sky Palms rise to the universe as we moonshine and molly Feel the warmth, we'll never die, we're like diamonds in the sky You're a ...

MABOMU YASABABISHA WATU ZAIDI YA ELFU 50 KUHAMA UJERUMANI

Operesheni kubwa ya kuwaondoa wakaazi wengi wa mji wa Hanover ulioko kaskazini mwa Ujerumani, inaendelea, ya kuwahamisha zaidi ya watu elfu 50 baada ya mabomu makubwa ya wakati wa vita vya dunia, kupatikana kama hayajalipuka. Wakaazi hao wanatarajiwa kuondoka majumbani mwao baadaye leo, ili kuwapa nafasi wataalamu wa kutegua mabomu, kuhamishia mahala salama mabomu hayo ambayo yanakisiwa kuwa matano. Operesheni hiyo itachukua siku nzima, na hata zaidi ikiwa mabomu mengineyatapatikana. Washambuliaji walivamia mji wa Hanover mara 125 kwa mabomu, wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Haki miliki ya picha Getty Images.     Wataalamu wanaamini kuwa mabomu ambayo hayakulipuka huenda yako chini ya jengo hili                 Zaidi ya asilimia 20 ya mabomu yaliyoangushwa mjini humo hayakulipuka. Baadhi ya mabomu mengine yalikuwa na vifaa vinavyochuku...

KIGOGO WA WEMA AMHONGA GARI KAJALA

NI madai mazito! Kwamba, nyota wa muvi za Kibongo, Kajala Masanja amehongwa gari na mtu anayedaiwa kuwa ni kigogo wa Ikulu. Hii ndiyo habari ya mjini kwa sasa na Risasi Jumamosi limeifukunyua. Kwa mujibu wa habari hizo ambazo zipo hadi kwenye mitandao ya kijamii, hasa Instagram, Kajala alinunuliwa gari hilo aina ya Toyota Brevis lenye rangi ya bluu iliyoiva wiki mbili zilizopita mara baada ya kutua Bongo akitokea nchini China ambako alikwenda kwa mambo yake binafsi. TAARIFA ZINAVYODAI Wasambaza taarifa hao walidai kuwa, kigogo huyo wa Ikulu ni yule Clement ambaye amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi wa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu. “Mmeisikia hii? Kajala amenunuliwa gari na Kile (Clement), lina thamani ya shilingi milioni kumi na moja, Wema alie tu nakwambia. We ukisema cha nini wenzako wanajiuliza watakipata lini? “Kwanza mnajua kama bifu la Wema na Kajala lilitokana na Clement? Alipoachana na Wema akatua kwa msichana anaitwa Naima, lakini akaona bado akaenda hadi kwa Kajala. We...

ZIFAHAMU TEKNOLOJIA 7 ZITAZOKAZOKUZA MAENDELEO YA MAJIJI MAKUBWA DUNIANI

Fikiria ulikuwa unafanya kazi katika taasisi ya maendeleo na kupunguza umasikini mwanzoni mwa miaka ya 1990. Mwandishi wa makala hii, Abhas Jha anasema yeye aliwahi kufanya kazi zama hizi. Anasema kipindi hicho kulikuwa na tovuti moja tu iliyokuwepo duniani mpaka kufikia Agosti mwaka 1991 (leo kuna zaidi ya tovuti bilioni 1.5 duniani kote). Anasema kipindi hicho simu za mkononi zilikuwa ghali sana, chache na zilikuwa nzito na za kishamba sana ukilinganisha na hizi za sasa. Ni watu wachache wangetazamia kuhusu hali iliyopo nchini India kwa sasa kwamba kungekua na idadi kubwa ya simu za mkononi kuilko idadi ya vyoo. Bill Gates aliwahi kusema "tunayapa uzito sana mabadiliko ambayo yatatokea ndani ya kipindi cha muda mfupi sana na kuyapuuza yale yaliyotokea kwa muda mrefu sana". Teknolojia inakua kwa kasi sana na kufanya na mabadiliko makubwa sana kwenye majiji ili kufikisha huduma kwa jamii. Teknolojia inafanya hivi ili sio tu kufikisha huduma haraka kwa wateja bali pia kuk...