Uganda imetoa tahadhari kwamba kundi la wanamgambo la Al Shabaab linapanga kutumia malori ya mafuta kama mabomu katika mahambulizi yao.
Taarifa hii inakuja siku moja baada ya polisi kuwakamata washukiwa wawili wa ugaidi waliokuwa na mabomu wakinuia kutekeleza mashambulizi mjini Mombasa.
Mkuu wa polisi wa Uganda,Kale Kayihura, amesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba idara ya polisi na ujasusi zina taarifa za kuthibitishwa kuwa kundi la Al-Shabaab linapanga kulipua malori ya mafuta nchini Uganda na kusababisha uharibifu mkubwa.
Ameshauri wananchi kuwa waangalifu na waweze kutoa taarifa zozote kwa polisi.
Uganda na Kenya ziko na wanajeshi wake nchini Somalia kusaidia wanajeshi wa Somalia na wale wa Muungano wa Afrika kupambana na kundi la Al Shabaab.
Wapiganaji hao wamekiri kufanya mashambulizi katika nchi hizo mbili na kutishia mashambulizi zaidi ikiwa Kenya haitaondoa wanajeshi wake kutoka Somalia.
Kundi la Al Shabaab liliwaua watu 76 katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwaka 2010.
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...
Comments
Post a Comment