Uganda imetoa tahadhari kwamba kundi la wanamgambo la Al Shabaab linapanga kutumia malori ya mafuta kama mabomu katika mahambulizi yao.
Taarifa hii inakuja siku moja baada ya polisi kuwakamata washukiwa wawili wa ugaidi waliokuwa na mabomu wakinuia kutekeleza mashambulizi mjini Mombasa.
Mkuu wa polisi wa Uganda,Kale Kayihura, amesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba idara ya polisi na ujasusi zina taarifa za kuthibitishwa kuwa kundi la Al-Shabaab linapanga kulipua malori ya mafuta nchini Uganda na kusababisha uharibifu mkubwa.
Ameshauri wananchi kuwa waangalifu na waweze kutoa taarifa zozote kwa polisi.
Uganda na Kenya ziko na wanajeshi wake nchini Somalia kusaidia wanajeshi wa Somalia na wale wa Muungano wa Afrika kupambana na kundi la Al Shabaab.
Wapiganaji hao wamekiri kufanya mashambulizi katika nchi hizo mbili na kutishia mashambulizi zaidi ikiwa Kenya haitaondoa wanajeshi wake kutoka Somalia.
Kundi la Al Shabaab liliwaua watu 76 katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwaka 2010.
Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...
Comments
Post a Comment