Rais wa Marekani Barrack Obama, amemualika waziri mkuu wa Ukraine, Arseniy Yatsenyuk, mjini Washington kwa mashauriano kuhusiana na mzozo unaokumba taifa lake.
Ikulu ya White House, imesema kuwa mkutano huo utakaofanyika siku ya Jumatano, utaangazia, mbinu za kutafuta suluhisho la amani, kuhusiana na operesheni za kijeshi zinazoendesha na jeshi la Urussi katika eneo la Crimea.
Waandishi wa habari wanasema kuwa mualiko huo ni ni ishara thabiti kuwa Marekani inaunga mkono utawala wa mpito wa Kiev.
Wakati huo huo, jamii ya kimataifa inaendelea kuishinikiza utawala wa Moscow, kuondoa wanajeshi wake katika eneo la Crimea.
Chansella wa Ujerumani, Angela Merkel, amemueleza rais wa Urussi, Vladimir Putin, kutilia maanani kuwa kura ya maoni kuhusu ikiwa eneo hilo la Crimea, litajiunga na Urussi inakiuka sheria na ni haramu.
Khodorkovsky apinga utawala wa Moscow
Huku hayo yakijiri, mfungwa wa zamani na mfanya biashara maarufu wa secta ya mafuta na mkoasoaji mkubwa wa rais Putin, Mikhail Khodorkovsky, anehutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika mji mkuu wa Ukraine Kiev.
Amewaambia maelfu ya watu waliofurika katika medani ya Uhuru kuwa serikali ya Urussi inawahadaa raia wake kwa kuwahusisha waandamanaji mjini Kiew na watu wanaopinga utawala wake na raia wake.
Mikutano kama hiyo imefanyika katika sehemu kadhaa za nchi hiyo.
Nyingi zikiwa za amani lakini mjini Sevastopol, katika eneo la Crimea, raia wa Ukraine wanaozungumza lugha ya Kirussi waliwapiga watu wanaounga mkono serikali ya Ukraine.
Televisheni zilizo na makao yao mjini Kiev zimezuiliwa kurusha matangazo katika eneo hilo la Crimea.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment