Skip to main content

KIGOGO WA WEMA AMHONGA GARI KAJALA

NI madai mazito! Kwamba, nyota wa muvi za Kibongo, Kajala Masanja amehongwa gari na mtu anayedaiwa kuwa ni kigogo wa Ikulu. Hii ndiyo habari ya mjini kwa sasa na Risasi Jumamosi limeifukunyua. Kwa mujibu wa habari hizo ambazo zipo hadi kwenye mitandao ya kijamii, hasa Instagram, Kajala alinunuliwa gari hilo aina ya Toyota Brevis lenye rangi ya bluu iliyoiva wiki mbili zilizopita mara baada ya kutua Bongo akitokea nchini China ambako alikwenda kwa mambo yake binafsi. TAARIFA ZINAVYODAI Wasambaza taarifa hao walidai kuwa, kigogo huyo wa Ikulu ni yule Clement ambaye amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi wa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu. “Mmeisikia hii? Kajala amenunuliwa gari na Kile (Clement), lina thamani ya shilingi milioni kumi na moja, Wema alie tu nakwambia. We ukisema cha nini wenzako wanajiuliza watakipata lini? “Kwanza mnajua kama bifu la Wema na Kajala lilitokana na Clement? Alipoachana na Wema akatua kwa msichana anaitwa Naima, lakini akaona bado akaenda hadi kwa Kajala. Wema alipogundua ndiyo akamnunia na kuanza ushoga na Aunt Ezekiel,” msambaza habari za mjini mmoja aliliambia Risasi Jumamosi juzi. Akaendelea: “Unajua nini? Naamini Wema alimwacha yule bwana na akurudi kwa Diamond baada ya kuona mambo yake siyo mazuri, lakini sasa jamaa (kigogo wa Ikulu) mambo ni safi kwa hiyo anataka kumwoneshea Wema ndiyo maana ameamua kumnunulia gari Kajala baada ya kuwa naye.” RISASI LALISAKA MITAANI Baada ya kuzinyaka habari hizo za kimjini, timu ya waandishi wa Risasi Jumamosi, Jumatano iliyopita iliingia mitaani kulisaka gari hilo hasa baada ya Kajala kutopokea simu. Awali, mtoa habari mmoja alisema Kajala yupo na gari hilo Kinondoni kwa Manyanya, lakini alipofuatwa hapo hakuonekana. Habari zikapatikana kwamba, alikuwa kwenye Mgahawa wa Steers uliopo jengo la Millennium Tower, lakini pia alipofuatwa eneo hilo hakuonekana. ALHAMISI SAA 9:06 ALASIRI Juzi, saa 9:06 alasiri, Kajala alipigiwa simu ambapo alipokea na mahojiano yakawa hivi: Risasi: Mambo Kajala? Kajala: Poa tu, mambo? Risasi: Mambo poa. Eti, namba za gari lako Toyota Brevis ni ngapi? Kajala: Mh! Yaani hata mimi mwenyewe sizijui, sijazishika kabisa. Risasi: Sasa, kuna habari kwamba hilo gari umenunuliwa na Clement, yule aliyekuwa na Wema zamani. Kuna ukweli wowote? Kajala: Mh! Hizo habari si za kweli. Wapo watu wanajiita Team Wema ndiyo wameamua kunipakazia hivyo, wameandika hadi kwenye Instagram, lakini siyo kweli kabisa. “Mimi nimelinunua hili gari kwa mtu. Aliniuzia kwa shilingi milioni kumi na moja (11,000,000). Sijahongwa wala sijanunuliwa. Kuna watu wanataka kunichafua tu. KUHUSU USHOGA WAO KUFA Kuhusu kufa kwa ushoga wao, awali Kajala hakutaka kulizungumzia suala hilo lakini alipobanwa alidai hana tatizo na Wema na kwamba kwa sasa yuko bize kutengeneza filamu zake. WEMA AKWEPA SIMU Kwa upande wake, Wema alipopigiwa simu hakupokea lakini siku za nyuma aliwahi kuanika kwamba haamini kama Kajala anaweza kutembea na Clement. Hapo ni wakati ule wakiwa mashoga. TUJIKUMBUSHE Katika gazeti la Ijumaa, Machi 21, mwaka huu ukurasa wa mbele kulikuwa na habari ndogo yenye kichwa; WEMA, KAJALA KIMENUKA! Katika habari hiyo, ilidaiwa kuwa, wawili hao si mashoga tena huku sababu mbalimbali zikianikwa. Ilidaiwa kuwa, kisa kilianzia kwenye saluni moja Kinondoni, Dar ambapo Kajala alifika akiendesha baiskeli iliyosababisha kuloa jasho sehemu kubwa ya mwili. Chanzo kilisema, Wema alipomuona Kajala alitaka kumkumbatia lakini Kajala alimkwepa kwa sababu alikuwa na jasho jambo lililomfedhehesha Wema na kununa. “Alichokifanya Wema, alimrushia Kajala maneno makali akimhoji kwa nini alimfanyia hivyo wakati hawana tatizo lolote kati yao,” kilidai chanzo. Siku nyingine ilidaiwa kwamba Kajala alikwenda nyumbani kwa Wema, Kijitonyama kwa lengo la kumchukua waende location (sehemu ya kurekodia sinema), lakini alipofika aliambiwa ‘bimkubwa’ huyo alilala na Diamond hawezi kuamshwa. Chanzo hicho kilisema Kajala aliwasiliana na Wema kwa njia ya simu ya mkononi akamwambia asubiri lakini alikaa kwa muda mrefu bila mafanikio hivyo hawakwenda kushuti siku hiyo. Chanzo hicho kilidai pia kwamba ushosti wa wawili hao ulianza kupepesuka muda mrefu lakini uzi wa mwisho umekuja kukatwa na Diamond mara baada ya kurudiana na Wema. GPL

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD  

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

LIST OF APPLICANTS SELECTED TO JOIN THE NATIONAL INSTITUTE OF TRANSPORT (NIT) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

To access the names of selected undergraduates click  HERE

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

DEADMEN SPEAKS: A POEM

Image generated with OpenArt AI tool It has been longtime since I published my poems on this platform, today I'm humbly inviting you to our section of poems. As you enjoy reciting this creativity, please don't forget to leave your comment after this post or writing via my contacts after this poem. Poem: Deadmen Speaks Poet: Venance Gilbert Composition: July 30, 2023 DEADMEN SPEAKS: A POEM BY VENANCE GILBERT I heard deadmen tells no tale but these ones do They are burdened with a lots Weak folks who talks nothing just talking in mind in the streets I say so because one of them is me I speak for deadmen. Six years with no stable duties to perform while responsibilities have taken-off This week this job next week none and I have to survive regardless But how without money How can I count money without job? I speak for deadmen. While I'm enjoying my jobless survival Executive wants to collect from my pocket I have to pay tariff to buy light tariff to withdraw my hard-earned sav...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

NExT-GPT: MFUMO WA LUGHA WA AKILI BANDIA UNAOKUPA MAJIBU KWA MAANDISHI, PICHA, SAUTI NA PICHA MJONGEO

Picha hii imetengenezwa kwa Akili Bandia na Decrypt. Katika uwanda mpana wa teknolojia unaotawaliwa na makampuni makubwa kama OpenAI na Google, NExT-GPT ambao ni mfumo huria wa lugha pana ya Akili Bandia (AI) [Large Language M odel (LLM)] unaweza kuwa na kile kinachohitajika ili kushindana na miamba hii miwili katika teknolojia. ChatGPT imeusisimua ulimwengu kwa uwezo wake wa kuelewa maswali katika lugha asilia na kutoa majibu kama ya binadamu. Lakini wakati Akili Bandia inaendelea kusonga mbele kwa kasi ya umeme, watu wametaka kuwepo na maendeleo zaidi. Zama za maandishi pekee zimekwisha sasa mifumo ya lugha ya Akili Bandia imeanza kuwa mingi kuleta ushindani. NExT-GPT imetengenezwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha taifa cha Singapore (NUS) na Chuo Kikuu cha Tsinghua. Inaweza kuchakata na kutoa majibu kwa kuchanganya maandishi, picha, sauti na picha mjongeo (video). Hii inaruhusu majibizano ya asili zaidi kuliko miundo ya maandishi pekee kama ilivyo kwenye ChatGPT. T...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...