MKAZI wa Kijiji cha Ikola katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi , Richard Clavery ( 34 ) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma ya kufukua kaburi la mwanamke, aliyekufa na kuzikwa kaburini humo.
Mtu huyo anatuhumiwa kukutwa na waombolezaji, akiwa amevua nguo zake zote na kuzitundika juu ya msalaba, uliosimikwa kaburini hapo.
Mwendesha Mashitaka, Godfrey Luzabila alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Ntengwa, Februari 25 mwaka huu kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Februari 18 mwaka huu saa nne usiku nyumbani kwa dada wa marehemu, Lenada Sakafu katika kijiji cha Ikola .
Luzabila alidai usiku wa tukio hilo, mtuhumiwa alifika nyumbani kwa Lenada Sakafu na kufukua maiti ya mdogo wa Lenada, Tabu Omera aliyekuwa amezikwa kaburini siku tatu kabla ya tukio hilo.
Kaburi alimozikwa marehemu, lilikuwa katika eneo la nyumba ya Lenada. Alidai usiku huo, Lenada akiwa nyumbani hapo pamoja na waombolezaji, wakiwemo majirani na ndugu, ghafla alitokea mtoto wa Lenada, aitwaye Brandina ambaye aliwaeleza kuwa ameona mtu nje ya nyumba yao akifukua kaburi la Tabu.
Waombolezaji hao papo hapo walitoka nje na kumkuta Clavery akifukua kaburi hilo, huku akiwa amevua nguo zake zote na kuzitundika juu ya msalaba uliosimikwa kaburini hapo.
Walipomsemesha mtuhumiwa huyo, alijifanya amepandisha majini na kujaribu kutoroka. Mtuhumiwa alikana shitaka hilo. Hakimu Ntengwa alilazimika kuahirisha shauri hilo hadi Machi 6 , mwaka huu litakapotajwa tena.
Hakimu aliamuru mshtakiwa arejeshwe rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana, ambapo alitakiwa adhaminiwe na mtu mmoja kwa kiasi cha Sh milioni moja .
Chanzo: Habari Leo
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment