UGANDA YATOA TAHADHARI KUHUSU AL SHABAAB

Uganda imetoa tahadhari kwamba kundi la wanamgambo la Al Shabaab linapanga kutumia malori ya mafuta kama mabomu katika mahambulizi yao. Taarifa hii inakuja siku moja baada ya polisi kuwakamata washukiwa wawili wa ugaidi waliokuwa na mabomu wakinuia kutekeleza mashambulizi mjini Mombasa. Mkuu wa polisi wa Uganda,Kale Kayihura, amesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba idara ya polisi na ujasusi zina taarifa za kuthibitishwa kuwa kundi la Al-Shabaab linapanga kulipua malori ya mafuta nchini Uganda na kusababisha uharibifu mkubwa. Ameshauri wananchi kuwa waangalifu na waweze kutoa taarifa zozote kwa polisi. Uganda na Kenya ziko na wanajeshi wake nchini Somalia kusaidia wanajeshi wa Somalia na wale wa Muungano wa Afrika kupambana na kundi la Al Shabaab. Wapiganaji hao wamekiri kufanya mashambulizi katika nchi hizo mbili na kutishia mashambulizi zaidi ikiwa Kenya haitaondoa wanajeshi wake kutoka Somalia. Kundi la Al Shabaab liliwaua watu 76 katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwaka 2010.

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI