WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

10. YUSUF MANJI

Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini.

9. FIDA RASHID

Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine.

8. GHALIB SAID MOHAMMED

Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha na uuzaji wa bidhaa za rejareja, usafirishaji wa vifaa na bidhaa, huduma za kifedha, vyombo vya habari na mengine mengi. Vyanzo vyote hivi vinamfanya kua miongoni mwa matajiri wakubwa nchini. Kama mjasiriamali aliamua kujihusisha zaidi na mazao ya kilimo pamoja na baba yake jambo ambalo limewafanya kufikia walipo kwa sasa.

7. SUBASH PATEL

Patel ni mwanachama wa Taasisi ya Wahandisi wa Umeme na ana ubia na kampuni ya MMI Steels Resource Limited na Nyaza Road Works. Katika kipindi cha miaka 20 amefanikiwa kupanua biashara zake mpaka kufikia kuwa na kampuni inayoitwa Motsun Group. Kampuni hii imegawanyika katika makampuni mengine 11 ambazo zinahusika na bidhaa za chakula, madini, majengo na kusaidia makampuni mengine kitaalamu.

6. SHEKHAR KANABAR

Shekhar ni meneja katika kampuni ya Synarge Group. Hii ni kampuni inayohusika na bidhaa za magari. Kampuni hii pia inahusika na utengenezaji wa madini ya risasi. Licha ya kwamba kampuni hii ni mali ya familia, Shekhar anabainishwa kuwa miongoni mwa matajiri nchini kutokana na uongozi wake mzuri katika kampuni hiyo. Kampuni hii pia inahusika na usambazaji wa spea za magari nchini. Huwezi kuzungumzia Teknolojia hii ya magari bila kumzungumzia Shekhar. Synarge imekua ikifanya vema katika mauzo ya bidhaa za magari nchini.

5. ALLY AWADH

Awadh ni miongoni mwa watu wenye akili ya biashara. Amefanya uwekezaji katika sekta za mafuta na gesi, ni muwekezaji muhimu sana katika sekta hizi. Alifanya kazi kwa juhudi sana ili apewe kibali na serikali na baadaye alifanikiwa katika hilo na sasa ana kampuni yake ya Lake Oil Group inayohusika na kuingiza pamoja na kusambaza mafuta ya petroli na gesi nchini. Biashara ya mafuta inatajirisha kwa haraka sana lakini kwa Awadh haikua hivyo, amepitia changamoto nyingi pamoja na magumu mengi mpaka hapo alipofikia.

4. REGINALD MENGI

Mengi ni mmiliki na mkuu wa kampuni kubwa ya habari nchini IPP Media Group. Kampuni hii ina jumla ya vituo vya redio 11, vituo vya televisheni, magazeti na huduma za mtandao (Internet). Mengi pia ni mmiliki wa kampuni ya Kilimanjaro Spring Water na Bonite Bottlers. Ndoto yake na mapenzi katika tasnia ya habari vimemfanya kutimiza malengo yake ya kutangaza na kufikisha habari kwa Watanzania. Anamiliki utajiri unaokadiriwa kuwa dola milioni 560.

3. SAID SALIM BAKHRESA

Bakhresa aliacha masomo ya shule ya sekondari akiwa na umri wa miaka 14. Kwa kipindi hicho alikua akifanya biashara ya kuuza viazi na akafungua mgahawa wa kuuza chakula na kisha akafungua mashine ya kusaga nafaka. Bakhresa ameijenga biashara yake kwa muda wa miaka 30 iliyopita mpaka kufikia leo, pia ni miongoni mwa matajiri wakubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki. Kampuni yake ya Bakhresa Group of Companies ni maarufu kwa uzalishaji wa bidhaa za chakula, mafuta ya petroli, usafirishaji ndani ya bahari ya Hindi na usagaji wa nafaka. Pia ni mmiliki wa king'amuzi cha Azam TV ambacho kinatoa huduma kwa malipo katika ukanda wa Afrika Mashariki. Akiwa ameajiri zaidi ya watu 3000 katika ukanda huu wa Afrika Mashariki, akiwa na matawi ya kibiashara nchini Msumbiji, Malawi na Uganda, Bakhresa anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia dola milioni 650 za Marekani. Bakhresa amekuwa akitoa msaada wa kifedha kwa watu wenye uhitaji nchini.

2. ROSTAM AZIZ

Rostam anashikiria rekodi ya kuwa bilionea wa mwanzo nchini Tanzania. Anamiliki kampuni ya madini inayotwa Caspian Mining, kampuni hii inatoa huduma za kitaalamu kwa makampuni makubwa ya madini nchini kama vile Barrick Mining na BHP Billiton. Alinunua 17.2% ya hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania mwaka 2014. Anamiliki mali zisizohamishika nchini Tanzania, Lebanon, Dubai na Oman. Pia ni mdau mkubwa wa bandari ya Dar es Salaam. Utajiri wake unakadiriwa kuwa dola bilioni 1 za Marekani. Alikua ndiye bilionea wa kwanza nchini mpaka pale MO Dewji alipochukua nafasi hii. Ndiye tajiri wa kwanza kuwahi kufikia kada hii ya matajiri bilionea kutoka Tanzania.


1. MOHAMMED DEWJI

MO Dewji ni miongoni mwa matajari wenye umri wa miaka 40 barani Afrika. Anamiliki 75% ya hisa zote katika kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd (METL) ambayo inamiliki viwanda vingi nchini. Baada kupata umiliki wa viwanda vya nguo na mimea ya mafuta kutoka serikali ya Uganda utajiri wake ukaanza kukua kwa kasi. Ana utajiri uanaokadiriwa kufikia dola bilioni 1.3 za Marekani, hii inamfanya kuwa tajiri namba 1 kwa sasa nchini. MO alitajwa na Forbes kuwa tajiri namba 1 nchini mwanzoni mwa mwaka huu na bado ameendelea kushikilia namba hiyo. 


Chanzo: Forbes Raking

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

KUZALIWA 

Celebrity wetu wa leo ni Shania Twain. Jina lake la kuzaliwa ni Eilleen Regina Edwards lakini umaarufu wake umetokana na jina lilizoeleka la Shania Twain. Wengine wanamuita Malkia wa Muziki wa Country.  Alizaliwa mnamo Agosti 28, 1965 leo anatimiza miaka 53 ya kuwepo duniani. Alizaliwa huko Windsor, Ontario, Canada akiwa ni mmoja kati ya mabinti 3 wa Clarence na Sharon (Morison) Edwards. Yeye ndiye mkubwa. Alipokua na miaka 6 mama yake aliolewa tena na Jerry Twain ambaye alimchukua kama mwanaye. Alianza kuimba katika vilabu vya pombe na alipokua na miaka 13 alionekana katika The Tommy Hunter Show. Alipokua na umri wa miaka 22 wazazi wake waliuawa katika ajali na hivyo akaacha sanaa muziki ili awalee wadogo zake Mark na Darryl pamoja na dada zake wawili aliozaliwa nao kwa baba yake na mama yake mzazi. Mwaka 1991 alibadilisha jina lake alilopewa na wazazi wake na kujiita Shania Twain na hapo ndipo jina hili lilipokua.  Mwaka huo huo pia alisaini mkataba na lebo ya muziki ya Mercury Nashville.
Shania siku za hivi Karibuni.


KUOLEWA

Shania amewahi kufunga ndoa mbili ambapo ndoa ya kwanza alifunga na Robert John Lange Desemba 28, 1993 na ilidumu hadi Juni 9, 2010. Katika ndoa hii walifanikiwa kupata mtoto 1 kabla hawajaachana. Baadaye January 1, 2011 aliolewa na Frederic Nicolas Thiebaud ambaye yuko naye mpaka sasa. Hawajabahatika kupata mtoto. 

TUZO


Shania amewahi kushinda tuzo kadhaa na kutajwa katika nyingine:

Mwaka 1996 alitajwa katika tuzo za Grammy kama msanii bora chipukizi lakini hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo.


Mwaka 1997 aliteuliwa kuwania tuzo za Gemini katika kipengele cha mtumbuizaji bora katika vipindi mbalimbali vya television, huku pia hakufanikiwa kutwaa tuzo.

Mwaka 1998 aliteuliwa kuwania tuzo za MTV kama Video Bora ya Msanii wa Kike: You're Still the One. Huku pia hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo. Mwaka huu alishinda tuzo ya Grammy na wimbo wake wa From this Moment on.

Mwaka 1999 aliteuliwa kuwania tuzo ya Grammy kama Wimbo wa Mwaka: You're Still the One, pia hakufanikiwa kupata tuzo hiyo. 

Mwaka 2004 alifanikiwa kutwaa tuzo ya Bambi katika kipengele cha Pop Kimataifa. 

Mwaka 2005 Grammy walimchagua katika vipengele viwili; mtumbuizaji bora wa kike wa muziki wa country na kolabo bora ya country. Bado hakufanikiwa pia kutwaa tuzo. 

Mwaka 2011 alitwaa tuzo kama Nyota wa tuzo za Walk of Fame. 
Shania Twain katika video ya For evre and for always. 

ALBUM ZAKE

Shania Twain (1993)
The Woman In Me (1995)
Come Over (1998)
Up (2003)
Now (2017)

MENGINE KUHUSU SHANIA TWAIN

Anakula mboga za majani na alipendekezwa kua na mvuto kutokana na hili.

Mwaka 1995 aliorodheshwa kama Mtu mwenye majibu Halisi anapoulizwa maswali katika jarida la People Weekly.

Amewahi kukaa kwenye namba za juu za muziki duniani kwa wimbo wake You're Still the One ambayo ilishika namba 1 kwenye chati ya Billboard mara 7. Pia alishika namba 2 katika chati za Hot 100 kwa wimbo huo mwaka 1998.

Wimbo wake "Love Gets Me Everytime" ulikua ni wimbo ulioshika nafasi ya juu zaidi ya Billboard kwa wiki 5 katika nyimbo za country tangu wimbo wa mwisho wa Dolly Parton "Here You Come Again" uliposhika nafasi hiyo mwaka 1997.

Mwaka 1999 alitajwa kama mtumbuizaji bora wa muziki wa country na mwaka huo huo CMA walimtuza tuzo ya mwaka ya mafanikio katika muziki huo.

Mwaka 1999 aliuza nakala milioni 19 za albam yake ya Come Over nchini Marekani peke yake.

Mwaka 2003 aliwahi kushinda tuzo ya Juno ka Chaguo la Mashabiki.

Album yake ya Come Over (mauzo na matamasha) viliingiza dola za Marekani milioni 40 nchini Australia pekee. Hii inaifanya kuwa miongoni mwa album zilizowahi kushika chati za juu za muda wote nchini humo.

Alishika namba 39 katika orodha ya Jarida la Maxim kama mwanamke mwenye mvuto katika wanawake 100 waliotajwa katika orodha hiyo ya mwaka 2005.

Album yake ya Up (2002) iliuza nakala milioni 2 nchini Marekani ndani ya mwezi 1 tangu ilipowekwa sokoni.

Alipokua mdogo alikua na aibu na alikua Tom boy.

Amekua katika familia maskini ambayo chakula tu ilikua ni tabu. Shania alikua akienda shule bila kula kutokana na hali ya maisha kifedha nyumbani kwao.

Anapenda kushinda nyumbani na kupika. 
Anaamini kwamba yeye ni kama watu wengine.

Ni miongoni mwa wasanii wa 4 kutoka nchini Canada waliowahi kushika namba za juu katika chati ya Billboard tangu kuanzishwa kwake mwaka 1944. Wengine kutoka Canada ni Hank Snow, Anne Murray na Terry Klark.

Aliwahi kusema kwamba anapendezwa na majukumu wanayofanya wanaume katika maisha ya kila siku.

Shania anawasema kuwa anasikitika siku zote kwa kua ndoa yake ya awali alivunjika.

Anao wafuasi 863K katika mtandao wa Instagram. Katika mtandao wa Twitter anao wafuasi 901K. Katika mtandao wa Facebook anao wafuasi zaidi ya milioni 5. Ukurasa wake wa YouTube umetazamwa na watu bilioni 1.2 huku akiwa na subscribers zaidi ya bilioni 1.1.

Haya ni machache kati ya mengi niliyokuandalia kuhusu mwanamuziki Shania Twain. Kama una maoni usisite kuniandikia kupitia barua pepe: venancegilbert@gmail.com ama ujumbe Whatsapp 0712586027. Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG na karibu tena kwa mengine mengi. 

LEO AGOSTI 6 KATIKA HISTORIA

Leo ni Agosti 6, 2018 ikiwa ni siku ya 218 katika mwaka 2018. Zimesalia siku 147 katika mwaka huu. Nakukaribisha tena katika muendelezo ya Leo Katika Historia. Kwa leo nimekuletea matukio kadhaa yaliyopata kutokea katika historia ya dunia, na tuanze kuyahesabu matukio hayo:

MATUKIO

1787 - Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Marekani ilianza kujadiliwa huko Philadelphia.

1890 - Hukumu ya kuuawa kwa kiti cha umeme ilianza kutekelezwa katika gereza la Auburn huko New York, Marekani ambapo William Kemmier alihukumiwa kifo katika kiti cha umeme kwa kumuua mpenzi wake Matilda Ziegler kwa shoka. Adhabu hii ya kifo ilipendekezwa mwaka 1881 na Dk. Albert Southwick baada kushuhudia mlevi akiuawa kwa shoti ya umeme. Katika kutekeleza adhabu hii zilitumika volti 700 za umeme na katika sekunde 17 umeme ulifeli kabla Kemmier hajafariki na baadaye waliongeza umeme hadi volti 1,030 ndani ya dakika 2 na ndipo Kemmier alifariki.
Kiti cha Umeme kilichotumika kutekeleza adhabu ya kifo kwa Kemmier.

1904 - Jeshi la Japan lililokua nchini Korea lilizunguka Jeshi la Urusi ambalo lilizidiwa nguvu na kuamua kurudi nyuma katika jimbo la Manchuria.

1945 - Ndege ya Marekani B-29 ikiongozwa na rubani Paul Tibbets ilidondosha bomu la nyuklia katika jimbo la Hiroshima. Bomu hilo liliua watu waliofikia 80,000 na pia watu 35,000 walijeruhiwa na inakadiriwa kua baadaye mwishoni mwa mwaka huo watu wengine 60,000 walifariki kwa madhara ya bomu hilo. Kulikua na majengo 90,000 katika mji wa Hiroshima lakini baada ya bomu kulipuka yalibaki majengo 28,000 tu, madakatari walikua 200 lakini waliosalia walikua 20 tu, manesi walikua 1,754 lakini walisalia 150 tu.
Ndege aina ya B-29 iliyodondosha bomu la nyuklia huko Hiroshima.
Baada ya bomu kudondoshwa hali ilikua hivi. 

Hivi ndiyo Hiroshima ilivyojengwa kwa sasa. 

1962 - Jamaica ilipata Uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza baada ya kutawaliwa kwa miaka 300.

1973 - Mwanamuziki wa Marekani Steve Wonder alipata ajali ya gari iliyopelekea kupoteza fahamu kwa siku 4.

1993 - Papa John Paul II alichapisha makala iliyohusu Umuhimu wa Kanisa Katoliki katika kufundisha maadili.

KUZALIWA

1809 - Mtunzi wa mashairi wa Uingereza Alfred Lord Tennyson alizaliwa. Moja kati ya mashairi yake maarufu ni "The Charge of the Light Bregade" la mwaka 1850.

1881 - Alexander Flemming mgunduzi wa dawa aina ya Penicillin mwaka 1928 alizaliwa.

1911 - Muigizaji na mchekeshaji wa Marekani Lucille Ball alizaliwa. 

1934 - Piers Anthony Dillingham Jacob mwandishi wa riwaya za kisayansi na matukio ya ajabu na ya kusimumua alizaliwa. 

TAZAMA HAPA MAGOLI 10 BORA YA KOMBE LA DUNIA 2018

Michuano ya Kombe la Dunia tayari imemalizika nchini Urusi jana Julai 15, 2018 ambapo Ufaransa ilii chapa 4 - 2 Croatia. Leo nakupa nafasi ya kuangalia magoli 10 bora yaliyofungwa katika michuano hii, magoli haya ni kama ifuatavyo:
10: Cristiano Ronaldo, Portugal vs Spain
09: Toni Kroos, Germany vs Sweden
08: Lionel Messi, Argentina vs Nigeria
07: Ricardo Quaresma, Portugal vs IR Iran
06: Nacho, Spain vs Portugal
05: Aleksandar Kolarov, Serbia vs Costa Rica
04: Angel Di Maria, Argentina vs France
03: Philippe Coutinho, Brazil vs Switzerland
02. Benjamin Pavard, France vs Argentina
01. Denis Cheryshev, Russia vs Croatia.


Unaweza kutazama magoli hayo katika video hii hapa chini:


Magoli haya ni kwa hisani ya Kwesé Sports ambao walikua ni washirika rasmi wa FIFA wa kuonesha michuano hii ya Kombe la Dunia 2018.

HAYA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA & UALIMU 2018

Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya Kidato cha Sita 2018 na yale ya wanafunzi wa Ualimu.


Kuangalia matokeo hayo BOFYA HAPA

FRIENDSHIP QUOTES OF THE DAY MAY 26, 2018


Today I invite you to read these quotes of the day. Enjoy your day.

1. One of the most beautiful qualities of true friendship is to understand and to be understood. ~Lucius Annaeus Seneca.


2. Walking with a friend in the dark is better than walking alone in the light. ~Helen Keller.

3. There is nothing on this earth more to be prized than true friendship. ~Thomas Aquinas.


4. My best friend is the one who brings out the best in me. ~Henry Ford.

5. It is one of the blessings of old friends that you can afford to be stupid with them. ~Ralph Waldo Emerson.

6. The strong bond of friendship is not always a balanced equation; friendship is not always about giving and taking in equal shares. Instead, friendship is grounded in a feeling that you know exactly who will be there for you when you need something, no matter what or when. ~Simon Sinek.

7. A friend is someone who gives you total freedom to be yourself. ~Jim Morrison.

8. Remember that the most valuable antiques are dear old friends. ~H. Jackson Brown, Jr.

9. A true friend is one who overlooks your failures and tolerates your success! ~Doug Larson.

10. Be true to yourself, help others, make each day your masterpiece, make friendship a fine art, drink deeply from good books - especially the Bible, build a shelter against a rainy day, give thanks for your blessings and pray for guidance every day. ~John Wooden.

11. Things are never quite as scary when you've got a best friend. ~Bill Watterson.

12. A single rose can be my garden... a single friend, my world. ~Leo Buscaglia.

13. In the sweetness of friendship let there be laughter, and sharing of pleasures. For in the dew of little things the heart finds its morning and is refreshed. ~Khalil Gibran.

14. My best friend is the man who in wishing me well wishes it for my sake. ~Aristotle.

15. True friendship multiplies the good in life and divides its evils. Strive to have friends, for life without friends is like life on a desert island... to find one real friend in a lifetime is good fortune; to keep him is a blessing. ~Baltasar Gracian.

16. Depth of friendship does not depend on length of acquaintance. ~Rabindranath Tagore.

17. I define friendship as a bond that transcends all barriers. When you are ready to expect anything and everything from friends, good, bad or ugly... that's what I call true friendship. ~Harbhajan Singh.

18. The language of friendship is not words but meanings. ~Henry David Thoreau.

19. I have learned that friendship isn't about who you've known the longest, it's about who came and never left your side. ~Yolanda Hadid.

20. The two most misused words in the entire English vocabulary are love and friendship. A true friend would die for you, so when you start trying to count them on one hand, you don't need any fingers. ~Larry Flynt.

21. True happiness arises, in the first place, from the enjoyment of one's self, and in the next, from the friendship and conversation of a few select companions. ~Joseph Addison.

22. A friend is what the heart needs all the time. ~Henry Van Dyke.

23. There is a magnet in your heart that will attract true friends. That magnet is unselfishness, thinking of others first; when you learn to live for others, they will live for you. ~Paramahansa Yogananda.

24. False friendship, like the ivy, decays and ruins the walls it embraces; but true friendship gives new life and animation to the object it supports. ~Richard Burton.

25. Of all the things which wisdom provides to make us entirely happy, much the greatest is the possession of friendship. ~Epicurus.

WAFUNGAJI BORA NA WALIOCHEZA MECHI NYINGI KATIKA KOMBE LA DUNIA 1930-2014

WAFUNGAJI 5 WA MUDA WOTE

1. Miroslav Klose - Ujerumani

Klose wakati wa droo ya kombe la dunia mwaka jana 2017.
Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29.  Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002. Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil.
Klose wakati wa mechi ya robo fainali kati ya Ujerumani na Ufaransa katika dimba la Marakana Rio de Jeneiro Julai 4, 2014.


2. Ronaldo de Lima - Brazil

Ronaldo de Lima alipokabidhiwa tuzo ya Hall of Fame nchini Italia mwaka 2016
Amezaliwa Septemba 22, 1976. Amecheza mechi 45; 19 za kombe la dunia, 15 za kufuzu kombe la dunia, 5 za kombe la mabara na 6 za Olimpiki. Katika mechi hizi alifunga jumla ya magoli 34; 15 ya kombe la dunia, 10 ya kufuzu michuano hii, 4 ya kombe la mabara na 5 ya Olimpiki. Akiwa katika timu ya Brazil walishinda mechi 31, suluhu 8 na kufungwa mechi 6. Umaarufu wake ulianza kuonekana katika michuano ya Olympic mwaka 1996 iliyofanyika Atlanta dhidi ya Japan. Brazil iliifunga Japan 1-0. Amewahi kupewa kadi za njano mara 4 tu katika michuano yote. Alipokuwa Brazil walitwaa kombe la dunia mwaka 1994 na 2002. Mwaka 2002 ndiye aliyekua mchezaji bora wa michuano ya kombe la dunia FIFA. Mwaka 1997 akiwa na timu yake walishinda kombe la dunia la mabara. Ronaldo amewahi kushinda tuzo ya mpira wa dhahabu ya Adidas kama mchezaji bora. Mwaka 2002 pia alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas. Amewahi kushinda tuzo ya Balloon d'Or ya Ufransa mwaka 1997 na 2002.
Ronaldo enzi za Brazil.


    3. Gerd Mueller - Ujerumani

    Mueller alipokua kocha wa Bayern Munich  II
    Alizaliwa Novemba 3, 1945. Amecheza mechi 19 na timu yake ya Ujerumani; 13 zikiwa za kombe la dunia na 6 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi hizo alizokuwepo walishinda mechi 16, suluhu 1 na kufungwa 2. Ana magoli 23; 14 yakiwa ya kombe la dunia la 9 yakiwa ya kufuzu michuano hiyo. Amewahi kupewa kadi za njano 2 tu katika michuano ya kombe la dunia. Mwaka 1970 alishinda tuzo mbili; kiatu cha dhahabu cha Adidas pamoja tuzo ya Ballon d'Or. Pia ni miongoni mwa waliokuwepo katika kikosi cha Ujerumani kilichotwaa kombe la dunia mwaka 1974.
    Gerd Mueller mwaka 1974 waliposhinda fainali ya kombe la dunia.

    4. Just Fontaine - Ufaransa

    Fountaine mwaka 2017
    Alizaliwa Agosti 18, 1933. Yeye alicheza 8 tu 6 zikiwa zakombe la dunia na 2 zikiwa za kufuzu michuano hiyo, katika mechi hizi alifunga magoli 16; katika hayo 13 yalikua ya kombe la dunia na 3 yalikuwa ya mechi za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza 6 walishinda na hawakusuluhu ila walipoteza nchi 2 tu. Alionekana katika kombe la dunia kwenye mechi ya kati ya Ufaransa na Luxembourg ambapo waliifunga nchi hiyo 8-0 na hapo nyota yake iling'aa. Hakuwahi kupewa kadi katika mechi zote alizocheza. Mwaka 1958 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas. Katika kipindi chote alichocheza hawakuwahi kushinda ubingwa. Ufaransa illitwaa ubingwa baadaye mwaka 1998. Fontaine aliwahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Morocco ambapo aliiongoza timu hiyo katika kufuzu kucheza kombe la dunia. Kama kocha timu yake ya Morocco ilicheza mechi 4. Mwaka 1982 Morocco ilicheza na Zambia na waliifunga 2-0.
    Fontaine mwaka 1958

    5. Pele (Edson Arantes do Nascimento) - Brazil

    Pele mwaka 2017
    Alizaliwa Oktoba 23, 1940. Alicheza mechi 20 ambapo 14 zilikuwa za kombe la dunia na 6 zikiwa za kufuzu kucheza kombe la dunia. Alifunga magoli 18 katika michuano hiyo 12 yakiwa ya kombe la dunia na 6 yakiwa katika hatua za kufuzu. Pele anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji pekee duniani aliyeshuhudia timu yake ya Brazil ikishinda kombe la dunia mara 3 (1958, 1962, 1970) akiwepo katika kikosi cha timu hiyo mara 3 zote. Mwaka 1958 alishinda tuzo ya Hyundai ya mchezaji mdogo wakati ule akiwa na miaka 18 tu. Mwaka 2007 Pele alishinda tuzo ya heshima ya Rais wa FIFA. Katika mechi hizo 20 alizocheza, 18 walishinda, 1 walisuluhu na 1 walifungwa.
    Pele katika enzi zake kwenye soka.


    WACHEZAJI 5 WALIOCHEZA MECHI NYINGI

    1. Luthar Matthaus - Ujerumani

    Matthaus kwa sasa yupo Sky Sport.
    Amezaliwa Machi 21, 1961. Amecheza mechi 36; 25 zikiwa za kombe la dunia, 8 zikiwa za kufuzu michuano hiyo na 3 zikiwa za kombe la mabara. Umaarufu wake ulitokana na mechi ya kombe la dunia 1982 na Chile ambapo waliichapa timu hiyo 4-1. Katika mechi zote 36 alishinda 22, alisuluhu 8 na kufungwa 6. Mwaka 1990 alishinda Ballon d'Or pamoja na kuchukua ubingwa wa dunia na timu yake ya Ujerumani. Mwaka 1991 alikuwa mchezaji bora wa mwaka. Alifunga magoli 10; 6 yakiwa ya kombe la dunia, 3 yakufuzu michuano hiyo na 1 ikiwa kombe la mabara. Amewahi kupewa kadi za njano mara 9. Pia amewahi kua kocha wa timu ya Croatia, kama kocha aliifunga Hungaria magoli 3-0.
    Lothar akibusu kombe la dunia waliposhinda mwaka 1990.

    2. Miroslav Klose - Ujerumani

    Klose akiwa na wanaye baada ya Ujerumani kutwaa kombe la dunia mwaka 2014 dhidi ya Ajentina.
    Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29. Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002. Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil.
    Klose katika kombe la dunia mwaka 2006.

    3. Paulo Maldini - Italia

    Maldin mwaka 2013.
    Alizaliwa Juni 26, 1968. Amecheza mechi 48; 23 zikiwa za kombe la dunia, 23 za kufuzu na 2 zikiwa za kombe la mabara. Alifunga magoli 3 tu katika mechi za kufuzu. Amewahi kupewa kadi za njano mara 3 tu. Katika mechi zote alizocheza 31 walishinda, 13 wakisuluhu na kupoteza 4. Mechi ya kombe la dunia mwaka 1990 wakati Italia ilipoifunga Austria 1-0 ilipelekea nyota yake kung'aa.
    Maldin mwaka 1998 katika robo fainalai ya kombe la dunia.

    4. Uwe Seeler - Ujerumani

    Seeler mwaka 2016
    Alizaliwa Novemba 5, 1936. Amecheza mechi 28; 21 zikiwa za kombe la dunia wakati 7 zikiwa za kufuzu. Amefunga magoli 23; 9 yakiwa ya kombe la dunia na 3 yakiwa ya kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza 19 walishinda, 5 walisuluhu na 4 walifungwa. Nyota ilianza kung'aa katika kombe la dunia 1958 wakati Ujerumani ilipoifunga 3- 1 Ajentina. Hakuwahi kupewa kadi.

    5. Diego Maradona - Ajentina

    Maradona.
    Alizaliwa Oktoba 30, 1960. Alicheza mechi 35; 21 zikiwa za kombe la dunia, 8 zikiwa za kufuzu kombe la dunia na 6 zikiwa za kombe la dunia chini ya miaka 20 (U-20). Maradona alifunga magoli 17; 8 yakiwa ya kombe la dunia, 3 ya kufuzu na 6 kombe la dunia U-20. Katika mechi alizocheza 23 walishinda, 6 walisuluhu na 6 walifungwa. Nyota ya Maradona iling'aa wakati wa michuano ya vijana nchini Japan mwaka 1979 wakati Ajentina ilipoifunga 5-0 Indonesia. Mwaka 1979 alishinda mpira wa dhahabu wa Adidas, FIFA U-20 pamoja na kombe hilo mwaka huo huo. Mwaka 1986 alishinda kiatu cha dhahabu pamoja na kushinda kombe la dunia. Maradona amewahi kuwa kocha wa timu ya taifa lake ambapo mechi 13 zilichelezwa akiwa kocha. Alishinda mechi 8 na kufungwa 5. Umaarufu wake kama kocha ulitokana katika mechi ya kirafiki dhidi ya Venezuela mwaka 2010 ambapo waliichapa timu hiyo 4-0.
    Maradona akinyanyua kombe la dunia mwaka 1986 dhidi ya Ujerumani.


    MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA MTANDAO WA FIFA.

    UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA YA 5G

    Logo rasmi ya teknolojia ya mtandao wa 5G.
    Katika teknolojia za mitandao ya simu iliyopita kulikua na suluhisho la matumizi ya sauti pekee katika mtandao wa 1G, sauti na jumbe za maneno katika mtandao wa 2G, kuliongezeka kufungua tovuti mbalimbali katika mtandao wa 3G na kuongezeka kwa kasi zaidi ya mtandao na kutazama video za moja kwa moja katika mtandao wa 4G. Mabadiliko kutoka 4G kwenda 5G yatasaidia si watumiaji wa mtandao tu bali pia wamiliki wa viwanda mbalimbali.

    Mabadiliko katika teknolojia ya simu na mtandao.

    Kwa teknolojia ya mtandao huu wa simu za mkononi kasi ya mtandao inatarajiwa kuwa mara 8 ya hii ya sasa mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2023 huku kukiwa na uhitaji wa teknolojia imara, viwango vikubwa vya data na wigo mpana wa matumizi ya mtandao huu tofauti na hii iliyopo sasa (4G). Vitumizi vipya kama vile 4K/8K vya kutazamia video mtandaoni moja kwa moja, uwezo wa mtandao ambao umeongezwa karibia na uhalisia pamoja matumizi ya data ambao kwa sasa yanachipukia kwa kasi, yote haya yatahitaji vipimo vikubwa vya data, uwezo wa hali ya juu, ulinzi pamoja na utulivu wa kusafirisha data katika mtandao. Haya yote ni miongoni mwa yatakayokuwa katika mtandao wa 5G. Mtandao huu utaleta fursa mpya kwa watu, jamii na biashara.

    Ericsson pamoja na washirika wake wamekuwa wakifanya kazi katika teknolojia ya mtandao wa 5G kwa miaka mingi sasa katika maabara za mtandao na katika miaka 2 iliyopita waliamua kuijaribu teknolojia hii kuiweka katika matumizi. Pia, tayari wameshaingia ubia wa kusaini mikataba ya mtandao huu wa 5G kwa awamu ya kwanza ambapo mpaka kufikia sasa kampuni 39 tu duniani zimesaini mkataba wa matumizi ya teknolojia hii.

    Kiwango cha teknolojia hii ya mtandao kimepelekea uwepo wa redio mpya ya mtandao wa 5G "5G New Radio" ambayo tayari imekamilika tangu Desemba mwaka jana 2017 na inatarajiwa kuanza kupatikana katikati mwa mwaka huu 2018. Mitandao ya kwanza ya kibiashara pamoja na vifaa vyenye teknolojia hii (simu, kompyuta, iPad, tablets n.k.) vya teknolojia hii vitakamilika  mwakani 2019 kwa mujibu wa Mpango wa Ushirikiano wa Mtandao wa Kizazi cha tatu "3GPP" lakini yote haya yataanza kutumika kuanzia 2020. Ericsson imekadiria idadi ya watumiaji wa teknolojia hii kwamba watafika bilioni 1 mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2023.

    UFAHAMU NA TAARIFA KUHUSU TEKNOLOJIA HII

    Mtandao huu utafanya mambo mengi sana na ndiyo sababu ukaitwa Mtandao wa Muunganiko wa Vitu (Internet of Things) utakuwa na mengi sana ya kufanya kupitia teknolojia hii. Haya ni baadhi ya mambo ambayo Ericsson inayataja kuwepo katika teknolojia hii:

    ULINZI 

    Vifaa vilivyounganishwa pamoja na vitumizi vitahitaji kuunganishwa katika mtandao ambao ni stahimilivu, wenye ulinzi na wenye uwezo wa kulinda siri na faragha za mtumiaji. Teknolojia hii imetengenezwa kwa kuyafanikisha haya.


    BIASHARA KWA NJIA YA MTANDAO ULIOIMARISHWA

    Modem za mtandao chini ya teknolojia hii zitakuwa na nguvu zaidi ili kuimarisha biashara za wateja. Tafiti zilizofanywa na Ericsson zinaonesha kwamba mabadiliko kuelekea 5G yanaweza kupunguza karibia mara 10 ya gharama ya mtandao kwa kila gigabaiti moja tofauti na ilivyo kwa mtandao wa sasa wa 4G.

    UFIKISHWAJI WA TEKNOLOJIA HII KWA NJIA YA MODEM KWANZA


    Ericsson wanadai kwamba jambo la kwanza litakuwa ni kuboresha modem za sasa ili ziendane na kasi ya 5G.

    MTANDAO HUU UTATEKA SOKO LA BIASHARA

    Ericsson wanadai kwamba mtandao huu utakuwa wa matumizi ya vitu kwa mfano vifaa vya kujiendesha venyewe kama vile magari. Wametaja fursa, changamoto pamoja mifano ya baadhi ya mambo yanayotokea katika usasa wa viwanda.

    VIWANDA VINAISUBIRIA TEKNOLOJIA HII

    Je ni kwa namna gani kampuni kubwa zitaitumia teknolojia hii katika biashara zao? Ericsson imewauliza wafanya maamuzi 900 katika viwanda 10 na ripoti hiyo ipo nitaizungumzia siku nyingine. 

    5G KWA VIWANDA

    Teknolojia hii itawawezesha wamiliki wa kampuni za simu za mikononi fursa ya kuwasaidia wamiliki wa viwanda kuwa viwanda vya kisasa na kuangalia faida za teknolojia hii kama vile utumiaji wa mitambo inayojiendesha (automation), akili bandia (artificial intelligence), ukweli thabiti (augmented reality) pamoja na mtandao wa muunganiko wa vitu (Internet of Things "IoT")

    FURSA KWA WATOA HUDUMA ZA AFYA

    Teknolojia hii itawasaidia watoa huduma za afya kwa urahisi zaidi kwa wateja wao. Hii itawezesha njia za mtandao kuwa kasi zaidi hivyo itawezesha hata kuwasiliana moja kwa moja kwa njia ya video bila mushkeri ya mtandao. Hii pia itawafanya watoa huduma kupanua huduma zao zaidi kuliko kusubiriana ofsini tu.

    MUHTASARI KUHUSU UTAYARI WA TEKNOLOJIA HII
    Ericsson wanadai kwamba utafiti mfupi uliofanywa mwaka jana 2017 unaonesha kwamba mtandao huu utakuwa na watumiaji bilioni 1 mpaka kufikia mwisho mwa mwaka 2023 kama nilivyosema hapo juu.


    KUONGEZA IDADI YA WATAZAMAJI WA MPIRA

    Watazamaji wa mpira wanaotumia simu hupenda kuangalia mpira bila kuwa na shida ya mtandao. Ericsson wanadai kwamba teknolojia hii ya 5G itamfanya mtazamaji kujihisi yuko uwanjani yani itakua kana kwamba anauzunguka uwanja wa mpira yeye mwenywe. Ongezeko la watu kuangalia mpira kwa njia ya mtandao utatokana na uimara wa mtandao ambao ulifanyiwa tafiti mwaka 2016 huko Rio de Jeneiro.


    MAJARIBIO YA TEKNOLOJIA YA MTANDAO WA 5G


    KOREA KUSINI

    Mwezi Februari mwaka huu 2018, Ericsson, Shirika la mawasiliano la Korea Kusini na Intel walifanya majaribio ya mtandao huu katikati ya jiji la Seoul ambapo kuna idadi ya watu milioni 25. Teknolojia ya 4K video ilijaribiwa ili kutoa picha kwa watumiaji kuona uwezo wake. Matumizi ya data yalifikia 900Mbps kwa upande wa kupakua (downloading) huku yale ya kupakia (uploding) yakifikia 600Mbps. Kwa kutumia bendi 28Ghz uunganishwaji wa mtandao ulikua imara kabisa licha ya kuwepo changamoto ya uenezi wa mtandao.

    ESTONIA

    Telia, Ericsson na Intel walifanya majaribio ya mtandao katika kampuni ya usafirishaji ya Tallink ambayo husafirisha watu na mizigo. Kila meli hubeba hadi kufikia watu 2,000. Mafanikio bado yalionekana kwa mtandao huu. Abiria waliweza kutumia mtandao huu safarini bila kuwepo na mushkeri ya aina yoyote ile.


    KASI MPYA YA 5G

    Ericsson wakishirikiana na SK Telecom na BMW Korea walitumia teknolojia hii ya 5G iliyoboreshwa kuangalia gari iliyounganishwa na mtandao huu kwa kuangalia mwendokasi wa gari iliyosafiri kilomita 170 kwa saa. Matumizi yalifikia uwezo wa kupakua hadi GB 3.6. Jaribio hili lilihusisha radio 4 tofauti za kusambaza mawasiliano. Pia, kulifanyika jaribio la kuhama kutoka radio moja ya mawasiliano kwenda nyingine na bado kasi ya mtandao ilifikia zaidi ya GB 1.5. Majaribio haya yote yalifanyika katika 28Ghz bendi.


    KAMPUNI ZILIZOINGIA UBIA NA ERICSSON

    Mpaka kufikia mwezi April mwaka huu 2018 ni kampuni 39 tu duniani ambazo zimeingia mkataba wa matumizi ya mtandao huu wa 5G kama jinsi inavyoonekana. Kwa bara la Afrika ni kampuni 2 tu za mawasiliano ambazo tayari zimesaini mkataba wa ubia na Ericsson. Kampuni hizo ni MTN ya Afrika Kusini na Etisalat ya nchini Misri. Unaweza kuziangalia nchi hizo kama jinsi kampuni zinavyoonekana kwenye ramani ya dunia akatika picha hii:

    MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA MTANDAO WA ERICSSON.