MABAKI YA NDEGE YA MISRI YAPATIKANA








Mamlaka ya Misri inasema mabaki ya ndege ya EgyptAir ambayo ilianguka katika bahari ya Mediteranian mwezi uliopita ikiwa imebeba abiria sitini na sita yameweza kubainika yalipo.
Katika maelezo yaliyotolewa na kamati husika ya uchunguzi wa ajali hiyo wanasema ,meli inayotafuta mabaki ya ndege ya EgyptAir imeweza kubaini maeneo kadhaa ambayo mabaki ya ndege ya A320 yapo na kutoa picha ya kwanza ya masalio hayo.

Kwa sasa kikosi hicho cha wakaguzi walioko melini watachora ramani wakionesha vielelezo vya mabaki ya ndege yalivyoeneo. Ndege hiyo iliyopotea baada ya kutoonekana kwenye rada wakati ikiwa inatokea Paris kuelekea Cairo. Huku ikiwa inadhaniwa kuwa lilishambuliwa na bomu.Lakini hakuna kikosi chochote cha kigaidi kilichodai kuhusika na kuangusha ndege hiyo.

Chanzo: BBC

MOVIE: X-MEN APOCALYPSE RELEASED TODAY

 

Release date: May 27, 2016

Director: Bryan Singer

Starring:James McAvoy
Jennifer Lawrence
Oscar Isaac
Michael Fassbender
Rose Byrne
Sophie Turner

Synopsis:

In this comic-book adventure set in the 1980s, the X-Men are forced to confront an ancient mutant called Apocalypse (Oscar Isaac). After the resurrected beast recruits a super-team to take over the world and destroy hunmanity, Professor X (James McAvoy) and his charges must come to the rescue for the fate of the planet. The film co-stars Michael Fassbender, Jennifer Lawrence and Olivia Munn.

OBAMA AZURU HIROSHIMA JAPAN

Obama akiweka shada ya maua Hiroshima.Obama amekuwa Rais wa kwanza wa Marekani aliyeko madarakani kuzuru eneo la mji wa Hiroshima ambalo Marekani ilishambulia kwa kutumia bomu la kwanza la atomiki mwaka 1945 na kuua takriban watu 140,000.

Baada ya kuweka shada ya maua katika bustani ya amani eneo la Hiroshima-Japan, rais Obama alitoa hotuba ya kumbukumbu ya mashambulizi hayo ya Hiroshima huku akisisitiza matumaini kuwa uhusiano kati ya Japan na Marekani utazidisha matumaini katika juhudi za kutupilia mbali matumizi ya silaha za atomiki.

Obama amekuwa rais wa kwanza wa Marekani aliyeko madarakani kuzuru eneo la mji wa Hiroshima ambalo Marekani ilishambulia kwa kutumia bomu la kwanza la atomiki mwaka 1945 na kuua takriban watu 140,000. Obama amefanya ziara hiyo ya kihistoria baada ya mkutano wa viongozi wa nchi saba tajiri kiviwanda duniani ambapo viongzo hao wamekubali kuimarisha uchumi wa dunia.


Upatanisho
Shambulizi la bomu la kwanza la atomiki eneo la Hiroshima mwaka 1945 na pia Nagasaki lilisababisha vifo maelfu ya watu papo hapo, na baadaye jumla ya watu 140,000 walifariki. Japo hakuomba msamaha jinsi Ikulu ya White House ilivyotangaza awali, Obama amesikitikia waliopoteza uhai wao miaka 71 iliyopita kufuatia mashambulizi hayo yaliyoifanya Japan kusalimu amri na hivyo vita vikuu vya pili vikakamalizika.

Waziri mkuu wa Japan Abe Shinzo ambaye ni mwenyeji wa Obama amesema, ziara ya Obama katika bustani ya Hiroshima inafungua ukurasa mpya wa upatanisho baina ya mataifa hayo mawili
Ziara ya Obama inajiri wakati viongozi wa mataifa saba tajiri kiviwanda wakikubaliana kuwa haja ya kuimarisha uchumi wa dunia inapaswa kupewa kipaumbele ya dharura. Viongozi hao pia wameonya kuwa huenda kukatokea athari kubwa ikiwa Uingereza itapiga kura ya kujiondoa katika Umoja wa Ulaya, katika kura ya maamuzi inayotarajiwa mwezi ujao. Mkutano huo wa siku mbili uliofanywa mji wa Ise-Shima Japan umekamilika.


Chanzo: Deutsche Welle (DW)

FURAHIA WIKENDI KWA KUANGALIA MUVI HIZI 5 KALI MPYA

Kill Zone 2 showtimes and tickets
JINA LA MUVI: KILL ZONE 2
STAR: TONY JAA (kutoka Ong Bak)
 After his true identity is exposed, undercover cop Kit (Wu Jing) is sent to a corrupt Thai prison by the gang he infiltrated, while his police unit erases all evidence that he was ever an officer. There, a guard named Chai (Tony Jaa) discovers that Kit is a bone-marrow match for his daughter, who desperately needs a transplant. The unlikely partners must find a way to secretly escape from the brutal prison and save Chai's daughter. Pou-Soi Cheang directed this martial-arts action thriller.





Last Days in the Desert showtimes and tickets
JINA LA MUVI: LAST DAYS IN THE DESERT

This biblical drama follows Jesus Christ (here referred to as "Yeshua" and played by Ewan McGregor) during the 40 days he spent fasting and wandering in the desert. He is approached by a demon (also McGregor) during his travels, who challenges him to help a troubled family living in the wilderness. Ciarán Hinds, Tye Sheridan, and Ayelet Zurer co-star as the members of the family. Written and directed by Rodrigo García





Money Monster showtimes and tickets
 JINA LA MUVI: MONEY MONSTER
TV stock-market guru Lee Gates (George Clooney) and his producer Patty (Julia Roberts) are held hostage during a live broadcast by a man (Jack O'Connell) who lost his life's savings due to Gates' financial advice. The captor soon forces the pair to probe a conspiracy involving the global economy. Jodie Foster directed this thriller.





A Monster With a Thousand Heads showtimes and tickets
JINA LA MUVI: A MONSTER WITH THOUSAND HEADS
 A woman (Jana Raluy) grows increasingly frustrated as she tries to navigate the bureaucracy of a health-care company in order to obtain cancer treatment for her terminally ill husband. She eventually holds a doctor hostage at gunpoint when she's pushed too far, sparking a crisis that threatens to spiral out of control. Hugo Albores and Sebastián Aguirre Boëda co-star. Directed by Rodrigo Plá







Love & Friendship showtimes and tickets
JINA LA MUVI: LOVE & FRIENDSHIP
In 18th century England, the widowed Lady Susan Vernon (Kate Beckinsale) attempts to solve her financial problems by landing a wealthy husband during a visit to her in-laws. However, her scheming is complicated by the sudden appearance of her teenage daughter Frederica (Morfydd Clark), and soon the two women are caught up in a love rectangle with a courtier (Xavier Samuel) and a suitor who's as rich as he is stupid (Tom Bennett). Chloë Sevigny co-stars as a friend of Susan's who tries to help with her matchmaking. Written and directed by Whit Stillman (who adapted the script from an early work by Jane Austen), Love & Friendship made its world premiere at the 2016 Sundance Film Festival.




Unaweza kuangalia muvi zote hizi kwa kubonyeza hapa FANDANGO.
 Picha zote na maelezo kwa msaada wa Fandango.com.











HEZBOLLAH YATAJA SABABU YA KUUAWA KIONGOZI WAO

Mustafa Amine Badreddine, file

 Kundi la Waislamu wa madhehebu ya Kishia la Hezbollah nchini Lebanon limetaja sababu ya kifo cha kiongozi wake wa ngazi ya juu wa kijeshi, Mustafa Badreddine kuwa kimetokana na makombora ya mizinga liliofanyika karibu na uwanja wa ndege wa Damascus nchini Syria.

 Hezbollah lilitangaza  kifo cha Badreddine hapo jana na alifanyiwa mazishi ya kijeshi siku hiyo hiyo katika eneo la ngome la kundi hilo huko kusini mwa Beirut. Taarifa ya kundi hilo imesema mashambulizi hayo yamefanywa na kundi linaloitwa Takfiri.

Takfiri ni neno linalotumiwa na kundi hilo la Kisunni kwa kuonesha msimamo mkali, kundi lenye kujihami na silaha, lililo na itikadi kali.

Badreddine alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa kundi la Hezbollah walioshutumiwa mwaka 2005 kuhusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanon Rafik Hariri.

Chanzo: Deutsche Welle (DW)

TEGEMEA PAMBANO KUTOKA KWA MAYWEATHER NA CONOR McGREGOR

 Floyd Mayweather

Conor McGregor
Mwanamasumbwi Floyd Mayweather amesema kuwa yeye ndiye aleanzisha uvumi wa kupambana na Conor McGregor ambaye anapambana kwa mtindo wa Mixed Martial Art (MMA).


McGregor alipost picha kwenye mtandao wa Twitter  iliyomuonesha yeye na Mayweather wakwa uso kwa uso.


Mayweather, mwanamasumbwi aliyestaafu mwenye miaka 39 amesema kuwa atahitaji kiasi cha fedha Dollar za kimarekani Milioni 100 sawa na Euro Milioni 69.3 kupambana na McGregor raia wa Ireland mwenye umri wa miaka 27.

"Muwe makini kusikiliza, linaweza kuwa pambano kati ya mcheza boxing na MMA" Mayweather aliiambia fighthype.com

"Ni pendekezo nililolitoa mimi, inaweza isiwe tetesi" aliongeza Mayweather.

Baba yake Mayweather alisema kuwa mwanaye huyo (Mayweather) aliwahi kumwambia kuwa atapambana na mwanamasumbwi yeyote kutoka MMA ambapo McGregor aliiambia BT Sport kuwa anataka pambano la Dola Bilioni na Muamerika, Floyd Mayweather.

McGregor, aliyeshindwa pambano lake hvi karibuni alipokuwa akipambana na Nate Diaz aliondolewa kwenye pambano la UFC 200 CARD mwezi uliopita baada ya kugomea kutimiza baadhi ya vigezo vilivyotaka kushiriki pambano hilo.

Pambano la 49 na la mwisho kutoka kwa Mayweather dhidi ya ANDRE BERTO mwezi wa tisa mwaka jana lilimfanya aamue uamuzi ambao haukutegemewa na wengi, ambapo alisema, "kazi yangu imefikia mwisho, na hii ni taarifa rasmi".

CHANZO: BBC

ANGALIA VIDEO YA JENNIFER LOPEZ-AIN'T YOUR MAMA HAPA



Jennifer Lopez ameachia video ya wimbo wake Ain't your Mama May 6 ambapo mpaka sasa wimbo huo umetazawa na watazamaji zaidi ya milioni na laki saba. Kama bado hujapata nafasi ya kuangalia video hiyo tazama hapa kwa hisani ya VENANCE BLOG kisha toa maoni yako kuhusu video hiyo.

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa. 

UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA TANZANIA NA UGANDA SASA NI RASMI

BOMBA la mafuta ghafi kutoka Hoima katika Ziwa Albert nchini Uganda, sasa ni rasmi kwamba litapita katika ardhi ya Tanzania kwenda Bandari ya Tanga, ambako ndiko meli kubwa za mafuta, zitakapotia nanga kubeba mafuta hayo kwenda sehemu mbalimbali duniani. Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, imeeleza kuwa Serikali ya Uganda imetangaza rasmi uamuzi wake wa kutumia bandari hiyo. Kwa hatua hiyo, bomba hilo linalotakiwa kuwa limekamilika ifikapo 2018, litaingilia Mkoa wa Kagera kutoka nchini Uganda na kupita katika mikoa ya Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma hadi Bandari ya Tanga. Rais Museveni Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, ndiye aliyetangaza uamuzi huo wakati wa mkutano wa 13 wa Ushoroba wa Kaskazini uliomalizika jijini Kampala jana. “Ujumbe wa Tanzania uliokamilisha mazungumzo hayo na kushuhudia utangazwaji wa hatua hiyo, uliongozwa na Dk Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,” imeeleza taarifa hiyo. Mbali na kiongozi huyo, taarifa hiyo imeeleza kuwa jopo la wataalamu lililoshiriki katika mazungumzo hayo, liliongozwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambalo litaendelea kubakia Kampala kukamilisha mpango huo wa bomba la mafuta ghafi, ambalo litanufaisha pia nchi zingine za Afrika Mashariki na Kati. Mchakato ulivyokuwa Awali, serikali za Uganda na Kenya, ziliwahi kufikiria kupitisha bomba hilo katika ardhi ya Kenya, kwa nia ya kutumia bandari itakayojengwa ya Lamu nchini humo. Hata hivyo, wakati hatua za kina hazijachukuliwa, Rais wa Tanzania, Dk John Magufuli na Rais Museveni walikutana mwanzoni mwa mwezi uliopita na baada ya mazungumzo yao, wakatoa agizo kuwa mchakato wa ujenzi wa bomba hilo, ufanyike kwa kasi. Baada ya kikao cha marais hao kutoa agizo hilo, kilifuata kikao cha Rais Magufuli na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Total, tawi la Afrika Mashariki, Javier Rielo, ambapo kiongozi huyo wa kampuni alimhakikishia Rais Magufuli kuwa kampuni yao itaanza ujenzi wa bomba hilo haraka iwezekanavyo, kwa kuwa fedha za kutekeleza mradi huo zipo. Katika mazungumzo hayo, Rielo alimueleza Rais Magufuli kuwa kampuni yake inatarajia kutumia Dola za Marekani bilioni 4 ambazo tayari zimeshaandaliwa. Bomba hilo litakuwa na urefu wa kilometa 1,410 na litasafirisha mafuta ghafi mapipa 200,000 kwa siku kutoka Ziwa Albert nchini Uganda, hadi Bandari ya Tanga na ujenzi wake unatarajiwa kuzalisha ajira za moja kwa moja 1,500 na ajira zisizo za moja kwa moja 20,000. Makubaliano ya awali Katika utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli na Rais Museveni, Machi 17 mwaka huu, serikali za Tanzania na Uganda pamoja na kampuni ya Total E&P Uganda na Shirika la Maendeleo ya Petroli la Tanzania (TPDC), walitia saini mpango wa pamoja wa utekelezaji wa mradi huo. Mpango huo ulitiwa saini na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania, Profesa Muhongo; Waziri wa Maendeleo ya Nishati na Madini wa Uganda, Irene Muloni; Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dk James Mataragio na Meneja Mkuu wa Total E&P Uganda, Adewale Fayemi. Kwa nini Tanzania Baada ya utekelezaji wa agizo hilo kufikia hatua ya mkataba kuliibuka mjadala kuhusu uhakika wa bomba hilo kupita Tanzania baada ya Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta kukutana na Rais Museveni, kujaribu kuangalia uwezekano wa bomba hilo kupitia Kenya kwenda Lamu. Pamoja na jitihada hizo, Bandari ya Tanga, ilibakia kuwa eneo pekee lenye mazingira bora, nafuu na yenye ufanisi kwa utekelezaji wa mradi huo. Uzoefu Mbali na Bandari ya Tanga kuwa ya kimkakati zaidi katika utekelezaji wa mradi huo, taarifa za ndani za wataalamu wa mafuta, zilionesha kuwa pia Tanzania ndiyo yenye uzoefu wa muda mrefu na wa hivi karibuni wa ujenzi, uendeshaji, ulinzi na uelimishaji jamii katika miradi ya bomba la mafuta. Uzoefu wa muda huo mrefu unatajwa kuwa ni wa ujenzi, uendeshaji na uhudumiaji wa Bomba la Mafuta la Tanzania na Zambia (Tazamaaaaaa tangu mwaka 1968, likitoka Dar es Salaam mpaka Ndola Zambia. Bomba hilo lenye kipenyo cha nchi 8 mpaka 12 na urefu wa kilometa 1,710; kati ya hizo kilometa 860 zipo kwenye ardhi ya Tanzania na limekuwa likipitisha mafuta tani milioni 1.1 kwa mwaka. Tanzania pia ina sifa ya uzoefu wa ujenzi, uendeshaji na uhudumiaji wa bomba la gesi kutoka Songo Songo mpaka Dar es Salaam, lenye kipenyo cha nchi 12 na urefu wa kilometa 25 kutoka kisiwa cha Songo Songo mpaka Somangafungu. Pia kuna bomba lingine la urefu wa kilometa 207 na kipenyo cha nchi 16, kutoka Somangafungu mpaka Ubungo Dar es Salaam, mbali na bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara mpaka Kinyerezi Dar es Salaam lenye zaidi ya kilometa 490. Lipo pia bomba la gesi linalotoka Mnazi Bay kwenda Mtwara, urefu wa kilometa 27 na kipenyo cha nchi 8, ambalo limeanza kutumika tangu 2006. Uzoefu wa kazi Katika ujenzi na uendeshaji wa mabomba hayo kwa miaka mingi, Tanzania imejijengea uzoefu wa kazi ya kupata ardhi kwa ajili ya kupitisha miundombinu ya bomba, tofauti na ugumu uliopo kwa nchi shindani ya Kenya na kusimamia masuala ya kimazingira. Tanzania pia imefanikiwa katika kusimamia wakandarasi wa kimataifa na matarajio ya umma wakati wa ujenzi na uendeshaji wa miradi hiyo na hata katika ulinzi wa miundombinu hiyo ambao umekuwa ukishirikisha jamii. Utayari Bandari ya Tanga Sifa nyingine iliyochangia Tanzania kukubalika zaidi katika mradi huo kwa kiwango cha kusaini mkataba wa utekelezaji tofauti na Kenya, ni utayari na mazingira wezeshi ya asili ya Bandari ya Tanga. Wakati Kenya wakijadili namna bomba hilo litakavyotumia bandari ambayo haijajengwa ya Lamu, kwa ajili ya kuuza mafuta, Bandari ya Tanga yenyewe iko tayari kwa kazi. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Bandari ya Tanga imeshakamilisha Tathimini ya Athari za Kimazingira (EIA) na Upembuzi Yakinifu, wakati njia ya Tanga ya bomba hilo imekwishaainishwa na haitapitia katika hifadhi za taifa wala mapori ya akiba. Bandari ya Tanga inayo fursa ya kutumika zaidi na mradi huo, kwa kuwa haina msongamano wa shughuli za bandari na tayari Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari (TPA), kwa mujibu wa taarifa hiyo, imeshatenga fedha za upanuzi utakaohitajika na eneo. Bandari hiyo pia imeunganishwa kwa reli na barabara za lami, zinazokwenda nchi za jirani na hivyo iko tayari kuanza kutumika kwa ajili ya kuingizia mizigo kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo. Bandari ya Tanga pia ndiyo yenye kingo za asili zinazoruhusu shughuli za upakiaji mafuta kufanyika mwaka mzima bila kusimama, tofauti na bandari zingine ambazo kipindi cha mawimbi makali ya bahari, huwa na wastani wa siku 40 ambazo husababisha shughuli za upakiaji au upakuaji mizigo kusimama. Pia bandari hiyo inatumika na hivyo kuwa tayari kwa matumizi ya haraka kama ilivyo dhamira ya Rais Magufuli na Rais Museveni, na hata ujenzi wa boya la kupakia mafuta unatarajiwa kuchukua mwaka mmoja tu hivyo kukamilika Juni 2017, kabla ya muda uliowekwa na mwekezaji wa kuanza kuuza mafuta wa 2018. Gesi mikoa saba Mbali na fursa hizo za pekee, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dk Mataragio, mradi huo unafungua fursa kwa usambazaji wa gesi asilia katika mikoa ya Kaskazini yaani Dodoma, Singida, Shinyanga, Tabora, Geita, Mwanza na Kagera na vile vile nchi za jirani ambazo zitahitaji gesi ya Tanzania. Pamoja na hayo, kutakua na ujenzi wa barabara mpya kiasi cha Kilometa 200 na uboreshaji wa barabara zilizopo kiasi cha Kilometa 150 na madaraja. Aidha utekelezaji wa mradi huo pia utachochea shughuli za utafiti wa mafuta Tanzania, kwani bomba hilo linapita maeneo ambayo yana uwezekana mkubwa wa kuwa na mafuta, hivyo uwapo wa miundombinu unavutia zaidi uwekezaji katika shughuli za utafiti wa mafuta na gesi. Fursa nyingine inayotajwa ni ya matumizi ya reli ambapo takribani mabomba 123,000 yatasafirishwa katika kipindi cha ujenzi huo. Chwnzo: Habari Leo

MALAWI IMETEKETEZA TANI 2 ZA PEMBE ZA NDOVU KUTOKA TANZANIA


Malawi imeteketeza tani 2.6 ya pembe za ndovu ambazo zilinaswa na maafisa wa usalama zikitokea nchi jirani ya Tanzania.

Meno hiyo 781 ya tembo ambayo inakisiwa kugharimu takriban dola milioni tatu ilipatikana baada ya operesheni dhidi ya ulanguzi na uwidaji haramu.

Mkurugenzi wa idara inayosimamia mbuga za wanyama pori Bright Kumchedwa, amesema kuwa hiyo ni ishara ya kwanza na dhabiti kutoka kwa Malawi kuwa haitaruhusu tena ardhi yake kutumika kulangua bidhaa za uwindaji haramu.
Hafla ya hiyo ya kihistoria ilifanyika katika eneo la Mzuzu kaskazini mwa nchi hiyo.

Kenya inatarajiwa kutekeleza hatua kama hiyo mwishoni mwa mwezi huu.

Kenya imekamata takriban tani 120 ya meno ya ndovu.

Chanzo: BBC

ZITTO KABWE: RAIS AMELIINGIZIA TAIFA HASARA YA TSH. BILIONI 36

Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa Rais John Pombe Magufuli ameliingizia taifa hasara ya bilioni 36 mpaka sasa toka alipoingia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

 Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook aliandika kuwa kitendo cha Rais Magufuli kushindwa kuchukua hatua juu ya malipo ya IPTL ambayo yanalipwa na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kila mwezi yamepelekea sasa hivi kufikia jumla ya bilioni 36. 

 "Tshs bilioni 8 kila mwezi TANESCO bado wanalipa IPTL. Rais haijampendeza kumaliza ufisadi huu. IPTL nadhani ni Jipu la Mgongoni (kwa kutumia maneno ya Hidaya wa Richard Mabala ). Rais, kwa kutochukua kwake hatua, ameshaliingizia taifa hasara ya tshs 36 bilioni toka aingie madarakani" aliandika Zitto Kabwe. 

Wakati Rais John Magufuli anatimiza siku 100 toka kutangazwa kama Rais Zitto Kabwe alitoa tathimini yake na kugusia sakata la Escrow pamoja na kampuni ya IPTL na kusema kuwa pesa ambazo wamelipwa IPTL/PAP kwa siku 100 tu zingeweza kununua CT Scan kwa hospitali zote za mikoa nchini.

 "Mkataba wa IPTL bado unaendelea kunyonya Nchi na Serikali inatazama tshs 8 bilioni zinalipwa Kwa matapeli wa IPTL na PAP kila mwezi. Katika siku 100 tangu Rais Magufuli aingie madarakani, jumla ya tshs 30 bilioni zimeshalipwa Kwa IPTL/PAP ambazo zingeweza kununua CT scan Kwa hospitali zote za mikoa nchini. Fedha hii ni zaidi ya mkopo ambao Serikali imechukua kutoka Benki ya Dunia ili kujenga ' fly over ' ya Ubungo jijini Dar Es Salaam" Alisema Zitto Kabwe.



 Chanzo: East Africa Television

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI: TRUMP NA RUBIO WATOFAUTIANA KUHUSU UISLAM

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Marco Rubio amemshtumu Donald Trump kwa kusema kuwa Uislamu unachukia Marekani katika mjadala uliokuwa moja kwa moja runingani. Bwana Rubio ambaye anakabiliwa na ushindani wa maisha yake katika jimbo la Florida siku ya Jumanne amesema kuwa Uislamu una tatizo la itikadi kali lakini akaongezea kuwa Waislamu wengi wanapenda Wamerekani. ''Marais hawawezi kusema kile wanachotaka ,kuna madhara'',alisema huku raia wakimpigia makofi. Wagombea hao wanne wa chama cha Republican walisikia maombi kutoka kwa viongozi wa chama hicho kuwa na mjadala wa amani. Ikilinganishwa na mjadala uliopita ambao ulikabiliwa na na matusi ya kibinafsi mjadala huu ulikuwa na muongozo mzuri huku wagombea wote wakitoa malengo ya sera zao. ''Kufikia sasa siamini vile tumekuwa watulivu hapa'',bwana Trump alinukuliwa akisema. Lakini katika swala la Uislamu,kulikuwa na tofauti kubwa kati ya Trump na wagombea wengine huku wenzake wote wakitofautiana naye kwamba familia za magaidi ziangamizwe. Chanzo: BBC

JANET JACKSON AAHIRISHA KUFANYA ZIARA YA MUZIKI ULAYA KUFUATIA MAUZO MABAYA YA TIKETI

Janet Jackson amefuta ziara yake kimuziki 'Unbreakable' barani Ulaya kufuatia mauzo mabaya ya tiketi barani humo. 'Alikuwa anaelekea kushindwa vibaya' kilisema chanzo cha habari. Muuza tiket mkuu alimuandikia barua pepe Janet mapema wiki hii kuhusu kurudishwa kwa hela za watu waliokuwa wamenunua tiketi. Hii ni wiki tatu kabla Janet alikuwa aende kufanya onesho jijini London, 'haitawezekana kwa sasa kusema ni lini tutapanga tena tarehe mpya ya onesho kwa hiyo tunarudisha hela kwa wale waliokuwa wamenunua tiketi' iliandikwa hivyo barua pepe hiyo. Upande wa Janet haukuzungumzia kuhusu kufutwa kwa onesho hilo lakini chanzo cha habari kilisema kuwa ni kufuatia mauzo mabay ya tiketi. 'Alikuwa anaelekea kushindwa vibaya, msanii anapofuta au kuahirisha ziara ya muziki sababu huwa ni mauzo mabaya ya tiketi' kilisema chanzo hicho na kuongeza 'ni bora kuahirisha kuliko kufanya onesho ukumbi ukiwa haujajaa watu haswa kwa msanii Janet Jackson'. Chanzo kutoka kwa waandaaji wa onesho la Janet, Live Nation kilidai kuwa mauzo ya tiketi hayakuwa mazuri 'bado hatuelewi japokuwa bado tuna matazamio mazuri ya onesho hili, lakini isingekuwa na maana kuendelea kusisitiza tarehe hizi . Ana mipango mingi kwa hiyo kunapokuwa na mambo mengi, kunakuwa na mgogoro kuhusu onesho'. Jana, Janet Jackson aliandika kwenye mtandao wa Twitter, 'najua mnanikumbukka, nawakumbuka pia. Nitapanga upya ziara ya Unbrekable Ulaya muda si mrefu kadiri ya uwezo wangu'
Janet Jackson alilazimika kuahirisha maonesho mbalimbali nchini Marekani kufuatia upasuaji aliokuwa amefanyiwa.Taarifa zinasema kuwa Janet atakamilisha maonesho hayo Marekani na anaweza kuongeza siku pia. Producer wa siku nyingi wa Janet, Jimmy Jam amesema kuwa Janet alikuwa anamalizia kurekodi baadhi ya nyimbo zake ili kuweka mambo sawa kwenye albamu yake. Janet anatarajia kufanya onesho kwenye Kombe la Dunia la Dubai tarehe 26 mwezi huu Machi. Anataraji kurudi Marekani kufanya maonesho kuanzia mwezi Mei hadi Septemba. Chanzo: Page Six

MECHI KATI YA LEICESTER NA WEST BROM FAHAMU HAYA

Mchezo wa leo kati ya Leicester city na West Bromwich Albion utapigwa katika dimba la King Power Stadium, ambapo Leicester watakuwa ni wenyeji wa dimba hilo. Mtanange utaanza saa 4 na dakika 45 usiku saa za Afrika Mashariki.

Novemba 1, 2013, West Brom alimfunga Leicester goli moja bila katika dimba la King Power Stadium.

Mwaka 2015, April 11 West Brom wakiwa wenyeji katika dimba la nyumbani, The Hawthorns walipigwa bao tatu dhidi ya mbili na Leicister city.

Lakini pia October 31, mwaka jana 2015, West Brom akiwa mwenyeji kwenye dimba la The Hawthorns alifungwa na Leicester city magoli 3 kwa mawili kama mechi iliyopita.

Leicester City inaongoza ligi ikiwa na pointi 56 ambapo imecheza mechi 27 imeshinda mechi 16, imetoka sare mechi 8, na kupoteza mechi 3 ikiwa na magoli ya kifunga 20.

Kwa upande wa West Brom wao wapo katika nafasi ya 13 wakiwa wamecheza mechi 27, wameshinda mechi 9, sare mechi 8 na kupoteza mechi 10 wakiwa wmemfungwa magoli10. West Brom wana pointi 35 ambapo wanahitaji kushinda mechi zaidi ili kuepuka kikombe cha kuporomoka nafasi waliopo kushuka daraja.

Leicester inaingia dimbani ikiwa na majeruhi wawili, Matthew James na Jeffrey Schlupp.

West Brom ina majeruhi watano, Johhny Evans, Gareth McAuley, Craig Dawson, James Morrison na Callum Mcmanamam.

MAMBO YA KUFAHAMU KATI YA CHELSEA NA NORWICH CITY

Chelsea imeshinda mechi saba na haijapoteza katika mechi tisa ilizokutana na Norwich City kwenye EPL.

Norwich City imefenikiwa kuifunga Chelsea magoli manne tu na kushindwa katika mechi nne ambazo walikutana mara ya mwisho na The Blues.

Steven Naismith wa Norwich City amefanikiwa kuifunga Chelsea magoli sita katima mechi saba walizokutana na The Blues EPL.

Norwich City imeshinda mechi nne tu, sare nne na kupotezaechi nane katika mechi 16 ilizocheza katika dimba lao la nyumbani, Carrow Road. (W4 D4 L8).

Norwich City imepata magoli 10 tu katika dimba lao la nyumbani, hii ni baada ya kushinda mechi mbili kati ya tano za EPL katika dimba hilo.

Katika mechi 7 za EPL na kufunga magoli 7 pamoja na kuwa na jumla ya magoli 19 kwenye ligi.

Chelsea imeshuhudia wachezaji wake 15 wakiifungia magoli timu hiyo msimu huu. Rekodi ambayo ni ya juu zaidi katika mashindani msimu huu.


Guus Hiddink amepoteza mechi moja tu kati ya mechi 23 kama kocha na meneja wa klabu katika ligi ya Uingereza msimu huu. Pia ametoa sare mechi 7 na kushinda 15. (W15 D7 L1)


Norwich City imekuwa na rekodi dogo ya kugusa box la goli msimu huu ambapo imesogeza jumla ya shuti 426 tu katika mechi zilizopita.

Chelsea wanataka kushinda mechi tatu mfululizo kwa mara ya kwanza yangu mwaka jana April, 2015.

Norwich inaingia uwanjani ikuwa na majeruhi mmoja tu, Andre Wisdom aliyeumia goti katika mechi ya tarehe 27 Februari mwaka huu.

Kwa upande wa Chelsea majeruhi ni John Terry,  Kout Zouma na Radamel Falcao García Zaráte.

Katika mechi tano zilizopita, Octoba 6, 2012, Chelsea alishinda Norwich magoli 4 dhidi ya moja  kwenye dimba la Stamford Bridge.

Desemba 26, 2012, Chelsea alimfunga Norwich goli moja bila katika uwanja wa Norwich Carrow Road.

Mwaka 2013 Octoba 6, Norwich alifungwa na Chelsea magoli 3 kwa moja, Carrow Road.

May 4, 2014, Norwich na Chelsea walitoka sare ya bila kufungana katika dimba la Stamford Bridge.

Novemba 21, mwaka jana 2015, Chelsea ilishinda goli moja bila dhidi ya Norwich katika dimba la nyumbani, Stamford Bridge.

Mtanange wa Leo utapigwa katika dimba la Norwich City, Carrow Road majira ya saa 4 na dakika 45 usiku saa za Afrika Mashariki.