ZIFAHAMU TEKNOLOJIA 7 ZITAZOKAZOKUZA MAENDELEO YA MAJIJI MAKUBWA DUNIANI

Fikiria ulikuwa unafanya kazi katika taasisi ya maendeleo na kupunguza umasikini mwanzoni mwa miaka ya 1990. Mwandishi wa makala hii, Abhas Jha anasema yeye aliwahi kufanya kazi zama hizi. Anasema kipindi hicho kulikuwa na tovuti moja tu iliyokuwepo duniani mpaka kufikia Agosti mwaka 1991 (leo kuna zaidi ya tovuti bilioni 1.5 duniani kote). Anasema kipindi hicho simu za mkononi zilikuwa ghali sana, chache na zilikuwa nzito na za kishamba sana ukilinganisha na hizi za sasa. Ni watu wachache wangetazamia kuhusu hali iliyopo nchini India kwa sasa kwamba kungekua na idadi kubwa ya simu za mkononi kuilko idadi ya vyoo.

Bill Gates aliwahi kusema "tunayapa uzito sana mabadiliko ambayo yatatokea ndani ya kipindi cha muda mfupi sana na kuyapuuza yale yaliyotokea kwa muda mrefu sana". Teknolojia inakua kwa kasi sana na kufanya na mabadiliko makubwa sana kwenye majiji ili kufikisha huduma kwa jamii. Teknolojia inafanya hivi ili sio tu kufikisha huduma haraka kwa wateja bali pia kukuza uchumi na kuimarisha namna ya kufanya mikakati ya kuboresha njia za kuongeza ufanisi wa kifedha.

Hizi hapa ni teknolojia 7 zilizofanya na zitakazokuja kufanya mabadiliko makubwa sana katika majiji duniani na kufanya mabadiliko ya ufikishaji wa huduma kwa wateja:

1. TEKNOLOJIA YA MTANDAO (INTERNET) YA 5G


5G inasimama kwa kumaanisha "kizazi cha tano". Hii ni teknolojia ambayo itatumika kwa simu za mikononi na kompyuta kurahisisha uharaka wa mtanadao, inategemewa kuanza kutumika rasmi kuanzaia mwaka 2020 kwa sasa bado iko katika majaribio. Itakuwa na uwezo mara 40-60 ya uwezo wa teknojia ya sasa ya mtandao wa simu za mkononi. Benki ya Dunia inasema kwamba "kwa ongezeko la 10% la kasi ya mtandao, uchumi utaongezeka kwa 1.3% na kupelekea kile kinachoitwa kitaalamu uhuru wa ugunduzi. Kwa mujibu wa Jukwaa la Uchumi la Benki ya Dunia wanasema kwamba "kama 40% tu ya watu wote wangetumia mtandao duniani, tungeweza kuongeza pato la dunia kwa kiasi cha dola za Marekani $1 trilioni kwa kuunganisha watu wengine milioni 327". Mtandao wa 5G utasaidia matumizi madogo, matumizi madogo ya vifaa vya kuhisi (sensor) ambavyo vitawekwa kwenye majengo, magari, vifaa vingine n.k. Kiufupi utakuwa ni "mtandao wa muunganiko wa vitu" yaani Internet of Things (ToT)

Benki Kuu ya Dunia inakubaliana na miradi mikubwa ambayo ufikishwaji wake unategemea mtandao kwa mfano mradi mkubwa unaojulikana kama BridgeIT nchini Tanzania unaofanya urahisishaji wa kuangalia video za kidijitali madarasani wakati wa kufundisha na kujifunza kwa kutumia teknolojia ya simu za mkononi. Mtandao wa 5G utarahisisha sana matumizi ya mambo haya na mengineyo.

2. TEKNOJIA YA MALIPO YA KIFEDHA "BLOCKCHAIN"

Hii ni teknolojia ya malipo ambayo inafanywa na bitcoin. Teknolojia hii itaweza kurahisisha malipo kama jinsi mtandao unavyofanya kufikisha taarifa kwa haraka zaidi. Lengo la teknolojia hii ni kusambaza mifumo ambayo itasaidia kufanya malipo kwa njia ya mtandao kwa haraka ziadi hata ya mifumo mingine kama Western Union, PayPal, MasterCard na VISA. Hii itasaidia miamala ya kifedha kufanyika bila kuwepo na upatanishi kwa mfano kupitia soko la hisa ambayo kwa sasa inafanya kazi kama mpatanishi wa miamala.

Teknolojia hii inatumiaka kwa matumizi mbalimbali kama vile kurahisisha usajili wa maeneo na kurahisisha usalama wa chakula nchini China. Benki ya Dunia inasema imechapisha makala ambayo inaitambua teknolojia hii kama kichocheo cha maendeleo ya kimataifa. Pia teknolojia hii imesaidia kuwalipa mamilioni ya watu wanaofanya michezo ya upatu mtandaoni na hata wale wanaofanya baadhi ya kazi za bitcoin.

3. TEKNOLOJIA YA AKILI BANDIA "ARTIFICIAL INTELLIGENCE" INAYOHUSISHA KUJIFUNZA KWA VIFAA "MACHINE LEARNING" NA DATA KUBWA "BIG DATA"

Kuna baadhi ya wataalamu kama Stephen Hawking (mtaalamu wa Fizikia aliyefariki Machi 14 mwaka huu) na Elon Musk waliowahi kuonya dhidi ya matumizi ya teknolojia hii ambayo ina madhara makubwa  baadaye. Wengine kama vile Fei-Fei Li, ambaye ni profesa wa Sayansi ya Kompyuta katika Chuo Kikuu Stanford anasema kwamba "tunakaribia kwenye mashine ya kufua kuliko kuharibu mambo" akiwa na maana kwamba tunaelekea kwenye urahisi zaidi wa mambo kuliko hatari ambazo watu wanafikiria kuhusu teknolojia hii.

Aliongezea kwamba teknolojia hii ya akili bandia "Artificial Intelligence" na data kubwa, ni teknolojia ambazo zinarahisisha urahisi wa mambo hasa katika majiji ambayo yanahitaji matumizi makubwa ya data kama vile Shanghai, Hong Kong, Sydney na New York hususani katika maeneo ambayo yanafanya maegesho ya magari kwa teknolojia hii, kusimamia ubora wa hewa na kuongeza matumizi ya nishati katika majengo makubwa na marefu.
Kwanza, tufahamu Artificial Intelligence na Machine Learning ni nini? Artificial Intelligence ama kwa ufupi AI kwa lugha nyepesi tunaweza kusema ni Akili Bandia, inaitwa hivi kwa vile Akili Asilia anayo mwanadamu tu. AI ni matokeo ya Akili Asilia. Pia, Machine Learning (ML) ama kwa tafsiri yangu nyepesi Ujifunzaji wa Vifaa kwa Kujazwa Taarifa ni tokeo la AI. Kwa hivyo AI na ML ni dhana mbili zinazokwenda sambamba, dhana hizi zinahusika na utengenezaji wa kanuni ambazo zinaruhusu Kompyuta kufanya kazi ambazo zinahitaji akili ya mwanadamu. AI ni uwanda mpana wa Sayansi ya Kompyuta ambao unalenga kutengeneza mifumo inayoweza kufanya kazi ambazo zikifanywa na mwanadamu huhitaji akili. Mambo hayo ni utatuzi wa changamoto, ufahamu na utambuzi wa lugha, kutambua kanuni na mifumo ya asili na kufanya maamuzi. AI ipo katika aina mbili: Akili Bandia Nyembamba (Narrow AI) ambayo imetengenezwa na kufunzwa kwa kazi mahsusi na Akili Bandia ya Jumla (General AI) ambayo iko na utambuzi na sifa zote za akili ya mwanadamu. 
ML ni kipengele cha AI ambacho kinahusika na utengenezaji wa kanuni (algorithms) ambazo zinaruhusu Kompyuta kujifunza na kufanya maamuzi kutokana na taarifa zinawekwa katika kifaa husika. Badala ya kujazwa taarifa za kufanya kazi mahsusi, kanuni za ML zinatumia njia za kitakwimu kujifunza mambo mbalimbali kutokana na taarifa zinazowekwa katika kifaa husika. Kuna aina kadhaa za ML ambazo nitazitaja tu kwa lugha ya kigeni:

(i) Supervised Learning
(ii) Unsupervised Learning
(iii) Reinforcement Learning

AI na ML zinatumika katika uwanda mpana wa mambo mengi mathalani:
• Utambuzi wa Sauti na Uzungumzaji (Voice and speech recognition) kwa mfano katika huduma kama Siri au Google Assistant. 
• Utambuzi wa Picha (Image recognition)
• Vipimo vya Kitabibu (Medical diagnosis)
• Utabiri wa masuala ya fedha (Financial forecasting)
• Njia tofauti za masoko (Personalized marketing)
• Gari zinazojiendesha (Self-driving cars) na mengine mengi. 

Na pili, tuangalie Big Data ama kwa tafsiri yangu nyepesi nimeamuia kuita Data Kubwa. Kwa maana nyepesi kabisa data kubwa ni taarifa ambazo ni kubwa (kama jina lenyewe) na hivyo huwa ni changamoto kuzipangilia, kuzichakata na kuzichanganua kwa kutumia njia za kawaida/asili za uchanganuzi wa taarifa. Big data inasifika kwa kuhusu mambo matatu ambayo ni ukubwa (volume), kasi (volume) na namna nyingi (variety). Matumizi ya data kubwa yanasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza ufanisi, kuchochea umaizi (insights) na maendeleo. Big data inasaidia katika nyanja zifuatazo:
(i) Afya, hapa teknolojia hii inasaidia kutabiri mlipuko wa magonjwa (disease outbreak prediction), namna ya kuboresha huduma ya afya kwa wagonjwa (optimized patient care), ugunduzi wa dawa (drug discovery) na mengine mengi.
(ii) Fedha, benki na taasisi nyingine za kifedha zinatumia teknolojia hii kugundua udanganyifu (fraud detection), kupima madhara (risk assessment), upangiliaji wa taarifa za kibiashara kutokana na mapendeleo ya mtu (algorithmic trading) na mgawanyo wa mateja (customer segmentation)
(iii) Elimu, taasisi na majukwaa ya kielimu yanatumia biga data kufahamu maendeleo ya wanafunzi katika masomo (student performance), kuboresha njia za ujifunzaji (personalized learning paths) na kutabiri kiwango cha idadi ya wanafunzi watakaoshindwa kuendelea na masomo (dropout rates).
(iv) Kilimo, wakulima wanatumia teknolojia hii kufanya kilimo kuwa cha kisasa (precision agriculture) ambacho kinatumia taarifa za kiteknolojia ili kuongeza uzalishaji wa mazao na kupunguza hasara zitokanazo na shughuli za kilimo. Teknolojia hii inawasaidia wakulima kupitia picha za satelaiti kuhusu upatikanaji au ukosefu wa mvua na majanga ya asili, vifaa vinavyohisi (sensor) katika kilimo, matumizi ya ndege zisizo na rubani (drones) katika kilimo hasa upuliziaji wa madawa ili kuboresha uzalishaji na matumizi ya raslimali.
(v) Mauzo, big data inasaidia watoa huduma za mauzo kufahamu vitu wapendavyo wateja (customer preference), kuboresha mikakati ya mauzo (optimize pricing strategies), kusaidia ugunduzi (managing inventory) na ufikishaji wa huduma za masoko kwa wateja wa aina tofauti kwa njia mbalimbali (tailor marketing campaigns)
(vi) Burudani, big data inatumika kupendekeza mambo ya kutazama/kusikiliza kwa watazamaji wa huduma za mtandaoni (streaming) kulingana upendeleo wa mtazamaji na historia ya mambo aliyotazama katika kwa mfano watumiaji wa YouTube, Netflix, Hulu, Amazon Prime Video, Max, Disney+, Apple TV+, Spotify, Tidal, Apple Music, Paramount+ n.k. Hapa teknolojia hii inapendekeza nyimbo na picha mjongeo (video) pamoja na filamu ama michezo ya kuigiza (drama series)
(vii) Nishati, kampuni zinatumia big data kufahamu vifaa ambavyo vimeshindwa kufanya kazi (equipment failure), kuboresha namna ya usambazaji wa nishati (optimize energy distribution) na matumizi ya njia za nishati zisizo na madhara katika mazingira na zinazoweza kutumika kwa ufanisi (integrate renewable sources efficiently)
(viii) Uboreshaji wa miji na majiji, teknolojia hii inasaidia mipango miji (urban planning), upatikanaji wa hewa safi (monitoring air quality), uboreshaji wa huduma za usafiri wa umma (optimize public transport) na usafi wa miji (waste management).
(ix) Viwanda, big data inasaidia viwandani kufahamu vifaa vinavyohitaji matengenezo (predict maintenance), kuhakikisha ubora ya bidhaa inayozalishwa kiwandani (product quality assurance) na uboreshaji wa mnyororo wa thamani (supply chain optimization).
(x) Mitandao ya Kijamii kama Facebook, Twitter, Instagram n.k. hutumia teknolojia hii kupendekeza maudhui anayoweza kuyapenda mtumiaji wa mtandao (tailor content suggestion), kufahamu maudhui yanayotazamwa au kufuatiliwa sana (detecting trending topics) na kupendekeza matangazo kulingana na tabia za mtumiaji wa mtandao (target advertisments)
(xi) Usafirishaji, teknolojia hii inasaidia kuboresha safari (route optimization), kupendekeza matengenezo ya vyombo vya usafirishaji (predictive maintenance of vehicles) na uchanganuzi wa taarifa za barabarani ili kupunguza msongamano barabarani na ucheleweshwaji wa huduma (analyzing traffic patterns to reduce congestion)
(xii) Michezo, walimu wa mpira wa miguu (coaches) na timu zao wanatumia big data kufahamu ufanisi wa wachezaji (evaluate player performance), kuboresha mikakati ya mchezo (strategize game plans), na kufatilia maendeleo na hatua za kumnunua na kumuajiri mchezaji katika timu (scouting and player recruitment)
(xiii) Biashara mtandao (E-commerce), watoa huduma za mauzo mtandaoni huchanganua taarifa za watumiaji (analyze customer behavior), kuboresha matokeo ya utafutaji wa bidhaa au huduma (optimize search results) na ufikishaji wa huduma za masoko kwa wateja wa aina tofauti kwa njia mbalimbali  (tailor marketing campaigns)
Hayo ni machache katika mengi ambayo teknolojia hii imesaidia utendaji kazi wa mambo kadha wa kadha.

4. TEKNOLOJIA YA MAGARI YANAYOJIENDESHA "AUTONOMOUS VEHICLES (AV)"

Licha ya kuwepo taarifa ya hivi karibuni kuhusu kifo cha mtembea kwa miguu kugongwa na gari linalojiendesha, teknolojia hii bado itakuwa ni ya kushangaza na bora zaidi na itakuwa na matokeo mazuri sana katika majiji makubwa na kwingineko ulimwenguni.
Mwaka 2016 John Zimmer ambaye ni miongoni mwa waanzilishi na Rais wa kampuni ya Lyft ambayo inahusika na utengenezaji wa magari hayo alichapisha chapisho refu ambapo alidai kuwa teknolojia hii ya magari yanayojiendesha itachukua nafasi ya teksi ndani ya miaka 5 na mpaka kufikia mwaka 2025 umiliki binafsi wa gari nchi Marekani katika majiji makubwa utafikia kikomo kutokana na teknolojia hii ya magari kuanza kutumika katika majiji hayo. Nimeamua kuiita teknolojia hii kama teknolojia ya magari huru kutokana na kutoendeshwa na mtu; ni magari yanayojiongoza yenyewe.


5. TEKNOLOJIA YA BEI RAHISI YA UTAFITI WA ANGA "LOW-COST SPACE EXPLORATION"

Kampuni ya Elon Musk, Heavy Reusable Rocket inao uwezo wa kutengeneza roketi kwa gharama za dola za Marekni 1000. Hii ni teknolojia ambayo itakuwa ni ya kushangaza na kurahisisha sana utafiti wa anga kwa maisha ya mwanadamu. Musk ana wazo la kufanya utafiti wa usafiri wa anga kutoka jiji moja hadi jingine kwa kutumia roketi ambayo kwa mawazo yake ni kwamba ingerahisisha kwenda mahala popote duniani ndani ya saa moja tu kwa kutumia teknolojia hii.
Kulingana na utafiti uliofanywa na taasisi ya tafiti ya Gartner, zaidi ya vitu bilioni 20 vitakuwa vimeunganishwa dunia nzima mpka kufikia mwaka 2020. Wanadai kuwa teknolojia hii itashirikiana na ile ya OneWeb ili kusambaza satelaiti ndogo ili kuunda mkusanyiko ambao utafanikisha kutataua changamoto kubwa ya kutoa urahisi wa kuunganisha watu zaidi ya bilioni 4 duniani kote kuwa na urahisi wa kupata huduma ya mtandao kwa wale ambao wasingefikiwa na huduma hii kutokana na kuwa katika maeneo ambayo mtandao ungekuwa kitendawili kwao. Huduma hii pia itaunganisha mambo bilioni 20 ambao yataletwa na teknolojia ya Mtandao wa Muunganiko wa Vitu "Internrt of Things (IoT)" 


6. TEKNOLOJIA YA UTAMBUZI YA KIELEKTRONIKI-BAIOMETRIKI (BIOMETRIC) INAYOHUSISHA VITAMBULISHO VYA KISASA (DIGITAL ID) NA MALIPO YA KISASA (DIGITAL PAYMENTS)

Idara ya Utambuzi kwa Mandeleo ya Benki ya Dunia (ID4D) imekediria kwamba takribani watu bilioni 1.1 hawana uwezo wa kuhakiki vitambulisho vyao (hii ni sawa na mtu 1 katika kila mkusanyiko wa watu 7) Haya ni mabadiliko ya haraka sana. Idara ya Aadhar nchini India imesajili takribani watu bilioni 1.1. Kwa kuruhusu Aadhar kama mfumo rasmi wa vitambulisho, kulingana na utafiti mmoja, kiwango cha ushirikishwaji wa kifedha nchini India umeongezeka kwa 24% miongoni mwa wanawake kati ya mwaka 2014 na 2015. Kwa pamoja, makadirio  yanaonesha kuwa akaunti takribani milioni 22o zilifunguliwa kufiki April 2016.
Kuunganisha malipo kwa mfumo huu kumesidia kufanya malipo ya ruzuku na pesa na mabo mengine kwa kutumia vitambylisho vya baiometriki kumepunguza udanganyifu, ujanja ujanja na rushwa kwa mfano kutambua watumishi hwa nchini Nigeria.

Mfumo wa Vitambulisho vya kisasa unaohusisha na progamu za simu za mkononi pia ulianzishwa nchini Algeria, Cameroon, Jordan, Italia, Senegal na Thailand ukienda sambamba na tangazo la kuwepo kwa matumizi ya mpango huu nchini Uholanzi, Bulgaria, Norway, Liberia, Poland, Jamaica na Sri Lanka pamoja na kujaribiwa jijini Mynmar nchini Burma. Teknolojia hii kwa sasa inahusisha mfumo ya kibaiometriki kwa mfumo wa alama za vidole (fingerprint).

7. TEKNOLOJIA YA VIFAA VYA ANGA VISIVYO NA WAONGOZAJI NDANI YAKE "UNMANNED AERIAL VEHICLES (UAVs) mathalani Drones

UAVs ni vifaa ambavyo vinajiongoza bila kuendeshwa na rubani ndani yake aidha kwa kuongozwa na mtu aliyeko chini au katika kifaa kingine ama kuongozwa na Kompyuta iliyoko ndani ya kifaa husika. Hii ni teknolojia ambayo kwa sasa imesaidia sana upatikanaji wa taarifa ndani ya muda mfupi sana hasa hasa kwa kamera ambazo huongozwa kwa kutumia rimoti. Mawasiliano yanakuwepo baina ya kamera hii na muongozaji ambaye anakua ardhini kuiongoza kamera hiyo. Wakati mwingine kamera hii inaweza kujiongoza yanyewe kwa kutumia kompuya inayokuwa ndani ya kamera hiyo. Teknolojia hii ilisaidia kupata taarifa kuhusu mafuriko yaliyosumbua jiji la Dar es Salaam mwezi April mwaka 2018.

Changamoto ya teknolojia hii ni nguzo za umeme, miti mirefu na upepo mkali ambavyo ni vikwazo vinavyozuia kamera hizi kwenda umbali mrefu sana. Kama kunakuwa hakuna vikwazo hivi, kamera hizi zinauwezo wa kusafiri kulingana jinsi kilivvyowekewa umbali husika.

Ndege zisizo na rubani (Drones) zimesaidia katika mambo mengi kwa sasa mathalani upuliziaji wa dawa na uangalizi wa afya ya mazao mashambani, ulinzi na usalama, upigaji picha za matukio mbalimbali, ukaguzi wa madaraja, nguzo za umeme, ufikishaji wa huduma kwa wateja na uangalizi wa mazingira hasa misitu, mbuga na kufatilia mabadiliko ya kimazingira.


Benki ya Dunia ina uwezo wa kufanya jambo la msingi katika teknolojia hizi ili kuhakikisha kuwa zinatumiaka kote duniani na kuzingatia kuwa hata masikini hawaachwi mbali sana na teknolojia hii. Kwa kuhitimisha ni kwamba Ripoti ya Mendeleo Duniani ya mwaka 2016 kuhusu mgawanyo wa teknolojia ya kisasa unatoe masomo  matatu:

1. Kutumia data ili kulenga maeneo ambayo yako mbali sana na upatikanaji wa mtandao kama jinsi Sao Paulo walifanya kuwa na taarifa za kijografia kufanya kipaumbele kuhusu makazi.

2. Kufungua data ili kurahisisha uwazi hii ikijumuisha kuwa na ramani za vitu, uchafuzi na mahitaji ya jamii huko Kiberia, eneo ambalo halina makazi yaliyipangiliwa jijini Nairobi; na

3. Kuwepo na teknolojia ya kuunganisha simu za mkononi ili kurahisisha ushiriki wa wanchi kama jinsi majiji ya nchini Ufilipino kwa kushirikisha wananchi wake katika bajeti za majiji hayo.


MAKALA HII IMENDALIWA NA BENKI YA DUNIA NA KUTAFSIRIWA NA KUONGEZWA MANENO MENGINE NA VENANCE BLOG.

MAWASILIANO
barua pepe: venancegilbert@gmail.com
simu: 0753400208

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: FIFA IMESEMA ITAZIPA DOLA MILIONI 2 NCHI ZA AFRIKA ZINAZOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA



FIFA itatoa zawadi ya dola milioni mbili kwa kila mojawapo ya timu tano za Afrika zilizofuzu kucheza kombe la dunia kuzisaidia katika maandalizi, amesema rais wa shirikisho la kandanda barani Afrika CAF.
Misri, Morocco, Nigeria, Senegal na Tunisia, zimefuzu kushiriki katika michuano ya kombe la dunia itakayofanyika nchini Urusi, na rais wa shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF, Ahmad Ahmad, alismea katika taarifa kwamba fedha hizo zitatumika "kushughulikia mapema, suala la bonasi za wachezaji."
"Migogoro juu ya malipo katika michuano iliyopita ilipelekea kuwepo na hali zilizoathiri vibaya taswira ya soka barani Afrika, ikiwa ni pamoja na kuathiri kwa kiwango kikubwa utendaji wa timu viwanjani," aliongeza.
Mwaka uliopita, shirikisho la kandanda la Nigeria (NFF) lilisaini makubaliano na wachezaji wake wakiahidi kujiepusha na migogoro ya bonasi na malipo ambayo imeharibu kampeni zao za nyuma za kombe la dunia.
Wachezaji wa timu ya Nigeria, Super Eagles walihusika katika mzozo wa muda mrefu kuelekea mashindano ya kombe la shirikisho la mwaka 2013 nchini Brazil, na mgogoro juu ya bonasi pia ukavuruga kampeni yao ya kombe la dunia mwaka 2014.
Matatizo sawa na hayo yameziathiri timu nyingine na bara la Afrika.
Time 32 zinashiriki katika michuano ya kombe la dunia inayofanyika kuanzia Juni hadi Julai, hupokea kitita cha dola milioni 1.5 kila mmoja kutoka FIFA katika mfumo wa malipo ya maandalizi, na zinahakikishiwa kingine kisichopungua dola milioni 8 katika fedha za zawaidi baada ya kumalizika kwa mashindano hayo.

Chanzo DW

FACEBOOK KUANZISHA PROGRAMU YA KUWAPATANISHA WAPENDANAO HUKU IKIIMARISHA KIWANGO CHA FARAGHA

Mark Zuckerberg mmiliki wa mtandao wa Facebook
Kampuni ya Facebook inaongeza faragha kwa watumiaji wake kwa kuweka sehemu ya kufuta historia ya ulichokitafuta katika mtandao huo wa kijamii.
Aidha amesema kwamba programu hiyo itaangazia uhusiano wa muda mrefu na sio urafiki wa muda mfupi na itawatenganisha marafiki na watu wanaotarajiwa kuwa na uhusiano.
''Programu hii itakuwa na kiwango cha juu cha siri na usalama kutoka mwanzo'', aliongeza.
Hivi karibuni kampuni hiyo ilikumbwa na kashfa ya kutothamini faragha za watumiaje wake huku watumiaji zaidi ya millioni hamsini walidukuliwa katika kipindi cha uchaguzi wa Marekani.
Facebook imekua katika sakata la faragha ya watumiaje hivi karibuni, mamilioni ya taarifa za watumiaji zilichukuliwa bila ridhaa na kampuni ya Cambridge Analytica kwa matumizi ya wanasiasa. Mark Zuckerberg amesema kuwa atahakikisha suala kama hilo halitajitokeza tena, kwa kutengeneza ulinzi zaidi wa mtandao huo. Kitendo hicho kilishusha mapato ya Facebook karibu asilimia 15 ya mapato ya awali.
''Kilichotokea kwa Cambridge Analytica ilikua uvunjifu wa uaminifu wa hali ya juu, walichukua data za watu na kuziuza, hivyo tunatakiwa kuhakikisha kuwa suala hili halitokei tena, kwanza tunaweka vizuizi kwa data ambapo mtu atakua anaombwa kwa ridhaa yake, na pili tunahakikisha tunazijua program mbaya zote'' alisema Zuckerberg.
Katika mkutano wa mwaka wa kampuni hiyo ya mjini California, Zuckerberg ameongeza pia wanaimarisha faragha ambapo itamruhusu mtumiaji kufuta historia ya kitu alichotafuta.

Chanzo BBC

MOHAMMED SALAH: ILIKUAJE AKAIMARIKA HARAKA? MAJIBU HAYA HAPA

Mohammed Salah
Huku wachezaji wakisherehekea kwa fujo baada 4-0 dhidi ya ENPPI, kocha Said Al Shesheni aliangalia upande mmoja na kugundua kwamba mchezaji mmoja wa kikosi cha al-Mokawloon wa kikosi cha wachezaji wasiozidi umri wa miaka 16 hakuwa akifurahia michuano iliokuwa Cairo. Alikuwa akibubujikwa na machozi kwamba jina lake halikuwa katika orodha ya wafungaji mabao. Akicheza kama beki wa kushoto ilikuwa vigumu kuchukua jukumu kubwa kama alivyotaka.
Akiwa mzaliwa wa eneo la Nagrig, kijiji kimoja kilichopo kilomita 130 Kaskazini mwa mji mkuu wa Misri, mchezaji huyo alilazimika kupitia tatizo la kusafiri kwa saa tisa kila siku mara nyingine akilazimika kutumia mabasi 10, ili kuweza kufika mazoezini mbali na kushiriki mechi.
Na baada ya kufurahishwa na ari ya kijana huyo Al Sheheni alimpatia fursa na kumpeleka safu ya mbele. Tangu wakati huo Mohammed Salah hajarudi nyuma tena.
Kijana katika uwanja wa Mo salah
Mchezaji huyo wa Liverpool alilazimika kulipia uwanja mpya katika shule yake ya zamani.

Habari hiyo ni jibu kwa swali ambalo limekuwa katika fikra za mashabiki wa soka duniani: Mchezaji ambaye hakuwa na athari yoyote kimchezo katika ligi kuu za Ulaya mara moja amekuwa mfungaji bora akilinganishwa na Lionel Messi na Christiano Ronaldo.
Katika soka inasaidia wakati mchezaji anapojikuta katika eneo analohitajika kuwa na katika wakati ufaao. Lakini ni watu wachache waliokuwa na hilo wakati Liverpool ilipotangaza usajili wa Salah kutoka klabu ya Italia ya Rome mwaka uliopita .
Kitita cha $55.7m kinaonekana kuwa cha juu kwa mchezaji ambaye alikuwa amefeli kuonyesha umahiri wake katika soka ya Uingereza baada ya kuhudumu kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa Chelsea 2015.
Pia ni muhimu kuona kwamba Misri sio timu yenye umaarufu mkubwa katika soka duniani, ijapokuwa ina umaarufu mkubwa barani Afrika, baada ya kushinda taji la kombe la Afrika mara saba.
Lakini The Pharaoh wamecheza katika michuano miwili ya kombe la dunia 1934 na 1990 na hadi Salah alipoimarika, ilikuwa rahisi kutajwa kwa kuwa kipa Essam El-Hadary yuko katika harakati za kuwa mchezaji mkongwe zaidi kushirki katika kombe la dunia, wakati Misri iliporejea katika kinyang'anyiro hicho nchini Urusi.
Timu ya taifa ya Misri
Misri imeshiriki katika michuano miwili pekee ya kombe la dunia lakini wamefaulu kushiriki Urusi 2018

Ni nini kilichofanyika kimakosa kwa Salah mapema alipocheza Uingereza? Kwanza Salah alishiriki katika ligi ya Switzerland, ambayo haina ushindani mkubwa kama ile ya Uingereza.
Akiwa Chelsea pia alikabiliwa na ushindani mkubwa kutoka kwa wachezaji walioimarika na hakupata fursa za kutosha kuonyesha umahiri wake.
Raia huyo wa Misri alicheza mechi 19 kwa klabu hiyo ya London huku akianzishwa katika mechi tisa pekee. Ni mara mbili pekee alipocheza dakika zote 90. Salah baadaye alipelekwa kwa mkopo kwa vilabu vya Italia kabla ya kusainiwa na Roma kwa msimu wa 2015/16
Ni wakati huo ambapo Salah alionyesha umahiri wake na kufunga mabao 34 katika misimu miwili kabla ya kuelekea Liverpool.
Image result for mohamed salah with mourinho at chelsea
Salah hakuweza kufanya vizuri chini ya usimamizi wa Mourinho akiwa Chelsea: Alicheza mechi 19 na kufunga mabao 2 pekee.
"Alikuwa mtoto alipowasili Chelsea na Chelsea ilikuwa na kikosi kizuri hivyo basi ilikuwa vigumu'', alisema mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp akizungumza na runinga ya Ujerumani wiki hii.
"Nadhani sote lazima tukubaliane kwamba Jose Mourinho ni kocha mzuri kwa hivyo mara nyengine mambo huwa hivyo. Kwa hivyo iwapo haiwezekani jiondoe ujaribu tena na hivyo ndivyo ilivyokuwa na Mohamed."
Katika ziara ya hivi karibuni Anfield, Mourinho, ambaye sasa ni mkufunzi wa Manchester United alionekana akimkumbatia raia huyo wa Misri.
Na mahojiano na ESPN Brasil yaliorushwa hewani Jumapili iliopita, raia huyo wa Ureno alizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na mchezaji huyo.
''Ni mimi ndiye niliyemsaini Salah na uamuzi wa kumuuza haukuwa wangu, bali ulikuwa wa Chelsea''.
''Ni mtu mzuri , lakini alikuwa mdogo na hakuwa amejiandaa kimaungo na kifikra wakati alipwasili. Pia alipata utamaduni tofauti. Nafurahi sana kumuona anaendelea vyema, hususan kwa sababu hajafunga dhidi ya United'', alifanya mzaha.
Image result for mohamed salah with klopp
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp akimkumbatia Mohammed Salah
Inawezekana kwamba magoli aliyofunga katika msimu wa 2017/18 yalipita kiwango ambacho mchezaji huyo alikuwa ametaka kuafikia. Katika mechi 48 alizochezea Liverpool katika mashindano yote, raia huyo wa Misri alifunga mabao 43 na kusaidia pasi za mabao 15.
Amekuwa nyota katika kombe la vilabu bingwa Ulaya ambapo ameisaidia Liverpool kukaribia kufika fainali ya kombe hilo kwa mara ya kwanza tangu 2007.
Raia huyo wa Misri ni baraka kwa aina ya mchezo wa Klopp kwa kasi na mashambulio.
Mbali na mafanikio yake, Salah anaweza kufanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza wa Afrika kushinda taji la mfungaji bora Ulaya, taji analokabidhiwa mfungaji bora katika ligi ya Ulaya.
Na msimu wa Salah hautakamilika katika wikendi ya mwisho ya ligi kuu ya Uingerza. Timu ya taifa imefanikiwa kufuzu katika kombe la dunia la 2018 ikiwa ni mara kwanza katika kipindi cha miaka 28 baada ya kampeni ya kuwania kufuzu ambapo Salah alifunga mabao matano kati ya manane huku akitoa usaidizi wa mabao mawili.
Ushujaa wake ulihusisha penalti ya dakika 94 dhidi ya Congo ambayo ilikamilisha kufuzu kwa taifa hilo katika kombe la dunia .
Mo Salah akiichezea Egypt
Salah alifunga mabao matano kati ya magoli ya Misri katika kombe la kombe la dunia.
Na kudhania kwamba kuimarika kwake kulianza kwa bahati. Mnamo mwezi Machi 2012, soka la Misri lilikuwa limedorora: ligi ya taifa hilo ilisitishwa kutokana na janga la uwanja wa Port Said - maandamano ambayo mapema takriban watu 70 walifariki huku wengine 500 wakijeruhiwa.
Huku wakitafuta kushiriki katika mechi kwa maandalizi ya michezo ya Olimpiki mjini London, timu hiyo ya Misri yenye wachezaji wasiozidi umri ya miaka 23 walipanga mechi za kirafiki hidi ya vilabu vya Ulaya.
Mojawapo ni klabu ya Uswizi ya Basel, ambaye rais wake, Bernhard Heusler, alimsajili Salah hapo kwa hapo.
"Kulikuwa na baridi kali lakini alionyesha mchezo mzuri. Alicheza kipindi cha pili pekee lakini sijaona mchezaji mwenye kasi katika maisha yangu yote'', alisema Heusler.
Wachezaji wenza wa Basel wanakumbuka kwamba Salah hakuchezshwa mara moja. Katika mwaka wake wa kwanza katika klabu hiyo mchezaji huyo alitumiwa kama mchezaji wa ziada na ni katika mechi 10 pekee kati ya 29 ambapo alicheza kwa zaidi ya saa moja.
Mchezaji mwenza Philipp Degen, aliambia Sky Sports habari kuhusu Salah alivyomshangaza kila mtu baada ya kufunga bao la ushindi dhidi ya Chelsea katika mechi ya kombe la vilabu bingwa.
Salah akiichezea Basel
Salah alijiunga na Basel mwaka 2012 baada ya kucheza kipindi kimoja pekee ya mechi dhidi ya timu ya Usiwzi
"Tulijaribu kumpa hongera lakini hakukubali. Anasema kuwa alipiga nje mikwaju sita na ni wa saba tu pekee kwa kuwa klabu ilimuamini. Umaruufu wake pia unatokana na kuwa mfuasi mkuu wa dini ya Kiislamu.
Anapendwa sana nchini Misri wakati ambapo taifa hilo limegawanyika katika misingi ya kisiasa ilioanzishwa mika michache iliopita na maandamano ya Uarabuni na mapinduzi ya 2013, lakini Salah anapenda mizizi yake.



Amelipia ujenzi wa shule na hospitali na kuweka jina lake katika mashirika ya hisani ikiwemo kuchangisha $280,000 kwa hazina ya serikali inayolenga kuimarisha kiuchumi familia za Wamisri masikini.
Picha ya Mo Salah mjini Cairo
Mchezaji huyo ni shujaa wa taifa lake la Misri.
Utata unaozunguka jina la Salah unashirikisha madai kwamba alikataa kusalimiana na wachezaji kutoka klabu ya Israel ya Maccabi Tel-Aviv katika mechi dhidi ya Basel mwaka 2013 - alienda kubadili viatu vyake kabla ya mechi kuanza wakati huo raia wengi wa Misri walikuwa wamepinga vitendo vyake na hata kumtaka mchezaji huyo kutoshirikishwa katika mechi ya ugenini ya Israel.
Hata hivyo mbali na kuzomewa na mashabiki wa Maccabi Salah alicheza mechi ya ugenini na kufanikiwa kufunga bao.
Wiki iliopita baada ya raia huyo wa Misri kuisaidia Liverpool kushinda 5-2 dhidi ya Roma katika kombe la vilabu bingwa, Waziri wa Ulinzi Avigdor Lieberman alituma ujumbe katika mtandao wa Twitter kwamba atampigia mkuu wa utumishi wa umma kumsaini Mohammed Salah kwa mkataba wa kudumu na jeshi la Israel.

Chanzo: BBC
Picha: Getty Images

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

tanzania flagLeo nakufahamisha baadhi ya mambo ambayo huenda hukuyafahamu ama ulichukulia kawaida tu. Mambo hayo ni hapahapa Tanzania.  Tanzania ina eneo la kilomita za mraba 945,087. Ina jumla mikoa 31 kote bara na visiwani. Mpaka kufikia mwaka 2017 idadi ya watu nchini ilikadiriwa kuwa milioni 52.554 kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya takwimu. Twende sasa tuanze kuhesabu moja baada ya jingine


#1. Wimbo wa taifa "Mungu Ibariki Tanzania" ni wimbo unaofanana na nyimbo za mataifa ya Afrika Kusini na Zambia. Wimbo huu ulitungwa na Enock Sontonga kwa lugha ya Xhosa "Nkosi Sikelel iAfrika". Wimbo huu pia uliwahi kutumiwa na nchi za Zimbabwe na Namibia.
Image result for enoch sontonga
Enock Sontonga mtunzi wa wimbo Mungu Ibariki Afrika


#2. Ni Tanzania pakee ambako kunapatikana Simba wenye uwezo wa kupanda juu ya miti. Simba hawa wanapatikana katika hifadhi ya taifa ya Ziwa Manyara.
bwindi-and-serengeti-safari_18889423181_o
Simba wenye uwezo wa kupanda miti hifadhi ya Ziwa Manyara.


#3. Tanzania ni nchi ambako fuvu la mtu wa kale zaidi liligunguliwa. Fuvu hili liligunguliwa katika bonde la Olduvai mwaka 1959 na Dr. Louis Leakey.
Olduvai Gorge


#4. Tanzania in Mlima Kilimanjaro ambao ni Mlima mrefu kuliko yote barani Afrika. Mlima huu una urefu wa mita 5895.
Related image



#5. Pamoja na kwamba Kiswahili ni lugha ya taifa, Tanzania inayo makabila 120 ambayo yana mila, desturi na tamaduni tofauti tofauti. Makabila haya yanaishi vyema na kuelewana chini ya mwamvuli wa Utanzania na lugha ya taifa ya Kiswahili.
Related image
Ramani ya Tanzania ikionesha Makabila

#6. Uwepo wa Ziwa Tanganyika ambalo ni ziwa lenye kina kirefu kuliko yote barani Afrika. Ziwa hili lina kina cha futi 4823 ambazo ni sawa na mita 1470. Ziwa hili pia lipo katika nchi za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na Zambia. Ziwa hili pia ni la pili duniani kwa kuwa na kina kirefu zaidi baada ya ziwa Baikal likifuatiwa na Caspian.
Related image
Ziwa Tanganyika

#7. Tanzania ina zaidi ya wanyama pori milioni 4 ambao wamegawanyia katika makundi 430 tofauti ya wanyama.



#8. Hifadhi ya taifa ya Serengeti ni hifadhi maarufu kwa kuwa na mimea na wanyama wa aina tofauti tofauti. Pia ni mbuga inayoongoza kwa kuwa na makundi makubwa ya wanyama wanaohama kila mwaka kundi kubwa likiwa ni kundi la nyumbu. Mwaka 1981 hifadhi hii ilitajwa na UNESCO kama sehemu ya urithi wa kujivunia duniani.
Image result for ngorongoro
Hifadhi ya Serengeti.


#9. Tanznaia ina hifadhi ya taifa ya Ngorongoro ambayo ni maarufu kwa kuwa na ziwa ambalo limetokana na mlipuko wa Volkano; Ziwa Magadi ziwa hili lina kilomita za mraba 264 na maarufu kwa kuwa na ndege wengi aina ya flamingo. Eneo hili la Ngorongoro lina aina mbalimbali za wanyama kama vile tembo, faru, kiboko, pundamilia, nyati n.k. Katika eneo hili jamii ya Wamasai hufanya shughuli zao za ufugaji. Hifadhi hii ilitajwa kama eneo la urithi wa kujivunia wa dunia mwaka 1979.
ngorongoro conservation area
Hifadhi ya Ngorongoro

Ngorongoro-Crater
Ziwa Magadi linalopatikana hifadhi ya Ngorongoro


#10. Tanzania ina mji eneo maarufu kwa kivutio cha utalii ambacho huitwa mji mongwe. Eneo hili lipo Unguja-Zanzibar. Kitovu cha historia yake ni Mji Mkongwe (Stone Town) ulioandikishwa katika orodha ya UNESCO ya “Urithi wa Dunia” (World Heritage). Nyumba za Mji Mkongwe zilijengwa tangu mwaka 1830 wakati Sultani Sayyid Said alipohamisha mji mkuu wake kutoka Omani kuja Unguja.
Image result for mji mkongwe wa zanzibar
Mji Mkongwe uliojengwa tokea enzi za utawala wa Waarabu wa Omani

#11. Uwepo wa daraja la Nyerere linalounganisha wilaya ya Kigamboni kupitia Kurasini. Ujenzi wa daraja hili ulianza Februari 2012 na kukamilika April 2016. Daraja hili lina urefu wa mita 680.
Image result for kigamboni bridge
Daraja la Nyerere linalounganisha wilaya ya Kigamboni na kata ya Kurasini kupitia mkondo bahari wa Kurasini


#12. Ziwa kubwa kulio yote Afrika na Ziwa la tatu kwa ukubwa duniani; Ziwa Victoria lipo Tanzania kwa kiasi kikubwa likipakana na nchi za Uganda na Kenya. Ziwa hili lina ukubwa wa eneo la mraba 68,870 likiwa na urefu wa kilomita 332 na kina cha mita 84 sawa na futi 276.
Related image
Ziwa Victoria

#13. Pengine kuna hili hukulifahamu. Tanzania ina majiji 6 kwa sasa Dar es Salaam likiwa ni jiji kubwa kuliko yote, likifuatia jiji la Mwanza, Arusha na majiji ya Mbeya, Tanga na jiji pipya la Dodoma ambalo limepata hadhi ya jiji April 26, 2018 siku ya kumbukumbu ya maandhimisho Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 19964.
Ramani ya Tanzania ikionesha mikoa yake (mikoa michache haijaoneshwa katika ramani hii)


#14. Kuna fukwe (beach) nzuri na za kuvutia pindi unapohitaji sehemu ya kupunga upepo baharini. Coco beach, Landmark, Ocean view, Lamada, Nungwi, Sea cliff, Zanzi Resort, Tanga beach, Mbezi beach, Malaika Beach Resort n.k. ni baadhi ya fukwe maarufu nchini
tanzania beach



#15. Tanzania inapakana na nchi 8 ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi, Zambia na Msumbiji.
Image result for tanzania map with lakes



#16. Tanzania ilisaidia nchi nyingi za Kusini mwa Afrika kupata uhuru wake kutoka kwa wakoloni; nchi hizo ni Jamhuri za Afrika ya Kusini, Angola, Namibia, Msumbiji na Zimbabwe. Mwalimu Nyerere aliwasaidia wapigani uhuru wa vyama vya ANC, MPLA, SWAPO, FRELIMO na ZANU. 
Related image


#17. Tanzania ina kisiwa kikubwa katika visiwa vyote vilivyo ndani ya maziwa ya bara la Afrika; Kisiwa cha Ukerewe ambacho kina eneo la kilomita za mraba 530. Kisiwa hiki kinapatikana ndani ya Ziwa Victoria. Huenda hukuifahamu hii, basi nimekufahamisha.
Image result for ukerewe map
Kisiwa cha Ukerewe kama jinsi ramani inavyoonekana kwa juu.
Image result for ukerewe map
Kisiwa cha Ukerewe (rangi nyekundu)
#18. Tanzania kuna mawe ambayo ni kuvutio kikubwa cha utalii nchini. Mawe haya yamebebana bila kudondoka kwa miaka mingi sasa. Ni maarufu kama Bismarck rock. Yapo jijini Mwanza na yamewekwa katika noti ya Tsh. 1,000/=
Image result for bismarck rock
Mawe ya Bismarck ambayo ni maarufu sana nchini

#19. Uwepo wa banadari ya Dar es Salaam ambayo inakuza uchumi na pato la taifa kwa kuingiza na kusafirisha bidhaa ndani na nje ya nchi. Bandari hii inasaidia pia nchi za Congo DR, Rwanda, Zambia, Burundi na Malawi.
An aerial view of a section of the port. Credit: Tanzania Ports Authority
Picha ya Bandari ya Dar es Salaam kama ilivyopigwa kutoka juu.

#20. Tanzania ina maeneno 7 ambayo yalitangazwa kuwa ni maeneo ya urithi wa kujivunia duniani. Maamuzi hayo yalitajwa kwa nyakati miaka tofauti na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia elimu, sayansi na utamaduni (UNESCO). Maeneo hayo ni haya yafuatavyo:
  • Hifadhi ya Taifa ya Serengeti
  • Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro
  • Mlima Kilimanjaro
  • Magofu ya kale ya Kilwa na Songa Mnara
  • Michoro ya Mapangoni ya Kondoa
  • Hifadhi ya Wanyama ya Selous
  • Mji Mkongwe Unguja.


Picha zote kwa msaada wa mtandao. Picha hizi si miliki ya blogu hii, kila picha ina mmliki wake.
Unaweza kuacha maoni yako chini ya chapisho hili ama kutuma barua pepe kupitia venancegilbert@gmail.com kama una lolote la kusema ama kuwasiliana nami kwa WhatsApp namba +255712586027 ama kunipigia kwa namba +255753400208.

JUAN MATA ATIMIZA MIAKA 30 HII NI HISTORIA YAKE KWA UFUPI

Mata 2017/2018

JUAN MATA

Mata alizaliwa April 28, 1988 huko Burgos, Hispania. Leo anatimiza miaka 30. Ana urefu wa cm 70 na uzito wa kg 63. Amewahi kucheza michezo 82 akiwa na timu ya Chelsea 2011 hadi 2014 akiifungia klabu hiyo jumla ya magoli 18 katika misimu yote mitatu katika klabu hiyo kabla ya kujiunga na timu ya Manchester United Januari 24, 2014 kwa usajili wa Euro 37.1 milioni. Mpaka sasa Mata ameifungia klabu ya Man U jumla ya magoli 30. Alisaini mkataba ya kuichezea Manchester United Januari 24, 2014 na mkataba wake wa sasa utamalizika June 30, 2019.

Kabla ya Umaarufu

Mata alianza kujihusisha na soka katika klabu ya Real Madrid kuanzia mwaka 2006-2007 na baadaye alijiunga na klabu ya Valencia 2007-2011. Mwaka 2011 alijiunga na klabu ya Chelsea na mwaka 2014 alijiunga na klabu ya Manchester United.

Mata alipokua Chelsea.

Nyongeza

Amewahi kuwepo katik kikosi cha timu ya taifa ya Hispania ambacho kilichukua kombe la dunia mwaka 2010.

Rekodi zake katika Ligi kuu ya Uingereza

Amecheza jumla ya mechi 219 akiwa na jumla ya magoli 48 na akiwa na jumla ya assist 47.
Pia, amewahi kuwa mchezaji wa mwezi katika ligi hii mezi Oktoba 2012 

Nidhamu

Mpaka sasa Mata amepewa jumla ya kadi za njano 15 na kadi nyekundu 1 tu katika ligi hiyo ya Uingereza akicheza fouls 117 na na offsides 87.

MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY SCHOLARSHIPS TENABLE IN EGYPT FOR THE ACADEMIC YEAR 2018/2019


1. Call for Application Applications are invited from qualified Tanzanians for 7 scholarships (5 for Undergraduate, 1 for Masters and 1 Doctorate Degrees ) tenable in Egypt at University of HELWAN for the academic year 2018/2019. 

2. QUALIFICATIONS FOR UNDERGRADUATES
Applicants must:
• have completed and passed Advanced Certificate of Secondary Education and have obtained an average grade of ‘C’ in the relevant subjects; 
• not be admitted in Higher Learning Institutions; 
• not be older than 25 years of age by September 2018; 
• note that studies will be in English or Arabic depending on the academic studies in the relevant faculty 
• apply to the following field: Tourism & Hoteling, Commerce, Engineering and Computer and Technology 
• Have good health. 

3. QUALIFICATIONS FOR POST UNDERGRADUATE 
• Applicant for Maters Degrees must accomplish his/her bachelor's degree with GPA at least 3.2
• Applicant for Doctorate he/she must finish the Msc Degree ,research based Masters 
• Applicant for postgraduate students(i.e Masters and Doctorate Degrees) must apply in the following field: Fine Art and Music NB: For More information please visit this link:  http://www.helwan.edu.eg/InternationalStudents_EN/?page_id=14

4. MODE OF APPLICATION 
• All applicants must attach certified photocopies of Academic Certificates, Transcripts, and birth certificates 
• Applicants must indicate reliable contact telephone numbers or e – mail. All applications should be addressed to: 
The Executive Secretary,
Tanzania Commission for Universities (TCU),
Mlimani Tower, Sam Nujoma, Opposite Mlimani City,
P.O. Box 6562,
DAR ES SALAAM.
Or Email:
es@tcu.go.tz 
so as to reach him not later than 16th September, 2018.

AN ALIEN AT HOME: A POEM BY VENANCE GILBERT


Venance Gilbert in 2017


My poems speaks about crosscutting issues to the Tanzania society at large. I write on political issues, social dynamism, economic issues, cultural aspects and related aspects. There are several issues happening in the Tanzania society at the moment, and today I invite you to recite the poem, "An Alien at Home". It speaks of the contemporary issues in the Tanzanian trending issues, after reading it you might have your comments, please write to me through the contacts after the poem.


An image taken from LasVegasWeekly.com

AN ALIEN AT HOME

It was once before a free boundaries
One could have a word on anything done erroneous
Handcuff men could seize no one
And the leader would come to act in response
But have the courage now to enunciate touching them
You be subjected to the undetectable like that rap man
Or be handcuffed to dark
Followed by late delivering to law paraphrase
Once delivered, the commandment paraphrase will stop the bail
For the argue to shield your being in sinister
From the fixture of seizing self as they crown you
They will ask over your belongingness
“Is you of this of these boundaries?”
But it is them insisting the belongingness
To become of the terra firma positively indeed
When one point their rubbish turns an alien
An alien at home has no mouth
But how is the kinsman an alien?
When he speak on their interests against them wishes.
April 2018.


If you have any comments write to me through one of the following contacts:
Email: venancegilbert@gmail.com
Facebook: VENANCE BLOG (send a message)
Twitter: @Venancetz (send a Direct Message)

ALL RIGHTS RESERVED
Venance Gilbert © 2018.