SCHOLARSHIPS FOR UNDERGRADUATE, GRADUATE AND PhD STUDIES

Tokeo la picha la VENANCE BLOG
The listed Universities below offer various scholarship programmes across the world. If you are interested you may follow the instruction basing on your status of education and interests of the course you wish to perform.



Rhodes Trust, Oxford University
Application Deadline: Various

China Three Gorges University, China
Application Deadline: July 7, 2017

Nanjing University of Information Science & Technology, China
Application Deadline: June 15, 2017

Beijing Sport University, China
Application Deadline: July 10, 2017

The Southeast Asian Regional Center for Graduate Study and Research in Agriculture (SEARCA)
Application Deadline: July 31, 2018

Durham University, United Kingdom
Application Deadline: July 28, 2017

University of New Mexico
Course Starts on June 12, 2017 

Queen Mary University of London, United Kingdom
Application Deadline: January 15, 2018

University of Ghana
Application Deadline: November 3, 2017

Plymouth University in United Kingdom
Application Deadline: June 30, 2017

University of Cape Town, South Africa
Application Deadline: July 31, 2017

Humboldt University of Berlin, Germany
Application Deadline: June 15, 2017

University of Maryland
Course Starts on August 21, 2017

European Commission
Application Deadline: September 8, 2017

Charles Sturt University, Australia
Application Deadline: June 12, 2017

Sapienza University of Rome, Italy
Application Deadline: July 31, 2017

University of Melbourne in Australia
Application Deadline: July 16, 2017

University of Zaragoza, Spain
Application Deadline: June 15, 2017

Trinity College Dublin, Ireland
Application Deadline: June 14, 2017

Penn State University and Coursera
MOOC starts from June 5, 2017

The Radio Television Digital News Association
Application Deadline: June 30, 2017

Government of Hong Kong
Application Deadline: June 19, 2017

University of Lausanne, Switzerland
Application Deadline: June 30, 2017

Uppsala University ,Sweden
Application Deadline: June 30, 2017

University of Greenwich, United Kingdom
Application Deadline: June 28, 2017

The Japan Foundation
Application Deadline: June 1, 2017

Government of Belize
Application Deadline: June 16, 2017

University of Sao Paulo, Brazil
Application Deadline: July 25, 2017

Oxford Internet Institute, UK
Application Deadline: June 26, 2017

University of North Carolina, USA
Application Deadline: August 2, 2017

University of Bristol, United Kingdom
Application Deadline: July 7, 2017

University of Newcastle, Australia
Application Deadline: June 30, 2017

Dublin City University, Ireland
Application Deadline: June 30, 2017

University of Cape Town, South Africa
Application Deadline: Open

University of Oslo, Norway
Application Deadline: June 26, 2017

University of New South Wales, Australia
Application Deadline: July10, 2017

Department of Science & Technology, India
Application Deadline: June 30, 2017

John S. Latsis Public Benefit Foundation
Application Deadline: June 7, 2017

Indian Institute of Management, Bangalore
Course Starts on August 3, 2017

RWTH Aachen University
Course Starts on July 19, 2017




Source: Scholarship Position

UONGOZI LEADERSHIP ESSAY COMPETITION FOR AFRICAN STUDENTS. FULLY-FUNDED TO JOHANNESBURG SOUTH AFRICA


African citizens between the age of 18-25 are invited to submit an essay for this year’s Leadership Essay Contest organised by the Institute of African Leadership for Sustainable Development (UONGOZI Institute).
Application Deadline: 14th July, 2017 (5pm GMT).
Eligible Countries: African countries
To be taken at (country): South Africa
About the Award: The essay contest aims to provide a space for the youth of Africa and the next generation of leaders in the region to contribute to important discussions on leadership.
Type: Essay Contest
Eligibility: The contest is open to all African citizens between the age of 18 – 25 years old, to write about their perspective on leadership as it relates to peace and security in Africa. The essays should respond to the following question:
“If you were a leader, what would you do to ensure that peace and security is achieved and sustained in Africa?”
  • The essays should be no more than 2 A4 pages long. The format shall be of single spaced, Arial font size 11, and sent as a Microsoft Word document.
  • Applicants must be African citizens between the age of 18-25 currently residing in Africa.
  • The selected winners will be required to travel to Johannesburg on 23 August, 2017, therefore valid identification and travel documents will be required for this purpose.
Selection Criteria: Essays will be judged on the basis of originality, creativity, use of language and appropriateness to the contest theme.
All essays must be written in English.
Number of Awards: 5
Value of Program: A grand prize of USD $2,000 will be awarded to the overall winner of the essay contest.  A total of five winners will be selected. Cash prizes will also be awarded to the second to fifth place winners.
The top 5 winners will travel to Johannesburg, South Africa, to receive their awards at a prize giving ceremony to be held during the Africa Leadership Forum Dinner Gala on 24 August, 2017, which will be attended by senior leaders from the public, private and civil society sectors. The overall winner will be asked to read the winning essay at the event.across Africa in
How to Apply: Essays should be submitted by email to submissions@uongozi.or.tz.
Applicants must also submit a written statement of originality and ownership of intellectual property rights.
The final deadline for submission will be Friday, 14th July, 2017 (5pm GMT). The top five finalists will be notified via email by the first week of August. Feedback will not be provided on individual essays.
Template for Statement of Originality:
I, (Enter full name), hereby confirm that the content of the essay I have submitted is my own work and it has not been submitted elsewhere for any other purpose.
I certify that the intellectual property rights for this essay are owned by me and that any information that was sourced elsewhere has been appropriately acknowledged.
(Enter Signature and date)
Award Provider: UONGOZI Institute
**NOTE: Due to the high number of requests to participate from African citizens between 18-25 residing outside of Africa, the eligibility criteria has been revised. The competition is now open to all African citizens residing in and outside of Africa.**

WABUNGE: "BILA KILIMO KWANZA HAKUNA SERIKALI YA VIWANDA"

 
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wamesema bila kuwekeza katika kilimo, azima ya Tanzania kuwa nchi ya viwanda haitatimia.

Kadhalika, wameipongeza Serikali kwa kuondoa tozo 108 zilizokuwa kero kwa wakulima na kuitaka Serikali kuhakikisha tozo zilizoondolewa zinawanufaisha zaidi wakulima na Watanzania, badala ya kuwanufaisha wafanyabiashara pekee. Waliyasema hayo jana kwa nyakati tofauti bungeni Dodoma wakati wakichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Mwaka wa Fedha 2017/18.

Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Ditopile (CCM), alisema kama Tanzania inataka kuwa ya viwanda, haina budi kuwekeza katika utafiti kwa ajili ya sekta ya kilimo ili kubaini namna bora zaidi za kutumia rasilimali na fursa zilizopo ili kuimarisha kilimo na hivyo kusaidia kufikia haraka azima ya kujenga Tanzania ya viwanda. Alisema tayari fursa za kuinua kilimo na kukifanya uti wa mgongo nchini zimeanza kuonekana kwani kwa sasa Tanzania ndiyo inayouza vyakula na bidhaa za biashara katika nchi mbalimbali duniani zikiwemo nchi za Sudan, Kenya na Uganda wanaonunua mazao ya chakula kama mahindi.

“Nchi kama India inanunua kwetu korosho, choroko na tumbaku. Kwa sasa mipango ni kuipeleka nchi kwenye viwanda ni wakati muafaka wa kuwekeza kwenye kilimo kwa kufanya utafiti za kisayansi za namna bora ya kuendeleza kilimo chetu kwa sababu kilimo ndio ajira, chakula na fedha,” alisisitiza. Alisema Tanzania inasifika kwa kufanya utafiti, lakini pamoja na kuwa na uwezo huo bado haujatumika vizuri kuendeleza mambo ya msingi yakiwamo maeneo ya kilimo, mifugo na uvuvi.

“Kwa mfano sisi ndio wenye eneo kubwa katika Ziwa Victoria, lakini takwimu za kidunia zinaonesha Uganda yenye sehemu ndogo katika ziwa hilo ndiyo inayoshika nafasi ya juu; ya sita duniani kwa uvuvi huku sisi Tanzania tukishika nafasi ya nane,” alisema. Mbunge wa Mbinga Mjini, Sixtus Mapunda (CCM) aliitaka serikali iwekeze kwenye utafiti wa kilimo ili kuyabaini maeneo ya kijiografia na kisayansi yanayoweza kuikuza kwa kasi sekta hiyo ya kilimo inayokwenda sambamba na sekta ya viwanda.

“Kwa mfano Morogoro ina udongo wenye rutuba na mito inayotiririsha maji kwa mwaka mzima, utafiti ukifanyika wa namna bora ya kutumia rasilimali hizo, ni wazi kuwa Morogoro pekee inaweza kulisha Tanzania nzima,” alisema. Pamoja na hayo mbunge huyo alisema si kweli utitiri wa kodi zilizofutwa na serikali umewalenga zaidi wafanyabiashara na wenye kampuni na si wakulima kwa kuwa wafanyabiashara na kampuni hizo kutokana na kufutwa kwa tozo hizo kuanzia sasa watanunua mazao na bidhaa hiyo kwa bei inayostahili.

Kwa upande wake Mbunge wa Hanang, Mary Nagu (CCM), alisema serikali haina budi kuzingatia kuwa kilimo ndicho kinachochangia ajira kwa Watanzania takribani asilimia 65, kinachozalisha chakula kwa Watanzania kwa asilimia 100 na kuingiza asilimia 28 katika pato la taifa. “Hii ni sekta muhimu sana, ni vema Serikali ione umuhimu wa kuifanyia mageuzi sekta ya kilimo na kuongeza bajeti ya wizara ya kilimo kwani hali ilivyo sasa badala ya kilimo kukua, kinashuka kwa kasi,”alisema.

Alisema takwimu zinaonesha kuwa, mwaka 2011 kilimo kilikuwa kwa wastani wa asilimia 3.5 lakini miaka sita baadaye yaani mwaka2016 kilimo hicho kilishuka na ukuaji wake kufikia asilimia 1.7 hali inayozidisha umasikini kwa Watanzania,” alisema Dk Nagu. Alisema pamoja na ukuaji wa kilimo pia bajeti ya Wizara ya Kilimo imekuwa ilishuka badala ya kupanda kila mwaka kwani mwaka 2011 bajeti ya Wizara hiyo ilikuwa asilimia 7.8 ya bajeti nzima ya Serikali, lakini katika bajeti ya mwaka 2016, bajeti ya Wizara hiyo ilishuka na kufikia asilimia 4.9.

Nagu aliyewahi kuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji katika Serikali ya Awamu ya Nne, kupongeza hatua ya Serikali kuondoa utitiri wa kodi zenye kero kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi, aliitaka Serikali ihakikishe kuwa hatua hiyo inawanufaisha zaidi wakulima, wafugaji na wavuvi na si kwa wafanyabiashara.

Kwa upande wake mbunge wa Malindi, Ally Saleh (CUF) aliishauri serikali iwekeze zaidi kwenye fikra za kuleta mabadiliko ya kilimo, mifugo na uvuvi kutokana na ukweli kuwa Tanzania imebarikiwa rasilimali kama vile maziwa, mito, bahari na mikoa yenye rutuba ambayo endapo itatumiwa vema itakuza sekta hizo.
“Sasa hivi tuna tatizo gani, badala ya kilimo kwenda mbele kinashuka. Leo hii haiwezekani sisi tunaongoza kwa kuwa na ng’ombe wengi kuliko Kenya, lakini wao wanatuzidi kwa kuzalisha maziwa. Tunahitaji fikra mpya,” alisema. Alisema Tanzania kuna hekta takribani milioni 13.5 zinazolimika na hekta milioni 1.5 za mikoko, pia ni nchi ya tatu Afrika lakini pia nchi ya 11 duniani kwa kuwa na wingi wa mifugo, lakini bado rasilimali hizo haijatumiwa vizuri.

Mbunge wa Momba, David Silinde (Chadema), aliishauri Serikali iwekeze zaidi katika kilimo kupitia mbolea ya uhakika, dawa za mimea, masoko na miundombinu bora kwa kuwa huo ndio usalama wa watanzania katika chakula.


Chanzo: Habari Leo

TRUMP AWASILI SAUDI ARABIA

Rais Donald Trump  akikaribishwa  kwa bashasha  kubwa  na  ukoo  wa  kifalme  wa  Saudi Arabia  jana , wakati  akiweka  kando, japokuwa  kwa  muda  tu , utata mkubwa  unaoukumba utawala  wake  mjini  Washington.
Saudi Arabien - Donald Trump zu Besuch in Riad (picture-alliance/dpa/AP/E. Vucci)
Rais Trump akilakiwa mjini Riyadh
Trump  amewazawadia  wenyeji wake  mpango  wa mauzo  ya  bilioni 110  wa  silaha  wenye  lengo  la  kuimarisha  usalama  wa  Saudi  Arabia pamoja  na  makubaliano  kadhaa  ya  kibishara.
"Hii  ni  siku  muhimu  sana, uwekezaji  mkubwa  katika  Marekani ," Trump  alisema wakati wa  mkutano  na  mwanamfalme Mohammed bin Nayef.
Auslandreise US-Präsident Trump in Saudi-Arabien (Getty Images/AFP/M. Ngan)
Rais Trump (Kushoto) akisalimiana na mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz(kulia)
Ziara  katika  mji  mkuu  wa  Saudi Arabia  ilikuwa  ni ziara  ya  kwanza  ya  Trump  nje  ya nchi  akiwa  rais, ikiwa  ni  ziara  itakayokuwa  na vituo  vitano ambayo  itamchukua  katika mataifa  ya  mashariki  ya  kati  hadi  Ulaya. Ni  rais  pekee  wa  Marekani kuifanya  Saudi Arabia , ama  taifa  lolote  lenye  Waislamu  wengi kuwa  kituo  chake  cha  kwanza  nje  ya nchi.
Trump  aliwasili  mjini  Riyadh akizongwa  na  hatua  yake  ya  kumfuta  kazi  mkurugenzi  wa FBI James Comey  na  hali  ya  kufichuka zaidi  juu  ya  uchunguzi  wa  serikali  kuu kuhusiana  na  uwezekano  wa  mahusiano  ya kampeni  na  Urusi.
Akikimbia  mambo  mjini Washington  na  kukumbatiwa  na  familia  ya  kifalme inaonekana kumpa  nguvu  Trump.
Melania  hakufunika nywele
Baada  ya  safari  ya  usiku  kucha , rais  alilakiwa  katika  uwanja  wa  ndege  na  Mfalme Salman , hali  iliyoonekana kuwa  ni  ya  aina  ya  kipekee  kwa  kuwa  mfalme  hakuonekana mwaka  jana  wakati  wa  kumlaki rais Barack Obama  katika  ziara  yake  ya  mwisho  nchini Saudi  Arabia.
Saudi Arabien US-Präsident Trump und König Salman bin Abdulaziz al-Saud unterzeichnen Verträge (Getty Images/AFP/M. Ngan)
Rais Trump akitia saini makubaliano ya mauzo ya silaha pamoja na mfalme Salman bin Abdulaziz al-Saud
Trump  aliongozana  katika  ziara  yake  hiyo  na  mkewe Melania  Trump, ambaye  alivalia suti  nyeusi na  mkanda  wa  dhahabu, lakini  hakufunika  nywele  zake  katika  nchi  hiyo  ya kifalme  ambayo ni  ya  kihafidhina  zaidi, kwa  mujibu  wa  utamaduni  wa  ujumbe  wa kimagharibi.
Mapokezi  makubwa  ya  Trump  yanaakisi  kiwango  ambacho  Saudi  Arabia  imekuwa hairidhishwi  na  Obama. Wasaudi  kwa  kiasi  kikubwa  hawakumuamini  Obama  kuhusiana na  mahusiano  yake  na  Iran na  wamekasirishwa  na  mtazamo  wake  wa  kujizuwia kuhusiana  na  vita  vya  wenyewe  kwa  wenyewe  nchini  Syria.
Auslandreise US-Präsident Trump in Saudi-Arabien - Melania Trump (Getty Images/AFP/M. Ngan)
Mke wa rais wa Marekani Melania Trump(kushoto) akiwa pamoja na mwanamfalme Muhammad nin nayef bin Abdulaziz al-Saud
Wairani wachagua rais
Wakati  Trump  anawasili , Wairani  walikuwa  wamemchagua  tayari  Hassan Rouhani , mmoja  kati  ya  washirika  wa  Obama   katika  makubaliano  ya  kihistoria  yaliyokuwa  na lengo  la  kudhibiti  nia  ya  Iran  ya  kujipatia  silaha  za  kinyuklia, kwa  muhula  wa  pili  wa miaka  minne kuwa  rais, akielezea  msukumo  wake  kwa  ajili  ya  uhuru  zaidi  na kuzijongelea  zaidi  nchi  nyingine  duniani.
Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Marekani  Rex Tillerson  amesema  ana  matumaini Rouhani  atatumia  kipindi chake  hicho  kipya  madarakani  "kuanza  mchakato  wa kuvunjilia  mbali  mtandao  wa kigaidi  wa  Iran."
Donald Trump, Melania Trump, König Salman (picture alliance/AP Photo/E.Vucci)
Rais Trump akiwasili katika kasri la mfalme wa Saudi Arabia



Trump  hakutoa  matamshi yeyote  katika  siku  yake  ya  kwanza  nje  ya  nchi  na  alitumia muda  wake  mwingi  akitembea  kati ya  vyumba  mbali  mbali  vya  kasri  la  mfalme.
Chanzo: DW

KOREA KASKAZINI IMEFANYA JARIBIO LINGINE LA KOMBORA

Korea Kaskazini yalifanyia majaribio kombora lingineJeshi la Korea Kusini linasema kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio kombora lingine.Ofisi ya kijeshi nchini Korea Kusini inasema kuwa kombora hilo lilirushwa siku ya Jumapili jioni saa za Korea.

Jaribio hilo linafanyika wiki moja baada ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora lingine ambalo inadai kuwa ni jipya na ambalo lina uwezo wa kubeba silaha kubwa ya nyuklia. Wachambuzi wanasema kwamba huko mbeleni linaweza kuifikia Alaska.

Jumatatu iliyopita baraza la usalama la Umoja wa Mataifa liliitaka Korea Kaskazini kusitisha majaribio kama hayo.

Baraza hilo la UN lilisisitiza umuhimu wa nchi hiyo kuachana na hatua hizo.Korea Kaskazini inafahamika kwa kuunda zana za nyuklia na imefanya jumla ya jaribio matano ya nyuklia na ya makombora yenye uwezo wa kusafirisha zana hizo hadi maeneo inayolenga.

Korea Kusini inasema kuwa jaribio la hivi punde lilifanyiwa eneo la Pukchang magharibi mwa nchi.

Chanzo: BBC & DW

VIDEO: JAY 2 THE HUSTLER X CAST BEEZY - TIME IS NOW (OFFICIAL VIDEO)

 

MGAHAWA WAKUMBWA NA KASHFA YA KUUZA NYAMA YA BINADAMU

Mkahawa wakumbwa na habari bandia za kuuza ''nyama ya binadamu''Mgahawa mmoja mjini London umekumbwa na habari bandia za kuuza nyama ya mtu.

Wafanyikazi katika mkahawa wa Karri Twist katika eneo la New Cross nchini Uingereza wamehangaishwa kwa kupigiwa simu kutoka kwa wateja wanaosema ''Kwa nini hamujafunga''?.
Mkahawa huo wa chakula cha jioni ni mwathiriwa wa habari za mzaha zilizodai kwamba mmiliki wake alikamatwa kwa kuweka nyama ya binadamu katika chakula na kwamba miili 9 ilipatikana katika jokovu la mkahawa huo.

Na watu wengine waliamini mzaha huo.
Habari hiyo ilichapishwa katika chombo cha habari cha channel23news.com, mtandao ambao wateja wake wanaweza kuchapisha habari za uwongo ili kuwafanyia mzaha rafiki zao kwa kuchapisha moja kwa moja katika mtandao wa fecbook.

Shinra Begum ambaye ndio mmiliki wake aliambia Newsbeat kwamba biashara hiyo ya familia imekumbwa na wakati mgumu tangu habari hiyo ilipochapishwa siku ya Alhamisi.
''Wakati watu walipoanza kunipigia simu na kuuliza iwapo tulikuwa tukiuza nyama ya binadamu sikuamini''.

''Nilishtuka nilipoaana habari hiyo katika mtandao na kuendelea kusambazwa katika mtandao wa facebook''.

Sasa watu wametishia kulivunja jengo letu na nimelazimika kuketi chini na mteja ili kumuelezea kwamba yote hayo ni madai ya uwongo.

Shinra anasema kuwa alilazimika kuripoti kwa maafisa wa polisi kwa sababu lilikuwa swala lililomtia wasiwasi mkubwa.

Njia ya pekee ambapo Karri Twist iliweza kukabiliana na chuki hiyo ni kupitia kuchapisha katika mtandao wao ili kuhakikisha kwamba watu wanajua kwamba hilo halikuwa la kweli.

Chanzo: BBC

NDEGE YA MAREKANI YAZUILIWA NA NDEGE ZA CHINA

Ndege za China zaizuia ndege ya MarekaniNdege mbili za kijeshi za China zimeizuia 'vibaya' ndege ya Marekani kulingana na jeshi la Marekani.

Ndege hiyo inayohusika na kufanya uchunguzi, ilikuwa katika safari yake ya kutaka kugundua mionzi katika anga ya kimataifa iliopo mashariki mwa bahari ya China.
Ndege hiyo ilikuwa imetumiwa kugundua ushahidi kuhusu majaribio ya kinyuklia ya Korea Kaskazini. 

China imekuwa ikituhumu vitendo vya Marekani karibu na maji hayo yenye utajiri mkubwa yaliopo katika pwani yake ,hatua ambayo imesababisha wasiwasi kati ya mataifa hayo mawili.
''Swala hilo linaangaziwa na China kupitia njia mwafaka ya kidiplomasia mbali na zile za kijeshi'', msemaji wa jeshi la angani la Marekani Luteni kanali Lori Hodge amesema.
''Uzuizi huo haukufanywa kwa njia ya ''utaalamu'' kutokana na hali ya rubani wa ndege hiyo ya China ikiwemo kasi ya ndege zote mbili'', aliongezea akisema uchungzi wa kijeshi unaendelea.
Bahari hiyo ya kusini mwa China
Bahari ya Kusini mwa China
Mnamo mwezi Februari , ndege moja ya Marekani ilianza kile Washington ilielezea kuwa doria yake ya kawaida kusini mwa bahari ya China ikiandamana na idadi fulani ya meli za kijeshi.
Ndege na meli hizo zilielekea katika eneo hilo licha ya onyo kutoka China dhidi ya kutoa changamoto yoyote kwa uhuru wa China katika eneo hilo.

Kwa nini bahari hiyo ya kusini mwa China inazozaniwa?
Mnamo mwezi Mei 2016 ndege mbili za kijeshi za China zilizuia ndege nyengine ya Marekani iliokuwa katika anga ya kusini mwa bahari ya China.

Wakati huo, jeshi la Marekani lilisema kuwa ilikuwa ikipiga doria ya kawaida katika eneo hilo.

Chanzo: BBC

MABOMU YASABABISHA WATU ZAIDI YA ELFU 50 KUHAMA UJERUMANI

Mabomu kutoka vita vya pili vya dunia bado yako Hannover

Operesheni kubwa ya kuwaondoa wakaazi wengi wa mji wa Hanover ulioko kaskazini mwa Ujerumani, inaendelea, ya kuwahamisha zaidi ya watu elfu 50 baada ya mabomu makubwa ya wakati wa vita vya dunia, kupatikana kama hayajalipuka.
Wakaazi hao wanatarajiwa kuondoka majumbani mwao baadaye leo, ili kuwapa nafasi wataalamu wa kutegua mabomu, kuhamishia mahala salama mabomu hayo ambayo yanakisiwa kuwa matano.

Operesheni hiyo itachukua siku nzima, na hata zaidi ikiwa mabomu mengineyatapatikana.
Washambuliaji walivamia mji wa Hanover mara 125 kwa mabomu, wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia.
Wataalamu wanaamini kuwa mabomu ambayo hayakulipuka huenda yako chini ya jengo hiliHaki miliki ya picha Getty Images.    Wataalamu wanaamini kuwa mabomu ambayo hayakulipuka huenda yako chini ya jengo hili                
Zaidi ya asilimia 20 ya mabomu yaliyoangushwa mjini humo hayakulipuka.
Baadhi ya mabomu mengine yalikuwa na vifaa vinavyochukua muda mrefu kulipuka, na ambayo kwa sasa yameanza kuoza, na kusababisha hatari kubwa.


Chanzo: BBC

WAPIGANAJI WA HAMAS WAPATA KIONGOZI MPYA

Ismael Haniyeh ndio kiongozi mpya wa kundi la Hamas
Ismael Haniyeh ndio kiongozi mpya wa kundi la Hamas
Wapiganaji wa Palestina Hamas wamepata kiongozi mpya.
Kiongozi huyo ni Ismail Haniyeh ambaye hadi hivi karibuni alikuwa ndio kiongozi wa kundi hilo katika ukanda wa Gaza.
Akijulikana kama kiongozi anayetumia akili nyingi wakati wa kutatua maswala, anachukua mahala pake Khaled Meshaal ambaye ameliongoza kundi hilo akiwa ughaibuni kwa miongo miwili.
Uchaguzi wa kiongozi mpya ulifanyika kupitia njia ya Video Link kati ya wajumbe waliopo katika ukanda wa Gaza na wale waliopo nchini Qatar ambako Meshaal ana makao yake.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa bwana Meshaal anaachia ngazi wakati ambapo Hamas limeanza kulegeza msimamo wa kisiasa.
Kwa mara ya kwanza wiki iliopita katika sera mpya kundi hilo liliwachilia wito wake wa kuiharibu Israel.
Hamas bado lina wapiganaji wake katika eneo la Gaza na bado linaaminika kuwa kundi la kigaidi na Israel Marekani na mataifa ya bara Ulaya.

Chanzo: BBC

MANCHESTER CITY YAIBURUZA VIBAYA CRYSTAL PALACE

Tokeo la picha la Machester City
Klabu ya Manchester City imerudi katika nafasi yake ya tatu katika ligi ya Uingereza baada ya kupata ushindi mkubwa dhidi ya Crystal Palace ambayo imeshindwa kwa mara ya tatu mfululizo.
City ilihitaji dakika mbili pekee kupata bao la kwanza baada ya David Silva kufunga baada ya kurudi kutoka kuuguza jereha.
Wenyeji waliongeza bao la pili dakika tatu katika kipindi cha pili wakati Vincent Kompany alipopiga mkwaju ulioingia katika kona ya ya juu ya goli na baadaye Kevin De Bruyne akafunga bao la tatu.
Ndoto ya Palace ilithibitishwa baada ya Raheem Sterling kufunga bao la nne kabla ya beki Otamendi kufunga bao la tano katika dakika za lala salama.
Kikosi hicho cha Sam Allardyce kiko pointi tano juu ya eneo la kushushwa daraja na kinaweza kuwa hatarini iwapo klabu za Hull City na Swansea zitaibuka washindi siku ya Jumamosi.

RAIS MAGUFULI AMETUMA SALAMU ZA POLE KWA WAFIWA WA AJALI ARUSHA

Tokeo la picha la magufuli
Hii hapa chini ni taarifa kama ilivyoandikwa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko mkubwa taarifa ya vifo vya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu 2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha vilivyotokea leo saa 3 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika eneo la Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.
Wanafunzi na walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni ambako limesababisha vifo hivyo na majeruhi watatu.
Kufuatia ajali hiyo, Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo na kueleza kuwa ajali hiyo imezima ndoto za watoto waliokuwa wakijiandaa kulitumikia Taifa na imesababisha uchungu, huzuni na masikitiko makubwa kwa familia za marehemu na taifa kwa ujumla.
"Ndugu Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo naomba unifikishie pole nyingi kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wote wa wanafunzi, walimu na dereva waliopoteza maisha, hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na uwaambie naungana nao katika majonzi na maombi.
"Muhimu kwa sasa tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema, majeruhi wapone haraka na wote walioguswa na msiba huu wawe na moyo wa subira, ustahimilivu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu" Amesema Rais Magufuli.