Kipofu alimpiga mtu mmoja hadi akamuua.
Akapelekwa mahakamani, Hakimu akamuuliza kwa nini umeua na wakati huoni?
Kipofu akajibu, marehemu aliniambia mwenyewe nipige uone, kwa vile mi nilikuwa na hamu kubwa ya kuona nikampiga kwa nguvu zangu zote bahati mbaya akafariki!!... Hakimu akaduwaa!!!
"KWA MUJIBU WA MAELEZO YA KIPOFU, KAMA WE UNGEKUWA HAKIMU UNGEAMUA NINI HAPO???!!"
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment