Tukio hilo lilitokea juzi tarehe 12 Juni 2013 katika wilaya ya Urambo mkoani Tabora akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa niaba ya kamanda wa jeshi la polisi mkoani humo Kaimu Kamanda, Edward Lukombe amemtaja marehemu kuwa ni Juvenali Wambura mwenye umri wa miaka 42, inadaiwa kuwa siku ya tukio baadhi ya wanywaji katika glosari moja waliandaa shindano ambalo si rasmi kuwa mnywaji atakayekunywa viroba 12 ataondoka na zawadi ya pesa taslimu ambapo inadaiwa marehemu alijigamba kuwa angekunywa viroba vyote na hivyo kuibuka mshindi inadaiwa kuwa marehemu alianza kunywa viroba hivyo kwa kasi ya ajabu ambapo alipomaliza kunywa kiroba cha mwisho cha 12 aliishiwa nguvu na hivyo wenzake kulazimika kumpeleka katika hospitali ya wilaya ya urambo kwa matibabu lakini bahati mbaya akafariki dunia muda mfupi.
Kaimu kamanda huyo amesema kuwa licha ya marehemu kunywa viroba vyote hivyo inaelekea hakuwa amepata lishe ya kutosha siku hiyo.
Kaimu kamanda huyo ametahadharisha wanywaji mkoani humo kunywa kwa wastani na kuwa wamekula na sio kunywa kwa mashindano ili kuepuka madhara kama hayo.
Venance ©Juni, 2013
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment