Tukio hilo lilitokea juzi tarehe 12 Juni 2013 katika wilaya ya Urambo mkoani Tabora akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa niaba ya kamanda wa jeshi la polisi mkoani humo Kaimu Kamanda, Edward Lukombe amemtaja marehemu kuwa ni Juvenali Wambura mwenye umri wa miaka 42, inadaiwa kuwa siku ya tukio baadhi ya wanywaji katika glosari moja waliandaa shindano ambalo si rasmi kuwa mnywaji atakayekunywa viroba 12 ataondoka na zawadi ya pesa taslimu ambapo inadaiwa marehemu alijigamba kuwa angekunywa viroba vyote na hivyo kuibuka mshindi inadaiwa kuwa marehemu alianza kunywa viroba hivyo kwa kasi ya ajabu ambapo alipomaliza kunywa kiroba cha mwisho cha 12 aliishiwa nguvu na hivyo wenzake kulazimika kumpeleka katika hospitali ya wilaya ya urambo kwa matibabu lakini bahati mbaya akafariki dunia muda mfupi.
Kaimu kamanda huyo amesema kuwa licha ya marehemu kunywa viroba vyote hivyo inaelekea hakuwa amepata lishe ya kutosha siku hiyo.
Kaimu kamanda huyo ametahadharisha wanywaji mkoani humo kunywa kwa wastani na kuwa wamekula na sio kunywa kwa mashindano ili kuepuka madhara kama hayo.
Venance ©Juni, 2013
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...
Comments
Post a Comment