BOMBA la mafuta ghafi kutoka Hoima katika Ziwa Albert nchini Uganda, sasa ni rasmi
kwamba litapita katika ardhi ya Tanzania kwenda Bandari ya Tanga, ambako ndiko meli kubwa za mafuta, zitakapotia nanga kubeba mafuta hayo kwenda sehemu mbalimbali duniani.
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, imeeleza kuwa Serikali ya Uganda imetangaza rasmi uamuzi wake wa kutumia bandari hiyo.
Kwa hatua hiyo, bomba hilo linalotakiwa kuwa limekamilika ifikapo 2018, litaingilia Mkoa wa Kagera kutoka nchini Uganda na kupita katika mikoa ya Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma hadi Bandari ya Tanga.
Rais Museveni
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, ndiye aliyetangaza uamuzi huo wakati wa mkutano wa 13 wa Ushoroba wa Kaskazini uliomalizika jijini Kampala jana.
“Ujumbe wa Tanzania uliokamilisha mazungumzo hayo na kushuhudia utangazwaji wa hatua hiyo, uliongozwa na Dk Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa,” imeeleza taarifa hiyo.
Mbali na kiongozi huyo, taarifa hiyo imeeleza kuwa jopo la wataalamu lililoshiriki katika mazungumzo hayo, liliongozwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambalo litaendelea kubakia Kampala kukamilisha mpango huo wa bomba la mafuta ghafi, ambalo litanufaisha pia nchi zingine za Afrika Mashariki na Kati.
Mchakato ulivyokuwa
Awali, serikali za Uganda na Kenya, ziliwahi kufikiria kupitisha bomba hilo katika ardhi ya Kenya, kwa nia ya kutumia bandari itakayojengwa ya Lamu nchini humo.
Hata hivyo, wakati hatua za kina hazijachukuliwa, Rais wa Tanzania, Dk John Magufuli na Rais Museveni walikutana mwanzoni mwa mwezi uliopita na baada ya mazungumzo yao, wakatoa agizo kuwa mchakato wa ujenzi wa bomba hilo, ufanyike kwa kasi.
Baada ya kikao cha marais hao kutoa agizo hilo, kilifuata kikao cha Rais Magufuli na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Total, tawi la Afrika Mashariki, Javier Rielo, ambapo kiongozi huyo wa kampuni alimhakikishia Rais Magufuli kuwa kampuni yao itaanza ujenzi wa bomba hilo haraka iwezekanavyo, kwa kuwa fedha za kutekeleza mradi huo zipo.
Katika mazungumzo hayo, Rielo alimueleza Rais Magufuli kuwa kampuni yake inatarajia kutumia Dola za Marekani bilioni 4 ambazo tayari zimeshaandaliwa.
Bomba hilo litakuwa na urefu wa kilometa 1,410 na litasafirisha mafuta ghafi mapipa 200,000 kwa siku kutoka Ziwa Albert nchini Uganda, hadi Bandari ya Tanga na ujenzi wake unatarajiwa kuzalisha ajira za moja kwa moja 1,500 na ajira zisizo za moja kwa moja 20,000.
Makubaliano ya awali
Katika utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli na Rais Museveni, Machi 17 mwaka huu, serikali za Tanzania na Uganda pamoja na kampuni ya Total E&P Uganda na Shirika la Maendeleo ya Petroli la Tanzania (TPDC), walitia saini mpango wa pamoja wa utekelezaji wa mradi huo.
Mpango huo ulitiwa saini na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania, Profesa Muhongo; Waziri wa Maendeleo ya Nishati na Madini wa Uganda, Irene Muloni; Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dk James Mataragio na Meneja Mkuu wa Total E&P Uganda, Adewale Fayemi.
Kwa nini Tanzania
Baada ya utekelezaji wa agizo hilo kufikia hatua ya mkataba kuliibuka mjadala kuhusu uhakika wa bomba hilo kupita Tanzania baada ya Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta kukutana na Rais Museveni, kujaribu kuangalia uwezekano wa bomba hilo kupitia Kenya kwenda Lamu.
Pamoja na jitihada hizo, Bandari ya Tanga, ilibakia kuwa eneo pekee lenye mazingira bora, nafuu na yenye ufanisi kwa utekelezaji wa mradi huo.
Uzoefu
Mbali na Bandari ya Tanga kuwa ya kimkakati zaidi katika utekelezaji wa mradi huo, taarifa za ndani za wataalamu wa mafuta, zilionesha kuwa pia Tanzania ndiyo yenye uzoefu wa muda mrefu na wa hivi karibuni wa ujenzi, uendeshaji, ulinzi na uelimishaji jamii katika miradi ya bomba la mafuta.
Uzoefu wa muda huo mrefu unatajwa kuwa ni wa ujenzi, uendeshaji na uhudumiaji wa Bomba la Mafuta la Tanzania na Zambia (Tazamaaaaaa
tangu mwaka 1968, likitoka Dar es Salaam mpaka Ndola Zambia.
Bomba hilo lenye kipenyo cha nchi 8 mpaka 12 na urefu wa kilometa 1,710; kati ya hizo kilometa 860 zipo kwenye ardhi ya Tanzania na limekuwa likipitisha mafuta tani milioni 1.1 kwa mwaka.
Tanzania pia ina sifa ya uzoefu wa ujenzi, uendeshaji na uhudumiaji wa bomba la gesi kutoka Songo Songo mpaka Dar es Salaam, lenye kipenyo cha nchi 12 na urefu wa kilometa 25 kutoka kisiwa cha Songo Songo mpaka Somangafungu.
Pia kuna bomba lingine la urefu wa kilometa 207 na kipenyo cha nchi 16, kutoka Somangafungu mpaka Ubungo Dar es Salaam, mbali na bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara mpaka Kinyerezi Dar es Salaam lenye zaidi ya kilometa 490.
Lipo pia bomba la gesi linalotoka Mnazi Bay kwenda Mtwara, urefu wa kilometa 27 na kipenyo cha nchi 8, ambalo limeanza kutumika tangu 2006.
Uzoefu wa kazi
Katika ujenzi na uendeshaji wa mabomba hayo kwa miaka mingi, Tanzania imejijengea uzoefu wa kazi ya kupata ardhi kwa ajili ya kupitisha miundombinu ya bomba, tofauti na ugumu uliopo kwa nchi shindani ya Kenya na kusimamia masuala ya kimazingira.
Tanzania pia imefanikiwa katika kusimamia wakandarasi wa kimataifa na matarajio ya umma wakati wa ujenzi na uendeshaji wa miradi hiyo na hata katika ulinzi wa miundombinu hiyo ambao umekuwa ukishirikisha jamii.
Utayari
Bandari ya Tanga
Sifa nyingine iliyochangia Tanzania kukubalika zaidi katika mradi huo kwa kiwango cha kusaini mkataba wa utekelezaji tofauti na Kenya, ni utayari na mazingira wezeshi ya asili ya Bandari ya Tanga.
Wakati Kenya wakijadili namna bomba hilo litakavyotumia bandari ambayo haijajengwa ya Lamu, kwa ajili ya kuuza mafuta, Bandari ya Tanga yenyewe iko tayari kwa kazi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Bandari ya Tanga imeshakamilisha Tathimini ya Athari za Kimazingira (EIA) na Upembuzi Yakinifu, wakati njia ya Tanga ya bomba hilo imekwishaainishwa na haitapitia katika hifadhi za taifa wala mapori ya akiba.
Bandari ya Tanga inayo fursa ya kutumika zaidi na mradi huo, kwa kuwa haina msongamano wa shughuli za bandari na tayari Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari (TPA), kwa mujibu wa taarifa hiyo, imeshatenga fedha za upanuzi utakaohitajika na eneo.
Bandari hiyo pia imeunganishwa kwa reli na barabara za lami, zinazokwenda nchi za jirani na hivyo iko tayari kuanza kutumika kwa ajili ya kuingizia mizigo kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.
Bandari ya Tanga pia ndiyo yenye kingo za asili zinazoruhusu shughuli za upakiaji mafuta kufanyika mwaka mzima bila kusimama, tofauti na bandari zingine ambazo kipindi cha mawimbi makali ya bahari, huwa na wastani wa siku 40 ambazo husababisha shughuli za upakiaji au upakuaji mizigo kusimama.
Pia bandari hiyo inatumika na hivyo kuwa tayari kwa matumizi ya haraka kama ilivyo dhamira ya Rais Magufuli na Rais Museveni, na hata ujenzi wa boya la kupakia mafuta unatarajiwa kuchukua mwaka mmoja tu hivyo kukamilika Juni 2017, kabla ya muda uliowekwa na mwekezaji wa kuanza kuuza mafuta wa 2018.
Gesi mikoa saba
Mbali na fursa hizo za pekee, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dk Mataragio, mradi huo unafungua fursa kwa usambazaji wa gesi asilia katika mikoa ya Kaskazini yaani Dodoma, Singida, Shinyanga, Tabora, Geita, Mwanza na Kagera na vile vile nchi za jirani ambazo zitahitaji gesi ya Tanzania. Pamoja na hayo, kutakua na ujenzi wa barabara mpya kiasi cha Kilometa 200 na uboreshaji wa barabara zilizopo kiasi cha Kilometa 150 na madaraja.
Aidha utekelezaji wa mradi huo pia utachochea shughuli za utafiti wa mafuta Tanzania, kwani bomba hilo linapita maeneo ambayo yana uwezekana mkubwa wa kuwa na mafuta, hivyo uwapo wa miundombinu unavutia zaidi uwekezaji katika shughuli za utafiti wa mafuta na gesi.
Fursa nyingine inayotajwa ni ya matumizi ya reli ambapo takribani mabomba 123,000 yatasafirishwa katika kipindi cha ujenzi huo.
Chwnzo: Habari Leo
MALAWI IMETEKETEZA TANI 2 ZA PEMBE ZA NDOVU KUTOKA TANZANIA
Malawi imeteketeza tani 2.6 ya pembe za ndovu ambazo zilinaswa na maafisa wa usalama zikitokea nchi jirani ya Tanzania.
Meno hiyo 781 ya tembo ambayo inakisiwa kugharimu takriban dola milioni tatu ilipatikana baada ya operesheni dhidi ya ulanguzi na uwidaji haramu.
Mkurugenzi wa idara inayosimamia mbuga za wanyama pori Bright Kumchedwa, amesema kuwa hiyo ni ishara ya kwanza na dhabiti kutoka kwa Malawi kuwa haitaruhusu tena ardhi yake kutumika kulangua bidhaa za uwindaji haramu.
Hafla ya hiyo ya kihistoria ilifanyika katika eneo la Mzuzu kaskazini mwa nchi hiyo.
Kenya inatarajiwa kutekeleza hatua kama hiyo mwishoni mwa mwezi huu.
Kenya imekamata takriban tani 120 ya meno ya ndovu.
Chanzo: BBC
ZITTO KABWE: RAIS AMELIINGIZIA TAIFA HASARA YA TSH. BILIONI 36
Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa Rais John Pombe Magufuli ameliingizia taifa hasara ya bilioni 36 mpaka sasa toka alipoingia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook aliandika kuwa kitendo cha Rais Magufuli kushindwa kuchukua hatua juu ya malipo ya IPTL ambayo yanalipwa na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kila mwezi yamepelekea sasa hivi kufikia jumla ya bilioni 36.
"Tshs bilioni 8 kila mwezi TANESCO bado wanalipa IPTL. Rais haijampendeza kumaliza ufisadi huu. IPTL nadhani ni Jipu la Mgongoni (kwa kutumia maneno ya Hidaya wa Richard Mabala ). Rais, kwa kutochukua kwake hatua, ameshaliingizia taifa hasara ya tshs 36 bilioni toka aingie madarakani" aliandika Zitto Kabwe.
Wakati Rais John Magufuli anatimiza siku 100 toka kutangazwa kama Rais Zitto Kabwe alitoa tathimini yake na kugusia sakata la Escrow pamoja na kampuni ya IPTL na kusema kuwa pesa ambazo wamelipwa IPTL/PAP kwa siku 100 tu zingeweza kununua CT Scan kwa hospitali zote za mikoa nchini.
"Mkataba wa IPTL bado unaendelea kunyonya Nchi na Serikali inatazama tshs 8 bilioni zinalipwa Kwa matapeli wa IPTL na PAP kila mwezi. Katika siku 100 tangu Rais Magufuli aingie madarakani, jumla ya tshs 30 bilioni zimeshalipwa Kwa IPTL/PAP ambazo zingeweza kununua CT scan Kwa hospitali zote za mikoa nchini. Fedha hii ni zaidi ya mkopo ambao Serikali imechukua kutoka Benki ya Dunia ili kujenga ' fly over ' ya Ubungo jijini Dar Es Salaam" Alisema Zitto Kabwe.
Chanzo: East Africa Television
KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI: TRUMP NA RUBIO WATOFAUTIANA KUHUSU UISLAM
Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Marco Rubio amemshtumu Donald Trump kwa kusema kuwa Uislamu unachukia Marekani katika mjadala uliokuwa moja kwa moja runingani.
Bwana Rubio ambaye anakabiliwa na ushindani wa maisha yake katika jimbo la Florida siku ya Jumanne amesema kuwa Uislamu una tatizo la itikadi kali lakini akaongezea kuwa Waislamu wengi wanapenda Wamerekani.
''Marais hawawezi kusema kile wanachotaka ,kuna madhara'',alisema huku raia wakimpigia makofi.
Wagombea hao wanne wa chama cha Republican walisikia maombi kutoka kwa viongozi wa chama hicho kuwa na mjadala wa amani.
Ikilinganishwa na mjadala uliopita ambao ulikabiliwa na na matusi ya kibinafsi mjadala huu ulikuwa na muongozo mzuri huku wagombea wote wakitoa malengo ya sera zao.
''Kufikia sasa siamini vile tumekuwa watulivu hapa'',bwana Trump alinukuliwa akisema.
Lakini katika swala la Uislamu,kulikuwa na tofauti kubwa kati ya Trump na wagombea wengine huku wenzake wote wakitofautiana naye kwamba familia za magaidi ziangamizwe.
Chanzo: BBC
JANET JACKSON AAHIRISHA KUFANYA ZIARA YA MUZIKI ULAYA KUFUATIA MAUZO MABAYA YA TIKETI

MECHI KATI YA LEICESTER NA WEST BROM FAHAMU HAYA
Mchezo wa leo kati ya Leicester city na West Bromwich Albion utapigwa katika dimba la King Power Stadium, ambapo Leicester watakuwa ni wenyeji wa dimba hilo. Mtanange utaanza saa 4 na dakika 45 usiku saa za Afrika Mashariki.
Novemba 1, 2013, West Brom alimfunga Leicester goli moja bila katika dimba la King Power Stadium.
Mwaka 2015, April 11 West Brom wakiwa wenyeji katika dimba la nyumbani, The Hawthorns walipigwa bao tatu dhidi ya mbili na Leicister city.
Lakini pia October 31, mwaka jana 2015, West Brom akiwa mwenyeji kwenye dimba la The Hawthorns alifungwa na Leicester city magoli 3 kwa mawili kama mechi iliyopita.
Leicester City inaongoza ligi ikiwa na pointi 56 ambapo imecheza mechi 27 imeshinda mechi 16, imetoka sare mechi 8, na kupoteza mechi 3 ikiwa na magoli ya kifunga 20.
Kwa upande wa West Brom wao wapo katika nafasi ya 13 wakiwa wamecheza mechi 27, wameshinda mechi 9, sare mechi 8 na kupoteza mechi 10 wakiwa wmemfungwa magoli10. West Brom wana pointi 35 ambapo wanahitaji kushinda mechi zaidi ili kuepuka kikombe cha kuporomoka nafasi waliopo kushuka daraja.
Leicester inaingia dimbani ikiwa na majeruhi wawili, Matthew James na Jeffrey Schlupp.
West Brom ina majeruhi watano, Johhny Evans, Gareth McAuley, Craig Dawson, James Morrison na Callum Mcmanamam.
MAMBO YA KUFAHAMU KATI YA CHELSEA NA NORWICH CITY
Chelsea imeshinda mechi saba na haijapoteza katika mechi tisa ilizokutana na Norwich City kwenye EPL.
Norwich City imefenikiwa kuifunga Chelsea magoli manne tu na kushindwa katika mechi nne ambazo walikutana mara ya mwisho na The Blues.
Steven Naismith wa Norwich City amefanikiwa kuifunga Chelsea magoli sita katima mechi saba walizokutana na The Blues EPL.
Norwich City imeshinda mechi nne tu, sare nne na kupotezaechi nane katika mechi 16 ilizocheza katika dimba lao la nyumbani, Carrow Road. (W4 D4 L8).
Norwich City imepata magoli 10 tu katika dimba lao la nyumbani, hii ni baada ya kushinda mechi mbili kati ya tano za EPL katika dimba hilo.
Katika mechi 7 za EPL na kufunga magoli 7 pamoja na kuwa na jumla ya magoli 19 kwenye ligi.
Chelsea imeshuhudia wachezaji wake 15 wakiifungia magoli timu hiyo msimu huu. Rekodi ambayo ni ya juu zaidi katika mashindani msimu huu.
Guus Hiddink amepoteza mechi moja tu kati ya mechi 23 kama kocha na meneja wa klabu katika ligi ya Uingereza msimu huu. Pia ametoa sare mechi 7 na kushinda 15. (W15 D7 L1)
Norwich City imekuwa na rekodi dogo ya kugusa box la goli msimu huu ambapo imesogeza jumla ya shuti 426 tu katika mechi zilizopita.
Chelsea wanataka kushinda mechi tatu mfululizo kwa mara ya kwanza yangu mwaka jana April, 2015.
Norwich inaingia uwanjani ikuwa na majeruhi mmoja tu, Andre Wisdom aliyeumia goti katika mechi ya tarehe 27 Februari mwaka huu.
Kwa upande wa Chelsea majeruhi ni John Terry, Kout Zouma na Radamel Falcao GarcÃa Zaráte.
Katika mechi tano zilizopita, Octoba 6, 2012, Chelsea alishinda Norwich magoli 4 dhidi ya moja kwenye dimba la Stamford Bridge.
Desemba 26, 2012, Chelsea alimfunga Norwich goli moja bila katika uwanja wa Norwich Carrow Road.
Mwaka 2013 Octoba 6, Norwich alifungwa na Chelsea magoli 3 kwa moja, Carrow Road.
May 4, 2014, Norwich na Chelsea walitoka sare ya bila kufungana katika dimba la Stamford Bridge.
Novemba 21, mwaka jana 2015, Chelsea ilishinda goli moja bila dhidi ya Norwich katika dimba la nyumbani, Stamford Bridge.
Mtanange wa Leo utapigwa katika dimba la Norwich City, Carrow Road majira ya saa 4 na dakika 45 usiku saa za Afrika Mashariki.
ROBOTI XINGHZE1 ATEMBEA KILOMITA 134 KUWEKA REKODI MPYA
Roboti aliyepewa jina la Xinghze No. 1 aliyetengenezwa nchini China, amevunja rekodi ya Dunia ya 'Guinness World Records' kwa kutembea kilomita 134.03 ambazo ni sawa na maili 83.28 (83.28 miles).
Roboti huyo aliyetengenezwa na team iliyoongozwa na Profesa Li Qingdu kutoka College of Automation of Chongqing University of Posts and Telecommunications.
Roboti huyo aina ya Quadruped ametengenezwa kwa mashine moja ambayo inaongozwa na program ya kompyuta au sakiti moja ya umeme. Pia, roboti huyo ameundwa kwa miguu minne (Four legs) isiyo na magurudumu (wheels).
Mwongozo uliotolewa na Guinness World Records ni kwamba ili Roboti avunje rekodi ya Dunia kutembeanumbali mrefu, anatakiwa kuchajiwa mara moja au kutumia tanki moja la mafuta na pia anatakiwa atembee mfululizo kwa masaa takribani 54 na dakika 34 ili kuipiku rekodi inayoshikiliwa na jopo Chuo Kikuu cha Cornell Ranger Robot ambapo roboti wao alitembea umbali wa kilomita 65.18 sawa na maili 40.5, roboti Walker 1, alivunja rekodi hiyo jijini New York Marekani mwaka 2011.
Kwa mujibu wa Profesa Qingdu utafiti wa roboti huyo ulianza mwezi Novembea mwaka jana 2014 na alisema kuwa lengo la kutengeneza roboti huyo ni kuelewa ufanisi wa umeme, kuongeza umbali ambao roboti anaweza kutembea, ufanyaji wa kazi, uwezo wa kupingana na kani za nguvu na uwezo wa roboti kutimiza malengo katika hali ambazo zinaweza kuwa hatari kwa binadamu.
Chanzo: Guinness World Records
Roboti huyo aliyetengenezwa na team iliyoongozwa na Profesa Li Qingdu kutoka College of Automation of Chongqing University of Posts and Telecommunications.
Roboti huyo aina ya Quadruped ametengenezwa kwa mashine moja ambayo inaongozwa na program ya kompyuta au sakiti moja ya umeme. Pia, roboti huyo ameundwa kwa miguu minne (Four legs) isiyo na magurudumu (wheels).
Mwongozo uliotolewa na Guinness World Records ni kwamba ili Roboti avunje rekodi ya Dunia kutembeanumbali mrefu, anatakiwa kuchajiwa mara moja au kutumia tanki moja la mafuta na pia anatakiwa atembee mfululizo kwa masaa takribani 54 na dakika 34 ili kuipiku rekodi inayoshikiliwa na jopo Chuo Kikuu cha Cornell Ranger Robot ambapo roboti wao alitembea umbali wa kilomita 65.18 sawa na maili 40.5, roboti Walker 1, alivunja rekodi hiyo jijini New York Marekani mwaka 2011.
Kwa mujibu wa Profesa Qingdu utafiti wa roboti huyo ulianza mwezi Novembea mwaka jana 2014 na alisema kuwa lengo la kutengeneza roboti huyo ni kuelewa ufanisi wa umeme, kuongeza umbali ambao roboti anaweza kutembea, ufanyaji wa kazi, uwezo wa kupingana na kani za nguvu na uwezo wa roboti kutimiza malengo katika hali ambazo zinaweza kuwa hatari kwa binadamu.
Chanzo: Guinness World Records
BIBI WA MIAKA 85 AKAMATWA KWA KUIBA HERENI
Bibi kizee mmoja mwenye umri wa miaka 85 raia wa Marekani na ambaye amekuwa akiiba vito vya thamani kwa zaidi ya miaka 60 amehukumiwa tena kwa kosa la wizi.
Doris Payne, anatuhumiwa kwa wizi wa herini ya thamani ya dola 690, kutoka katika duka moja la uuzaji wa vitu vya thamani la Saks katika kiunga kimoja mjini Atlanta-Marekani.
Wakili wake anatafuta namna ataachiwa huru kwa sababu ya kudorora kwa afya yake.
Payne, ambaye maisha yake ya wizi yaliwekwa katika filamu mwaka 2013, amewahi kufungwa jela mara kadhaa kwa makosa mengi tu ya wizi na uhalifu.
Wakuu nchini Marekani wanasema kuwa, ametumia majina 22 ya bandia tangu alipoiba almasi kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 23, na akaweza kukwepa kutiwa mbaroni.
Muungano wa Walinzi wa vitu vya thamani JSA, kampuni moja kubwa ya kibiashara, ilituma tahadhari kwa maduka yote yanayouza bidhaa na mapambo ya thamani kujihadhari na mwizi huyo sugu mapema miaka ya 70.
Rais wa kampuni hiyo kubwa alitaja tabia ya bi kizee huyo kama wizi au uhalifu wa aina yake.
Aidha anastaajabu kuwa angali anaiiba hata akiwa na umri huo mkubwa.
Akihojiwa na shirika la habari la Associated Press mwaka 2005, akiwa jela, bibi huyo Payne, alisema kuwa haibi kwa sababu ya pesa ila yeye hujikuta tu akiiba na haoni kama ataacha tabia hiyo, labda baada ya kufa.
Chanzo: BBC
Doris Payne, anatuhumiwa kwa wizi wa herini ya thamani ya dola 690, kutoka katika duka moja la uuzaji wa vitu vya thamani la Saks katika kiunga kimoja mjini Atlanta-Marekani.
Wakili wake anatafuta namna ataachiwa huru kwa sababu ya kudorora kwa afya yake.
Payne, ambaye maisha yake ya wizi yaliwekwa katika filamu mwaka 2013, amewahi kufungwa jela mara kadhaa kwa makosa mengi tu ya wizi na uhalifu.
Wakuu nchini Marekani wanasema kuwa, ametumia majina 22 ya bandia tangu alipoiba almasi kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 23, na akaweza kukwepa kutiwa mbaroni.
Muungano wa Walinzi wa vitu vya thamani JSA, kampuni moja kubwa ya kibiashara, ilituma tahadhari kwa maduka yote yanayouza bidhaa na mapambo ya thamani kujihadhari na mwizi huyo sugu mapema miaka ya 70.
Rais wa kampuni hiyo kubwa alitaja tabia ya bi kizee huyo kama wizi au uhalifu wa aina yake.
Aidha anastaajabu kuwa angali anaiiba hata akiwa na umri huo mkubwa.
Akihojiwa na shirika la habari la Associated Press mwaka 2005, akiwa jela, bibi huyo Payne, alisema kuwa haibi kwa sababu ya pesa ila yeye hujikuta tu akiiba na haoni kama ataacha tabia hiyo, labda baada ya kufa.
Chanzo: BBC
DOGMATIC BLUSTERY WEATHER A POEM BY VENANCE GILBERT
Poet: Venance Gilbert
Composed September 27, 2015
Published on October 21, 2015.
The blustery
weather blows wherever
By a hair's
breadth in the oceans and ponds
Wind vane regularly
measure the breeze.
The blustery
weather has now turned to policies
Particularly in
this phase of the GE
Propelling hard
to the populations; the electorates
Populations frequently
size them lyrics
Whichever the runners’
dogmas or troop expression.
It is the blustery
weather since it blows to constituents
The dogmatic blustery
weather will measured in the poll
Majority, make
it take place on October
Be pacific under
open and just environments.
ALL RIGHTS RESERVED.
Venance Gilbert © 2015
DOWNLOAD WIMBO MPYA: TOFA EMCEE-KUNG FU PANDA
Anaitwa Christopher Robert jina la kazi ya sanaa 'Tofa Emcee'.
Tofa Emcee katika picha. Picha kwa hisani ya Facebook account Christoper TofaEmcee Robert
Tofa Emcee katika picha. Picha kwa hisani ya Facebook account Christoper TofaEmcee Robert
![]() |
Donload Kung Fu Panda kwa kubofya HAPA.
BEN POL AELEZEA ALIVYONUSURIKA KIFO KATIKA AJALI YA BOTI
Msanii wa Bongo Fleva,Ben Pol amesimulia alivyonusurika kifo baada ya boti waliokuwa wakisafiria wakitokea visiwani Mbudya,jijini Dar kuzima ghafla katika ya bahari na kukaa kwa muda wa saa nzima bila kupata msaada.
Ben Pol alisema kuwa baada boti kuzima maji yalianza kuingia ndani na engine ya boti ikazimika na boti hiyo ikaanza kuzama kilichowaokoa walikuwa wamevaa makoti ya kuogelea ‘life jackets’.
‘’Baada ya kukaa kwa saa nzima baharini kwa bahati nzuri ilipita boti ya wavuvi ikatuona ikatuokoa ila mmoja wetu hakuwepo kati ya tuliokolewa na hatujamuona ambao ni wanawake watatu, watoto hao walikuwa watatu, wanaume tulikuwa nane, lakini mmoja ndiye hatujui alipo.’alisema Ben Pol.
VAN VICKER AKUMBWA NA MAFURIKO AKIELEKEA KWAKE
Mafuriko makubwa yaliyoikumba jiji la Accra nchini Ghana usiku wa
kuamkia juzi na kuleta maafa ya kuua watu 175 wakiwa wamejihifadhi
kwenye kituo cha mafuta baada ya kituo hicho kulipuka moto,yamemkumba
pia Staa wa filamu nchini humo Van Vicker akiwa barabarani akielekea
nyumbani kwake.
Kupitia akaunti yake Instagram Van Vicker aliandika kuwa ameshuhudia mafuriko kwa macho yake (live),huku taa za barabarani zikiwa haziwaki,kuna mashimo,matakataka,umeme ukiwa umekatika na barabara zilikuwa zimefurika maji, na magari yalikuwa yameharibika.
Pia aliongeza kuwa waliokuwa wakitembea barabarani walikuwa wakitafuta pa kujihifadhi,madereva walipaniki na bado wakati huo mvua ilikuwa ikinyeesha na pia foleni ilikuwa kubwa na barabara ni ndogo.
Ambapo alisema kuwa kawaida huwa inamchukua dakika 45 kwenda nyumbani kwake lakini siku hiyo ilimchukua masaa sita kufika nyumbani kwake.
Chanzo; Udaku Specially
Kupitia akaunti yake Instagram Van Vicker aliandika kuwa ameshuhudia mafuriko kwa macho yake (live),huku taa za barabarani zikiwa haziwaki,kuna mashimo,matakataka,umeme ukiwa umekatika na barabara zilikuwa zimefurika maji, na magari yalikuwa yameharibika.
Pia aliongeza kuwa waliokuwa wakitembea barabarani walikuwa wakitafuta pa kujihifadhi,madereva walipaniki na bado wakati huo mvua ilikuwa ikinyeesha na pia foleni ilikuwa kubwa na barabara ni ndogo.
Ambapo alisema kuwa kawaida huwa inamchukua dakika 45 kwenda nyumbani kwake lakini siku hiyo ilimchukua masaa sita kufika nyumbani kwake.
Chanzo; Udaku Specially
URUSI NA QATAR HUENDA ZISIANDAE KOMBE LA DUNIA
Mkuu wa kamati ya uhasibu wa shirikisho la soka duniani FIFA Domenico
Scala amesema huenda Urusi na Qatar zikapoteza nafasi za kuyaandaa
mashindano ya kombe la dunia mwaka 2018 na 2022 mtawalia iwapo ushahidi
utaonyesha kulikuwa na ufisadi katika shughuli ya kinyanganyiro cha
kupata kibali cha kuandaa mashindano hayo. Scala hata hivyo amesema
mpaka kufikia sasa hawajapokea ushahidi wowote wa kudhihirisha kuwa nchi
hizo mbili zilitoa hongo. Matamshi yake ndiyo ya kwanza kutolewa na
afisa wa ngazi ya juu wa FIFA kuwa kuna uwezekano nchi hizo zikapokonywa
uenyeji wa mashindano hayo. Maafisa wa idara ya mahakama wa Uswisi
tayari wameanzisha uchunguzi kuhusu kutolewa kwa kandrasi hiyo ya
kuandaa mashindano ya 2018 na 2022 kama sehemu ya uchunguzi wa madai ya
ufisadi katika FIFA.
Chanzo: DW
Chanzo: DW
MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA
Chanzo: DW