Skip to main content

MAJARIBIO KATI YA ChatGPT, BING CHAT NA GOOGLE BARD

Maendeleo ya teknolojia ya Akili Bandia (AI) yamebadilisha jinsi tunavyofanya kazi na mambo mengine mengi katika miezi ya hivi karibuni na hivyo kumpa karibu mtu yeyote uwezo wa kuandika msimbo (code), kuunda sanaa na hata kuwekeza.

Kwa watumiaji wa kitaalamu na wale wenye mapenzi na teknolojia, programu zalishi za AI, kama vile ChatGPT, huangazia uwezo wa hali ya juu ili kuunda maudhui yenye ubora kutokana na maelezo rahisi anayotoa mtumiaji.

Microsoft imeongeza GPT-4 katika Bing, OpenAI inaongeza uwezo mpya kwenye ChatGPT na Bard inaunganisha kwenye mfumo mzima wa Google yani kwamba chochote kinachoweza kupatikana kupitia Google utakipata kwenye Bard pia. Uwepo wa robotisogozi hizi 3 za hivi punde za AI kunaweza kumtatanisha mtumiaji ipi inamfaa zaidi.

Kujua ipi kati ya robotisogozi tatu maarufu za AI ni bora kuandika msimbo, kutoa maandishi, au kusaidia kuunda wasifu ni changamoto, kwa hivyo nakueleza hapa tofauti kubwa zaidi ili uweze kuchagua inayolingana na mahitaji yako kwa wakati huo.

Majaribio kati ya ChatGPT, Bing Chat & Google Bard
Ili kubaini ni robotisogozi gani la AI linatoa majibu sahihi zaidi, tutatumia swali hili kuzilinganisha zote hizi tatu:
"Nina machungwa 5 leo, nilikula machungwa 3 wiki iliyopita. Nimebakiza machungwa mangapi?"
Jibu linapaswa kuwa tano, kwani idadi ya machungwa niliyokula wiki iliyopita haiathiri idadi ya machungwa niliyonayo leo. Tuangalie majibu ya robotisogozi hizi.

Tuanze na ChatGPT

Unapaswa kutumia ChatGPT kama:

1. Unataka kujaribu robotisogozi maarufu ya AI
ChatGPT iliyoundwa na OpenAI ililenea Novemba mwaka jana baada ya kuzinduliwa rasmi. Tangu wakati huo, robotisogozi hii imepata watumiaji zaidi ya milioni 100, na tovuti pekee ikishuhudia watembeleaji wapatao bilioni 1.8 kwa mwezi. Imekuwa ikighubikwa na shutuma mbalimbali hasa watu wanapoifichua uwezo wake wa kufanya kazi za vyuoni na kuchukua nafasi ya wafanyikazi wengine.
Toleo lisilolipishwa la ChatGPT, ambalo linatumia mfumo wa GPT-3.5, lilitoa jibu lisilo sahihi kwa swali letu.

Nimekuwa nikijaribu ChatGPT mara kwa mara tangu kutolewa kwake. Muonekano wake kwa mtumiaji umebaki kuwa rahisi, lakini mabadiliko madogo yameiboresha zaidi, kama vile kuongezwa kwa kitufe cha kunakili, uwezo wa kuhariri, maelekezo maalum na ufikiaji rahisi wa akaunti yako.

Ingawa ChatGPT imejidhihirisha kama app muhimu ya AI, inaweza kukabiliwa na habari potofu. Kama mifumo mingine mikubwa ya lugha (LLMs), GPT-3.5 si kamilifu bado kwani imefunzwa kuhusu taarifa iliyoundwa na binadamu hadi 2021. Pia mara nyingi inashindwa kuelewa nuances, kama vile katika mfano wa swali letu la hesabu ambapo ilijibu vibaya kwa kusema tuna machungwa mawili yaliyobaki wakati inapaswa kuwa matano.

2. Uko tayari kulipa ziada kwa ajili ya kutumia toleo la juu zaidi
OpenAI huruhusu watumiaji kufikia ChatGPT inayoendeshwa na mfumo wa GPT-3.5 bila malipo kwa akaunti iliyosajiliwa. Lakini ikiwa uko tayari kulipia toleo la juu zaidi, unaweza kufikia GPT-4 kwa kulipia $20 kwa mwezi.

GPT-4 ndiyo LLM kubwa zaidi inayopatikana kwa matumizi ikilinganishwa na robotisogozi nyingine zote za AI na imefunzwa kwa taarifa za hadi 2022. Inasemekana kuwa GPT-4 ina zaidi ya maingizo trilioni 100 wakati GPT-3.5 ina maingizo bilioni 175. Maingizo zaidi inamaanisha kwamba kimsingi, mfumo umefunzwa kwa taarifa zaidi, ambayo inafanya uwezekano mkubwa wa kujibu maswali kwa usahihi.
ChatGPT Plus, inayotumia mfumo wa GPT-4, ilijibu swali kwa usahihi.

Kwa mfano, unaweza kuona mfano wa GPT-4, unaopatikana kwa kulipia toleo la juu la ChatGPT, ulijibu swali la hesabu kwa usahihi, kwani ulielewa muktadha kamili wa hesabu hiyo tangu mwanzo hadi mwisho.

Hebu sasa tuiangalie Bing Chat, ambayo ni njia nzuri ya kufikia GPT-4 bila malipo, kwani imeunganishwa katika toleo lake jipya la Bing.

Unapaswa kutumia Bing Chat ikiwa:

1. Unataka AI zalishi inayofikiwa kwa mtandao
Tofauti na ChatGPT ambayo inadhibitiwa kuwa programu ya AI ambayo hutoa maandishi kwa mtindo wa mazungumzo na habari hadi kufikia 2021. Bing sasa ina chaguo la gumzo ambalo linapangilia matokeo ya utafutaji kama mazungumzo na robotisogozi ya AI.

Kuna faida nyingine, pia. Bing Chat inaendeshwa na GPT-4, mfumo mkubwa wa lugha wa OpenAI na ni bure kabisa kutumia.
Mtindo sahihi wa mazungumzo ya Bing ulijibu swali kwa usahihi, ingawa mitindo mingine ilikuwa na utata. 

Muonekano wa mtumiaji wa Bing Chat si wa kupendeza sana kama cha ChatGPT, lakini ni rahisi kutumia.

Ingawa Bing Chat inatumika kwa kuunanisha na mtandao ili kukupa matokeo ya kisasa zaidi ikilinganishwa na ChatGPT, ina uwezekano mkubwa wa kukwama katika kujibu na kukosa vidokezo kuliko mshindani wake.

2. Unapendelea vipengele zaidi vya kuona
Kupitia mfululizo wa matoleo kwenye jukwaa lake, Microsoft iliongeza vipengele vya kuona kwenye Bing Chat. Kwa wakati huu, unaweza kuuliza maswali ya Bing kama, 'Shetani wa Tasmania ni nini?' na upate maelezo inayojibu kwa picha, muda wa kuishi, chakula, na zaidi kwa matokeo ya kuchanganua zaidi ambayo ni rahisi kuchimba kuliko ukuta wa maandishi.

Unapotumia Bing katika muundo wa gumzo, unaweza pia kuiomba ikutengenezee picha. Andika maelezo ya jinsi unavyotaka picha ionekane, na kisha acha Bing ikutengenezee picha nne ambapo utachagua uipendayo.

Bing Chat pia huangazia mitindo tofauti ya mazungumzo unapokuwa unaitumia ikijumuisha Ubunifu (Creative), Uwiano (Balanced) na Usahihi (Precise), ambayo hubadilisha jinsi utumiaji ulivyo, mwepesi au wa moja kwa moja.
Mitindo yote miwili ya mazungumzo ya Usawazishaji (Balanced ) na Ubunifu (Creative ) ilijibu swali isivyo sahihi.

Hatimaye, hebu tugeukie Google Bard, ambayo inatumia LLM tofauti na imekuwa matoleo mengi katika miezi michache iliyopita.

Unapaswa kutumia Google Bard ikiwa:

1. Unataka uzoefu wa haraka na usio na kikomo
Katika wakati wa kujaribu robotisogozi tofauti za AI, nimeona Google Bard ikipata dosari nyingi kwa mapungufu tofauti. Ingawa sitasema kuwa sio za kuzingatia sana, nitasema kuwa robotisogozi la AI ya Google lina mazuri yake na mojawapo ni kasi.

Google Bard ina kasi na majibu yake, hata kama inajibu kwa makosa baadhi ya nyakati. Haina kasi zaidi kuliko ChatGPT Plus, lakini inaweza kuwa haraka zaidi katika kutoa majibu kuliko Bing na toleo lisilolipishwa la GPT-3.5 la ChatGPT, ingawa umbali wako unaweza kutofautiana.
Bard pia alipata jibu lisilo sahihi katika swali hili.

Bard ilifanya makosa sawa na roboti zingine kwa kutumia kanuni isiyo sahihi ya 5 - 3 = 2.

Bard pia haizuiliwi na idadi fulani ya majibu kama vile Bing Chat ilivyo. Unaweza kuwa na mazungumzo marefu na Google Bard, lakini Bing ina kikomo cha majibu 30 katika mazungumzo moja. Hata ChatGPT Plus huwawekea watumiaji kikomo cha jumbe 50 kila baada ya saa tatu.

2. Unataka matumizi zaidi ya 'Google'
Google ilitangaza maboresho mengi ya AI wakati wa mkutano wake wa I/O miezi michache iliyopita pamoja na jinsi inavyopanga kuiboresha Bard na injini yake ya utafutaji. Tangu wakati huo Bard imepata toleo jipya la PaLM 2, toleo la hivi punde na kubwa zaidi la Google LLM, ambalo lilitangazwa wakati wa hafla ya Mei.

PaLM 2 ilisaidia Bard kutumia zaidi ya lugha 100 kwa wakati, na pia kuboresha pakubwa ujuzi wake wa usimbaji (coding), utatuzi (debugging) na hesabu. Kwa wakati huu, hata hivyo, ChatGPT inasemekana kutumia zaidi ya lugha 80.

Google pia ilijumuisha vipengele vingi vya kuona kwenye jukwaa lake la Bard kuliko vile vinavyopatikana kwenye Bing Chat. Google iliamua kwamba watumiaji wanaweza kupakia picha kupitia Google Lens na utengenezaji wa picha kupitia Adobe Firefly (ingawa bado uamuzi huu haujajumuishwa) pamoja na programu jalizi za Kayak, OpenTable, Instacart, na Wolfram Alpha.


MAKALA HII IMEANDIKWA NA MARIA DIAZ KATIKA TOVUTI YA ZDNET NA KUSIMULIWA KWA KISWAHILI NA VENANCE GILBERT.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

FRIENDSHIP QUOTES OF THE DAY MAY 26, 2018

Today I invite you to read these quotes of the day. Enjoy your day. 1.  One of the most beautiful qualities of true friendship is to understand and to be understood. ~Lucius Annaeus Seneca. 2.  Walking with a friend in the dark is better than walking alone in the light. ~Helen Keller. 3.  There is nothing on this earth more to be prized than true friendship. ~Thomas Aquinas. 4.  My best friend is the one who brings out the best in me. ~Henry Ford. 5.  It is one of the blessings of old friends that you can afford to be stupid with them. ~Ralph Waldo Emerson. 6.  The strong bond of friendship is not always a balanced equation; friendship is not always about giving and taking in equal shares. Instead, friendship is grounded in a feeling that you know exactly who will be there for you when you need something, no matter what or when. ~Simon Sinek. 7.  A friend is someone who gives you total freedom to be yourself. ~Jim Mo...

IDADI YA WATU WALIOFARIKI UGANDA YAFIKIA 33

Moto mkubwa uliowaka baada yaajali mbaya ya barabarani iliohusisha lori la mafuta, umewauwa takriban watu 33 mjini kampala Uganda. Watu wengine 30 wanadaiwa kujeruhiwa vibaya kufuatia tukiohilo. Maafisa wa polisi wanasema kuwa kati ya waliofariki ni raia waliokuwa wanakimbilia eneo hilo la mkasa kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwa lori hilo. maafisa wa serikali walikuwa katika harakati za kutambua mili ya waliofariki baada ya wengi wao kuchomeka vibaya. Idara ya polisi imesema kuwa waliofariki waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.

VITAMBULISHO VYA URAIA KUVUKIA MIPAKA KENYA, RWANDA NA UGANDA

Wananchi wa mataifa ya Rwanda, Uganda na Kenya wamepokea kwa shangwe kuanza kwa mpango wa kutumiwa kwa vitambulisho vya uraia kama cheti cha kuwaruhusu kuvuka mpaka na kuingia moja wapo wa nchi hizo.Mpango huu wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kusafiria katika nchi hizo tatu umeanza kutumiwa rasmi tarahe Mosi Januari 2014, kufuatia makubaliano kati ya viongozi wa mataifa hayo.Mpango wenyewe unatokana na makubaliano kati ya viongozi wa nchi tatu waliofikia wakati wa mkutano uliofanyika nchini Uganda mwezi Juni mwaka jana.Pia mpango huu unalenga kurahisisha usafiri wa watu wa jumuiya katika mataifa wanachama kama awamu ya pili ya ushirikiano kati ya mataifa wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.Hata hivyo siku moja tu baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kuwaruhusu raia wa nchini tatu, Uganda, Kenya na Rwanda kuvuka mpaka na kuingia mojawapo ya nchi hizo sasa inaonekana mpango huo huenda ukawanufaisha watu wachache peke yake.Sio ...

CHANGES QUOTES OF THE DAY MAY 23, 2018

Hello dear reader, welcome once again. Today I have gathered the quotes concerning changes in life. I should not write more since I am not not the speaker in this category, take your time to dive in and become intellectual with full equipped knowledge from the great men of history Remember, someday it might be you. Do not rely on inspiration from friends while you are needy, VENANCE BLOG is here for you. Welcome all the time by searching Quotes. Now proceed. 1. Every great dream begins with a dreamer. Always remember, you have within you the strength, the patience, and the passion to reach for the stars to change the world. ~Harriet Tubman. 2. Change your thoughts and you change your world. ~Norman Vincent Peale. 3.  If you don't like something, change it. If you can't change it, change your attitude. ~Maya Angelou 4.  Change will not come if we wait for some other person or some other time. We are the ones we've been waiting for. We are the change that...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...