Skip to main content

MAJARIBIO KATI YA ChatGPT, BING CHAT NA GOOGLE BARD

Maendeleo ya teknolojia ya Akili Bandia (AI) yamebadilisha jinsi tunavyofanya kazi na mambo mengine mengi katika miezi ya hivi karibuni na hivyo kumpa karibu mtu yeyote uwezo wa kuandika msimbo (code), kuunda sanaa na hata kuwekeza.

Kwa watumiaji wa kitaalamu na wale wenye mapenzi na teknolojia, programu zalishi za AI, kama vile ChatGPT, huangazia uwezo wa hali ya juu ili kuunda maudhui yenye ubora kutokana na maelezo rahisi anayotoa mtumiaji.

Microsoft imeongeza GPT-4 katika Bing, OpenAI inaongeza uwezo mpya kwenye ChatGPT na Bard inaunganisha kwenye mfumo mzima wa Google yani kwamba chochote kinachoweza kupatikana kupitia Google utakipata kwenye Bard pia. Uwepo wa robotisogozi hizi 3 za hivi punde za AI kunaweza kumtatanisha mtumiaji ipi inamfaa zaidi.

Kujua ipi kati ya robotisogozi tatu maarufu za AI ni bora kuandika msimbo, kutoa maandishi, au kusaidia kuunda wasifu ni changamoto, kwa hivyo nakueleza hapa tofauti kubwa zaidi ili uweze kuchagua inayolingana na mahitaji yako kwa wakati huo.

Majaribio kati ya ChatGPT, Bing Chat & Google Bard
Ili kubaini ni robotisogozi gani la AI linatoa majibu sahihi zaidi, tutatumia swali hili kuzilinganisha zote hizi tatu:
"Nina machungwa 5 leo, nilikula machungwa 3 wiki iliyopita. Nimebakiza machungwa mangapi?"
Jibu linapaswa kuwa tano, kwani idadi ya machungwa niliyokula wiki iliyopita haiathiri idadi ya machungwa niliyonayo leo. Tuangalie majibu ya robotisogozi hizi.

Tuanze na ChatGPT

Unapaswa kutumia ChatGPT kama:

1. Unataka kujaribu robotisogozi maarufu ya AI
ChatGPT iliyoundwa na OpenAI ililenea Novemba mwaka jana baada ya kuzinduliwa rasmi. Tangu wakati huo, robotisogozi hii imepata watumiaji zaidi ya milioni 100, na tovuti pekee ikishuhudia watembeleaji wapatao bilioni 1.8 kwa mwezi. Imekuwa ikighubikwa na shutuma mbalimbali hasa watu wanapoifichua uwezo wake wa kufanya kazi za vyuoni na kuchukua nafasi ya wafanyikazi wengine.
Toleo lisilolipishwa la ChatGPT, ambalo linatumia mfumo wa GPT-3.5, lilitoa jibu lisilo sahihi kwa swali letu.

Nimekuwa nikijaribu ChatGPT mara kwa mara tangu kutolewa kwake. Muonekano wake kwa mtumiaji umebaki kuwa rahisi, lakini mabadiliko madogo yameiboresha zaidi, kama vile kuongezwa kwa kitufe cha kunakili, uwezo wa kuhariri, maelekezo maalum na ufikiaji rahisi wa akaunti yako.

Ingawa ChatGPT imejidhihirisha kama app muhimu ya AI, inaweza kukabiliwa na habari potofu. Kama mifumo mingine mikubwa ya lugha (LLMs), GPT-3.5 si kamilifu bado kwani imefunzwa kuhusu taarifa iliyoundwa na binadamu hadi 2021. Pia mara nyingi inashindwa kuelewa nuances, kama vile katika mfano wa swali letu la hesabu ambapo ilijibu vibaya kwa kusema tuna machungwa mawili yaliyobaki wakati inapaswa kuwa matano.

2. Uko tayari kulipa ziada kwa ajili ya kutumia toleo la juu zaidi
OpenAI huruhusu watumiaji kufikia ChatGPT inayoendeshwa na mfumo wa GPT-3.5 bila malipo kwa akaunti iliyosajiliwa. Lakini ikiwa uko tayari kulipia toleo la juu zaidi, unaweza kufikia GPT-4 kwa kulipia $20 kwa mwezi.

GPT-4 ndiyo LLM kubwa zaidi inayopatikana kwa matumizi ikilinganishwa na robotisogozi nyingine zote za AI na imefunzwa kwa taarifa za hadi 2022. Inasemekana kuwa GPT-4 ina zaidi ya maingizo trilioni 100 wakati GPT-3.5 ina maingizo bilioni 175. Maingizo zaidi inamaanisha kwamba kimsingi, mfumo umefunzwa kwa taarifa zaidi, ambayo inafanya uwezekano mkubwa wa kujibu maswali kwa usahihi.
ChatGPT Plus, inayotumia mfumo wa GPT-4, ilijibu swali kwa usahihi.

Kwa mfano, unaweza kuona mfano wa GPT-4, unaopatikana kwa kulipia toleo la juu la ChatGPT, ulijibu swali la hesabu kwa usahihi, kwani ulielewa muktadha kamili wa hesabu hiyo tangu mwanzo hadi mwisho.

Hebu sasa tuiangalie Bing Chat, ambayo ni njia nzuri ya kufikia GPT-4 bila malipo, kwani imeunganishwa katika toleo lake jipya la Bing.

Unapaswa kutumia Bing Chat ikiwa:

1. Unataka AI zalishi inayofikiwa kwa mtandao
Tofauti na ChatGPT ambayo inadhibitiwa kuwa programu ya AI ambayo hutoa maandishi kwa mtindo wa mazungumzo na habari hadi kufikia 2021. Bing sasa ina chaguo la gumzo ambalo linapangilia matokeo ya utafutaji kama mazungumzo na robotisogozi ya AI.

Kuna faida nyingine, pia. Bing Chat inaendeshwa na GPT-4, mfumo mkubwa wa lugha wa OpenAI na ni bure kabisa kutumia.
Mtindo sahihi wa mazungumzo ya Bing ulijibu swali kwa usahihi, ingawa mitindo mingine ilikuwa na utata. 

Muonekano wa mtumiaji wa Bing Chat si wa kupendeza sana kama cha ChatGPT, lakini ni rahisi kutumia.

Ingawa Bing Chat inatumika kwa kuunanisha na mtandao ili kukupa matokeo ya kisasa zaidi ikilinganishwa na ChatGPT, ina uwezekano mkubwa wa kukwama katika kujibu na kukosa vidokezo kuliko mshindani wake.

2. Unapendelea vipengele zaidi vya kuona
Kupitia mfululizo wa matoleo kwenye jukwaa lake, Microsoft iliongeza vipengele vya kuona kwenye Bing Chat. Kwa wakati huu, unaweza kuuliza maswali ya Bing kama, 'Shetani wa Tasmania ni nini?' na upate maelezo inayojibu kwa picha, muda wa kuishi, chakula, na zaidi kwa matokeo ya kuchanganua zaidi ambayo ni rahisi kuchimba kuliko ukuta wa maandishi.

Unapotumia Bing katika muundo wa gumzo, unaweza pia kuiomba ikutengenezee picha. Andika maelezo ya jinsi unavyotaka picha ionekane, na kisha acha Bing ikutengenezee picha nne ambapo utachagua uipendayo.

Bing Chat pia huangazia mitindo tofauti ya mazungumzo unapokuwa unaitumia ikijumuisha Ubunifu (Creative), Uwiano (Balanced) na Usahihi (Precise), ambayo hubadilisha jinsi utumiaji ulivyo, mwepesi au wa moja kwa moja.
Mitindo yote miwili ya mazungumzo ya Usawazishaji (Balanced ) na Ubunifu (Creative ) ilijibu swali isivyo sahihi.

Hatimaye, hebu tugeukie Google Bard, ambayo inatumia LLM tofauti na imekuwa matoleo mengi katika miezi michache iliyopita.

Unapaswa kutumia Google Bard ikiwa:

1. Unataka uzoefu wa haraka na usio na kikomo
Katika wakati wa kujaribu robotisogozi tofauti za AI, nimeona Google Bard ikipata dosari nyingi kwa mapungufu tofauti. Ingawa sitasema kuwa sio za kuzingatia sana, nitasema kuwa robotisogozi la AI ya Google lina mazuri yake na mojawapo ni kasi.

Google Bard ina kasi na majibu yake, hata kama inajibu kwa makosa baadhi ya nyakati. Haina kasi zaidi kuliko ChatGPT Plus, lakini inaweza kuwa haraka zaidi katika kutoa majibu kuliko Bing na toleo lisilolipishwa la GPT-3.5 la ChatGPT, ingawa umbali wako unaweza kutofautiana.
Bard pia alipata jibu lisilo sahihi katika swali hili.

Bard ilifanya makosa sawa na roboti zingine kwa kutumia kanuni isiyo sahihi ya 5 - 3 = 2.

Bard pia haizuiliwi na idadi fulani ya majibu kama vile Bing Chat ilivyo. Unaweza kuwa na mazungumzo marefu na Google Bard, lakini Bing ina kikomo cha majibu 30 katika mazungumzo moja. Hata ChatGPT Plus huwawekea watumiaji kikomo cha jumbe 50 kila baada ya saa tatu.

2. Unataka matumizi zaidi ya 'Google'
Google ilitangaza maboresho mengi ya AI wakati wa mkutano wake wa I/O miezi michache iliyopita pamoja na jinsi inavyopanga kuiboresha Bard na injini yake ya utafutaji. Tangu wakati huo Bard imepata toleo jipya la PaLM 2, toleo la hivi punde na kubwa zaidi la Google LLM, ambalo lilitangazwa wakati wa hafla ya Mei.

PaLM 2 ilisaidia Bard kutumia zaidi ya lugha 100 kwa wakati, na pia kuboresha pakubwa ujuzi wake wa usimbaji (coding), utatuzi (debugging) na hesabu. Kwa wakati huu, hata hivyo, ChatGPT inasemekana kutumia zaidi ya lugha 80.

Google pia ilijumuisha vipengele vingi vya kuona kwenye jukwaa lake la Bard kuliko vile vinavyopatikana kwenye Bing Chat. Google iliamua kwamba watumiaji wanaweza kupakia picha kupitia Google Lens na utengenezaji wa picha kupitia Adobe Firefly (ingawa bado uamuzi huu haujajumuishwa) pamoja na programu jalizi za Kayak, OpenTable, Instacart, na Wolfram Alpha.


MAKALA HII IMEANDIKWA NA MARIA DIAZ KATIKA TOVUTI YA ZDNET NA KUSIMULIWA KWA KISWAHILI NA VENANCE GILBERT.

Comments

Popular posts from this blog

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

MOVIE: X-MEN APOCALYPSE RELEASED TODAY

  Release date: May 27, 2016 Director: Bryan Singer Starring: James McAvoy Jennifer Lawrence Oscar Isaac Michael Fassbender Rose Byrne Sophie Turner Synopsis: In this comic-book adventure set in the 1980s, the X-Men are forced to confront an ancient mutant called Apocalypse (Oscar Isaac). After the resurrected beast recruits a super-team to take over the world and destroy hunmanity, Professor X (James McAvoy) and his charges must come to the rescue for the fate of the planet. The film co-stars Michael Fassbender, Jennifer Lawrence and Olivia Munn.

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD  

MAMBO YA MUHIMU KUFAHAMU NA KUZINGATIA KABLA YA KUCHAGUA KOZI (TAALUMA) CHUO KIKUU

Picha kwa hisani ya Debt.org 1.0 UTANGULIZI Nilipokuwa mwanafunzi wa chuo kikuu nilisikia manung'uniko miongoni mwa wanafunzi wenzangu wengi wa vyuo vikuu ambayo yalitokana na taaluma wanazosoma. Kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea manung'uniko hayo miongoni mwa wasomi hawa tukiachilia mbali suala la ucheleweshwaji wa mikopo miongoni mwa wasomi hawa (kwa sasa changamoto hii inapungua kadiri siku zinavyosonga). Tatizo lingine ambalo linawasumbua wasomi hawa ni suala la uchaguzi wa taaluma gani akaisome Chuo Kikuu. Uchaguzi wa taaluma (career choice) ni jambo nyeti sana na la kuzingatia kwa muhitimu yeyote wa elimu ya kuanzia kidato cha nne. Jamii yetu ya Tanzania haifahamu kwa undani kuhusu umuhimu wajambo hili lakini huku ndiko msingi hundaliwa. Mtu anapohitimu kidato cha nne na kupata ufaulu wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ama ngazi ya astashahada (certificate) na stashahada (diploma) hapo ndipo uchanguzi wa taaluma huanza. Kwa kuandika makala haya ninakusudia ...