WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

10. YUSUF MANJI

Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini.

9. FIDA RASHID

Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine.

8. GHALIB SAID MOHAMMED

Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha na uuzaji wa bidhaa za rejareja, usafirishaji wa vifaa na bidhaa, huduma za kifedha, vyombo vya habari na mengine mengi. Vyanzo vyote hivi vinamfanya kua miongoni mwa matajiri wakubwa nchini. Kama mjasiriamali aliamua kujihusisha zaidi na mazao ya kilimo pamoja na baba yake jambo ambalo limewafanya kufikia walipo kwa sasa.

7. SUBASH PATEL

Patel ni mwanachama wa Taasisi ya Wahandisi wa Umeme na ana ubia na kampuni ya MMI Steels Resource Limited na Nyaza Road Works. Katika kipindi cha miaka 20 amefanikiwa kupanua biashara zake mpaka kufikia kuwa na kampuni inayoitwa Motsun Group. Kampuni hii imegawanyika katika makampuni mengine 11 ambazo zinahusika na bidhaa za chakula, madini, majengo na kusaidia makampuni mengine kitaalamu.

6. SHEKHAR KANABAR

Shekhar ni meneja katika kampuni ya Synarge Group. Hii ni kampuni inayohusika na bidhaa za magari. Kampuni hii pia inahusika na utengenezaji wa madini ya risasi. Licha ya kwamba kampuni hii ni mali ya familia, Shekhar anabainishwa kuwa miongoni mwa matajiri nchini kutokana na uongozi wake mzuri katika kampuni hiyo. Kampuni hii pia inahusika na usambazaji wa spea za magari nchini. Huwezi kuzungumzia Teknolojia hii ya magari bila kumzungumzia Shekhar. Synarge imekua ikifanya vema katika mauzo ya bidhaa za magari nchini.

5. ALLY AWADH

Awadh ni miongoni mwa watu wenye akili ya biashara. Amefanya uwekezaji katika sekta za mafuta na gesi, ni muwekezaji muhimu sana katika sekta hizi. Alifanya kazi kwa juhudi sana ili apewe kibali na serikali na baadaye alifanikiwa katika hilo na sasa ana kampuni yake ya Lake Oil Group inayohusika na kuingiza pamoja na kusambaza mafuta ya petroli na gesi nchini. Biashara ya mafuta inatajirisha kwa haraka sana lakini kwa Awadh haikua hivyo, amepitia changamoto nyingi pamoja na magumu mengi mpaka hapo alipofikia.

4. REGINALD MENGI

Mengi ni mmiliki na mkuu wa kampuni kubwa ya habari nchini IPP Media Group. Kampuni hii ina jumla ya vituo vya redio 11, vituo vya televisheni, magazeti na huduma za mtandao (Internet). Mengi pia ni mmiliki wa kampuni ya Kilimanjaro Spring Water na Bonite Bottlers. Ndoto yake na mapenzi katika tasnia ya habari vimemfanya kutimiza malengo yake ya kutangaza na kufikisha habari kwa Watanzania. Anamiliki utajiri unaokadiriwa kuwa dola milioni 560.

3. SAID SALIM BAKHRESA

Bakhresa aliacha masomo ya shule ya sekondari akiwa na umri wa miaka 14. Kwa kipindi hicho alikua akifanya biashara ya kuuza viazi na akafungua mgahawa wa kuuza chakula na kisha akafungua mashine ya kusaga nafaka. Bakhresa ameijenga biashara yake kwa muda wa miaka 30 iliyopita mpaka kufikia leo, pia ni miongoni mwa matajiri wakubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki. Kampuni yake ya Bakhresa Group of Companies ni maarufu kwa uzalishaji wa bidhaa za chakula, mafuta ya petroli, usafirishaji ndani ya bahari ya Hindi na usagaji wa nafaka. Pia ni mmiliki wa king'amuzi cha Azam TV ambacho kinatoa huduma kwa malipo katika ukanda wa Afrika Mashariki. Akiwa ameajiri zaidi ya watu 3000 katika ukanda huu wa Afrika Mashariki, akiwa na matawi ya kibiashara nchini Msumbiji, Malawi na Uganda, Bakhresa anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia dola milioni 650 za Marekani. Bakhresa amekuwa akitoa msaada wa kifedha kwa watu wenye uhitaji nchini.

2. ROSTAM AZIZ

Rostam anashikiria rekodi ya kuwa bilionea wa mwanzo nchini Tanzania. Anamiliki kampuni ya madini inayotwa Caspian Mining, kampuni hii inatoa huduma za kitaalamu kwa makampuni makubwa ya madini nchini kama vile Barrick Mining na BHP Billiton. Alinunua 17.2% ya hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania mwaka 2014. Anamiliki mali zisizohamishika nchini Tanzania, Lebanon, Dubai na Oman. Pia ni mdau mkubwa wa bandari ya Dar es Salaam. Utajiri wake unakadiriwa kuwa dola bilioni 1 za Marekani. Alikua ndiye bilionea wa kwanza nchini mpaka pale MO Dewji alipochukua nafasi hii. Ndiye tajiri wa kwanza kuwahi kufikia kada hii ya matajiri bilionea kutoka Tanzania.


1. MOHAMMED DEWJI

MO Dewji ni miongoni mwa matajari wenye umri wa miaka 40 barani Afrika. Anamiliki 75% ya hisa zote katika kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd (METL) ambayo inamiliki viwanda vingi nchini. Baada kupata umiliki wa viwanda vya nguo na mimea ya mafuta kutoka serikali ya Uganda utajiri wake ukaanza kukua kwa kasi. Ana utajiri uanaokadiriwa kufikia dola bilioni 1.3 za Marekani, hii inamfanya kuwa tajiri namba 1 kwa sasa nchini. MO alitajwa na Forbes kuwa tajiri namba 1 nchini mwanzoni mwa mwaka huu na bado ameendelea kushikilia namba hiyo. 


Chanzo: Forbes Raking

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

KUZALIWA 

Celebrity wetu wa leo ni Shania Twain. Jina lake la kuzaliwa ni Eilleen Regina Edwards lakini umaarufu wake umetokana na jina lilizoeleka la Shania Twain. Wengine wanamuita Malkia wa Muziki wa Country.  Alizaliwa mnamo Agosti 28, 1965 leo anatimiza miaka 53 ya kuwepo duniani. Alizaliwa huko Windsor, Ontario, Canada akiwa ni mmoja kati ya mabinti 3 wa Clarence na Sharon (Morison) Edwards. Yeye ndiye mkubwa. Alipokua na miaka 6 mama yake aliolewa tena na Jerry Twain ambaye alimchukua kama mwanaye. Alianza kuimba katika vilabu vya pombe na alipokua na miaka 13 alionekana katika The Tommy Hunter Show. Alipokua na umri wa miaka 22 wazazi wake waliuawa katika ajali na hivyo akaacha sanaa muziki ili awalee wadogo zake Mark na Darryl pamoja na dada zake wawili aliozaliwa nao kwa baba yake na mama yake mzazi. Mwaka 1991 alibadilisha jina lake alilopewa na wazazi wake na kujiita Shania Twain na hapo ndipo jina hili lilipokua.  Mwaka huo huo pia alisaini mkataba na lebo ya muziki ya Mercury Nashville.
Shania siku za hivi Karibuni.


KUOLEWA

Shania amewahi kufunga ndoa mbili ambapo ndoa ya kwanza alifunga na Robert John Lange Desemba 28, 1993 na ilidumu hadi Juni 9, 2010. Katika ndoa hii walifanikiwa kupata mtoto 1 kabla hawajaachana. Baadaye January 1, 2011 aliolewa na Frederic Nicolas Thiebaud ambaye yuko naye mpaka sasa. Hawajabahatika kupata mtoto. 

TUZO


Shania amewahi kushinda tuzo kadhaa na kutajwa katika nyingine:

Mwaka 1996 alitajwa katika tuzo za Grammy kama msanii bora chipukizi lakini hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo.


Mwaka 1997 aliteuliwa kuwania tuzo za Gemini katika kipengele cha mtumbuizaji bora katika vipindi mbalimbali vya television, huku pia hakufanikiwa kutwaa tuzo.

Mwaka 1998 aliteuliwa kuwania tuzo za MTV kama Video Bora ya Msanii wa Kike: You're Still the One. Huku pia hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo. Mwaka huu alishinda tuzo ya Grammy na wimbo wake wa From this Moment on.

Mwaka 1999 aliteuliwa kuwania tuzo ya Grammy kama Wimbo wa Mwaka: You're Still the One, pia hakufanikiwa kupata tuzo hiyo. 

Mwaka 2004 alifanikiwa kutwaa tuzo ya Bambi katika kipengele cha Pop Kimataifa. 

Mwaka 2005 Grammy walimchagua katika vipengele viwili; mtumbuizaji bora wa kike wa muziki wa country na kolabo bora ya country. Bado hakufanikiwa pia kutwaa tuzo. 

Mwaka 2011 alitwaa tuzo kama Nyota wa tuzo za Walk of Fame. 
Shania Twain katika video ya For evre and for always. 

ALBUM ZAKE

Shania Twain (1993)
The Woman In Me (1995)
Come Over (1998)
Up (2003)
Now (2017)

MENGINE KUHUSU SHANIA TWAIN

Anakula mboga za majani na alipendekezwa kua na mvuto kutokana na hili.

Mwaka 1995 aliorodheshwa kama Mtu mwenye majibu Halisi anapoulizwa maswali katika jarida la People Weekly.

Amewahi kukaa kwenye namba za juu za muziki duniani kwa wimbo wake You're Still the One ambayo ilishika namba 1 kwenye chati ya Billboard mara 7. Pia alishika namba 2 katika chati za Hot 100 kwa wimbo huo mwaka 1998.

Wimbo wake "Love Gets Me Everytime" ulikua ni wimbo ulioshika nafasi ya juu zaidi ya Billboard kwa wiki 5 katika nyimbo za country tangu wimbo wa mwisho wa Dolly Parton "Here You Come Again" uliposhika nafasi hiyo mwaka 1997.

Mwaka 1999 alitajwa kama mtumbuizaji bora wa muziki wa country na mwaka huo huo CMA walimtuza tuzo ya mwaka ya mafanikio katika muziki huo.

Mwaka 1999 aliuza nakala milioni 19 za albam yake ya Come Over nchini Marekani peke yake.

Mwaka 2003 aliwahi kushinda tuzo ya Juno ka Chaguo la Mashabiki.

Album yake ya Come Over (mauzo na matamasha) viliingiza dola za Marekani milioni 40 nchini Australia pekee. Hii inaifanya kuwa miongoni mwa album zilizowahi kushika chati za juu za muda wote nchini humo.

Alishika namba 39 katika orodha ya Jarida la Maxim kama mwanamke mwenye mvuto katika wanawake 100 waliotajwa katika orodha hiyo ya mwaka 2005.

Album yake ya Up (2002) iliuza nakala milioni 2 nchini Marekani ndani ya mwezi 1 tangu ilipowekwa sokoni.

Alipokua mdogo alikua na aibu na alikua Tom boy.

Amekua katika familia maskini ambayo chakula tu ilikua ni tabu. Shania alikua akienda shule bila kula kutokana na hali ya maisha kifedha nyumbani kwao.

Anapenda kushinda nyumbani na kupika. 
Anaamini kwamba yeye ni kama watu wengine.

Ni miongoni mwa wasanii wa 4 kutoka nchini Canada waliowahi kushika namba za juu katika chati ya Billboard tangu kuanzishwa kwake mwaka 1944. Wengine kutoka Canada ni Hank Snow, Anne Murray na Terry Klark.

Aliwahi kusema kwamba anapendezwa na majukumu wanayofanya wanaume katika maisha ya kila siku.

Shania anawasema kuwa anasikitika siku zote kwa kua ndoa yake ya awali alivunjika.

Anao wafuasi 863K katika mtandao wa Instagram. Katika mtandao wa Twitter anao wafuasi 901K. Katika mtandao wa Facebook anao wafuasi zaidi ya milioni 5. Ukurasa wake wa YouTube umetazamwa na watu bilioni 1.2 huku akiwa na subscribers zaidi ya bilioni 1.1.

Haya ni machache kati ya mengi niliyokuandalia kuhusu mwanamuziki Shania Twain. Kama una maoni usisite kuniandikia kupitia barua pepe: venancegilbert@gmail.com ama ujumbe Whatsapp 0712586027. Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG na karibu tena kwa mengine mengi. 

LEO AGOSTI 6 KATIKA HISTORIA

Leo ni Agosti 6, 2018 ikiwa ni siku ya 218 katika mwaka 2018. Zimesalia siku 147 katika mwaka huu. Nakukaribisha tena katika muendelezo ya Leo Katika Historia. Kwa leo nimekuletea matukio kadhaa yaliyopata kutokea katika historia ya dunia, na tuanze kuyahesabu matukio hayo:

MATUKIO

1787 - Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Marekani ilianza kujadiliwa huko Philadelphia.

1890 - Hukumu ya kuuawa kwa kiti cha umeme ilianza kutekelezwa katika gereza la Auburn huko New York, Marekani ambapo William Kemmier alihukumiwa kifo katika kiti cha umeme kwa kumuua mpenzi wake Matilda Ziegler kwa shoka. Adhabu hii ya kifo ilipendekezwa mwaka 1881 na Dk. Albert Southwick baada kushuhudia mlevi akiuawa kwa shoti ya umeme. Katika kutekeleza adhabu hii zilitumika volti 700 za umeme na katika sekunde 17 umeme ulifeli kabla Kemmier hajafariki na baadaye waliongeza umeme hadi volti 1,030 ndani ya dakika 2 na ndipo Kemmier alifariki.
Kiti cha Umeme kilichotumika kutekeleza adhabu ya kifo kwa Kemmier.

1904 - Jeshi la Japan lililokua nchini Korea lilizunguka Jeshi la Urusi ambalo lilizidiwa nguvu na kuamua kurudi nyuma katika jimbo la Manchuria.

1945 - Ndege ya Marekani B-29 ikiongozwa na rubani Paul Tibbets ilidondosha bomu la nyuklia katika jimbo la Hiroshima. Bomu hilo liliua watu waliofikia 80,000 na pia watu 35,000 walijeruhiwa na inakadiriwa kua baadaye mwishoni mwa mwaka huo watu wengine 60,000 walifariki kwa madhara ya bomu hilo. Kulikua na majengo 90,000 katika mji wa Hiroshima lakini baada ya bomu kulipuka yalibaki majengo 28,000 tu, madakatari walikua 200 lakini waliosalia walikua 20 tu, manesi walikua 1,754 lakini walisalia 150 tu.
Ndege aina ya B-29 iliyodondosha bomu la nyuklia huko Hiroshima.
Baada ya bomu kudondoshwa hali ilikua hivi. 

Hivi ndiyo Hiroshima ilivyojengwa kwa sasa. 

1962 - Jamaica ilipata Uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza baada ya kutawaliwa kwa miaka 300.

1973 - Mwanamuziki wa Marekani Steve Wonder alipata ajali ya gari iliyopelekea kupoteza fahamu kwa siku 4.

1993 - Papa John Paul II alichapisha makala iliyohusu Umuhimu wa Kanisa Katoliki katika kufundisha maadili.

KUZALIWA

1809 - Mtunzi wa mashairi wa Uingereza Alfred Lord Tennyson alizaliwa. Moja kati ya mashairi yake maarufu ni "The Charge of the Light Bregade" la mwaka 1850.

1881 - Alexander Flemming mgunduzi wa dawa aina ya Penicillin mwaka 1928 alizaliwa.

1911 - Muigizaji na mchekeshaji wa Marekani Lucille Ball alizaliwa. 

1934 - Piers Anthony Dillingham Jacob mwandishi wa riwaya za kisayansi na matukio ya ajabu na ya kusimumua alizaliwa.