Skip to main content

KUTOKA TCU: TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UDAHILI AWAMU YA KWANZA 2017/2018



TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA (TCU)

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UDAHILI 2017/2018

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inautangazia umma kuwa Awamu ya Kwanza ya kudahili wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na masomo ya shahada za awali ilimalizika tarehe 30 Agosti 2017. Katika awamu hiyo, kama ilivyoelezwa katika tangazo la Tume la tarehe 20 Julai 2017 wanafunzi watarajiwa walituma maombi yao moja kwa moja kwenye vyuo hapa nchini. Vyuo vilichakata maombi hayo na hatimaye kuyawasilisha Tume kwa ajili ya uhakiki.Tume inapenda kuuarifu umma kuwa imekamilisha zoezi la uhakiki wa majina ya waombaji wote walioomba kujiunga na Vyuo vya Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo wa 2017/18. Matokeo ya uhakiki ni kama ifuatavyo:a) Jumla ya idadi ya majina yaliyowasilishwa toka vyuoni yalikuwa 180,640 (wanaume 109,399, wanawake 71,241). Hata hivyo majina haya yalikuwa na kasoro kadhaa kama vile kujirudia. Tume iliyahakiki na kubakisha majina 77,756 (wanaume 47,501 wanawake 30,255) ambayo ni jumla ya maombi yote.b) Jumla ya wanafunzi ambao wamechaguliwa na vyuo (kati ya
waombaji 77,756) ni 44,627 (wanaume 27,116 wanawake 17,511).


Hiyo ni sawa na asilimia 57.4 ya waombaji wote. Waombaji 33,129 

waliosalia (42.6%) hawakuchakuguliwa na vyuo kutokana na 
ushindani au kukosa sifa katika programu walizoomba.
c) Katika waombaji 44,627 ambao wamechaguliwa na vyuo, Tume 
imejiridhisha kuwa waombaji 20,247 (45.4%) wanaweza kujiunga na 
vyuo walivyoomba moja kwa moja (wanaume 12,396 wanawake 
7,851). Waombaji 16,584 (37.2%), wanaume 9,923 wanawake 6,661, 
wamechaguliwa zaidi ya chuo kimoja. Aidha waombaji 7,796 (17.4%), 
wanaume 4,797 wanawake 2,999, Tume imebaini kuwa hawana sifa 
za kujiunga na vyuo vilivyowapendekeza. Hii ina maana waombaji 
36,831 (wanaume 22,319 wanawake 14,512) wanatarajiwa kujiunga 
na vyuo katika Awamu hii ya Kwanza.
Taarifa kuhusu majina ya waombaji waliochaguliwa na wale 
waliochaguliwa zaidi ya chuo kimoja zimewasilishwa kwenye vyuo husika.
Hivi sasa Tume imefungua maombi kwa Awamu ya Pili kuanzia tarehe 4 
hadi 10 Oktoba 2017 ili kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili:
a) Waombaji ambao wamechaguliwa zaidi ya chuo kimoja; waombaji 
hawa watatakiwa kuamua mara moja na kuchagua chuo kimoja tu na 
hatimaye kukiarifu chuo hicho
b) Waombaji ambao wamekosa nafasi kwenye awamu ya kwanza 
kutokana na ushindani au kukosa sifa katika programu walizoomba;
Aidha Tume imetumia fursa hii kuruhusu makundi yafuatayo kuomba 
udahili:
a) Waombaji wa Kidato cha Sita walioshindwa kuomba katika awamu ya
kwanza;
b) Waombaji wenye vigezo vya Stashahada waliochelewa kupata 
Namba ya Uhakiki wa Tuzo (AVN);
c) Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya “Cambridge” mwaka 2017 
na matokeo yao yameshatoka; na
d) Waliokuwa wanafunzi wa vyuo vikuu watakaokuwa na uthibitisho 
toka vyuo vyao vya awali.
Tume inapenda kusisitiza kuwa utaratibu wa kutuma maombi katika 
Awamu ya Pili ni ule ule uliotumika katika Awamu ya Kwanza ya Udahili. 
Hii ina maana kuwa waombaji watatakiwa kuwasilisha maombi yao moja 
kwa moja vyuoni na siyo kwenye Tume (TCU).
Tume inawashauri waombaji wote kutumia fursa hii fupi kukamilisha 
maombi yao ili kuepuka kukosa udahili kwa mwaka wa masomo 2017/18. 
Aidha Tume inawataka waombaji wote kutembelea Tovuti za vyuo ili 
kufahamu hatima ya maombi yao. Kwa wale ambao wamechaguliwa zaidi 
ya chuo kimoja wathibitishe sawia chaguo la chuo kimoja tu ili kuepuka 
uwezekano wa kukosa udahili kwa mwaka wa masomo 2017/18. 
Prof. Eleuther Mwageni
Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
5 Oktoba 2017

Unaweza kuipata taarifa hii kama PDF kwa KUBOFYA HAPA

Comments

Popular posts from this blog

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

EYMAEL: NIPENI YANGA NIIUE AL-AHLY

KOCHA Luc Eymael ambaye tayari ameshafanya mazungumzo ya awali na viongozi wa Yanga, ameuambia uongozi wa klabu hiyo kuwa anaijua vizuri Klabu ya Al-Ahly ya Misri na endapo watampatia kibarua hicho, atawasaidia kuwang’oa katika Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Akizungumza na Mwanaspoti kwa njia ya mtandao, Eymael ambaye ni raia wa Ubelgiji, alisema amefanya mazungumzo ya awali na mmoja wa viongozi wa Yanga kupitia barua pepe, ambapo alisema kama klabu hiyo itampatia ajira hiyo hana wasiwasi na uwezo wake katika kuwang’oa Al-Ahly ambao Yanga inatarajia kukutana nao raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Yanga itaanza michuano hiyo dhidi ya timu ya Comoronize ya Visiwa vya Comoro inayotajwa kuwa ni dhaifu na baada ya hapo itakuwa na kibarua kizito dhidi ya wababe hao wa Misri. Eymael aliyezaliwa miaka 54 iliyopita katika mji mdogo wa Tongeren, Ubelgiji alisema hajajua Yanga inaundwa na nyota wenye uwezo kiasi gani lakini anachoweza kuwaambia viongozi wa klabu hiyo ni k...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA

Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz . Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika. Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya  HAPA  ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya  HAPA  ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa: 1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3) SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno ku...

DIRISHA LA UFADHILI WA MASOMO "SAMIA SCHOLARSHIP" 2023/2014 LIMEFUNGULIWA

TANGAZO LA SAMIA SCHOLARSHIP MWAKA 2023/2024 UFADHILI KUPITIA SAMIA SCHOLARSHIP KWA WAHITIMU WENYE UFAULU WA JUU KATIKA MITIHANI YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2023 KATIKA TAHASUSI ZA SAYANSI 1.0 UTANGULIZI Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatangaza programu ya Ufadhili iitwayo SAMIA SCHOLARSHIP kwa masomo ya shahada ya kwanza kwa wanafunzi waliopata ufaulu wa juu katika mitihani ya Kidato cha Sita mwaka 2023 iliyoendeshwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) katika Tahasusi za Sayansi (PCB, PCM, PGM, CBG, CBA, PMC na CBN).  SAMIA SCHOLARSHIP itagharamia kwa asilimia mia moja (100%) masomo ya Elimu ya Juu kwa wanafunzi hao ambao wamepata udahili katika fani za Teknolojia, Uhandisi, Hisabati na Tiba. 2.0 SIFA ZA KUPATA UFADHILI Ufadhili huu utatolewa kwa wahitimu wa kidato cha sita wenye sifa zifuatazo: 1. Awe Mtanzania; 2. Awe na ufaulu wa juu kwenye mitihani ya taifa ya kidato cha sita mwaka 2023 iliyoendeshwa na NECTA katika tahasusi za sayansi; 3. Awe amepata ...

MGAHAWA WAKUMBWA NA KASHFA YA KUUZA NYAMA YA BINADAMU

Mgahawa mmoja mjini London umekumbwa na habari bandia za kuuza nyama ya mtu. Wafanyikazi katika mkahawa wa Karri Twist katika eneo la New Cross nchini Uingereza wamehangaishwa kwa kupigiwa simu kutoka kwa wateja wanaosema ''Kwa nini hamujafunga''?. Mkahawa huo wa chakula cha jioni ni mwathiriwa wa habari za mzaha zilizodai kwamba mmiliki wake alikamatwa kwa kuweka nyama ya binadamu katika chakula na kwamba miili 9 ilipatikana katika jokovu la mkahawa huo. Na watu wengine waliamini mzaha huo. Habari hiyo ilichapishwa katika chombo cha habari cha channel23news.com, mtandao ambao wateja wake wanaweza kuchapisha habari za uwongo ili kuwafanyia mzaha rafiki zao kwa kuchapisha moja kwa moja katika mtandao wa fecbook. Shinra Begum ambaye ndio mmiliki wake aliambia Newsbeat kwamba biashara hiyo ya familia imekumbwa na wakati mgumu tangu habari hiyo ilipochapishwa siku ya Alhamisi. ''Wakati watu walipoanza kunipigia simu na kuuliza iwapo tulikuw...

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI: TRUMP NA RUBIO WATOFAUTIANA KUHUSU UISLAM

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Marco Rubio amemshtumu Donald Trump kwa kusema kuwa Uislamu unachukia Marekani katika mjadala uliokuwa moja kwa moja runingani. Bwana Rubio ambaye anakabiliwa na ushindani wa maisha yake katika jimbo la Florida siku ya Jumanne amesema kuwa Uislamu una tatizo la itikadi kali lakini akaongezea kuwa Waislamu wengi wanapenda Wamerekani. ''Marais hawawezi kusema kile wanachotaka ,kuna madhara'',alisema huku raia wakimpigia makofi. Wagombea hao wanne wa chama cha Republican walisikia maombi kutoka kwa viongozi wa chama hicho kuwa na mjadala wa amani. Ikilinganishwa na mjadala uliopita ambao ulikabiliwa na na matusi ya kibinafsi mjadala huu ulikuwa na muongozo mzuri huku wagombea wote wakitoa malengo ya sera zao. ''Kufikia sasa siamini vile tumekuwa watulivu hapa'',bwana Trump alinukuliwa akisema. Lakini katika swala la Uislamu,kulikuwa na tofauti kubwa kati ya Trump na wagombea wengine huku wen...

FACEBOOK KUANZISHA PROGRAMU YA KUWAPATANISHA WAPENDANAO HUKU IKIIMARISHA KIWANGO CHA FARAGHA

Mark Zuckerberg mmiliki wa mtandao wa Facebook Kampuni ya Facebook  inaongeza faragha kwa watumiaji wake kwa kuweka sehemu ya kufuta historia ya ulichokitafuta katika mtandao huo wa kijamii. Aidha amesema kwamba programu hiyo itaangazia uhusiano wa muda mrefu na sio urafiki wa muda mfupi na itawatenganisha marafiki na watu wanaotarajiwa kuwa na uhusiano. ''Programu hii itakuwa na kiwango cha juu cha siri na usalama kutoka mwanzo'', aliongeza. Hivi karibuni kampuni hiyo ilikumbwa na kashfa ya kutothamini faragha za watumiaje wake huku watumiaji zaidi ya millioni hamsini walidukuliwa katika kipindi cha uchaguzi wa Marekani. Facebook imekua katika sakata la faragha ya watumiaje hivi karibuni, mamilioni ya taarifa za watumiaji zilichukuliwa bila ridhaa na kampuni ya Cambridge Analytica kwa matumizi ya wanasiasa.  Mark Zuckerberg amesema kuwa atahakikisha suala kama hilo halitajitokeza tena, kwa kutengeneza ulinzi zaidi wa mtandao huo. Kitendo hicho kilishusha...