YANGA KUMKOSA COUTINHO KATIKA MCHEZO WA NGAO YA HISANI


Coutinho aliumia katika mechi ya kirafiki kati ya timu yake na Polisi Dar es Salaam mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Loyola, unaotumiwa na Yanga kwa mazoezi



TIMU ya Yanga huenda ikakosa huduma ya kiungo wake mshambuliaji wa kimataifa kutoka Brazili Andrew Coutinho,katika mchezo wa Ngao ya Jamii Jumapili wakati timu hiyo itakapokuwa inapambana na Azam FC,kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam Goal inafahamu.

Coutinho ameumia kifundo cha mguu na taarifa za madaktari wa Yanga zinasema huenda Mbrazili huyo aliyejiunga Yanga kwa mkataba wa miaka miwili huenda akakaa nje kwa wiki mbili hadi tatu.

Daktari wa Yanga Juma Sufiani,ameiambia Goal,bado wanaendelea kuangalia uwezekano wa kumtibu mchezaji huyo ili aweze kuichezea timu yake kwenye mchezo wa Jumapili kutokana na umuhimu wake ndani ya kikosi chao.

Kuelekea mchezo huo Azam tayari wametangaza nahodha wake John Bocco,kutocheza mechi hiyo ya Jumapili kutokana na kuumia misuli kwenye mchezo wa robo fainali ya michuno ya Kombe la Kagame iliyomalizika mwezi uliopita Kigali Rwanda.

Coutinho aliumia katika mechi ya kirafiki kati ya timu yake na Polisi Dar es Salaam mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Loyola, unaotumiwa na Yanga kwa mazoezi.



Chanzo: Goal.com

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI