HISTORIA KWA UFUPI KUHUSU NELSON MANDELA

Rais Nelson Mandela amefariki baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya maambukizi ya pafu. Katika maisha yake Mandela alifungwa jela kifungo cha maisha lakini alikaa jela kwa miaka 27 katika gereza lililo katika kisiwa cha Robben huko Afrika Kusini na baadaye aliachiwa huru mwaka 1990. Mandela alipigania ukombozi na uhuru wa mwafrika kwa amani na iliposhindikana yeye pamoja na wanachama wenzie wa ANC waliamua kutumia nguvu ya mtutu wa bunduki mpaka walipofanikiwa. Mwaka 1994 alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini. Tofauti na viongozi wengine wa Afrika, Mandela alihudumu kwa miaka 5 tu kisha alistaafu mwaka 1999 na kubaki kama balozi wa Afrika Kusini dhidi ya UKIMWI. Alizaliwa mwaka 1918 Mashariki mwa Rasi ya Tumaini Jema na amefariki akiwa na umri wa miaka 95. Harakati zake katika kupigania ukombozi wa mwafrika zinafanana na zile za watu weusi huko Amerika. Enzi za uhai wake aliwahi kuyasema haya: "During my lifetime I have dedicated myself to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination". Alishinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1993 iliyompa heshima kubwa ulimwenguni kote licha kuwa aliwahi kufungwa jela miaka 27. Alishiriki katika juhudi za kutafuta amani nchini Burundi, DRC na kwingeneko barani Afrika. Hakika atakumbukwa kwa mengi sana.
MWENYEZI MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI. 

NELSON MANDELA AFARIKI NYUMBANI KWAKE JOHANESBURG

Jana usiku shujaa wa Afrika Mzee Nelson Mandela alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 95. Amefariki kwa ugonjwa wa maambukizi ya pafu, ugonjwa uliomsumbua kwa muda mrefu. Pia katikati ya mwaka huu alikaa hospitali kwa muda wa miezi 3 na baadaye mwezi wa tisa alitolewa hospitali na kwenda kutibiwa nyumbani kwake Johanesburg mpaka mauti yalipomfika. Rais wa nchi hiyo, Jackob Zuma amesema taifa limempoteza shujaa wao na kwamba mwili wake utasifirishwa kwenda kuhifadhiwa katika mochwari ya mji mkuu Pretoria na kwa taratibu za mazishi zitafanywa Jumamosi ijayo pia atazikwa kwa heshima kubwa ya kitaifa na pia bendera zote zitapepea nusu mlingoti nchini humo kama maombolezo ya shujaa huyo... MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI..

MAINDA AWACHANA LIVE CHUCHU NA JOHARI

Hapo majuzi kupitia mtandao mmoja wa kijamii mwanadada Mainda aliamua kuvunja ukimya baadaya kuamua kuwachana live ‘wabaya’ waka Chuchu hans, na Johari kuhusu sakata linaloendelea la wao kumgombania mwigizaji Vicent kigosi ambaye anadaiwa alikuwa mpenzi wa mrembo huyo. Bila kupoteza muda soma hapo chini alivyofunguka mwanadada huyu… "Hizi salamu zako Johari, ni hivi naomba usinitaje kwenye huo upumbavu wenu, Huyo mwanaume mnae mzungumzia mimi kwangu namuona mtu wa kawaida tu ndio maana nikatupa kule. Nadhani umenipata alafu sitaki kumpandisha mtu jina sawa?. Ni hivi mimi si mpinzani wako, nadhani mpinzani wako unamjua mliopiganana (Sakata la Johari na Chuchu hans kupigana) mkataka kutoana roho kisa shingo ya kuku mlivyokuwa wajinga na malimbukeni wa mapenzi wanaume hapawiganiwi. Nimewakalia kimya naona wewe mwenye kilanga umejitoa kimasomaso ukaenda kiu ukasema Mainda amebip wewe unataka kumpigia, ni hivi usiniweke kwenye upumbavu wenu, mimi huyo mwanaume wenu kwangu ni kuku kama kumtafuna nimemtafuna mpaka mifupa alafu nikatupa kwenye shimo la taka, sasa nyiyni mbwa koko mlio kosa wafugaji ndio mnaruka ovyo hamjui mle nini, pumbavu kabisa wewe na mke mwenzio sindio amkauki kunisema me mgonjwa, sasa kama me mgonjwa huyo bwana wenu ni hivi wewe mwenye shape kama ubao usiejielewa nakushauri achaha na mimi nenda sinza" SOURCE: babamzazi.com

TODAY'S QUOTES

1. Love cures people-both the ones who give it and the ones who receive it. -Dr. Karl Minnesinger.

2. There is a land of the living and a land of the dead and the bridge is love. -Thornton Wilder

3. Children will not remember you for the material things you provided but for the feeling that you cherished them. -Richard L. Evans

 4. The heart of a fool is in his mouth, but the mouth of a wise man is in his he art. -Benjamin Franklin

FURAHI KIDOGO KWA KUSOMA HAPA

Kuna jamaa alkuwa anaumwa malaria daktari alpompima akasema huyu mgonjwa anatakiwa apewe KITANDA....jamaa kuckia hvyo akasema hapana kitanda ninacho labda SOFA, KABATI na KING'AMUZI