Skip to main content

GOOGLE INAADHIMISHA MIAKA 25

Ni miaka 25 tangu kuzaliwa kwa Google. Kwa kusema hivi namaanisha Google Inc. ambayo kwa sasa inafahamika kama Google LLC.

Google ilianzishwa Septemba 4, 1998, lakini imekua ikisherekea kumbukumbu ya kuanzishwa kwake tarehe tofauti tofauti hadi Septemba 27 mwaka 2005 ilipoanza kusherekea katika siku hii.

Miaka 25 ya Google imekua ya muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku hapa duniani kutokana na kuwepo makampuni mama amabyo yanashirikiana Google kuhakikisha huduma za mtandao zinakuwa sehemu ya kurahisisha maisha ya kila siku katika nyanja tofauti tofauti.

Google pia imeunda Doodle maalum kwa ajili ya siku yake ya kuzaliwa. Doodle ni ile picha ambayo huwa unaiona pale juu kabisa ukiwa utafuta kitu kwa kutumia Google Search. Tazama kwenye picha hapa chini.


Aida, imeonesha mabadiliko ya muda ya nembo ya kawaida ya Google ambayo mtambo wa kutafuta, mabadiliko hayo hufanywa kwa likizo, matukio mbalimbali kama kumbukizi ya siku ya uhuru wa nchi fulani mathalani Tanzania, au kuwaenzi watu mashuhuri katika siku zao za kuzaliwa.


Google Doodle ya Kwanza

Google Doodle ya kwanza ilikuja muda mfupi baada ya Google kuanzishwa. Ilikuwa rahisi, ikiwa na kiashiria cha mtu akiwa na fimbo juu ya nembo ya injini ya utafutaji mwaka 1998 wakati waanzilishi-wenza Larry Page na Sergey Brin walipochukua mapumziko kuhudhuria tamasha la Burning Man.

Tangu wakati huo,kumekuwa na zaidi ya Google Doodles 5,000 za kipekee zilizoundwa, kutoka Siku ya Wapendanao, kumbukumbu za kuenzi siku za kuzaliwa watu maarufu, maadhimisho ya siku za uhuru na mengine mengi. Timu ya wahandisi na wachoraji, wanaoitwa doodlers, wanawajibika kwa Google Doodles mbalimbali unaziona katika tovuti ya Google kila siku.

Doodle Maalumu ya kumbukumbu ya miaka 25 ya Google.

Katika kumbukumbu hii ya miaka 25 Google wameandika haya katika Doodle Maalum ya kumbukumbu ya miaka 25:

"Doodle ya leo inaadhimisha mwaka wa 25 wa Google. Ingawa hapa Google tunalenga siku zijazo, siku za kuzaliwa pia zinaweza kuwa wakati wa kutafakari. Wacha tutembee kwenye njia ya kumbukumbu ili tujifunze jinsi tulivyozaliwa miaka 25 iliyopita.

Kwa hatma au bahati nzuri, wanafunzi wa udaktari Sergey Brin na Larry Page walikutana katika programu ya sayansi ya kompyuta ya Chuo Kikuu cha Stanford mwishoni mwa miaka ya 1990. Wawili hawa wakafahamu kwamba wote walikua na maono sawa: "kufanya Wavuti ya Ulimwenguni kuwa mahali pa kufikiwa zaidi".

Wawili hao walifanya kazi bila kuchoka kutoka kwenye vyumba vyao vya kulala ili kutengeneza mfano wa injini bora ya utafutaji (search engine) Walipofanya maendeleo ya maana kwenye mradi huo, walihamishia operesheni hiyo hadi ofisi ya kwanza ya Google katika gereji iliyokodishwa.

Septemba 27, 1998, Google Inc. ilizaliwa rasmi. Mengi yamebadilika tangu 1998 ikiwa ni pamoja na nembo yetu kama inavyoonekana katika Doodle ya leo lakini dhamira imesalia ile ile: "kupanga taarifa za ulimwengu na kuifanya ipatikane na manufaa kwa wote". Mabilioni ya watu kutoka ulimwenguni kote hutumia Google kutafuta, kuunganisha, kufanya kazi, kucheza na mengi zaidi.

Asante kwa kuendelea kukua nasi katika kipindi cha miaka 25 iliyopita. Hatuwezi kusubiri kuona siku zijazo tukikua pamoja".

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

10. YUSUF MANJI Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini. 9. FIDA RASHID Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine. 8. GHALIB SAID MOHAMMED Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

ZIFAHAMU TEKNOLOJIA 7 ZITAZOKAZOKUZA MAENDELEO YA MAJIJI MAKUBWA DUNIANI

Fikiria ulikuwa unafanya kazi katika taasisi ya maendeleo na kupunguza umasikini mwanzoni mwa miaka ya 1990. Mwandishi wa makala hii, Abhas Jha anasema yeye aliwahi kufanya kazi zama hizi. Anasema kipindi hicho kulikuwa na tovuti moja tu iliyokuwepo duniani mpaka kufikia Agosti mwaka 1991 (leo kuna zaidi ya tovuti bilioni 1.5 duniani kote). Anasema kipindi hicho simu za mkononi zilikuwa ghali sana, chache na zilikuwa nzito na za kishamba sana ukilinganisha na hizi za sasa. Ni watu wachache wangetazamia kuhusu hali iliyopo nchini India kwa sasa kwamba kungekua na idadi kubwa ya simu za mkononi kuilko idadi ya vyoo. Bill Gates aliwahi kusema "tunayapa uzito sana mabadiliko ambayo yatatokea ndani ya kipindi cha muda mfupi sana na kuyapuuza yale yaliyotokea kwa muda mrefu sana". Teknolojia inakua kwa kasi sana na kufanya na mabadiliko makubwa sana kwenye majiji ili kufikisha huduma kwa jamii. Teknolojia inafanya hivi ili sio tu kufikisha huduma haraka kwa wateja bali pia kuk...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

WATU 23 WANADAIWA KUUAWA NA WAASI WA UGANDA HUKO DRC

Maafisa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanasema kuwa watu ishirini na watatu wameuawa kikatili na wanaodaiwa kuwa waasi wa Uganda. Wanane kati ya waliofariki ni wanajeshi wa DRC. Shambulizi hilo lilifanyika Jumatano usiku. Waasi wengi wao wakiwa wa Allied Democratic Forces (ADF) wamefanyana mashambulizi kadhaa kusini mwa mji wa Beni katika siku za hivi karibuni. Umoja wa mataifa unasema kuwa huenda walifanya makosa ya uhalifu wa kivita na vitendo vinavyokiuka ubinadamu . ADF imewaua mamia ya watu wakati mwingine na ndo, panga na visu. Chanzo: BBC

MIAKA 5 YA VENANCE BLOG NAWASHUKURU SANA KUWEPO HAPA TANGU KUANZISHWA KWAKE MEI 2013

VENANCE BLOG ilianzishwa Mei 2, 2013. Alhamis ya tarehe 2 Mei, 2013 nilitimiza kiu yangu ya kufungua Blog hii, lilikuwa ni wazo lililoishi toka mwaka 2012 nilipoanza kufahamu matumizi ya mtandao na tarehe hiyo lengo hili lilitimia. Huu ni mwaka wa 5 sasa nikiwa katika tasnia hii. Kuna wakati majukumu ya kitaaluma shuleni yanakaba sana mpaka nashindwa kuwa active kutokana na kufanya kazi hii nikiwa bado masomoni toka mwaka 2013 mpaka sasa. Kuwepo kwa Blog hii kumesaidia baadhi ya watu kupata taarifa na habari nyingine kwa mfano zile za kielimu hasa wakati wa selection za vyuo vikuu. VENANCE BLOG imekua msaada kwa baadhi ya watu, nimekua nikiwapa taarifa za habari hizi hasa wale walio katika mazingira ya kutokua na access ya mtandao. Pamoja na mengine mengi kama haya nimekua nikiitumia Blog hii kama platform ya kuchapisha mashairi yangu ambayo nimekua nikiyaandika kwa nyakati tofauti tofauti. Nawashukuruni sana wasomaji wangu kwa kutembelea Blog hii na kuyasoma mashai...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...