Skip to main content

ZIFAHAMU GAUNI BORA 20 ZA MWAKA 2017

Uhali gani msomaji wa VENANCE BLOG? Natumai u mzima, leo nakukaribisha kuzifahamu gauni 20 bora za mwaka 2017 zilizovaliwa na nyota wa fasheni na mitindo uli mwenguni.  Tuanze uchambuzi wetu.

Huyuy ni Natalie Potman. Muigizaji maarufu katika kiwanda cha filamu Marekani Hollywood. Huenda miezi tisa ya ujauzito huwa migumu sana lakini Natalie hakuchoka katika hilo. Gauni hili ni ubunifu wa Prada na alilivaa katika tuzo za Golden Globe Awrds, unaweza kuona gauni lilivo zuri na kumpendeza mjamzito na mimba yake hapo juu. Unapenda fasheni na mitindo? Basi hili litamfaa zaidi mjamzito.

Mwingine huyu. Anaitwa Brie Leson muigizaji mwingine kutoka kiwanda cha filamu Marekani. Brie alivaa gauni hili katika katika tuzo za 89 za Academy Awards. Ni ubunifu wa mwanamitindo Oscar de la Renta. Unaionaje gauni hiyo? Bila shaka kimpasuo hiko kidogo kinapendeza sana pamoja na mchanuo ule wa nyuma kama maua. Haya kazi kwako kupendeza na mtindo huu kwenye red carpet.

Huwezi kushindwa kumtambua mdada huyu mpenda fasheni na mitindo. Anafahamika kama Rihanna. Mtindo huu unafahamika kwa jina la Kawakubo. Nadhani unaona jinsi ulivyompendeza Rihanna pamoja na kiatu chake. Je, unaweza kuuvaa mtindo huu? Haya jibu liwe siri yako.

Mwanamitindo wa Uingereza Bella Hadid pia yupo katika orodha yetu. Mwanamitindo huyu alitimiza miaka 21 mwaka huu. Gauni hii imebuniwa na Ralph & Russo. Imekaaje hii gauni kwa upabde wako? Unaweza kuvaa? Bila shaka jibu lako ni ndio na mazingira yake pia unayafahamu.

Anaitwa Gigi Hadid. Huyu ni ndugu na mwanamitindo wetu hapo juu, Bella Hadid. Ana miaka 22. Ni ubunifu wa Mary-Kate na Asley Olsen. Haya kazi kwako mpenda fashion.

Anafahamika kama Isabelle Huppert. Kama unavyoona hapo katika red carpet, mdada huyu alipendeza katika gauni lake alipokuwa akifanya promo ya tangazo la Elle. Chukua nyingine hiyo.

Huyu ni Natalie Dyer. Unaambiwa vazi hili linafaa kwa mtoko na mpenzi wako. Ni vazi la mchanganyiko wa rangi za pinki na nyekundu. Unapotoka na mpenzi wako kwa mara ya kwanza kabisa baada ya makuba baada ya kukaa muda mrefu bila kutoka, gauni hili litakupendeza sana.

Wanafahamika kama The Dutches of Cambridge. Gauni hili ni ubunifu kutoka McQueen na lilivaliwa katika tuzo za Bafta. Nadhani unaona hapo rangi nyeusi inavyopendeza. Kiujumla couple hii ilipendeza sana.

Anaitwa Penelope Cruz. Huu ni ubunifu wa kampuni maarufu ya nguo duniani Versace. Penelope alipendeza katika red carpet ya British Academy Film Awards.

Unapenda gauni za kubana juu bila kuwa na mikanda ya kukushikilia kwenye mabega? Hii inakufaa sana. Rangi ya pinki nzuri sana kwa wadada. Anaitwa Lily-Rose Depp. Hkika gauni hii inapendeza sana sio siri. Ubunifu huu unaitea The Channel.

Muigizaji Kristin Scott Thomas pia alipendeza na ggauni hili. ilikuwa ni katika kusherehekea miaka 70 ya Cannee. Make up aliyofanyiwa siku hii pamoja na gauni lake vilimfanya apendeza sana.

Sienna Miller pia amehusika katika orodha yetu kwa gauni lake hili la ubunifu wa Gucci. Hii ilikuwa mapema sana mwezi Januari katika uzinduzi wa gauni la Alessandro Michelle. Gauni lake hilo lenye muundo wa mawimbi fulani na lipsi nyekundu vilimfanya apendeze sana.

Claire Foy pia anahusika katika orodha yetu. Gauni hili lenye mkia nyuma pamoja na utepe hapo kiunoni ilimfanya apendeze sana. Claire amekuwa moja ya waigizaji na wanamitindo aliypamba katika ukurasa wa mbele wa jarida maarufu la mitindo nchini Uingereza la Vogue. Ubunifu huu ni maarufu kama Erdem. Hii ilikuwa ni katika jukwaa maarufu la maonesho la The Crown.

Hakika red carpet inapendeza sana. Unamuoana Elle Fanning alivyopendeza? Ni katika anniversary ya Cannes. Gauni hili limetengenezwa kwa vito pamoja na material za almasi. Nadhani unafahamu kwamba madini ya almasi hung'aa sana.

Bila shaka unaona rangi hii sio ya kizungu zaidi. Anaitwa Ruth Negga ni muigizaji anaykuja vizuri katika tasnia ya filamu nchini Uingereza bila shaka na duniani kote. Muigizaji huyu ni raia wa Uingerza mwenye asili ya Ethiopia na Ireland. Bai gauni lake hili ni ubunifu wa Louis Vuitton. Hii ilikuwa ni katika tuzo za Golden Globe Awards. 

 Anaitwa Emma Stone. Ubunidu guu unajulikana kama Givenchy Haute Couture ambao ni hatimiliki ya mbunifu Riccardo Tisci. Ubunifu huu ulimfanya Emma awe na muonekano mzuri.

Unamuona Marion Cotillard, yupo katika ubunifu wa Halpern. Mwaka 2017 ni mwaka ambao Halpern amehitimu kutoka Central Saint  Martins ambako alikuwa akisomea mabo ya mitindo hasa hasa ubunifu wa kumpendezesha mtu kwenye red carpet. Gauni hili hili limewapa sifa mbunifu pamoja Marion kiasi cha kufanya mbunifu Halpern kuchukua tuzo yake ya kwanza katika masuala ya fashion.

Anaitwa Cara Delevingne. Huu ni ubunifu wa Iris van Heprn.Bila shaka unafahamu kwamba unapotakiwa kufanya tangazo la kitu chochote lazima uonekane vizuri. Hapa Cara alikuwa katika tangazo la Valerian.

Emma Watson alihitajika katika kutengeneza muvi ya Disney ambayo ina maudhui ya karne ya 21. Ili kupata vazi linaloendana na maudhui ya muvi iliwapa Emma na team yake kuandaa documentary ya The Press kwa ajili ya upatikanaji wa nguo hii ambapo alishinda mwanamitindo Emilia Wickstead kwa ubunifu huo unaouona hapo pichani.

Tumalize na Keira Knightley. Hii ni kutoka katika collection maarufu ya mavazi ijulikanayo kama Spring/Summer 2018 Colletion. Keira pia aliamua kupanda kwenye red carpet kwa gauni hili mapema mwezi hu. Gauni hili ni maarufu kwa jina la Valentino.

Kama una maoni kuhusu makala hii na mengineyo, nitumie kwa WhatsApp namba 0712586027, ama barua pepe venancegilbert@gmail.com, pia Facebook VENANCE BLOG pamoja na Twitter @Venancetz. Usisite kutembelea VENANCE BLOG wakati wowote.

MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA JARIDA MAARUFU LA MITINDO NCHINI UINGEREZA LA THE VOGUE NA KULETWA KWAKO NA VENANCE GILBERT. PICHA ZOTE NI KWA HISANI YA GETTY IMAGES.

Comments

  1. Helllo to every body, it's my first go too see of
    this blog; this weblog includes amazing and genuinely excellent stuff
    in support of readers.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

FRIENDSHIP QUOTES OF THE DAY MAY 26, 2018

Today I invite you to read these quotes of the day. Enjoy your day. 1.  One of the most beautiful qualities of true friendship is to understand and to be understood. ~Lucius Annaeus Seneca. 2.  Walking with a friend in the dark is better than walking alone in the light. ~Helen Keller. 3.  There is nothing on this earth more to be prized than true friendship. ~Thomas Aquinas. 4.  My best friend is the one who brings out the best in me. ~Henry Ford. 5.  It is one of the blessings of old friends that you can afford to be stupid with them. ~Ralph Waldo Emerson. 6.  The strong bond of friendship is not always a balanced equation; friendship is not always about giving and taking in equal shares. Instead, friendship is grounded in a feeling that you know exactly who will be there for you when you need something, no matter what or when. ~Simon Sinek. 7.  A friend is someone who gives you total freedom to be yourself. ~Jim Mo...

IDADI YA WATU WALIOFARIKI UGANDA YAFIKIA 33

Moto mkubwa uliowaka baada yaajali mbaya ya barabarani iliohusisha lori la mafuta, umewauwa takriban watu 33 mjini kampala Uganda. Watu wengine 30 wanadaiwa kujeruhiwa vibaya kufuatia tukiohilo. Maafisa wa polisi wanasema kuwa kati ya waliofariki ni raia waliokuwa wanakimbilia eneo hilo la mkasa kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwa lori hilo. maafisa wa serikali walikuwa katika harakati za kutambua mili ya waliofariki baada ya wengi wao kuchomeka vibaya. Idara ya polisi imesema kuwa waliofariki waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.

VITAMBULISHO VYA URAIA KUVUKIA MIPAKA KENYA, RWANDA NA UGANDA

Wananchi wa mataifa ya Rwanda, Uganda na Kenya wamepokea kwa shangwe kuanza kwa mpango wa kutumiwa kwa vitambulisho vya uraia kama cheti cha kuwaruhusu kuvuka mpaka na kuingia moja wapo wa nchi hizo.Mpango huu wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kusafiria katika nchi hizo tatu umeanza kutumiwa rasmi tarahe Mosi Januari 2014, kufuatia makubaliano kati ya viongozi wa mataifa hayo.Mpango wenyewe unatokana na makubaliano kati ya viongozi wa nchi tatu waliofikia wakati wa mkutano uliofanyika nchini Uganda mwezi Juni mwaka jana.Pia mpango huu unalenga kurahisisha usafiri wa watu wa jumuiya katika mataifa wanachama kama awamu ya pili ya ushirikiano kati ya mataifa wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.Hata hivyo siku moja tu baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kuwaruhusu raia wa nchini tatu, Uganda, Kenya na Rwanda kuvuka mpaka na kuingia mojawapo ya nchi hizo sasa inaonekana mpango huo huenda ukawanufaisha watu wachache peke yake.Sio ...

CHANGES QUOTES OF THE DAY MAY 23, 2018

Hello dear reader, welcome once again. Today I have gathered the quotes concerning changes in life. I should not write more since I am not not the speaker in this category, take your time to dive in and become intellectual with full equipped knowledge from the great men of history Remember, someday it might be you. Do not rely on inspiration from friends while you are needy, VENANCE BLOG is here for you. Welcome all the time by searching Quotes. Now proceed. 1. Every great dream begins with a dreamer. Always remember, you have within you the strength, the patience, and the passion to reach for the stars to change the world. ~Harriet Tubman. 2. Change your thoughts and you change your world. ~Norman Vincent Peale. 3.  If you don't like something, change it. If you can't change it, change your attitude. ~Maya Angelou 4.  Change will not come if we wait for some other person or some other time. We are the ones we've been waiting for. We are the change that...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...