Skip to main content

FAHAMU MAKALA BORA ZA KISAYANSI ZILIZOSAIDIA JAMII 2017


Karibu ndugu msomaji wa VENANCE BLOG. Leo nimekuletea makala fupi zakisayansi ambazo zilipata umaarufu kwa mwaka huu kwa ufupi sana, na tuanze sasa

Biashara ya siri kuuzwa sokwe Afrika Magharibi









Nemley junior, the infant rescued from traffickers after our investigation

David Shukman na Sam Piranty walifanya utafiti mrefu Afrika Magharibi na BBC kugundua mipango ya siri inayohusiana na uuzwaji wa wanyamapori hasa sokwe. Hii ilisaidia kunusurika kwa sokwe aitwaye Nemley Jr ambaye alikuwa na umri wa mwaka mmoja.


Mtambo wa Kupunguza Kabonidayoksaidi angani

fans
Katika mwaka 2017, riport zilionesha kwamba kuna mrundikano mwingi wa gesi ya kabonidayoksaidi angani mpaka kufikia wingi huo kuvunja rekodi huku juhudi za kimataifa zikishindwa kutatua changamoto hiyo ili kuepuka hatari ya kuongezeka kwa joto duniani. Je teknolojia hiyo inaweza kuondoa gesi hiyo ya kabonidayoksaidi ili kujibu maswali mengi ambayo juhudi za kimataifa zimekua zikishinwa kujibu? Hii iliandikwa na Matt McGrath.

Misheni ya Anga ya Cassini kuitafiti sayari ya Sarateni ilivyokamilika

Artist impression of Saturn and its rings 
Misheni ya anga ijulikanayo kwa jina la Cassini space missionilifikia tamati  mwezi Septemba 2017, baada ya kutumia miaka13 kuchunguza sayari ya Sarateni (Saturn) pamoja na mwezi wa sayari hiyo. BBC iliweza kuonesha makala ya utafiti huo wa anga na jinsi utafiti huu wa anag unaharibu tabaka la hewa la sayari hiyo, lakini pia walihakikisha misheni hiyo walipata nafasi ya kuelezea uzoefu wao kuhusu utafiti huo wa aga. Makala hii iliandikwa na Paul Rincon.

Jinsi dunia yetu inavyofanya kazi zake kijiolojia

Dan McKenzie
Je, ni mambo gani ungeyaweka katika orodha ya mambo makubwa ya kisayansi yaliyowahi kutokea katika karne ya 20? Ugunduzi mkubwa zaidi ni ule unaofahamika kisayansi kama plate tectonic. Nadharia hii ina miaka 50 sasa, ni nadharia iliyotoa majibu ambayo kwa kiasi kikubwa yanaelezea sababu za kutokea kwa volkano na matetemeko ya ardhi. Makala hii iliandikwa na Jonathan Amos.

Ugunduzi ma utengenezaji wa Mtandao (Internet) wa kizazi kijacho

The global internet
Kompyuta zenye kasi zaidi zinagunduliwa na kutengenezwa mahali kote duniani. Lakini je, ni kwa nanmna gani kizazikijacho kitatumia komputa hiyo? Wanasayansi tayari wameanza kufikiria namna ya spidi ya mtandao (internet) abayo itaendana na kompyuta hizo. Makala hii iliandikwa na Mary-Ann Runson.

Trump kujenga ukuta mpakani na Mexico kunaharibu uoto wa jangwani mahala hapo pakijengwa

Skull
Rais wa Marekani Donald Trump aliahidi kujenga ukuta  ambao ungetumika kama mpaka kutenganisha nchi hiyo na Mexico, lakini ahadi hii bado inakua ngumu kutekelezeka katika utawala wake huu. Wanasayansi tayari wameanza kuzungumzia madhara ya kiikolojia yatakoyotokana na ujenzi wa ukuta huo. Ujenzi huo utaathiri uoto wa jangwa. Wasayansi hao wanafanya utafiti katika jangwa la Sonoran ambalo tayari lina mpaka unaolitenganisha Marekani na Mexico.Makala hii iliandikwa na Victoria Gill.

Mapinduzi katika ugunduzi wa kupata taarifa za kigenetiki (urithi) kuwafikia watu bilioni1 nchini India

Delhi Metro
Je, jitihada inaweza kutumika nchini India kukusanya taarifa hizi za kijenetiki kutoka katika idadi yake ya watu bilioni 1 ili kuboresha huduma za afya nchini humo? Hii iliandikwa na Kat Arney.

Ndege wanaoukamwatwa na kuuzwa kwa kuwa na sauti zinavutia

SongbirdNdege waliokuwa wanaimba vizuri zaidi yani sauti zao zinavutia wamekuwa wakikamatwa kwenye misitu huko Indonesia na kuuzwa. Hali hii inahatarisha uwepo wa viumbe hawa. Makala hii iliandikwa na Victoria Gill.


Mapinduzi katika utabiri wa hali ya hewa baada ya mwaka 1987

SupercomputerOktoba 15, 1987 kituo cha hali ya hewa cha nchini Uingereza kupitia BBC kilikanusha taarifa za kuwepo kwa kimbunga hatari cha Hurricane ambacho kingeikumba Uingereza. Usiku ule, nchi ilikumbwa na upepo mkali uliosababisha watu 18 kufariki. Katika kumbukumbu ya miaka 30 ya tukio hilo David Shukman aliangalia ni kwa namna gani teknolojia ingeweza kubadilisha utabiri wa hali ya hewa.


Binadamu anayeishi na viumbe wa ajabu na hatari zaidi

Ronald JennerHuwezi kuamini katika fikra zako kwamba kuna viumbe hatari sana ambao bado wanaishi mpaka sasa. Dr. Ronald anasoma kwa karibu tabia za viumbe anaoishi nao hasa wale wenye sumu za hatari kwa maisha ya binadamu. Hii ni makala iliyoandikwa na Jonathan Amos.


Jinsi mtafiti wa mimea wa Uingereza alivyoisadia Sayansi

Plant specimens are pressed under large rocks

Katika miaka ya mwanzoni mwa karne ya 20, muwindaji maarufu nchini Uingereza aliyekuwa akiwinda kwa kupanda juu ya miti alihatarisha maisha yake kwa kuingia nchini China kuchunguza mimea iliyokuwa nchini China kwa mgongo wa Sayansi. Kumbukumbu aliyoicha baada ya utafiti huo inapatikana katika bustani zilizopo nchini Uingereza. Makala hii iliandikwa na Helen Briggs.

Utafiti mpya kuhusu ugunduzi wa kufahamu uwezekano kuweko na maisha kwingineko

View of Europa taken in the 1990s by the Galileo spacecraft 
Baada ya miongo miwili (miaka 20) na kushindwa kukamilisha tafiti, wanasayansi hatimaye walifanikiwa kuitafiti bahari ya Europa. Je, huu utakuwa ni utafiti ambao unaweza kujibu maswali kwamba kuna uwezekano wa kuwepo na maisha katika sehemu nyingine tofauti na duniani? Makala hii iliandikwa na Paul Rincon.

Je, nguo zetu zinachafua mazingira?

Washing on the line 
Utafiti wa kisayansi ulionesha kuwa nguo za material ya polyster na acrylic zinatoa material ya plastiki ambayo wakati wa kufua husababisha uchafuzi wa mazingira hasa bahari. Je, tunawezaje kuzuia tatizo hili la uchafuzi wa mazingira. Makala hii iliandikwa na Victoria Gill.

Utafiti mpya kuhusu ndege jamii ya Dodo kuandikwa tena

Rodrigues Solitaire
Wanasayansi wapo katika hatua za mwisho kutengeneza makala ya kibailojia ambao ilipelekea ndege hawa aina ya Dodo kutoweka duniani. Uandishi huo utakuwa ni muendelezo wa utafiti wa mtafiti wa kifaransa aliyewatafiti ndege hao alipokuwa katika safari zake bahari ya Hindi. Makala hii iliandikwa na Rolly Galloway.

Kuna ugumu gani kumkata nzi?

Housefly 
 Jaribu kukamata nzi yeyeote na utagundua kwamba wao huwa na haraka kuliko wewe. Haraka zaidi. Lakini je ni kwa namna gani viumbe hawa wadogo ubongo wao huweza kuhisi hatari mapema sana na kukimbia? Huu ni utafiti wa kisayansi uliofanywa na Rolly Gallway.

Wadudu hatari ambao pia ni muhimu katika mazingira

Wasp
Mapema mwezi wa nane mwaka huu viumbe hawa walivamia hafla iliyokua imeandaliwa na August Bank nchini Uingerza kuliko hata ambavyo mawaingu yangetanda kuashiria mvua. Profesa Adam Hart mwanasayansi wa Uingerza anasema kwamba licha ya kuwa hatari sana, wadudu hawa ni muhimu sana katika ikolojia.

 
Nitumie maoni yako kupitia Whatsapp 0712586027 ama barua pepe venancegilbert@gmail.com. Facebook VENANCE BLOG na Twitter @Venancetz.


MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA SHIRIKA LA UTANGAZAJI LA NCHINI UINGEREZA; BBC. PICHA KWA HISANI YA GETTY IMAGES, NASA, CLIMEWORKS, THE GEOLOGICAL SOCIETY; MCKENZIE ARCHIEVE, JULIAN HUME, ROYAL BOTANIC GARDEN; EDINBURGH AND RHS, MET OFFICE, NHM, JPL CATECH, SETI INSTITUTE NASCIENCE PHOTO LIBRARY

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD  

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

LIST OF APPLICANTS SELECTED TO JOIN THE NATIONAL INSTITUTE OF TRANSPORT (NIT) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

To access the names of selected undergraduates click  HERE

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

DEADMEN SPEAKS: A POEM

Image generated with OpenArt AI tool It has been longtime since I published my poems on this platform, today I'm humbly inviting you to our section of poems. As you enjoy reciting this creativity, please don't forget to leave your comment after this post or writing via my contacts after this poem. Poem: Deadmen Speaks Poet: Venance Gilbert Composition: July 30, 2023 DEADMEN SPEAKS: A POEM BY VENANCE GILBERT I heard deadmen tells no tale but these ones do They are burdened with a lots Weak folks who talks nothing just talking in mind in the streets I say so because one of them is me I speak for deadmen. Six years with no stable duties to perform while responsibilities have taken-off This week this job next week none and I have to survive regardless But how without money How can I count money without job? I speak for deadmen. While I'm enjoying my jobless survival Executive wants to collect from my pocket I have to pay tariff to buy light tariff to withdraw my hard-earned sav...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

NExT-GPT: MFUMO WA LUGHA WA AKILI BANDIA UNAOKUPA MAJIBU KWA MAANDISHI, PICHA, SAUTI NA PICHA MJONGEO

Picha hii imetengenezwa kwa Akili Bandia na Decrypt. Katika uwanda mpana wa teknolojia unaotawaliwa na makampuni makubwa kama OpenAI na Google, NExT-GPT ambao ni mfumo huria wa lugha pana ya Akili Bandia (AI) [Large Language M odel (LLM)] unaweza kuwa na kile kinachohitajika ili kushindana na miamba hii miwili katika teknolojia. ChatGPT imeusisimua ulimwengu kwa uwezo wake wa kuelewa maswali katika lugha asilia na kutoa majibu kama ya binadamu. Lakini wakati Akili Bandia inaendelea kusonga mbele kwa kasi ya umeme, watu wametaka kuwepo na maendeleo zaidi. Zama za maandishi pekee zimekwisha sasa mifumo ya lugha ya Akili Bandia imeanza kuwa mingi kuleta ushindani. NExT-GPT imetengenezwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha taifa cha Singapore (NUS) na Chuo Kikuu cha Tsinghua. Inaweza kuchakata na kutoa majibu kwa kuchanganya maandishi, picha, sauti na picha mjongeo (video). Hii inaruhusu majibizano ya asili zaidi kuliko miundo ya maandishi pekee kama ilivyo kwenye ChatGPT. T...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...