Skip to main content

TETESI ZA UHAMISHO ULAYA: NANI WANATARAJIWA KUHAMIA KLABU MPYA JANUARI?

Ni wakati mwengine wa mwaka ambapo uvumi utaanza kusambaa. Uhamisho wa mwaka uliopita haukuwa na changamoto nyingi kutoka kwa timu sita bora katika ligi ya Uingereza huku timu zote za ligi hiyo zikitumia £215m mwezi Januari.
Wakati huu itakuwaje, Je timu kubwa zitagharamika kununua wachezaji?

Barani Ulaya...
Dirisha la uhamisho katika ligi tano kuu litafungwa kwa wakati mmoja. Dirisha la uhamisho la klabu za Uingereza, Ufaransa , Ujerumani , Italia  na Uhispania litafungwa Desemba 31 mwaka huu

DIEGO LOPEZ (klabu: Espanyol; Safu: kipa; Umri: 36)
DIEGO LOPEZ (klabu: Espanyol; Safu: kipa; Umri: 36) 
Anahusishwa na uhamisho wa :Crystal Palace.
Ni kipa anayejulikana kwa kupigania nafasi ya kipa na Iker Casillas katika klabu ya Real Madrid, alikuwa katika benchi wakati Reala Madrid iliposhinda kombe la vilabu bingwa 2014 na amekuwa mchezaji wa Ziada wa Espanyol kwa kipindi kirefu cha msimu. Pia aliichezea Villarreal, Sevilla na AC Milan.

KEVIN TRAPP (Paris St-Germain; kipa; 27)
Kevin Trapp
Anahusishwa na uhamisho wa : Crystal Palace, Borussia Dortmund, Liverpool.
Mkufunzi wa PSG boss Unai Emery ana mpendelea sana kipa Alphonse Areola, na kipa raia wa Ujerumani Trapp ameanza kukerwa kutokana na ukosefu wa fursa ya kuiwakiulisha timu yake hususan wakati huu ambapo wachezaji wanajianda kuziwakilisha timu zao za kimataifa katika kombe la dunia

DANIEL OPARE (Augsburg; Beki; 27)
DANIEL OPARE (Augsburg; Beki; 27)
Anahusishwa na uhamisho wa : West Ham, Stoke City, Everton, Swansea.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ghana ana uwezo wa kucheza kama beki wa kulia ama kushoto na anasakwa na baadhi ya vilabu vya Uingereza.Amekamilisha kandarasi yake na Augsburg na huenda klabu hiyo ya UJerumani inataka kumuuza.

LEON GORETZKA (Schalke; kiungo wa kati ; 22)
LEON GORETZKA (Schalke; kiungo wa kati ; 22)
 Anahusishwa na uhamisho wa: Manchester United, Arsenal, Barcelona.
Alikuwa katika kikosi cha Ujerumani kilichoshinda kombe la shirikisho ,Goretzka anafananishwa na kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Paul Scholes. Anakamilisha kandarasi yake mna yuko tayari kuondoka ili kupata changamoto mpya.

STEVEN NZONZI (Sevilla; kiungo wa kati; 29)
Steven N'Zonzi 
Anahusishwa na uhamisho wa: Everton, Arsenal.
Mchezaji huyo wa zamani wa Stoke na Blackburnalihusishwa na uhamisho wa kurudi katika ligi ya Uingereza baada ya kudaiwa kuzozana na mkufunzi wa zamani wa Sevilla Eduardo Berizzo, ambaye alifutwa kazi mnamo tarehe 22 Disemba. Uzoefu wake wa soka ya Uingereza kunaweza kumfanya kuwa kiungo muhimu.

ARDA TURAN (Barcelona; kiungo wa kati ; 30)
ARDA TURAN (Barcelona; kiungo wa kati ; 30)

Anahusishwa na uhamisho wa : Arsenal, Trabzonspor.
Mchezaji huyo wa Uturuki hajaichezea Barcelona tangu mkufunzi Ernesto Valverde kuchukua usimamizi wa klabu hiyo. Ametngaza wazi kwamba anataka kuondoka Nou Camp mnamo mwezi Januari.

JEAN MICHAEL SERI (Nice; kiungo wa kati ; 26)
JEAN MICHAEL SERI (Nice; kiungo wa kati ; 26)
Anahusishwa na uhamisho wa : Barcelona, Manchester City, Liverpool.
Mchezaji huyo wa Ivory Coast alikuwa akiwindwa na Barcelona katika dirisha la uhamisho lililopita, lakini Nice ilikataa ombi la viongozi hao wa La Liga . Nice imaimarika baada ya kupata matyokeo mabaya , na huku uwezo wa klabu hiyo wa kufuzu kushiriki katika kombe la vilabu bingwa ukiwa mchache , Seri anaweza kutaka kuondoka mwezi Januari.

JAVIER PASTORE (Paris St-Germain; kiungo wa kati mshambuliaji ; 28)
 JAVIER PASTORE (Paris St-Germain; kiungo wa kati mshambuliaji ; 28)
Anahusishwa na uhamisho wa klabu za: Liverpool, Sevilla, Inter Milan.
Mchezaji mwenye kipaji ambaye hajathibitishiwa kuwa ataorodheshwa katika kikosi cha kwanza cha PSG , Pastore alitajwa kuwa mchezaji bora duniani na Eric Cantona, ambaye anasema angependelea iwapo Patore angesajiliwa na man United .Mchezaji huyo wa Argentina anapigiwa upato kuwa mchezaji muhimu katika kombe la dunia.

GELSON MARTINS (Sporting Lisbon; Winga; 22)
GELSON MARTINS (Sporting Lisbon; Winga; 22)
Anahusishwa na uhamisho wa : Liverpool.
Sporting Lisbon inahitaji kitita kikubwa , na Martins anasemekana kuwa dau la kuondoka lakini mchezo wake katika ligi ya Ureno umevutia maoni yasio ya kawaida.

THOMAS LEMAR (Monaco; Winga/kiungo wa kati mshambuliaji; 22)
Thomas Lemar
Anahusishwa na uhamisho wa : Arsenal, Chelsea, Liverpool.
NI miongoni mwa nyota wa klabu ya Monaco ilioshinda ligi msimu uliopita , na sasa ameorodheshwa katika kikosi cha Ufaransa ambapo amefunga mabao mawili dhidi ya Uholansi katika mechi ya kirafiki mnamo mwezi Novemba.
Arsenal na Liverpool zilijaribu kumsajili katika dirisha la uhamisho lililopita.

HATEM BEN ARFA (Paris St-Germain; Winga/mshambuliaji /kiungo wa kati ; 30)
HATEM BEN ARFA (Paris St-Germain; Winga/mshambuliaji /kiungo wa kati ; 30)
 
Anahusishwa na uhamisho wa : Leicester City.
Baada ya msimu mzuri na Nice msimu uliopita 2015-2016, uhamisho wake hadi PSG haikuingiliana. Soka yake imekwama chini ya usimamizi wa Emery, ambaye haonekani kutakab kumpatia fursa ya kucheza katika kikosi cha kwanza. Meneja wa Ben Arfa's katika klabu ya Nice alikuwa Claude Puel, na huenda kuna uvumi kwamba huenda wakakutana tena katika klabu ya Leicester.

MAKALA HII NI KWA HISANI YA BBC.

Comments

Popular posts from this blog

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

MAMBO YA MUHIMU KUFAHAMU NA KUZINGATIA KABLA YA KUCHAGUA KOZI (TAALUMA) CHUO KIKUU

Picha kwa hisani ya Debt.org 1.0 UTANGULIZI Nilipokuwa mwanafunzi wa chuo kikuu nilisikia manung'uniko miongoni mwa wanafunzi wenzangu wengi wa vyuo vikuu ambayo yalitokana na taaluma wanazosoma. Kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea manung'uniko hayo miongoni mwa wasomi hawa tukiachilia mbali suala la ucheleweshwaji wa mikopo miongoni mwa wasomi hawa (kwa sasa changamoto hii inapungua kadiri siku zinavyosonga). Tatizo lingine ambalo linawasumbua wasomi hawa ni suala la uchaguzi wa taaluma gani akaisome Chuo Kikuu. Uchaguzi wa taaluma (career choice) ni jambo nyeti sana na la kuzingatia kwa muhitimu yeyote wa elimu ya kuanzia kidato cha nne. Jamii yetu ya Tanzania haifahamu kwa undani kuhusu umuhimu wajambo hili lakini huku ndiko msingi hundaliwa. Mtu anapohitimu kidato cha nne na kupata ufaulu wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ama ngazi ya astashahada (certificate) na stashahada (diploma) hapo ndipo uchanguzi wa taaluma huanza. Kwa kuandika makala haya ninakusudia ...

JAY Z FT. MR. HUDSON-YOUNG FOREVER SONG LYRICS

Let's dance in style, let's dance for a while Heaven can wait, we're only watching the skies Hoping for the best but expecting the worst Are you gonna drop the bomb or not? Let us die young or let us live forever We don't have the power but we never say never Sitting in a sandpit, life is a short trip The music's for the sad man Forever young, I wanna be forever young Do you really want to live forever, forever, and ever? Forever young (young) I wanna be (Aye, may the best of your todays) Forever young (Be the worst of your tomorrows) Do you really want to live forever (But we ain't even thinking that far) Forever (ya know what I mean?) Forever young So we're living life like a video (video) Where the sun is always out and you never get old And the champagne's always cold and the music's always good And the pretty girls just happen to stop by in the hood And they hop their pretty ass up on the hood of that pretty ass car Without a wrinkle in today, ...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 12.10.2017

Viunganis Image caption Phillipe Coutinho Afisa mkuu mtendaji wa klabu ya Bercelona Oscar Grau anasema kuwa klabu hiyo itajaribu tena kumsajili kiungo wa kati wa Brazil Philippe Coutinho, 25, wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa mwezi Januari. (Guardian) Liverpool itaendelea kukataa kuingia katika makubaliano ya kumuuza Coutinho Barcelona (Independent) Vilevile , Liverpool imekubali kumkubali Coutinho kuelekea Nou Camp mnmao mwezi Januari katika makubaliano yenye thamani ya £98.6m. (Mundo Deportivo via Daily Mail) Image caption Mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho Meneja Jose Mourinho yuko tayari kutia saini kandarasi ya miaka mitano na klabu ya Manchester United itakayokuwa na thamani ya £65m (Sun) Mchezaji wa Manchester United Juan Mata, 29, amekataa fursa ya kuhamia katika ligi ya China(Daily Mirror) Kiungo wa kati wa Uingereza Jack Wilshere, 25, anaaminika kutaka kuondoka Arsenal mwezi Januari ili kuimarisha uwezo wake wa kujumuishwa...