HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI


KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA

Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay.
Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza.
Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa kuchaguliwa. Hungaria, Italia, Uholanzi, Hispania na Uswidi (Sweden) ziliwasilisha maombi  ya kuandaa michuano hiyo kwa mara ya kwanza. Kwa kipindi hicho Urugwai ilikua ni nchi iliyokua ikipigiwa upatu kuandaa michuano hiyo si tu kwa sababu nchi hiyo ilishinda medali ya dhahabu ya Olimpiki mwaka 1924 na 1928 bali pia nchi hiyo ilikuwa ikijiandaa kusherehekea maazimisho ya miaka 100 ya uhuru wa nchi hiyo mwaka 1930. Hili pia lilikua ni kivutio kikubwa sana kwa nchi ya Urugwai pamoja na kule kushinda medali ya dhahabu katika michuano ya soka ya Olimpiki.

Mbali na hapo Urugwai ilikua tayari kugharamia gharama zote za usafiri pamoja na makazi na malazi kwa timu zote ambazo zingeshiriki michuano hiyo kwa makubaliano kwamba faida yoyote ambayo ingepatikana basi nchi hiyo ingegawana  na FIFA hata kwa kuchukua kiasi kidogo tu. Makubaliano haya yaliazimiwa na hivyo kongamano hilo la FIFA lililofanyika jijini Barcelona, Uhispania mwaka 1929 kuipa kibali Urugwai kuwa nchi ya kwanza kuandaa michuano hiyo ya kombe la dunia. Hii ilifanya nchi nyingine zilizowasilisha maombi hayo kujitoa katika kinyang'anyiro hicho cha kuwania uandaaji wa michuano hiyo.

Kwa kipindi hiki bara la Ulaya lilikuwa katika mdororo mkubwa wa uchumi ambao ni mkubwa zaidi kuwahi kutokea duniani na hivyo hii ilipekea idadi ndogo ya ushiriki wa nchi za Ulaya. Pia, katika kipindi hiki usafiri wa ndege ulikuwa bado haujapanuka sana kwa hivyo ilizigharimu nchi za Ulaya kusafiri umbali mrefu kwa meli mpaka kufika huko Urugwai ambayo ni nchi katika bara la Amerika ya Kusini. Nchi washiriki wa michuano hii walitakiwa kutangaza wachezaji wao miezi miwili kabla ya michuano hii ili kurahisisha safari kuelekea Urugwai.

Mashirikisho mengi ya soka barani Ulaya yalivunja ahadi hii ya ushiriki katika michuano hii na ilitumia muda sana kwa Rais wa FIFA wa kipindi kile Rimet kuzishawishi nchi za Ufaransa, Ubelgiji, Romania na Yugoslavia kukubaliana naye katika safari ya kuelekea Buenos Aires, Ajentina kwa safari ya kuelekea Urugwai. Mara ya kwanza hakukuwepo na vigezo vya ushiriki kwa hatua ya makundi. FIFA ilizialika nchi zote ambazo zilikua wanachama wake kwa kipindi kile lakini ni nchi 13 tu zilizoshiriki michuano hiyo. Nchi hizo ni Urugwai, Ajentina, Brazil, Bolivia, Chile, Mexico, Paragwai, Peru, Marekani, Ubeligiji, Ufaransa, Romania na Yugoslavia. Timu zilikua katika makundi 4; kundi A likiwa na timu 4 na makundi B-D yakiwa na timu 3 kila moja. Timu hizi zilicheza mechi 18 na jumla ya magoli 70 yalifungwa, hii ni sawa na wastani wa magoli 3.89 kwa kila mechi. Mechi zote zilichezwa katika viwanja vitatu vyote vikiwa jijini Montevideo mji mkuu wa Uruguay. Guillermo Stábile (Ajentina) ndiye alikua mfungaji bora wa michuano hii. Alifunga jumla ya magoli 8.
Guillermo Stabile (Argentina) mfungaji bora wa Kombe la Dunia la kwanza 1930.
Michuano hii ya kombe la dunia kwa mara ya kwanza ilifunguliwa katika dimba jipya la Estadio Centenario katika jiji la Montevideo, hii ilikuwa Julai 13, 1930. Tukio hili likafungua mwanzo mpya wa soka duniani na kupelekea mafanikio makubwa katika soka  na kifedha pia. Kiukweli, wandaaji wa michuano hii hawakuridhishwa na ushiriki wa nchi 4 tu za Ulaya nilizozitaja hapo juu. Yaliyotokea huko katika michuano hiyo nchini Urugwai yalikuwa ya mafanikio makubwa sana na hii ikapelekea bingwa wa michuano hiyo ya dunia kutotwaaa taji hilo tena kwa miaka minne iliyofuata baadaye. Kwa hivyo Urugwai ndiye mshindi wa kwanza wa michuano hii ya kombe la dunia mwaka 1930 wakiwa nyumbani kwao.
Dimba la Estadio Centenario mwaka 1930 ambako mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia ilichezwa
Baraza la Kongresi la FIFA lilipokutana tena baadaye mwaka huo 1930 jijini Budapest, Hungaria waliishukuru sana Uruguay kwa kukubali kuandaa michuano hiyo ya kwanza ya kombe la dunia katika mazingira magumu. Sambamba na shukrani hizo, baraza hilo la FIFA lilielezea masikitiko yake kwa ushiriki ambao haukuridhisha hasa hasa kwa nchi za Ulaya.

Umuhimu wa tukio jipya la michuano hiyo uliongezeka zaidi kufuatia kushindwa kwa kufanyika michuano ya Olimpiki mwaka 1932 ambayo ilipangwa kufanyika Los Angels, California nchini Marekani. Hii ikachochea zaidi ushiriki katika michuano ya FIFA ya kombe la dunia lililofuata.

FIFA iliichagua Italia ambayo ilikuwa ikiwania uandaaji na Sweden kuwa waandaaji wa pili wa michuano hiyo. Safari hii kulikuwa na mechi za kufuzu tofauti na ilivyokua katika michuano ya awali kufuzu katika hatua ya makundi tofauti na michuano ya awali ambayo kulikua timu ikifungwa basi inaondolewa katika michuano hiyo. Brazil na Argentina ziliondolewa katika mechi moja tu za awali katika michuano ya mara ya kwanza. Kwa mara nyingine tena kama ilivyokua kwa timu waandaaji Uruguay kutwaa ubingwa 1930, timu waandaaji Italia walishinda wakiifunga Czechoslovakia katika muda wa nyongeza. Safari hii michuano hii ya kombe la dunia ilitangazwa redioni kwa mara ya kwanza.

Miaka 4 iliyofuata, Rais wa FIFA, Rimet alishuhudia matarajio yake yakitimia pindi michuano hiyo ilipoandaliwa kwa mara ya tatu nchini Ufaransa ambapo ni nyumbani kwake. Kwa mara nyingine tena mambo hayakwenda sawa na matarajio baadaya kuona Austria ikijiondoa kwenye michuano hiyo na kufanya Sweden kukosa timu ya kucheza nayo raundi ya kwanza. Uruguay haikutaka tena kushiriki na pia Argentina ilijitoa katika michuano hiyo ya tatu na hii ndiyo ilikuwa sababu nchi za Cuba na Indonesia (wakati ule ikiitwa jimbo la Udachi ya Mashariki ya Hindi) zikielekea Ufaransa kushiriki michuano hiyo ya tatu. Italia ilichukua tena ubingwa kwa mara ya pili ikitetea ubingwa wake wa mwaka 1934 waliochukua wakiwa nyumbani.

Michuano mingine ya kombe la dunia ilitakiwa kufanyika mwaka 1942 lakini kutokana na mapigano ya Vita ya Pili ya Dunia ambayo ilidumu kuanzia 1939 hadi 1945, michuano hiyo haikuweza kufanyika hivyo Italia iliendelea kuwa kuwa bingwa mtetezi kwa kipindi chote hicho hadi mwaka 1950 ilipochezwa tena michuano hiyo.

Licha ya Vita hiyo ya Dunia, makao makuu ya FIFA yaliendelea kuwa jijini Zurich nchini Uswisi. Julai 1, 1946 baraza la Kongresi la FIFA lilikutana tena nchini Luxembourg ambapo jumla ya mashirikisho 34 ya soka yalikutana katika jubilei ya miaka 25 ya Urais wa Rimlet FIFA. Kuanzia hapo kombe la dunia liliitwa jina la Kombe la Jules Rimet (Jules Rimet Cup) kwa heshima ya Rais huyu katika michuano hii hadi mwaka 1970. Baadaye mwaka 1974 kombe liliitwa Kombe la Dunia la FIFA (FIFA World Cup) hadi sasa.
Kombe la Dunia la Jules Rimet mwaka 1966.

Brazil ilichaguliwa kuandaa michuano ya mwaka 1949 lakini baadye iliahirishwa kwa sababu za muda na kusogezwa hadi mwaka 1950. Uswisi ilipewa nafasi ya kuandaa michuano ya mwaka 1954. Hii ndiyo ilikuwa historia ya michuano hii ya kombe la dunia mpaka kufikia mwaka 1949.

HISTORIA YA USHIRIKI

Katika historia ya kombe la dunia mwaka 1930 ni nchi 13 zilishiriki bila kufuzu, zilialikwa nchi wanachama wa FIFA tu. Michuano hiyo ilifanyika kati ya Julai 13 hadi 30, 1930. Mataifa yaliyoshiriki mwaka huo ni Argentina, Ubelgiji, Chile, Bolivia, Brazil, Ufaransa, Mexico, Paraguay, Peru, Romania, Uruguay, Marekani na Yugoslavia.

Mwaka 1934 zilishiriki timu 16 zikipitia kufuzu kwa hatua ya makundi. Michuano ilifanyika kuanzia Mei 27 hadi Juni 10, 1934. Hapa michuano hii ilihusisha mataifa kutoka kanda 4 za FIFA ambazo ni Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF), Shirikisho la Soka barani Amerika ya Kaskazini (CONCAF) na lile la Amerika ya Kusini (CONMEBOL) pamoja na Shirikisho la Soka barani Ulaya (UEFA). Mataifa yaliyoshiriki ni Argentina, Austria, Ubelgiji, Brazil, Czechoslovakia kabla haijagawanyika kuunda nchi mbili za Jamhuri ya Czech na Jamhuri ya Slovakia, Misri, Ufaransa, Ujerumani, Hungaria (Hungary), Italia, Uholanzi, Romania, Uhispania (Spain), Uswidi (Sweden), Uswisi (Switzzerland) na Marekani.

Mwaka 1938 zilifuzu timu 16 lakini Austria alijitoa baadaye na hivyo kubaki na timu 15 kutoka mashirikisho ya CONMEBOL, CONCAF, UEFA na Shirikisho la Soka barani Asia AFC. Michuano ilichezwa kuanzia Juni 4 hadi 19, 1938. Mataifa yaliyoshiriki ni Ubelgiji, Brazil, Cuba, Ufaransa, Czechoslovakia, Ujerumani, Hungaria, Italia, Norway , Poland, Romania, Uholanzi, Uswisi, Sweden na Dutch East Indies ambayo kwa sasa inafahamika kama Indonesia.

Mwaka 1950 pia zilifuzu nchi 16 baadaye India, Uturuki na Uskochi (Scotland) zilijitoa na hivyo yakabaki mataifa 13. Hii ilichezwa kuanzia Juni 24 hadi Julai 16, 1950 ikihusisha kanda 3 za FIFA; CONCAF, CONMEBOL na UEFA. Mataifa yaliyoshiriki ni Bolivia, Brazil, Chile, Uingereza, Italia, Mexico, Paragwai, Uhispania, Sweden, Uswisi, Uruguay, Marekani na Yugoslavia.

Mwaka 1954 zilicheza timu 16 kutoka kanda nne za FIFA duniani. Hii ilifanyiaka Juni 16 hadi Julai 4, 1954. Kanza zilishiriki ni AFC, CONCAF, CONMEBOL na UEFA. Mataifa yaliyoshiriki ni  Austria, Ubelgiji, Brazil, Czechoslovakia, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Hungaria, Italia, Korea ya Kusini, Mexico, Uskochi, Uswidi, Uturuki, Uruguay na Yugoslavia.

Mwaka 1958 timu 16 zilishiriki lakini hakukua na timu ya bara la Asia wala Afrika. Hii ilifanyika kuanzia Juni 8 hadi 29, 1958. Kanda 3 za FIFA; CONCAF, CONMEBOL na UEFA ndizo zilishiriki mwaka huu. Mataifa washiriki ni Argentina, Austria, Brazil, Czechoslovakia, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Hungaria, Mexico, Ireland, Paraguay, Uskochi, Umoja wa Kisovieti (USSR), Uswidi, Wales na Yugoslavia.

Mwaka 1962 zilishiriki timu 16 bila nchi za Asia na Afrika kwa mara nyingine. Mechi zilichezwa kuanzia May 30 hadi June 17, 1962 kutoka Kanda 3 za FIFA; CONCAF, CONMEBOL na UEFA. Mataifa yaliyoshiriki ni Argentina, Brazil, Bulgaria, Chile, Colombia, Czechoslovakia, Uingereza, Ujerumani, Hungaria, Italia, Mexico, Umoja wa Kisovieti (USSR), Uhispania, Uswisi, Uruguay, na Yugoslavia.

Mwaka 1966 zilishiriki timu 16 katika kanda 4 za FIFA huku Korea Kaskazini ikishiriki kwa mara ya kwanza. Michezo ilianza Julai 11 hadi 30, 1966 safari hii ikihusisha kanda 4 za FIFA; AFC, CONCAF, CONMEBOL na UEFA. Mataifa washiriki ni Argentina, Brazil, Bulgaria, Chile, Korea ya Kaskazini, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Hungaria, Italia, Mexico, Umoja wa Kisovieti, Uhispania, Uswisi, Ureno na Uruguay.

Mwaka 1970 zilishiriki timu 16 kutoka kanda 5 za FIFA; CAF, AFC, CONCAF, CONMEBOL na UEFA huku Morocco ikiwa ni nchi ya kwanza ya Afrika kufuzu kucheza michuano hii. Michuano ilifanyika kuanzia Mei 31 hadi Juni 21. Mataifa yaliyoshiriki ni Ubelgiji, Brazil, Bulgaria, Czechoslovakia, El Salvador, Uingereza, Ujerumani, Israel, Italia, Mexico, Morocco, Peru, Romania, Umoja wa Kisovieti, Uswidi na Uruguay.

Mwaka 1974 timu 16 kutoka kanda 5 za FIFA; AFC, CAF, CONCAF, CONMEBOL na UEFA. Michuano ilichezwa kuanzia Juni 13 hadi Julai 7, 1974. Mataifa ya Argentina, Australia, Brazil, Bulgaria, Chile, Ujerumani ya Mashariki na Magharibi, Haiti, Italia, Uholanzi, Poland, Uskochi, Uswidi, Uruguay, Yugoslavia na Zaire (kwa sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo) yalishirki.

Mwaka 1978 zilishiriki timu 16 kutoka kanda 5 za FIFA, AFC, CAF, CONCAF, CONMEBOL na UEFA. Michezo ilifanyika kuanzia Juni 1 hadi 25, 1978. Mataifa washiriki ni Argentina, Austria, Brazil, Ufaransa, Ujerumani, Hungaria, Iran, Italia, Mexico, Uholanzi, Uskochi Peru, Poland, Uhispania, Uswidi na Tunisia.

Mwaka 1982 ushiriki wa timu ukaongezeka hadi timu 24 kutoka kanda 6 za FIFA ikiwa ni mara ya kwanza kwa kanda zote kushiriki. Kanda hizo ni AFC, CAF, CONCAF, CONMEBOL, UEFA na OFC; Ukanda wa Visiwa vya Bahari ya Pasifiki ama kwa jina moja la kingereza, Oceania. Michuano ilianza Juni 13 hadi Julai 11, 1982 ikihusisha mataifa ya Algeria, Argentina, Austria, Ubeligiji, Brazil, Cameroon, Chile, Czechoslovakia, El Salvador, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Honduras, Hungaria, Italia, Ireland, Peru, New Zealand, Kuwait, Poland, Uskochi, Umoja wa Kisovieti, Uhispania na Yugoslavia.

Mwaka 1986 zilishiriki timu 24 zikicheza jumla ya mechi 52. Kanda 5 za fifa zilishiriki isipokuwa Ukanda wa Oceania, OFC.  Mei 31 hadi Juni 29, 1986 ndiyo kipindi michuano hii ilichezwa. Mataifa yaliyoshiriki ni Algeria, Argentina, Ubelgiji, Brazil, Bulgaria, Canada, Denmark, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Hungaria, Iraq, Italia, Korea ya Kusini, Mexico, Morocco, Ireland, Paraguay, Poland, Ureno, Uskochi, Umoja wa Kisovieti, Uhispania na Uruguay.

Mwaka 1990 zilishiriki timu zaidi ya 24 kukiwa na timu zaidi ya moja kutoka Asia. Kanda 5 za FIFA zilishiriki isipokua Ocenia kuanzia Juni 8 hadi Julai 8,1990.  Mataifa yaliyoshiriki ni Argentina, Austria, Ubelgiji, Brazil, Cameroon, Colombia, Costa Rica, Czechoslovakia, Misri, Uingerea, Ujerumani, Italia, Korea ya Kusini, Uholanzi, Jamhuri ya Ireland, Romania, Uskochi, Umoja wa Kisovieti, Uhispania, Uswidi, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Uruguay, Marekani na Yugoslavia.

Mwaka 1994 zilishirki timu 24 kama kawaida kutoka kanda 5 za FIFA isipokua Ocenia. Michuano ilifanyika kuanzia Juni 17 hadi Julai 17, 1994. Mataifa washiriki ni Argentina, Ubelgiji, Bolivia, Brazil, Bulgaria, Cameroon, Colombia, Ujerumani, Ugiriki, Italia, Korea ya Kusini, Mexico, Morocco, Uholanzi, Nigeria, Norway, Jamhuri ya Ireland, Romania, Urusi, Saudi Arabia, Uhispania, Uswidi, Uswisi na Marekani.

Mwaka 1998 timu ziliongezeka hadi 32 katika makundi 8 ya timu 4 kila kundi. Mashirikisho kutoka kanda 5 za FIFA yalishiriki isipokua ukanda wa Ocenia. Michuano hii ilifanyika kati ya Juni 10 hadi Julai 12, 1998. Mataifa 32 yaliyoshirki ni Argentina, Austria, Ubelgiji, Brazil, Bulgaria, Cameroon, Chile, Colombia, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Iran, Jamaica, Japan, Croatia, Denmark, Korea ya Kusini, Mexico, Morocco, Uholanzi, Naijeria, Norway, Paragwai, Romania, Saudi Arabia, Uskochi, Afrika ya Kusini, Uhispania, Tunisia, Marekani na Yugoslavia.

Mwaka 2002 timu 32 huku ikiwa ni mara ya kwanza kwa michuano hii kuchezwa barani Asia. Ilifanyika katika nchi mbili tofauti; Korea ya Kusini na Japan kuanzia Mei 31 hadi Juni 30, 2002 ikihusisha Kanda 5 za FIFA  isipokua Ocenia. Mataifa washiriki ni Cameroon, Nigeria, Senegal, Afrika ya kusini, Tunisia, Argentina, Brazil, Ecuador, Paraguay, Uruguay, China, Japan, Korea ya Kusini, Saudi Arabia, Costa Rica, Mexico, Marekani, Ubelgiji, Croatia, Denmark, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Poland, Ureno, Jamhuri ya Ireland, Urusi, Slovenia, Uhispania, Uswidi na Uturuki.

Mwaka 2006 timu zilikua 32 zikiweka rekodi ya kucheza mechi 64. Michuano ilianza June 9 hadi Julai 9, 2006 ikihusisha kanda 5 za FIFA isipokua Ocenia. Mataifa washiriki ni Angola, Ivory Coast (Cote D'Ivore), Ghana, Togo, Tunisia, Australia, Iran, Japan, Korea ya Kusini, Saudi Arabia, Argentina, Brazil, Ecuador, Paraguay, Costa Rica, Mexico, Trinidad & Tobago, Marekani, Croatia, Jamhuri ya Czech, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Uholanzi, Poland, Ureno, Serbia na Montenegro, Uhispania, Uswidi, Uswisi na Ukraine.

Mwaka 2010 zilicheza timu 32 huku ikiwa ni mara ya kwanza kwa michuano hii kuchezwa barani Afrika. Huenda michuano hii iliyochezwa katika ardhi ya bara la Afrika ilikua na msisimko sana kutokana na kuchezwa kwa mara ya kwanza katika ardhi hii ya kifahari. Ilikua ni kati ya Juni 11 hadi Julai 11, 2010. Pamoja na yote binafsi huwa nazikumbuka zile nyimbo 3 ambazo zilikua na msisimko wa kipekee tangu kuanzishwa kwa michuano hii; wimbo wa kwanza ni ule wa Shakira - Waka Waka (This Time for Africa) ambao umetazamwa zaidi ya mara bilioni 3.4 katika mtandao wa YouTube, Shakira aliutendea haki huu wimbo na huenda ndiyo maana Mwenyezi Mungu akamkutanisha na Gerard Pique kabla hawajatengana 2022. Wimbo mwingine ni ule wa R. Kelly - Sign of Victory, huu nao ulikua ni 'wa moto' hadi dakika hii unaposoma hapa, mashairi yake yako 'relevant' sana. Kuna ule wa 3 aliuimba K'Naan - Wavin' Flag, nadhani unapata picha ya msisimko. Mataifa yaliyoshiriki kukipiga pale kwa Madiba ni  Algeria, Cameroon, Ivory Coast, Ghana, Nigeria, Afrika ya Kusini, New Zealand, Honduras, Mexico, Marekani, Argentina, Brazil, Chile, Paraguay, Uruguay, Australia, Japan, Korea ya Kaskazini na Kusini, Denmark, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ugiriki, Italia, Uholazi, Ureno, Serbia, Slovakia, Slovenia, Uhispania na Uswisi.

Mwaka 2014 zilicheza timu 32 kutoka kanda 5 za FIFA isipokua Oceania. Michuano hii ilianza Juni 12 hadi Julai 13, 2014. Mataifa washiriki yalikua ni Algeria, Cameroon, Ivory Coast, Ghana, Nigeria, Ubelgiji, Bosnia & Herzegovina, Croatia, Italia, Ugiriki, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi, Ureno, Urusi, Uhispania, Uswisi, Australia, Iran, Japan, Korea ya Kusini, Argentina, Brazil, Chile, Colombia, Ecuador, Uruguay, Costa Rica, Honduras, Mexico na Marekani.
 
Mwaka 2018 zilicheza timu  32 kutoka kanda 5 za FIFA isipokua Ocenia. Michuano ilianza Juni 14 hadi Julai 15, 2018. Mataifa washiriki ni Misri, Morocco, Nigeria, Senegal, Tunisia, Argentina, Australia, Ubelgiji, Brazil, Colombia, Costa Rica, Croatia, Denmark, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Iceland, Iran, Japan, Korea ya Kusini, Mexico, Panama, Peru, Poland, Ureno, Urusi, Saudia Arabia, Serbia, Uhispania, Sweden, Uswisi na Uruguay.

Mwaka 2022 zilicheza jumla ya timu 32. Michuano hii ilifanyika nchini Qatar kuanzia Novemba 21 hadi Desemba 18 mwaka 2022 ikijumuisha kanda 5 za FIFA isipokua Ocenia. Mataifa yaliyofuzu kushiriki michuano hiyo yenye msisimko wa kipekee duniani ni Qatar, Senegal, Ecuador, Uholanzi, Uingereza, Iran, Marekani, Wales, Argentina, Mexico, Poland, Saudi Arabia, Australia, Denmark, Ufaransa, Tunisia, Ujerumani, Japan, Uhispania, Costa Rica, Morocco, Ubelgiji, Canada, Croatia, Brazil, Cameroon, Serbia, Uswisi, Ghana, Ureno, Korea ya Kusini na Urugwai.

Mwaka 2026 kwa mara ya kwanza dunia itashuhudia michuano hii ikichezwa katika majiji 16 ya mataifa matatu ya bara la Amerika ya Kaskazini; Marekani, Canada na Mexico. Ni kwa mara ya kwanza pia michuano hii itajumuisha jumla ya timu 48 kutoka katika kanda sita za FIFA. Marekani itahusika katika mechi 60 ikiwa ni pamoja na mechi zote za robo fainali hadi fainali. Canada na Mexico zitachezwa mechi 10 kila taifa na kufanya jumla ya mechi kuwa 80. Katika michuano hii ukanda wa Afrika (CAF) utakuwa na uhakika kupeleka timu 9 na moja italazimika kucheza play-off na timu kutoka ukanda mwingine wa FIFA. Ocenia (OFC) pia ina uhakika wa timu 1 na nyingine kama itafuzu kwenye play-off.

WAANDAAJI (1930-2026)

1930 Uruguay.
1934 Italia.
1938 Ufaransa.
1950 Brazil.
1954 Uswisi.
1958 Sweden.
1962 Chile.
1966 Uingereza.
1970 Mexico.
1974 Ujerumani.
1978 Argentina.
1982 Hispania.
1986 Mexico.
1990 Italia.
1994 Marekani.
1998 Ufaransa.
2002 Japan/Korea ya Kusini.
2006 Ujerumani.
2010 Afrika Kusini.
2014 Brazil.
2018 Urusi.
2022 Qatar.
2026 Canada/Marekani/Mexico.

WASHINDI WA KOMBE LA DUNIA (1930-2022)

1930 Uruguay ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Argentina.

1934 Italia ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Czechoslovakia.

1938 Italia ilitwaa ubingwa mara ya pili kwenye fainali dhidi ya Hungaria.

1950 Uruguay ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Brazil.

1954 Ujerumani ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Hungaria.

1958 Brazil ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Sweden.

1962 Brazil ilitwaa ubingwa mara ya pili kwenye fainali dhidi ya Czechoslovakia.

1966 Uingereza ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Ujerumani.

1970 Brazil ilitwaa ubingwa mara ya tatu kwenye fainali dhidi ya Italia.

1974 Ujerumani ilitwaa ubingwa mara ya pili kwenye fainali dhidi ya Uholanzi.

1978 Argentina ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Uholanzi.

1982 Italia ilitwaa ubingwa mara ya tatu kwenye fainali dhidi ya Ujerumani.

1986 Argentina ilitwaa ubingwa mara ya pili kwenye fainali dhidi ya Ujerumani.

1990 Ujerumani ilitwaa ubingwa mara ya tatu kwenye fainali dhidi ya Argentina.

1994 Brazil ilitwaa ubingwa mara ya nne kwenye fainali dhidi ya Italia.

1998 Ufaransa ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Brazil.

2002 Brazil ilitwaa ubingwa mara ya tano kwenye fainali dhidi ya Ujerumani.

2006 Italia ilitwaa ubingwa mara ya nne kwenye fainali dhidi ya Ufaransa.

2010 Hispania ilitwaa ubingwa kwenye fainali dhidi ya Uholanzi.
 
2014 Ujerumani ilitwaa ubingwa mara ya nne kwenye fainali dhidi ya Argentina.
 
2018 Ufaransa ilitwaa ubingwa mara ya pili kwenye fainali dhidi ya Croatia.

2022 Argentina ilitwaa ubingwa mara ya tatu kwenye fainali dhidi ya Ufaransa. 

REKODI ZA MICHUANO  (1930-2022)

  • Tangu 1930 imechezwa michuano 22 ya Kombe la Dunia (1930-2022).
  • Hadi 2022 ni mataifa 80 tu ambayo yamecheza michuano hii.
  • Kwa sasa Argentina ndiye bingwa mtetezi (2022). Hii ni mara ya tatu kwa taifa hili kutwaa ubingwa huu wa dunia (1978, 1986 na 2022).
  • Ni nchi 8 tu duniani zimeshawahi kutwaa ubingwa wa michuano hii (Brazil, Ujerumani, Italia, Argentina, Ufaransa, Uruguay, Uingereza na Hispania).
  • Ni timu 13 tu katika michuano yote 22 ambazo zimefika hatua ya fainali (Brazil, Ujerumani, Italia, Argentina, Ufaransa, Uruguay, Uingereza, Hispania, Uholanzi, Hungaria, Czechoslovakia , Sweden na Croatia).
  • Ni timu za Ulaya na Amerika ya Kusini pekee zilizotwaa ubingwa wa kombe la dunia mpaka sasa.
  • Brazil ndiyo timu pekee ambayo imeshiriki michuano yote 22 tangu 1930 ikifuatiwa na Ujerumani mara 20. Italia na Argentina mara 18 na Mexico mara 17.
  • Brazil ndiyo timu iliyotwaa ubingwa mara nyingi kuliko nchi nyingine. Imetwaa ubingwa mara tano (1958, 1962, 1970, 1994 na 2002) wakifungwa katika fainali mbili (1950 na 1998).
  • Timu 5 zimecheza fainali bila Ubingwa (Uholanzi, Czechoslovakia, Hungaria, Sweden na Croatia).
  • Ujerumani na Italia zimetwaa ubingwa mara nne. Ujerumani ndiyo nchi iliyoshindwa kutwaa ubingwa mara nyingi katika fainali za kombe la dunia, imefungwa mara nne katika fainali (1966, 1982, 1986 na 2002). Italia imepoteza mara mbili tu (1970 na 1994).
  • Uholanzi ndiyo nchi pekee iliyofika finali na kucheza na timu zaidi ya mbili na kushindwa kutwaa ubingwa. Wamepoteza katika finali tatu (1974, 1978 na 2010).
  • Marekani na Uturuki ndiyo nchi pekee nje ya mabara ya Ulaya na Amerika ya Kusini kumaliza katika nafasi ya 3.
  • Ujerumani ndiyo timu inayoongoza kwa kucheza finali nyingi za kombe la dunia. Imecheza mara nane (1954, 1966, 1974, 1982, 1986, 1990, 2002 na 2014) Brazil inaifuatia Ujerumani kwa kucheza fainali mara 7, Italia na Argentina mara 6.
  • Ni nchi 2 tu ambazo zimetwaa ubingwa mara mbili mfululizo. Italia (1934 na 1938) na Brazil (1958 na 1962).
  • Mabingwa watetezi walioondolewa kwenye hatua za makundi michuano iliyofuata; Italia (1950), Brazil (1966), Ufaransa (2002), Italia (2010), Hispania (2014) na Ujerumani (2018).
  • Lionel Messi ndiye mchezaji aliyecheza mechi nyingi katika michuano hii. Amecheza jumla ya mechi 26 katika michuano 5 (2006, 2010, 2014, 2018 na 2022).
  • Pele ni mchezaji pekee aliyetwaa ubingwa na timu yake ya Brazil mara tatu (1958, 1962 na 1970). Rekodi hii bado haijavunjwa. 
  • Norman Whiteside (Ireland Kaskazini) ndiye mchezaji mdogo kuwahi kucheza katika michuano hii akiwa na miaka 17 na siku 41 (Ireland Kaskazini vs.  Yugoslavia, Juni 17, 1982).
  • Pele anashikiria rekodi ya kuwa mchezaji mwenye umri mdogo kucheza katika fainali ya kombe la dunia akiwa na miaka 17 na siku 249, fainali hii ilikuwa ni Brazil vs. Sweden Juni 29, 1958.
  • Essam El-Hadary (Misri) ndiye mchezaji mwenye umri mkubwa kucheza katika michuano hii akiwa na miaka 45  na siku 161 (Misri vs. Saudi Arabia, Juni 25, 2018).
  • Dino Zoff (Ujerumani) ndiye mchezaji mwenye umri mkubwa aliyecheza katika fainali za kombe la dunia akiwa na miaka 40 na siku 133 (Italia vs. Ujerumani Magharibi Julai 11, 1982).
  • Kylian Mbape ndiye aliyefunga magoli mengi katika hatua ya fainali akifunga jumla ya magoli 4 dhidi ya Croatia (2018) na Argentina (2022).
  • Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji pekee aliyefunga magoli katika michuano mingi, akifunga magoli 8 katika michuano mitano (2006, 2010, 2014, 2018 na 2022).
  • Lucien Laurent (Ufaransa) ndiye mfungaji wa bao la kwanza kabisa katika historia ya kombe la dunia (Ufaransa vs. Mexico, Julai 13, 1930).
  • Angelo Schiavio (Italia) ndiye mfungaji wa bao la 100 na michuano hii ya Kombe la Dunia (Italia vs. Marekani, Mei 27, 1934).
  • Miroslav Klose ndiye mfungaji mwenye magoli mengi katika michuano hii akifunga jumla ya magoli 16 katika mechi 24 kwenye michuano minne (2002, 2006, 2010 na 2014).
  • Asamoah Gyan ndiye mchezaji pekee barani Afrika kufunga magoli mengi katika michuano hii akifunga jumla ya magoli 6. Hii ni sawa na kusema Gyan ndiye mchezaji pekee nje ya bara la Ulaya na Amerika ya Kusini kufikia idadi hiyo ya magoli.
  • Mwaka 2022 yalifungwa jumla ya magoli 172 ikiwa ndiyo michuano yenye magoli mengi zaidi katika michuano yote 22.
  • Rekodi ya mechi iliyokuwa na watazamaji wengi uwanjani ilichezwa Julai 16, 1950 kati ya Uruguay vs Brazil katika uwanja wa Maracanã jijini Rio de Janeiro, Brazil. Mechi hii ilihudhuriwa na watu 173,850.
  • Vittorio Pozzo ndiye kocha mwenye mafanikio ya kubeba ubingwa wa kombe la dunia mara mbili kama kocha akiwa na timu ya Italia akishinda mara 2 mfululizo (1934 na 1938).


MAKALA HII HUHARIRIWA MARA KWA MARA KUENDANA NA WAKATI TANGU MEI 2018. IMEANDALIWA NA KUANDIKWA NA VENANCE GILBERT KWA HISANI YA MTANDAO WA FIFA NA MITANDAO MINGINE.

KWA UANDISHI WA MAKALA MBALIMBALI ZA SOKA, ELIMU, BURUDANI, SIASA N.K WASILIANA NAMI KWA BARUA PEPE venancegilbert@gmail.com ama namba ya simu 0753400208.

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika.
Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo:


1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia.

2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti.

3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takribani 25% ya lugha zote duniani zinazungumzwa barani Afrika huku kukiwa na lugha za makabila zaidi ya 2,000.

4. Afrika ni bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu duniani ambao wanakadiriwa kuwa bilioni 1.1 huku zaidi ya 50% ya wakazi wake wakiwa ni vijana wenye umri chini ya miaka 25. Inakadiriwa kwamba mpaka kufikia mwaka 2050 bara la Afrika litakuwa na takribani watu bilioni 2.3. Hii ni kwa mujibu wa taarifa za idadi ya watu iliyotolewa na Umoja wa Mataifa mwaka 2015.

5. Takribani 40% ya wazee wakazi wa bara hili hawajui kusoma na kuandika.

6. Vita ya pili ya Kongo ndiyo vita hatari kutokea duniani baada ya Vita ya Pili ya dunia. Vita hii iligharimu uhai wa watu takribani milioni 5.4

7. Jangwa la Sahara ni kubwa kuliko yote duniani na ukubwa wake ni zaidi ya nchi ya Marekani.

8. Kuna zaidi ya wachina milioni 1 katika baraka la Afrika. Nchi ya Angola ikiwa na zaidi ya wachina 350,000.

9. Kiwango cha ukataji miti barani Afrika ni mara mbili ya kiwango chote cha ukataji miti duniani. Zaidi ya hekta milioni 4 zinakatwa miti barani hapa kila mwaka.

10. Ziwa Victoria ni ziwa kubwa kuliko yote barani Afrika huku likiwa ni ziwa la pili kwa ukubwa duniani na kuwa na maji laini duniani.

11. Wanyama kama vile twiga, pundamilia, viboko, sokwe na nyumbu ni wanyama pekee wanaopatikana katika bara hili.

12. Ziwa Nyasa ambalo kwa jina jingina linaitwa Ziwa Malawi ndilo ziwa lenye aina nyingi za samaki (fish species) kuliko maziwa mengine duniani.

13. Bara hili lina zaidi ya asilimia 85 ya Tembo wote wanaopatikana duniani kote, pia, 99% ya Simba waliosalia duniani wanapatikana katika bara hili. 

14. Mto Naili ambao una urefu wa kilomita 6,650 ni mto mrefu kuliko yote duniani na unapatikana katika bara hili.

15. Mbuga ya Serengeti ambayo inapatikana nchini Tanzania ni hifadhi pekee ambayo ina kundi kubwa la wanyama duniani ikiwa na pundamilia zaidi ya 750,000. Katika hifadhi hii nyumbu zaidi ya milioni 1.2 huhama kila mwaka kutoka hifadhi ya Serengeti nchini Tanzania kuelekea katika hifadhi ya Masai Mara iliyoko Kenya. Katika kundi hilo la nyumbu wanaohama kila mwaka kutafuta malisho wanyama kama pundamilia, swala na pofu huwepo katika uhamaji huo ambalo ni tukio la kipekee duniani.

16. Bara la Afrika lina zaidi ya 25% ya aina ya ndege wote wanaopatikana duniani.

17. Zaidi ya mabwawa 1,270 yamejengwa kandokando ya mito barani hapa. Mabwawa haya yana kazi kubwa ya kuzalisha umeme unaotumia ngumu za maji.

18. Bara la Afrika ni la pili kwa ukubwa na bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu baada ya bara la Asia. Afrika ina takribani watu bilioni 1.2 na hii ni kwa mujibu wa ripoti za Umoja wa Mataifa mwaka 2015. Hii ni sawa na 16% ya idadi yote ya watu waliopo duniani.

19.  Afrika ni bara la pili kwa kuwa na joto baada ya bara la Australia.

20. Uislamu ni dini yenye wafuasi wengi barani Afrika ikifuatiwa na dini ya Kikristo huku ikikadiriwa kwamba takribani 38% ya Wakristo wote wataishi kusini mwa jangwa la Sahara mpaka kufikia mwaka 2050.

21. Afrika ni bara lililopo katika nyuzi 0 (0°) katika mstari wa grinwichi meridiani na ikweta.

22. Nchi kubwa kuliko zote barani Afrika ni Algeria ikiwa na eneo la kilomita za mraba milioni 2.381 ikifuatiwa na DR Congo yenye eneo la kilomita za mraba 2.844 wakati nchi ndogo kuliko zote ni Shelisheli yenye eneo la kilomita za mraba 459.

23. Nigeria ndiyo nchi yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika ikiwa na takribani watu wanaokadiriwa kufika milioni 218.5 hadi kufikia mwezi Septemba 2023. Hii ni sawa na 18% ya watu wote wanaoishi barani hapa. Pia, hii ni sawa na 2% ya watu wote wanaoishi duniani.

24. Umbali mfupi kati ya Ulaya na Afrika ni kilomita 14 sawa na maili 8.7 ukipitia mlango bahari wa Gibraltar.

24. Maporomoko ya Victoria yaliyopo kati ya mpaka wa Zambia na Zimbabwe ni maporoko ya makubwa zaidi ya maji kuliko yote duniani. Pia, ni moja kati ya maajabu saba ya dunia.

25. Kiboko ni mnyama hatari sana barani Afrika kuliko hata Simba na Chui. Anaua watu wengi kuliko Simba na Mamba wakijumlishwa kwa pamoja.

26. Takribani 90% ya wagonjwa wa Malaria duniani kote wanapatikana barani hapa. Ugonjwa huu unaua takribani watoto 30,000 kila mwaka.


27. Nchini Eswatini (Swaziland) katika kila watu 4 kati yao 1 ni muathirika wa UKIMWI.


28. Tanzania ni nchi inayoongoza kuwa na walemavu wengi wa ngozi (albino) kuliko nchi nyingine duniani. Wakati katika mataifa mengine ya kusini mwa jangwa la Sahara ikikadiriwa kuwa mtu 1 katika watu 5,000 hadi 15,000 ana ualbino, kwa Tanzania mtu 1 katika watu 1,500 ana ualbino. Hii inaifanya Tanzania kuwa na watu wengi wenye ulemavu huu wa ngozi kuliko nchi nyingine duniani kote. Takwimu hizi ni kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. 


29. Misri ni nchi inayoongoza kwa kutembelewa na idadi kubwa ya watalii kuliko nchi nyingine barani hapa. Inapokea watalii zaidi ya milioni 10 kila mwaka 


30. Bendera ya nchi ya Msumbiji ni bendera pekee barani Afrika kuwa bendera ya taifa yenye silaha aina ya AK-47. Silaha hiyo inaashiria ulinzi wa nchi hiyo. Msumbiji ni nchi pekee yenye bendera yenye silaha ya aina hiyo duniani. Nchi nyingine zenye bendera zenye silaha duniani ni Guatemala na Haiti.


31. Bara la Afrika lilikuwa limeungana na mabara mengine miaka mingi iliyopita, lilitengana na mabara hayo katika kipindi cha kijiolojia (taaluma ya miamba na muundo wa ndani wa dunia) katika kipindi cha kijiolojia kiitwacho Mesozoic.


32. Ustaarabu (Civilization) ulianzia barani Afrika. Misri inapata sifa hii kwa kuwa nchi ya kwanza duniani kuwa ustaarabu wa kifarao ambao ulianza mwaka 3300 kabla ya Kristo.


33. Shelisheli ndiyo nchi inayoongoza kwa kuwa na pato kubwa la taifa (GNP). Pato lake linakadiriwa kuwa takribani dola za marekani milioni  15,400 huku Sudan Kusini ikiwa ndiyo yenye pato dogo zaidi ambalo linakadiriwa kuwa dola milioni 245.9.


34. Jangwa la Sahara ndilo jangwa lenye joto zaidi kuliko yote duniani. Linachukua eneo la mraba takribani milioni 9.1 ya majangwa yote duniani.

35. Kama jinsi ilivyo katika bara la Asia, barani hapa pia watu hutembea takribani maili 3.7 kila siku kutafuta maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali.


36. Madagascar ni kisiwa kikubwa kuliko vyote barani Afrika na kisiwa cha 4 kwa ukubwa duniani. Kinapatikana mashariki mwa bahari ya Hindi.


37. Tembo ni mnyama mkubwa kuliko wote duniani na anakadiriwa kuwa na uzito wa tani 6 hadi 7 anapatikana barani Afrika pekee huku Twiga akiwa ni mnyama mrefu kuliko wote dunani naye anapatikana Afrika tu. Pia, mnyama anayekimbia sana kuliko wote ambaye ni Duma anapatikana Afrika pekee huku Mamba akiwa ni mnyama mkubwa kuliko wote katika jamii ya reptilia naye anapatiakana Afrika pekee.


38. Mabaki ya mtu wa kale zaidi yalipatikana barani hapa nchini Ethiopia. Mabaki hayo yanaaminika kuwepo toka miaka laki 2 iliyopita. Charles Darwin alikua akishikilia dai hili lakini lilipingwa na waz
ungu mpaka ilipogundulika katika karne ya 20.

39. Inakadiriwa kwamba takribani watu milioni 12.5 walitekwa barani hapa na kuuzwa katika bara la Amerika kama watumwa kati ya mwaka 1525 hadi 1866.


40. Wakati nchi ya Misri inasifika kwa umaarufu wa kuwa na mapiramidi mengi duniani, Sudan ni nchi pekee yenye idadi kubwa ya mapiramidi hayo ambayo yanakadiriwa kufikia 223 hii ikiwa ni mara mbili ya mapiramidi yote yanayopatikana nchini Misri.


41. Nchini Kenya kuna kabila linalojulikana kama Kalenjin ambalo ni kabila maarufu kwa kutoa wakimbiaji wanaoongoza kwa mbio za riadha duniani.


42. Taasisi ya Elimu kongwe kuliko zote duniani ambayo bado inatumika mpaka leo ipo barani hapa. Taasisi hiyo ni Chuo Kikuu cha Al-Karaouine ambayo iko Morocco. Taasisi hii ilianza kama madrasa na ilianzishwa mwaka 859 baada ya Kristo na ilianzishwa na Fatima Al-Fihri.


43. Takribani 60% ya bara la Afrika ni kame. Sehemu hii inasababishwa na uwepo wa majangwa ya Kalahari, Sahara na Namib.


45. Bara la Afrika lina 30% ya madini yote yanayopatikana duniani.


46. Nigeria ni nchi ya 4 kwa kuzalisha mafuta duniani. Nchi 10 zinazoongoza kwa kuzalisha mafuta barani hapa ni Nigeria, Algeria, Angola, Libya, Misri, Sudan, Guinea ya Ikweta, Congo Brazzaville, Gabon na Afrika ya Kusini.


47. Bara hili lina 40% ya akiba madini ya dhahabu, 60% ya ziada ya madini ya shaba na 90% ya madini ya platini.


48. Zaidi ya 55% ya nguvu kazi ya Afrika wanajihusisha na kilimo cha mazao ya chakula ambayo pia ni sekta inayokuza uchumi barani hapa.


49. Zaidi ya 90% ya udongo wa bara hili sio rafiki kwa kilimo, ni 0.25% ya udongo ambayo ni rafiki kwa kilimo barani hapa.


50. Zaidi ya watu milioni 300 barani hapa wanategemea maji yanayotoka chini kwa matumizi ya kunywa. Maji ni tatizo katika bara hili.


51. Bara la Afrika lina naeneo zaidi ya 3,000 yanayolindwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya utalii duniani. Takribani maeneo 198 ya bahari, maeneo 129 yanayohifadhiwa na UNESCO kama maeneo ya urithi wa kujivunia na maeneo 80 chepechepe (wetland) ambayo ni ni muhimu kimataifa.


52. Afrika ni bara maskini kuliko yote duniani. Pato lake ni 3.1% ya pato lote la dunia kwa mwaka kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia.


53. Wayunani wa kale na Warumi walitumia neno Afrika wakimaanisha ukanda wa kaskazini mwa Afrika peke yake. Katika lugha ya kilatini Afrika ina maana ya ~enye hali ya jua. Wayunani wanatambua kama Aphrike wakiwa na maana kwamba ~isiyo na baridi.


54. Afrika ni bara pekee lenye kingo fupi za kanda za pwani licha ya kua bara la pili kwa ukubwa.


55. Katika bara hili wanawake wanakadiriwa kufanya kazi masaa mengi kuliko wanaume. Wanawake hufanya kazi masaa 12 hadi 14 kwa siku barani hapa.


56. Chura mkubwa zaidi kuliko wote duniani maarufu kwa jina la Goliath anapatikana nchini Guinea ya Ikweta.


57. Benin ni nchi pekee duniani ambayo inashikiria rekodi ya kuwa nchi yenye vizazi mapacha kuliko nyingine zaidi duniani. Katika kila vizazi 1,000 nchini Benin 27.9 ni vizazi vya watoto mapacha. Takwimu ya dunia ni utokeaji wa vizazi mapacha 13.6 katika vizazi 1,000.


58. Niger ni nchi inayoongoza kwa kuwa wanawake wenye uwezo mkubwa wa kuwa na vizazi. Inakadiriwa kua kila mwanamke nchini humo ana watoto 6.62. Burundi ni nchi inayofuatia baada ya Niger ikiwa na 6.04 na hii ni kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2016 kutoka mtandao wa Statista "The Statistical Portal"


59. Kahun ni jiji la kwanza chini ya mipango miji duniani. Jiji hili lipo nchini Misri. 


60. Afrika ni bara linaloongoza kwa vifo vya Mama na mtoto wakati wa kujifungua.


61. Takribani watu milioni 589 kusini mwa jangwa la Sahara wanaishi bila umeme. Hii ni sawa na 20% tu wakati 80% wakiishi kwa kutegemea vyanzo vingine vya nishati kama vile kuni na mkaa kwa ajaili ya kupikia.


62. Inakadiriwa kwamba mtoto 1 katika 3 kusini mwa jangwa la Sahara barani Afrika wana utapiamlo.


63. Bara la Afrika linakadiriwa kua na watumiaji wa mtandao (Internet) milioni 453.3 ambao ni sawa na 35.2% ya wakazi wote wa bara hili. mpaka kufikia Desemba 31, 2017 huku kukiwa na watumiaji milioni 177 wa Facebook. Mwaka 2000 bara la Afrika lilikua na watumiaji wa mtandao milioni 4.5. Takwimu hizi ni kwa mujibu wa mtandao wa Internet World Stats.


64. Nchi zote 54 za bara hili ni nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU). Morocco iliwahi kujitoa katika umoja huu na baadaye iliamua kurejea tena. Umoja huu ulianzishwa mwaka 1963 kama OAU na baadaye ulibadilishwa kua AU mwaka 2002. Makao yake makuu yapo Addis Ababa, Ethiopia.

65. Bara la Afrika ndilo lenye nchi nyingi kuliko bara lilingine duniani.



Orodha hii imeandaliwa kwa msaada wa mtandao. Haya ni baadhi ya machache kati ya mengi unayopaswa kuyafahamu na ni jukumu lako kutafuta mengine mengi ya kufahamu. Kwa maoni na ushauri niandikie kupitia:
📧 venancegilbert@gmail.com
📞 0753400208.

PREMIER: A POEM BY VENANCE GILBERT FOR CELEBRATING THE WORLD MOTHERS' DAY 2018



Venance Gilbert: A composer of this poem.

Today is a very special day to all Mothers in the World. It is called World Mothers' Day. As one among the people who were raised by a mother, I found an interest in holding a pen and a piece of paper at least to write the few from the collection of what I did as I was growing up and my mother was there for me to make sure that I grow up wisely and intelligently. On March 28, 2017 I completed the long lasting composition of this poem. IT IS VERY SPECIAL FOR MY DEAR MAMA FLORENTINA AND ALL MOTHERS' IN THE WORLD. May be your mother has passed away (sorry for the loss) but due to spiritual faith, we believe that the resting mothers in heaven can hear our voices, so you can also recite the poem for your mom and she will hear you in one way or another. The poem is called Premier. I welcome you once again to this field of language use. I have hired a very simple language in composing this poem, it is very understood and straightforward:

Poem: Premier
Poet: Venance Gilbert
Composition: March 28, 2017

My premier
That genuine premier of me
I say genuine since he skilled me to be material
Premier I know you are delighted of me
Your harvest is gratified of you most
My premier, my duplicate
You accentuate me to premise on goodness
Those generations when I operated capricious
Honorably your pampering is now honoured
Not only me some folks also say
But premier they never be fluent in it loud
In a nutshell this blameless make-up ensued after you
And this is why I say you are packed with conceit.

Premier
Into blackness and perky you hiked
Probably some are uncovered in this
But them handier certainly not branded this
Premier you are the only that Supernatural being gifted me
Your depth gloss upon me like not any gilt
And I see your craving never catch antediluvian
Above and beyond it is protracted fixed interminably
Just like no one can sort out healthier than you
This has building I for one I am at the moment
What else can I for one say? I hearting you premier.

I dredge up those generations I was vulgar
Those livings when the deeds was unworldly
I also hark back to the switch into teens
A tick when I operated sagacious
Premier you performed in conformity with the phase
You drafted the role and set me on the route
I was half-hearten but you never let that alive in me
If you could leave me, who else would carry me delicately?
Undeniably, Not any. I treasure you premier.

Premier
Where I wailed you also get in
Just to spectacle that the realm was not only mine
And when entirety put me downcast
You battled my angle, you bout for me
Your maws could voice to me devotedly
If you give up I will despond
Be solid I am with you to soar the massif
And we scrabbled collectedly directioning to the ultimate
And our flight was at least efficacious
God, take the appreciations for the exquisite premier

Premier
In our day as I let my big hand ink about you
I summon up those beings you contended on hard working
At the phase I didn’t grasp but you adage for me
My produce work, work hard, work as you can
If you work, you have a warranty to live healthier
The troop will worth your being there in time off
But if you no toil, publics will be drowsy of you
Thank you premier, I grasp it in their gates.

Premier
Our life-cycle is an encyclopedia
There is no way it apt the lone script
I set aside those archetype existences you stressed
You lodged the rising germs inside me
And their fruit is seen in prospect
Premier, I worth how you upturned me
I upkeep and pledge to animate in noble
Sometime I wish to amend the wheel
To reword the deportment, but you discern
That I was just on the rise, thank you premier one.



Thank you for taking time and interest in reciting this 6 stanzas poem. If you have anything to comment or advice please leave your comment below or you can write to me through:
 ðŸ“§ venancegilbert@gmail.com
📞 0753400208.

ZIJUE FAIDA NA HASARA ZA KUWA NA AKAUNTI BINAFSI "PRIVATE" KATIKA MTANDAO WA INSTAGRAM


Uhali gani mpenzi msomaji wa segment yetu ya Fahamu? Nakukaribisha katika segment yetu ya kila siku ya Fahamu, kama ilivyo kawaida, hapa nakufahamisha mambo kadhaaa ambayo labda hukuyafahamu ama uliyafahamu ila si kwa kina basi huwa nakufahamisha hapa. Kumekuwepo na akaunti nyingi binafsi hasa hasa zile za watoto wa kike kwenye mtandao wa Instagram. Kuna faida na hasara za kuweka akaunti yako kuwa binafsi na hasara zake pia. Leo nakuletea mada kuhusu faida na hasara za kuwa na akaunti binafsi ambazo hizi ndizo zinazotofautisha kua na akaunti huru na binafsi:
Related image
Huu ni mfano wa akaunti binafsi ya Instagram ukiitembelea
FAIDA ZAKE
1. KUA NA MAMLAKA YA KURUHUSU AMA KUTORUHUSU NANI AKUFUATE
Unapaokuwa na akaunti private ya instagram basi unakua na uwezo wa kuamua mwenyewe kwamba nani akufuate (following) na nani asikufuate kwa mfano unaweza kuzuia watu ambao ni wanafamilia ikiwa akaunti yako ina mambo yako ya siri lakini hii haizuii wao kuangalia kwa maana bado wanaweza kutumia majina usiyoyafahamu. Kila anayetaka kua mfuasi wako anapata ruhusa kutoka kwako kabla ya kua mfuasi. Huu ni usalama binafsi kwa namna moja ama nyingine.

2. INAZUIA MUINGILIANO NA MITANDAO NA TOVUTI NYINGINE
Unapokuwa na akaunti binafsi unazuia muingiliano wa mitandao mingine na tovuti nyingine kwa mfano muingiliano wa tovuti nyingine hii inakupunguzia uwezo wa kupata wafuasi wapya kwa maana.

3. INAZUIA WATU KUDOWNLOAD PICHA NA VIDEO UNAZOWEKA
Hii kwa namna moja ama nyingine inaweza kua ni faid na pia hasara kwa namna nyingine. Instagrama inazuuia uwezo wa watu kudownload picha na video zako kama akaunti yako ni private hii inatokana na kufunga link ya kudownload. Hii ni kwa wafuasi wako kwa maana ndiyo wenye uwezo wa kuiona akaunti yako.

4. INAZUIA WATU KUWAONA WAFUASI WAKO NA WALE ULIOWAFUATA
Kama bado hujakubaliana na ombi la mtu kukufuata inakua ni vigumu kwa yeye kuwaona wafusai wako hii ni kwa sababu sera ya faragha inazuia isntagram kutoa taarifa zako kama hizi; wafuasi na uliowafuata, picha na video zako lakini hii haizuii wasifu wako (bio) kutoonekana.


HASARA ZAKE
1. INAKUPUNGUZIA IDADI YA WAFUASI
Wapo watu ambao kwa namna moja huja kwenye akaunti yako kuangalia picha na video unazoweka ili wakufuate mtandaoni hapo hivyo wanapokuta akaunti yako ni binafsi na kutoona taarifa zako kama vile picha na ama makala zako basi wanaamua hata kutokukufuata kabisa. Kuna wakayti unashea na watu picha yako katika mitandao ya Facebook na Twitter na hivyo watu wakavutiwa na kukufuata lakini wanapokuta aaunti yako ni binafsi wanaamua kuachana na akaunti yako.

2. INAPUNGUZA MUINGILIANO
Unapokua na akaunti binafsi unapunguza uwezo wa watu kuingiliana na akaunti yako kwa mfano kupata watembeleaji wapya, kufanya biashara na watu kupitiaa Instagram na hata kufanya matangazo na mtaandao wa Instagram (Sponsored links) Ni lazima iwe akaunti huru kwa umma ili uweze kupata miingiliano kama hii na mingineyo.

3. INAKUPUNGUZIA WATEJA KAMA NI AKAUNTI YA BIASHARA
Kama wewe ni mfanya biashara na akaunti yako unaiendeza kwa msingi wa kuwa akaunti binafsi fahamu kwamba unapunguza idadi kubwa sana ya wateja yako. Hii inafanya watembeleaji wapya wasiwe na uwezo wa kuziona picha zako za matangazo ya biashara. Instagram ni mahala pazuri sana kutangaza biashara yako kwa vile inaruhusu picha na maelezo yake.

4. INACHOSHA KUPITIA MAOMBI YA WATU WANAOTAKA KUKUFUATA
Inaweza kua suala la kawaida kupitia maombi ya watu wanaotaka kukufuata lakini ni usumbufu pia na inachosha kupitia maombi yote has pale idadi ya watu wanaotaka kukufuata inapokuwa kubwa. Unapokua na akaunti huru unapata tu taarifa kwamba mtu fulani kakufuata basi.


Kwa Maoni na Ushauri wasiliana nami kwa moja kati ya njia hizi:
Barua pepe: venancegilbert@gmail.com
Simu: 0712586027 (na WhatsApp pia) na 0753400208.