FAHAMU WATU AU MAMBO YALIYOTAFUTWA SANA GOOGLE MWAKA 2016


Kila mwisho wa mwaka Mtandao wa Google hutoa orodha ya yale yaliyotafutwa kupitia mtandao huo. Tutaangalia katika nyanja za kiujumla, habari za dunia, watu, bidhaa za kiteknolojia, habari za michezo duniani, vifo, muvi/sinema, wasanii na vipindi vya runinga. Katika kila nyanja tutaangalia mambo au watu 10. Tuanze kuangalia trends hizo:

KIUJUMLA 

1. Pokeman Go
2. iPhone 7
3. Donald Trump
4. Prince
5. Powerball
6. David Bowie
7. Deadpool
8. Olympics
9. Slither.io
10. Sucide Squad


HABARI ZA DUNIA

1. Uchaguzi wa Marekani (US Election)
2. Olympics
3. Brexit
4. Mauaji ya Orlando (Orlando Shooting)
5. Virusi vya Zika
6. Panama Papers
7. Nice
8. Brussels
9. Mauaji ya Dallas (Dallas Shooting)
10. Tetemeko la ardhi Kumamoto (Kumamoto Earthquake)

WATU

1. Donald Trump
2. Hillary Clinton
3. Michael Phelps
4. Melania Trump
5. Simone Biles
6. Bernie Sanders
7. Steven Avery
8. Celine Dion
9. Ryan Lochte
10. Tom Hiddleston


BIDHAA

1. iPhone 7
2. Freedom 251
3. iPhone SE
4. iPhone 6S
5. Google Pixel
6. Samsung Galaxy S7
7. iPhone 7 Plus
8. Note 7
9. Nintendo Switch
10. Samsung J7

HABARI ZA MICHEZO KIDUNIA

1. Rio Olympics
2. World Series
3. Tour de France
4. Wimbledon
5. Australian Open
6. EK 2016
7. T20 World Cup
8. Copa América
9. Royal Rumble
10. Ryder Cup


VIFO

1. Prince
2. David Bowie
3. Christina Grimmie
4. Alan Rickman
5. Muhammad Ali
6. Leonard Cohen
7. Juan Gabriel
8. Kimbo Slice
9. Gene Wilder
10. José Fernández 
 

MUVI

1. Deadpool
2. Suicide Squad
3. The Revenant
4. Captain America Civil War
5. Batman v Superman
6. Doctor Strange
7. Finding Dory
8. Zootopia
9' The Conjuring 2
10. Hacksaw Ridge 
 

WANAMUZIKI


1. Céline Dion
 

VIPINDI VYA RUNINGA 

 

1. Stranger Things
2. Westworld
3. Luke Cage
4. Game of Thrones
5. Black Mirror
6. Fuller House
7. The Crown
8. The Night Of
9. Descendants of the Sun
10. Soy Luna 
 
 
 

TAARIFA HII IMEANDALIWA KWA MSAADA KUTOKA GOOGLE.

Sogea karibu na VENANCE BLOG  kwenye mitandao ya kijamii
facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venancegilbert
Barua pepe (e-mails): venancegilbert@gmail.com & venanceblog@gmail.com

KUELEKEA MWISHONI 2016 LADY JAY DEE KAYAANDIKA HAYA INSTAGRAM



Kuelekea mwisho wa mwaka 2016 msanii mkongwe Lady Jay Dee ameyaandika haya katika mtandao wa Instagram:

"Kiukweli comeback yangu ya 2016 ilikuwa kubwa sana kuliko watu wengi walivyoitegemea mbali na changamoto ngumu na nyingi nilizowahi kupitia na ninazoendelea kuzipitia kuliko msanii yeyote yule wa kike wala wa kiume Tanzania nadiriki kusema bado nimesimama Imara *Kejeli *Dhihaka *Mabezo *Kutengwa *Story za kusingiziwa ikiwemo kuambiwa nyumba yangu inauzwa sijui inapigwa mnada na mengine yote mnayoyajua ni vitu vinavyovunja moyo sana. Ila Wa Tanzania ninawaheshimu sana linapokuja swala la kupigania kitu mnachokipenda. Hivi bila nyie si ningekuwa marehemu??? Bila fans JayDee ni nani??? Ninawashukuru kwa kuniamsha. Ninawashukuru kwa kuniamini. Ninawashukuru kwa kunipa nguvu na jeuri. Kuanzia Ndindindi mpaka Together *Mliijaza Mlimani City *Mkajaza mikoa niliyopita. Nawaomba muendelee kujaa 2017. Ili kuwadhihirishia wanadamu kuwa Mungu huwa ni mmoja tu. Happy new year to my fans all around the world. Nawapenda hata nikinuna. Kaeni tayari kwa album ya WOMAN 2017."

Hiyo ilikuwa ni sehemu ya kwanza, aliyoiandika jana na hii hapa chini ni sehemu ya pili:

"Kama nilivyoeleza hapo awali mwaka 2015 vitu vingi  vilisimama ili nijpange upya. Na 2016 vitu vingi vilianza kurudi Ikiwemo kuendelea kuperform na Band yangu THE BAND ambayo niliondoa jina la MACHOZI BAND na tulizunguka sehemu nyingi nchini. Mwaka 2017 nitarudisha kitu kingine ambacho kimekuwa kikiulizwa na watu wengi sana kutokana na kutokuwepo hewani kwa takribani mwaka na nusu. DIARY YA LADY JAYDEE Itarudi tena kwa mfumo na muonekano wa tofauti na wa mwanzo ukizingatia maisha yangu pia yamebadilika Hivyo naomba sponsor kujitokeza kwa wingi pia kwani mambo yakuwa ni moto sana. Itakuwa ni kuhusu misha yangu binafsi ya kimuziki, kibiashara, mapenzi na kila kinachonizunguka. Kaeni tayari kwa Msimu mpya wa Diary ya Lady JayDee yenye production bora zaidi ya jana. Diary ya Lady JayDee pia itapatikana kwenye YouTube channel yangu fanya kusubscribe"

Hii ni sehemu ya pili aliyoiandika katika mtandao wa Instagram. Kama kuna lolote usikose kutembelea VENANCE BLOG kwa mengine zaidi. Jay Dee anapatikana Instagram @jidejaydee





 Unaweza kulike VENANCE BLOG facebook kwa kubofya HAPA
Nifolo kwenye Twitter @Venancetz au bofya HAPA
Nipo Instagram pia @venancegilbert au bofya HAPA

TATHIMINI KWA UFUPI CHELSEA vs EVERTON KABLA YA MECHI SAA 2:30 EAT

Timu hizi mbili zimekutana katika michezo 49 ambapo Chelsea imeshinda mechi 22 na Everton imeshinda mechi 10 na kudroo mechi 17. Chelsea imeshinda nyumbani mechi 13 wakati Everton imeshinda mechi 9. Nje, Chelsea imeshinda mechi 9 wakati Everton imeshinda 2.

Katika mechi 3 zilizopita Chelsea ilifungwa na Everton magoli 2 kwa nunge, hii ilikuwa mechi ya Machi 12, 2016. Lakini pia mechi ya Januari 16, 2016 timu hizi zilitoka sare ya magoli 3. Na ile ya Septemba 12, 2015 Chelsea alipigwa magoli 3 kwa 1.

Katika msomu huu Chelsea ipo katika nafasi ya 4 wakati Everton ipo nafasi ya 6 kwenye msimamo wa Ligi. Chelsea imeshinda 70% ya mechi ilizocheza huku Everton ikishinda 50%. Mechi za nyumbani Chelsea ina asilimia 80% dhidi ya mpinzani wake Everton 50% huku mechi zilizopigwa nje Chelsea ana 60% na Everton 40%. Chelsea ina wastani wa 2.1 katika magoli iloshinda wakati Everton ana wastani wa 1.5 Lakini pia Chelsea imefungwa wastani wa 0.9 wakati Everton ina 0.8.

TAHLISO YATOA WIKI MOJA KWA SERIKALI KUTOA MIKOPO

Shirikisho la serikali za wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu Tanzania (TAHLISO) limetoa muda wa wiki moja kwa wanafunzi waliokosa mikopo licha ya kuwa na vigezo vyote ikiwemo uhitaji kusikilizwa na serikali kabla hatua nyingine hazijachukuliwa.


Tamko hilo limetolewa leo na Mwenyekiti wa shirikisho hilo Bwana Stanslaus Peter, katika kikao cha pamoja kilichohusisha marais wa vyuo vyote nchini, waliokutana Jijini Dar es Salaam leo, kujadili sintofahamu inayowakumba wanafunzi wanaojiunga mwaka wa kwanza katika vyuo mbalimbali nchini.


Stanslaus amesema kuwa kuna kundi kubwa la wanafunzi ambao wameondolewa kwenye orodha ya wanufaika, na wengine kunyimwa kabisa ama kwa visingizio au bila sababu, jambo linalowafanya waishi katika mazingira magumu na kuhatarisha hatma yao kimasomo.


Amesema wamekubalina kuwa, endapo serikali haitafanyia kazi ombi hilo ndani ya wiki moja, basi shirikisho hilo litachukua hatua ikiwa ni pamojana kuhamasisha wanafunzi wa mwaka wa pili na wa tatu kuungana na wale wa mwaka kwanza katika kudai haki hiyo.


Chanzo: EATV

IFAHAMU ANDROID NOUGAT VERSION 7

Google Inc. kupitia teknolojia yao ya Android wanakuja na Version nyingine 7.0 na 7.1 Android Nougat.


Katika historia ya version za Android zilizowahi kuwagunduliwa version ya Kwanza ilikuwa Android Alpha 1.0 ya mwaka 2007. Hapo katikati zikaletwa Zombie Arts, Jeally Bean, KitKat, Lollipop na Mashallow. Sasa ni zamu ya Android Nougat.


TUANGALIE SIFA ZA ANDROID NOUGAT 7

Android Nougat ipo kwa ajili hako. Ina njia nyingi za kufanya uhisi teknolojia hii ni ya kwako. Kwa mujiu wa Android, Nougat ni toleo zuri kuwahi kutolewa katika teknolojia hii.

1. Ni Mfumo wa Uendeshaji (Operating System, OS) unaotumia lugha yako. Inayasogeza karibu maneno ya lugha yako ikiwa na emoj mpya na uwezo wa kutumia lugha 2 kwa wakati mmoja. Ina zaidi ya emoj 1500 ikijumuisha emoj mpya 72.



2. Inakuruhusu kufanya mambo 2 kwa wakati mmoja. Sasa unaweza kutumia vitumizi viwili (applications) kwa kugusa mara mbili (double trap) na kutumia vitumizi viwili pande mbili. Kwa mfano, unaweza kuangalia muvi na kutuma ujumbe.



3. Jionee Android yako katika ubora mpya. Version hii inakuja na Graphics za Vulkan™ API ambayo ina muonekano bora zaidi katika michezo ya simu (games). Inatumia Three Dimension (3D). Graphics hizi zina sifa ya eye-candy effects.



4. Furahia vitumizi vyako (applications) pendwa katika hali inayokaribia uhalisia. Hii itakupeleka katika ulimwengu mpya.


5. Endelea kufurahia ama kutumia simu yako yenye betri imara. Version hii inakuja na feature mpya inayoitwa Doze (hii ni sawa na Battery Saver). Hii itakusaidia kutunza chaji wakati simu yako ikiendelea kutumika ama inapokuwa mfukoni mwako.



6. Inakufanya uende na wakati. Android Nougat inakurahisishia kukufanya uende na wakati ikiwa na mipangilio iliyoboreshwa zaidi na taarifa. Unaweza kupangilia mipangilio yako ya taarifa za haraka ili kupata unachokipenda kwa haraka. Pia sasa unaweza kujibu taarifa moja kwa moja bila kufungua kitumizi chochote. Inakusanya taarifa nyingi kwa wakati mmoja kutoka katika vitumizi vyako vyote hivyo unaweza kugusa na kupanua wigo wa kuangalia taarifa bila kufungua kitumizi (application).



7. Ina njia nyigi za kufanya uhisi Android ni ya kwako. Inakufungulia njia nyingi za kuipangilia simu yako. Pangilia ni kwa jinsi gani data zako zitatumika, jinsi unavyotaarifiwa na jinsi muonekano wa simu yako utakavyokuwa. Ina Data Saver na Notification Controls kama zilivyo version zilizopita Na sasa unaweza kubadili muonekano wa icons zako kwa kubadili ukubwa wake.


8. Usalama wa simu yako ni mahsusi kabisa. Kama ilivyo kwa version zilizopita usalama wa simu yako ni muhimu. Nougat 7.0 na 7.1 zinakuhakikishia usalama wa taarifa zako binafsi na safari hii inakuja maboresho zaidi.


Hii ndiyo Android Nougat 7 na kwa kuanza itapatikana katika simu ya LG V20. Hii itakwa smartphone ya kwanza kutengenezwa ikiwa na Android Nougat 7. Itakujia hivi karibuni.




Chanzo: Android.com

BATCH 4 WALIOCHAGULIWA MZUMBE (DEGREE, DIPLOMA, CERTIFICATE & TRANSFER)

Yafuatayo ni majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu Mzumbe kwa awamu ya 4 kwa mwaka 2016/2017. Pia yapo na majina ya waliohamishwa kutoka kwingineko kwenda Mzumbe.


👉BOFYA HAPA KUONA NA KUPAKUA MAJINA HAYO👈

SIMBA YAZIONYA AFRICAN LYON NA PRISONS

Nahodha wa Simba, Jonas Mkude amesema ari waliyokuwa nayo hivi sasa ana uhakika wa kupata pointi sita nyingine kwenye mechi mbili zilizobaki kabla ya kumaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mkude alisema pointi sita walizozipata Shinyanga dhidi ya Mwadui na Stand United, zimedhihirisha ubora waliokuwa nao msimu huu na atahakikisha wanaendelea na kasi hiyo ili kutimiza kile ambacho wamekikusudia.

“Lengo ni ubingwa na kwakuwa tunautaka ubingwa kwanza lazima tumalize kinara kwenye mzunguko wa kwanza kwa kuchukua pointi zote sita kwenye michezo yetu miwili iliyobaki na baadaye tujipange kwa ajili ya mzunguko wa pili,” alisema Mkude.

Simba imebakiwa na mechi dhidi ya Africany Lyon na Prisons. Mkude alisema anafurahi kuona kila mchezaji ndani ya kikosi chao akicheza kwa kujituma na kufuata kikamilifu maelekezo kutoka kwa wakuu wa benchi lao la ufundi na anaamini ari hiyo itaendelea hadi mwishoni mwa msimu huu na hatimaye kuwa mabingwa.

“Hatujafungwa hata mchezo mmoja katika michezo 13 ambayo tumecheza hadi sasa hii ni rekodi nzuri lakini tunatakiwa kuiendeleza kwenye mechi zijazo ili tuweze kufanya vizuri zaidi na zaidi kwakuwa bado tuna safari ndefu hadi kufikia mwisho wa ligi,” alisema Mkude.

Nahodha huyo amewataka mashabiki na wanachama wa timu hiyo kuendelea kuwasapoti katika mechi zao ili kushinda mtihani uliopo mbele yao ambao ni kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu na Kombe la FA, baada ya kufanya vibaya kwa misimu mitatu iliyopita jambo ambalo lilipoteza heshima yao.

Simba inatarajia kucheza na African Lyon keshokutwa na tayari imesharejea kutoka Shinyanga na kuweka kambi Ndege Beach. Simba inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 35 baada ya kucheza mechi 13.

SERIKALI IMEPELEKA TSH. BILIONI 177 KWENYE HALMASHAURI ZA WILAYA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema serikali imepeleka katika halmashauri nchini Sh bilioni 177 Oktoba mwaka huu kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, amempongeza Rais John Magufuli, kwa kufikisha siku 365 za kuwapo madarakani na mafanikio makubwa ya utawala wake tangu alipopewa na Watanzania ridhaa ya kuwa Rais wa Tano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana.

Licha ya pongezi zake, amewaomba Watanzania waendelee kumuunga mkono Rais Magufuli ili afanikishe zaidi dhamira yake njema ya kuwatumikia wananchi. Majaliwa aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma ambapo alizungumzia mambo mbalimbali katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu.

Akizungumzia suala la fedha kupelekwa katika halmashauri, alisema serikali imechukua muda kupeleka fedha mara baada ya bajeti kupitishwa na Bunge kwa kuwa ilitaka kufanya mambo muhimu ya kujiridhisha.

Aliyaja maeneo muhimu ambayo serikali ilitaka kuyafanyia kazi kabla ya kupeleka fedha kuwa ni kujiridhisha kuwepo kwa takwimu muhimu za mapato na matumizi na kupeleka watumishi watakaosimamia shughuli za ukusanyaji wa mapato na matumizi katika halmashauri zote nchini.

Alisema pia serikali ilitaka kuratibu na kutathmini miradi yote iliyokuwa imeanza na haikuwa imeendelezwa kabla ya kuanza miradi mipya ili kutambua thamani zake.

“Baada ya kuwa tumejiridhisha, sasa tumeanza kupeleka fedha kwenye halmashauri zote nchini na kwa mujibu wa kumbukumbu zangu kutoka Hazina wakati napewa taarifa ofisini kwangu, kufikia Oktoba tumeshapeleka zaidi ya Sh bilioni 177,” alisema Majaliwa.

Alisema fedha hizo ni za miradi ya maendeleo kwenye halmashauri zetu nchini na alisema kudhihirisha hilo, aliwaambia wabunge ni shahidi wameanza kuona katika wiki tatu kwenye magazeti kumekuwa na matangazo ya zabuni. Alisema hali hiyo inadhihirisha kuwa miradi iliyokuwepo na inayoendelea imeshaanza kutengewa fedha na kuanza kutekelezwa.

Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Munde Abdallah (CCM), alimuuliza Majaliwa katika maswali ya papo kwa hapo, kwamba serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha katika halmashauri kutekeleza miradi.

Mbunge huyo alisema miradi mingi imesimama na akitolea mfano wa mkoa wa Tabora anakotoka, akisema halmashauri zote saba hazijapata fedha hizo na kwa nini katika robo ya mwaka wa utekelezaji wa bajeti fedha hazijapelekwa.

“Kabla ya kujibu Mheshimiwa Naibu Spika uridhie niwakumbushe Watanzania kuwa Rais John Magufuli amefikisha siku 365 kwa mafanikio makubwa, tumuombee aendelee vizuri, kila mmoja kwa dhehebu lake amuombee nchi ipate mafanikio makubwa,” alisema Majaliwa kabla ya kujibu swali hilo.

Baada ya kumpongeza Rais Magufuli ambaye aliapishwa Novemba 5 mwaka jana kuwa Rais wa Tanzania baada ya kushinda Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huo, alijibu swali la Abdallah alisema ni kweli baada ya bajeti serikali inapaswa kupeleka fedha katika halmashauri.

Alisema baada ya tathmini tayari fedha zimeanza kupelekwa katika halmashauri hizo. Akijibu swali la Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) kuhusu mgawanyo wa fedha za Mfuko wa Bunge kuchelewa kufika na kueleza kuwa ni dalili za serikali kufilisika.

Waziri Mkuu alisema serikali haijafilisika na katika kipindi cha mwaka bado kuna miezi saba ya kuzipeleka fedha hizo zinazopelekwa mara moja kwa mwaka.

Aidha, akijibu swali la nyongeza la Waitara kwamba Segerea inapata fedha nyingi (Sh milioni 33) ingawa ina watu wachache wakati Ukonga inapata Sh milioni 16 pekee, Majaliwa alisema atalishughulikia kwa kuwa jimbo lenye watu wengi linapaswa kupewa fedha nyingi.



Chanzo: Habari Leo

WAHAMIAJI 239 WAHOFIWA KUZAMA KATIKA AJALI YA MELI WAKITOKEA LIBYA

Wahamiaji 239 wamehofiwa kuzama katika ajali ya meli wakitokea nchini Libya. Hii ni kwa mujibu wa habari kutoka shirika la Wakimbizi UNHCR.

Msemaji wa UNHCR mjini Roma Italia amesema kuwa taarifa hizo zimethibitishwa na manusura wa ajali walipofikishwa katika ukingo wa bahari katika kisiwa cha Lampedusa.

Mpaka sasa hakuna ambaye amekwishapatikana katika hao 239.

Sami alisema kuwa watu 31 wamenusurika katika ajali za meli mbili zilizopata ajali baharini kufuatia dhoruba kali.

Walisema kuwa watu 29 walinusurika katika meli ya kwanza huku wengine 120 hawajulikani walipo.

Katika jitihada za kuokoa watu, wanawake 2 waliokuwa wakiogelea kujinusuru waliwambia waokoaji kuwa watu hao 120 walikufa katika meli hiyo.

Katika matukio yote mawili, wengi wa wahamiaji hao wanaonekana kuwa ni raia kutoka eneo la Jangwa la Sahara.

Leonard Doyle, msemaji mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) amesema kuwa watu 4,220 wamepoteza maisha katika mwaka huu 2016 kwenye ajali za meli katika bahari ya Mediterania wakijaribu kuvuka kwenda barani Ulaya. Idadi hii ni kubwa kuwahi kurekodiwa.

Zaidi wa watu 330,000 wamevuka bahari ya Mediterania mwaka huu ikilinganishwa na watu Milioni moja waliovuka mwaka jana 2015.


Vyanzo: Al Jazeera & BBC World News

OBAMA AWATAHADHARISHA WAPIGA KURA KUHUSU TRUMP

Rais Barrack Obama amewahimiza wafuasi wa chama cha Democratic kumpigia kura Hillary Clinton na kuonya kwamba Donald Trump ni tishio kwa haki za kijamii, taifa la Marekani na dunia nzima kwa ujumla.


Rais wa Marekani Barrack Obama amewahimiza wafuasi wote wa chama cha Democratic kumpigia kura kwa wingi Hillary Clinton siku ya uchaguzi wiki ijayo na kuonya kwamba Donald Trump mgombea urais wa chama cha Republican ni tishio kwa haki za kijamii ambazo ziliafikiwa kupitia hali ngumu , taifa la Marekani na dunia nzima kwa ujumla.

Akigusia chaguo la rais siku ya Jumanne wiki ijayo, rais Barrack Obama alimpuuzilia mbali Trump kuwa mtu asiyestahili kabisa kuwa rais.

Kufikia sasa Clinton bado anaonyesha uwezekano wa kuwa rais wa 45 wa Marekani lakini huku zikiwa zimesalia siku sita kabla ya uchaguzi huo mkuu, wafuasi wa chama cha Demokratic bado wako chonjo hasa kutokana na mienendo ya Trump isiyotabirika.

Obama aliwaambia wapiga kura katika mji wa Chapel Hill kuwa hatima ya taifa hilo imo mikononi mwao . Aliongeza kwa kusema, „"hatima ya dunia inawategemea nyinyi, wapiga kura wa North Carolina itawabidi kuhakikisha munachukuwa hatua katika mwelekeo bora."

Mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton

Wikileaks yaendelea kutoa barua pepe

Huku kampeini hizo zikipamba moto, barua pepe nyingine za siri zinazomhusu Hillary Clinton zilitolewa hapo jana na mtandao wa wikileaks unaofanya udukuzi na kuchapisha taarifa za siri, hizi zikiwa sehemu ya barua pepe zinazotolewa na mtandao huo kila siku tangu mwezi uliopita.

Mtandao huo umesema kuwa unanuia kutoa barua pepe hizo zilizoibwa kutoka kwa akaunti ya mkuu wa kampeini ya Hillary Clinton , Podesta kila siku katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Hata hivyo msemaji wa wizara ya mashauri ya kigeni ya Marekani John Kirby alisema hapo jana kuwa wizara hio haitatoa taarifa yoyote kuhusiana na madai hayo ya stakabadhi zilizoibwa lakini akasema kuwa juhudi za wizara hiyo za kutoa taarifa sahihi kwa vyombo vya habari kuhusiana na kipindi cha kuhudumu kwa Hillary katika wizara hiyo mara nyingine ilihitajika kuwasiliana na waakilishi wake kuhakikisha kuwepo kwa usawa.

Kundi la kampeini la Clinton hata hivyo limekuwa likionya kuwa mtandao huo wa wikileaks umeharibu barua pepe zilizoibwa na wadukuzi ambao huenda wanafanyia kazi serikali ya Urusi.

Chanzo: DW

MAJINA YA MKOPO MZUMBE MWAKA WA KWANZA 2016/2017 HAYA HAPA


Chuo Kikuu Mzumbe kimetoa majina ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza walionufaika na Mkopo wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2016/2017. 

Ili kuona majina haya kwa simu hakikisha una Office App kwenye simu yako (WPS Office, OfficeSuite ama Polaris Office n.k.)


MAJINA YA WALIOCHAGULIWA MZUMBE AWAMU YA TATU HAYA HAPA (BATCH/ROUND 3)

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Chuo Kikuu Mzumbe, imetoa majina ya waliochaguliwa chuoni hapo kwa awamu ya tatu (Third Batch/Round)

Tumia mojawapo kati ya Browser hizi kuangalia selection hizo; UC Browser, Mozilla Firefox, Google Chrome au Dolphin Browser, Opera Mini haitaonesha baadhi ya vipengele katika kudownload majina haya. Link itakupeleka moja kwa moja juu kabisa kutakuwa na mshale wa kupakua majina hayo, bofya hapo na majina yatashuka moja kwa moja.

👉BOFYA HAPA KUONA NA KUDOWNLOAD MAJINA👈

HAYA HAPA MAJINA YA HOSTEL MZUMBE MWAKA WA KWANZA (JINA LA HOSTELI NA NAMBA YA CHUMBA)

Haya hapa majina ya Hosteli mwaka wa kwanza Mzumbe (Jina la Hosteli pamoja na namba ya Chumba unachotakiwa kuishi) 

RAIS MAGUFULI AAHIDI KUENDELEA KUTOA MIKOPO 2016/2017 KWA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU NA KUTOA RAI SUALA HILO KUSHUGHULIKIWA

Tokeo la picha la magufuli udsm leo oktoba 21

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo kwa nafsi yake ametoa matumaini kwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali nchini kuhusu hatima yao ya mkopo wa Elimu ya Juu alipokuwa akihudhuria sherehe ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Rais Magufuli amebainisha haya, namnukuu;

"Tunapopitia katika challenge hii muivumilie serikali kutengeneza utaratibu ulio mzuri, ninafahamu, katika bajeti ya mwaka 2015/2016, fedha iliyotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa sababu Mh. Waziri umezungumza hapa zilikuwa bilioni 340 ambazo  zilikjuwa zinatosha karibu wanafunzi tisini elfu (90,000)  baada ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani  ili kutimiza yale tuliyokuwa tumeahidi tuliongeza fedha hizo za mkopo hadi kfikia bilioni 473 bajeti ilikuwa ya bilioni 340 tukaongeza zikafika bilioni 473 kutokana na makusanyo na tukaweza kutoa mikopo kwa wanafunzi 124,358 mwaka huu ameeleza ni zaidi ya bilioni 483 zimepitishwa katika bajeti  kwa hiyo wanafunzi wengi zaidi watapata mkopo ninafahamu kwa mfano wanafunzi wanaoendelea ambao wako karibu 93,000 wote wamekuwa accommodated kwenye mkopo pamoja na wanafunzi wapya ambao nafikiri ni zaidi ya 25,000 lakini ni lazima kweli nikiri hapakuwepo na coordination palitakiwa kwanza vyuo vyote vya elinu ya juu viwe na tarehe moja ya kufungua kwa sababu wapo wengine walifungua mwezi mzima uliopita wako wengine wamefungua jana wako wengine watafungua keshokutwa ukishafungua haraka haraka wanafunzi wakakaa pale kwa mwezi mmoja halafu unawambia kufanya registration lazima walipe wakati Bodi ya Mikopo haijatoa orodha ya majina ya vijana ambao watakaokopeshwa ni contradiction.

Palikuwa pawepo na communication kati ya Bodi ya Mikopo sijui ni TCUsijui ni nani, Wizara ya Elimu na Wizara ya Fedha kwamba katika orodha ya wanafunzi watakaopata mikopo ni hawa hapa majina yao ni haya hapa mnapeleka majina hayo na orodha, amount ya fedha zinazotakiwa Wizara ya Fedha, Wizara ya Fedha nao wanaprocess zao fedha hizi tunazitoa baadaye zikishapelekwa kwenye benki kwenye hizo akaunti za wanafunzi, mngeweza mkafungua vyuo hapakuwa na sababu ya kufungua mwezi mzima kabla wanafunzi wanakaa pale hajui kama atapata mkopo au hatapata mkopo halafu unamwambia hakuna registration  kwa sababu hujapata mkopo inaleta usumbufu wa ajabu, na hilo.

Nitoe wito kwa Wizara ya Elimu na hili nasema kwa dhati lengo la serikali si kuleta usumbufu kwa wanfunzi  lakini ni ukweli pia kwamba haitatoa mikopo kwa wanafunzi ambao wenye uwezo unamkuta mtoto wa Profesa Rwekaza na wewe upate mkopo mtoto wa Ndalichako naye apate mkopo mtoto wa Katibu Mkuu Kijazi naye apate mkopo haiwezekani mkopo huu umelenga kwa ajili ya kutoa watoto masikini lakini nafahamu na ninasikia hata katika Bodi ya Mikopo kule kuna upendeleo upendeleo wa aina fulani katika kutoa mkopo hata ambao hawastahili wanapewa mikopo na ambao hawastahili wananyimwa mkopo sasa hili Waziri na Bodi zinazohusika mulisimamie sitaki siku moja nije huko kwenye Bodi ya mikopo nichukue orodha ya wanafunzi wote niangalie shule walizosoma na particulars walizozijaza halafu nije nipewe majina ya watu ambao hawakustahili kupewa mkopo wanafunzi 25 wa mwaka huu siwezi kushindwa kusoma kwa siku 1 ntapekua page by page 25,000 ukigawa kwa masaa 12 ambayo naweza nikajifungia kila jina naweza nikalisoma kwa sekunde ngapi ninajua naweza, sasa tusifikie huko.

Ninashukuru Waziri baada ya kuona hii changamoto ukawa umelileta hili suala haraka haraka na tukatoa instruction Wizara ya Fedha watoe bilioni 80 za mwanzo haraka haraka na nimeambiwa zimeshatolewa, sasa niwaombe wanafunzi msiwe na haraka haraka kwa sababu katika changamoto hizi ambazo zinapita ndani ya serikali wanafunzi hewa, mikopo hewa, mishahara hewa hatutaki hela yetu ipotee ovyo pameshatokea changamoto na najua haitatokea tena vyuo vikuu vitakuwa vinafunguliwa siku ambapo wana uhakika na fedha zitakuwa zimeshapelekwa kwenye wanafunzi.

Lakini pia pamekuwa na utitiri mwingi mno wa vyuo vikuu unakuta shule ilikuwa inaitwa sekondari leo ukisoma kwenye orodha nayo inaitwa Chuo Kikuu na saa nyingine inafikia wanafunzi unaanza kuwagombania, Chuo Kikuu kwa mfano cha Dodoma kina capacity ya kuweka wanafunzi mpaka 45,000 waliopo ni 30,000 lakini unakuta kinafunguliwa chuo kingine Bagamoyo kina wanafunzi 20 mabweni hayapo maabara hayapo natoa mfano tu labda nimesema Bagamoyo kingine kinafunguliwa Chato.

Sasa ninachotaka kutoa wito kwa Bodi, TCU, Wizara hebu mpitie vizuri hivi vyuo mnatoa vibali mnatoa vibali mno vya kuanzisha chuo kikuu kila mahali wakati vyuo vilivyopo havijajaa watu na mnawachanganya saa nyingine hawa watoto kwa sababu mnakuwa mnawagombania, na vyuo vikuu vingine havina walimu unakuta mwalimu leo yuko  Dar es Salaam kesho yuko Mbeya keshokutwa yuko Iringa keshokutwa Moshi ataconcentrate namna gani kufundisha kwa hiyo matatizo haya mengine yameletelezwa na nyinyi mnnaopendwa kuitwa maVice Chancellors wenye vyuo vilivyopo sijasema wewe (akimaanisha Prof. Rwekaza, VC wa UDSM) kwa hiyo nikuombe Waziri simamia hili, kwanu kuna ubaya gani tukiwa hata na vyuo vikuu vinne tu kila chuo kina watu milioni moja moja watu wako palepale wanalipwa mshahara mzuri na wanaconcentrate vizuri."


KWA MSAADA KUTOKA KWA MWANAFUNZI ALIYEFATILIA SPEECH HII CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM NA KUSAMBAZA KWA WATANZANIA.

MFAHAMU HILLARY CLINTON KWA MAMBO HAYA 15

Tokeo la picha la hillary clinton
Jina Kamili: Hillary Diane Rodham Clinton
Kuzaliwa: Oktoba 26, 1947
Alikozaliwa: Chicago, Illinois

Kwa Ufupi

Alipochaguliwa kuwa Seneta mwaka 2001 alikuwa mwanamke wa kwanza First Lady kuwa mtumishi wa serikali. Baadaye alikuwa Katibu Mkuu wa Ikulu ya Marekani mwaka 2009 akitumikia wadhifa huo hadi mwaka 2013 katika utawala wa Rais Barrack Obama. Mwaka huu (2016), amekuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kugombea Urais kwa tiketi ya chama cha The Democratics.

Tokeo la picha la hillary clinton
Hillary alizaliwa  Oktoba 26, 1947 huko Chicago, Illinois. Alipata Shahada yake ya Sheria kutoka Yale University. Alifunga ndoa na mwanafunzi mwenziye aliyekuwa akisoma sheria Bill Clinton mwaka 1975. Baadaye alitumikia taifa la Marekani kama First lady  mwaka 1993 hadi 2001, na baadaye akiwa Seneta mwaka 2001 hadi 2009. Mapema mwaka 2007 Clinton alitangaza kugombea Urais nchini Marekani. Katika kura za maoni mwaka 2008 alichuana na Barrack Obama lakini kura hazikumruhusu kugombea Urais kwa ticket ya Democratic. Rais Obama alipoingia madarakani alimchagua kuwa Katibu Mkuu mwaka 2009 hadi 2013.

HillaryRodham ni mtoto  mkubwa katika familia ya Hugh Rodham na Dorothy Emma Howell Rodham. Ana wadogo zake wawili wanaume; Hugh Jr. aliyezaliwa 1950 na Anthony aliyezliwa 1954.

Kama kijana Hillary aliingia katika siasa na kumfanyia kampeni mgombea wa chama cha Republican Barry Goldwater mwak 1954. Alivutiwa kufanya kazi za umma baada ya kusikia hotuba ya Martin Luther King Jr. huko Chicago na hapo alijiunga na chama cha Democratic mwaka 1968.

Elimu

Tokeo la picha la hillary clinton at yale
Hillary enzi za Yale
Hillary alisoma Wellesley College ambapo alikuwa akishiriki katika masuala ya siasa shuleni na alichaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa darasa lake kabla hajahitimu mwaka 1959. Baadaye alijiunga na Shule ya Sheria Yale ambako alikutana na Bill Clinton. Alitunukiwa Shahada ya Heshima katika sheria mwaka 1973 na aliendelea na alijiunga na Kituo cha masomo ya watoto Yale ambako alisoma kozi za masomo ya watoto na madawa nakwa mwaka mmoja.

Ndoa

Tokeo la picha la hillary clinton and bill wedding
Hillary na Bill Clinton siku ya harusi yao 1975

Alifunga ndoa na Bill Clinton mwaka 1975 na wana mtoto mmoja anayeitwa Chelsea. Ndoa hii ipo katika orodha ya watu maarufu duniani ambao wameanza mahusiano tokea wakiwa masomoni. Hillary alipomaliza chuo kwa wakti ule alikaa mwaka mzima chuoni hapo akimsubiri mpenzi wake Bill Clinton ahitimu masomo yake.

Vitabu alivyoandika

1996- It Takes a Village
1997- The Unuque Voice of Hillary Clinton
1998- Dear Socks, Dear Buddy
 2000- An Invitation to the White House
2003- Living History
2014- Hard Choices
2015- Solutions: American Leaders Speak Out on Criminal Justice
2016- Stronger Together

First Lady wa Marekani

Tokeo la picha la the clintons during bill inauguration
Siku ya kiapo, Bill Clinton kama Rais akiwa na mkewe Hillary na binti yao Chelsea

Katika Uchaguzi wa mwaka 1992 Hillary alishiriki vyema katika kuaslimia wapiga kura, kuhutubia na kuwa miongoni mwa washauri wakuu wa Bill Clinton.


MAMBO 15 UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU HILLARY CLINTON

15. Ameshinda tuzo ya Grammy mwaka 1997 lakini sio tuzo ya muziki. Ni kuhusu kitabu chake cha It Takes a Village lakini sio pekee aliyeshinda tuzo hizo, Obama pia alishachukua tuzo hii katika kitabu chake pia.

14. Hillary hajaendesha gari toka mwak 1996 alilisema hili mwaka 2012.

13.  Mama yake Bill Clinton (mama mkwe wa Hillary) hakufikiria kwamba Hillary ni mzuri sana kuwa na mwanaye kuwa hana mvuto.

12. Moja kati ya kesi za awali za Hillary kama mwanasheria ilikuwa inahusisha Panya.

11. Hillary Clinton mwanzoni alikuwa mfuasi wa chama cha Republican kabla ya kuhamia Democratic mwaka 1968 baada ya kuvutiwa na moja kati ya hotuba za Martin Luther King Jr.

10.Katika utawala waRais Bill Clinton FBI walichukua picha za viganja (fingerprints) vya Bill na Hillary kuona kama wawili hao waliweza kuangalia nyaraka za FBI.Ilibainika kwamba hawakuhusika kuangalia nyaraka hizo lakini miaka miwili baadaye zilikutwa nyumbani kwa Hillary zikiwa na alama za viganja vyake.

9. Utambulisho wake wa Huduma za Siri ni "Evergreen" na alipewa utambulisho huu akiwa First lady na Huduma za Siri.Amekua akitumia utambulisho huu hata katika kampeni zake za Urais. Katika kipindi cha 2008 alipokuwa akigombea utambulisho huu ulirejeshwa tena. Bill Clinton pia amekuwa akitumia utambulisho wa "Eagle" katika kipindi cha harakati za mkewe kuelekea Ikulu .

8. Ni First lady pekee ambaye amegombea Useneta na kushinda kiti hicho akiwa pia ni First lady. Alikuwa Seneta wa New York mwaka 2001 na kukabidhiwa Ofisi Januari 3 mwaka huo.

7. Jarida la Sheria la Marekani 'The National Law Journal' lilimtaja Hillary kuwa miongoni mwa wanasheria 100 wenye ushawishi nchini humo mwaka 1988 na 1991. Umahiri wake katik sheria ulimfanya awe na pesa nyingi hata kumshinda mumewe Bill aliyekuwa Gavana wa Arkansas kwa wakati huo. Umahili wa Clinton ktik sheria ulichangia pia kwa kiasi kikubwa kumfanya Bill awe Rais wa nchi hiyo kwa kipindi hicho.

6. Ni Katibu Mkuu aliyesafiri kuliko makatibu wengine katika Historia katika kipindi chake cha miaka 4. Alizuru nchi 112 na kusafiri kwa ndege maili milioni 1 na kutumia 25% ya kipindi chake katika safari.

5. Amekuwa akituhumiwa kujihusisha na Usagaji "mapenzi ya jinsia moja". Baadhi ya watu wamekuwa wakithibitisha hili kwa mfano Edward Klein ambaye ameandika ktika kitabu chake The Truth About Hillary kuwa amekuwa akishiriki usagaji na msaidizi wake Huma Abedin na wasagaji wengine.

4. Hillary na mumewe Bill waliwahi kuitwa Mahakamani kutoa ushahidi kuhusika katik scandal ya Whitewater Development. Hata hivyo baadaye hawakukutwa na hatia ya kufanya mabaya katika scandal hiyo.

3. Hillary aliamua kutumia jina la Clinton baada ya kushawishiwa na wapiga kura wa Arkansas. Baada ya ndoa yao Hillary aliendelea kutumia jina lake la Hillary Rodham, Wapiga kura hao walitaka kujua kama ndoa yao ni ndoa kweli ama fasheni tu hivyo Hillary akaamua kutumia jina la Hillary Rodham Clinton. Kwa hiyo ili kufanya mumewe ashinde katika Uchaguzi kuwa Gavana wa jimbo la Arkansas aliamua kujiita Hillary Rodham Clinton.

2. Alishiriki katika jopo la wanasheria 43 kumtia hatiani Rais Richard Nixon. Wanajopo wenzie walimtuhumu kama muongo na kutofuata maadili ya kumtia hatiani Rais Nixon. Bosi wa Hillary alisema mara kwa mara Hillary alikuwa akikosea katik kuuliza maswali lakini hakuwa na uwezo wa kumfukuza Hillary kazi.

1. Japokuwa alipmba kurasa za jarida la The Vogue mwaka 1998, alikataa kuonekana katika Jarida hilo mwaka 2007 kwa kuhofia kuwa mfeministi sana kitu ambacho kingeleta shida katika mbio zake za uchaguzi wa Urais mwaka 2008.








Tokeo la picha la hillary clinton
 Tokeo la picha la hillary clinton

MAKALA HII IMEHARIRIWA KWA HISANI YA MTANDAO.

VIDEO: TRUMP AKATAA KUJIBU SWALI KUHUSU KUKUBALI MATOKEO KAMA ATASHINDA KWENYE UCHAGUZI

Ni katika Mdahalo wa tatu na wa mwisho ukiofanyika Nevada, Las Vegas.

Swali liliulizwa kwa Bwana Trump "utakubali matokeo ya Urais baada ya kushindwa na mpinzania wako Hillary Clinton?"

Trump hakujibu moja kwa moja, alisema "nitaliangalia hilo kwa wakati huo".

Awali ya hapo Rais Obama alishangazwa na kutokujiamini kwa Trump kuhusu kuwa na mashaka na Uchaguzi hata kabla ya Uchaguzi wenyewe kufanyika.

Nitakuandalia makala kamili kutoka kwenye Mdahalo huo.

Hii hapa video ikimuonesha Trump alivyokataa kujibu swali aliloulizwa:

Video kwa hisani ya France24.

WALIOCHAGULIWA MZUMBE AWAMU YA PILI MAJINA HAYA HAPA

Chuo Kikuu Mzumbe kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa chuoni hapo kwa mwaka wa masomo 2016/2017 kwa ngazi ya Cheti, Stashahada na Shahada kwa awamu ya pili.


>>>BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA<<<

HAYA HAPA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA AWAMU YA PILI RUAHA, MWALIMU NYERERE & ECKERNFORDE

Hapa kuna selection za Vyuo vitatu; Ruaha, Mwalimu Nyerere na Eckernforde

1. KWA RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY (RUCU)
👉BOFYA HAPA👈


2. KWA MWALIMU NYERERE MEMORIAL ACADEMY (MNMA)
👉BOFYA HAPA👈


3. KWA ECKERNFORDE TANGA UNIVERSITY (ETU)
👉BOFYA HAPA👈

ORODHA YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA AWAMU YA PILI (SAUT MBEYA, TUDARCo, MWECAU, HKMU, TIA SJUT & MUHIMBILI)

1. KWA MUHIMBILI
👉BOFYA HAPA👈


2. KWA SAUT MBEYA
👉BOFYA HAPA👈


3. KWA TUMAINI DSM (TUDARCo)👉BOFYA HAPA👈


4. KWA MWECAU
👉BOFYA HAPA👈


5. KWA HURBERT KAIRUKI
     °👉DOCTOR OF MEDICINE BOFYA HAPA👈
     °👉BACHELOR OF SCIENCE IN NURSING BOFYA HAPA👈


6. KWA TIA
👉BOFYA HAPA👈


7. KWA ST. JOHN
👉BOFYA HAPA👈

WALIOCHAGULIWA MZUMBE MAJINA YAO YAKO HAPA (FIRST BATCH/ROUND 1)

Chuo Kikuu Mzzumbe kimetangaza majina ya waliochaguliwa chuoni hapo.

👉BOFYA HAPA KUDOWNLOAD MAJINA👈

WALIOCHAGULIWA UDSM, DUCE, MUCE & IFM AWAMU YA PILI HAWA HAPA



Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na matawi yake DUCE na Mkwawa (MUCE) pamoja na Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM) vimetoa majina ya waliochaguliwa awamu ya pili kujiunga na chuo hicho.

1. KWA UDSM, DUCE NA MKWAWA (MUCE)
👉BOFYA HAPA👈


2. KWA IFM
👉BOFYA HAPA👈


3. KWA IFM MWANZA
👉BOFYA HAPA👈

ORODHA YA MAJINA WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI (AWAMU YA PILI)

Hii ni list ya majina ya vyuo vilivyotoa majina ya waliochaguliwa leo October 5, 2016.

1. KWA CHUO KIKUU SAUT AWAMU YA KWANZA NA PILI ZOTE
👉BOFYA HPA👈

2. KWA TEKU
👉BOFYA HAPA👈

3. KWA ARCHBISHOP JAMES (AJUCO)
👉BOFYA HAPA👈

4. KWA JORDAN ROUND 1 & 2
👉BOFYA HAPA👈

5. KWA BUGANDO (CUHAS)
👉BOFYA HAPA👈



Endelea kufuatilia Blog hii kwa selection za vyuo vingine zaidi kwa round zilizosalia.

WALIOCHAGULIWA JORDAN (AWAMU 1 & 2)

Chuo Kikuu Kishiriki cha Jordan kimetangaza majina ya waliochaguliwa chuoni hapo mwaka wa masomo 2016/2017.

👉BOFYA HAPA KUONA MAJINA👈

SELECTED STUDENTS TO JOIN KAMPALA INTERNATINONAL UNIVERSITY FOR ACADEMIC YEAR 2016/2017 (FIRST & SECOND BATCHES)

Chuo Kikuu chq Kimataifa cha Kampala (KIU) kimetoa majina ya awamu ya kwanza na ya pili (first and second batches) za wanafunzi waliochaguliwa chuoni hapo kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

👉BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD NA KUANAGALIA MAJINA HAYO👈