Skip to main content

Posts

MALAWI IMETEKETEZA TANI 2 ZA PEMBE ZA NDOVU KUTOKA TANZANIA

Malawi imeteketeza tani 2.6 ya pembe za ndovu ambazo zilinaswa na maafisa wa usalama zikitokea nchi jirani ya Tanzania. Meno hiyo 781 ya tembo ambayo inakisiwa kugharimu takriban dola milioni tatu ilipatikana baada ya operesheni dhidi ya ulanguzi na uwidaji haramu. Mkurugenzi wa idara inayosimamia mbuga za wanyama pori Bright Kumchedwa, amesema kuwa hiyo ni ishara ya kwanza na dhabiti kutoka kwa Malawi kuwa haitaruhusu tena ardhi yake kutumika kulangua bidhaa za uwindaji haramu. Hafla ya hiyo ya kihistoria ilifanyika katika eneo la Mzuzu kaskazini mwa nchi hiyo. Kenya inatarajiwa kutekeleza hatua kama hiyo mwishoni mwa mwezi huu. Kenya imekamata takriban tani 120 ya meno ya ndovu. Chanzo: BBC

ZITTO KABWE: RAIS AMELIINGIZIA TAIFA HASARA YA TSH. BILIONI 36

Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa Rais John Pombe Magufuli ameliingizia taifa hasara ya bilioni 36 mpaka sasa toka alipoingia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.   Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook aliandika kuwa kitendo cha Rais Magufuli kushindwa kuchukua hatua juu ya malipo ya IPTL ambayo yanalipwa na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kila mwezi yamepelekea sasa hivi kufikia jumla ya bilioni 36.   "Tshs bilioni 8 kila mwezi TANESCO bado wanalipa IPTL. Rais haijampendeza kumaliza ufisadi huu. IPTL nadhani ni Jipu la Mgongoni (kwa kutumia maneno ya Hidaya wa Richard Mabala ). Rais, kwa kutochukua kwake hatua, ameshaliingizia taifa hasara ya tshs 36 bilioni toka aingie madarakani" aliandika Zitto Kabwe.  Wakati Rais John Magufuli anatimiza siku 100 toka kutangazwa kama Rais Zitto Kabwe alitoa tathimini yake na kugusia sakata la Escrow pamoja na kampuni ya IPTL na kusema kuwa pesa amba...

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI: TRUMP NA RUBIO WATOFAUTIANA KUHUSU UISLAM

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Marco Rubio amemshtumu Donald Trump kwa kusema kuwa Uislamu unachukia Marekani katika mjadala uliokuwa moja kwa moja runingani. Bwana Rubio ambaye anakabiliwa na ushindani wa maisha yake katika jimbo la Florida siku ya Jumanne amesema kuwa Uislamu una tatizo la itikadi kali lakini akaongezea kuwa Waislamu wengi wanapenda Wamerekani. ''Marais hawawezi kusema kile wanachotaka ,kuna madhara'',alisema huku raia wakimpigia makofi. Wagombea hao wanne wa chama cha Republican walisikia maombi kutoka kwa viongozi wa chama hicho kuwa na mjadala wa amani. Ikilinganishwa na mjadala uliopita ambao ulikabiliwa na na matusi ya kibinafsi mjadala huu ulikuwa na muongozo mzuri huku wagombea wote wakitoa malengo ya sera zao. ''Kufikia sasa siamini vile tumekuwa watulivu hapa'',bwana Trump alinukuliwa akisema. Lakini katika swala la Uislamu,kulikuwa na tofauti kubwa kati ya Trump na wagombea wengine huku wen...

JANET JACKSON AAHIRISHA KUFANYA ZIARA YA MUZIKI ULAYA KUFUATIA MAUZO MABAYA YA TIKETI

Janet Jackson amefuta ziara yake kimuziki 'Unbreakable' barani Ulaya kufuatia mauzo mabaya ya tiketi barani humo. 'Alikuwa anaelekea kushindwa vibaya' kilisema chanzo cha habari. Muuza tiket mkuu alimuandikia barua pepe Janet mapema wiki hii kuhusu kurudishwa kwa hela za watu waliokuwa wamenunua tiketi. Hii ni wiki tatu kabla Janet alikuwa aende kufanya onesho jijini London, 'haitawezekana kwa sasa kusema ni lini tutapanga tena tarehe mpya ya onesho kwa hiyo tunarudisha hela kwa wale waliokuwa wamenunua tiketi' iliandikwa hivyo barua pepe hiyo. Upande wa Janet haukuzungumzia kuhusu kufutwa kwa onesho hilo lakini chanzo cha habari kilisema kuwa ni kufuatia mauzo mabay ya tiketi. 'Alikuwa anaelekea kushindwa vibaya, msanii anapofuta au kuahirisha ziara ya muziki sababu huwa ni mauzo mabaya ya tiketi' kilisema chanzo hicho na kuongeza 'ni bora kuahirisha kuliko kufanya onesho ukumbi ukiwa haujajaa watu haswa kwa msanii Janet Jackson'. Cha...

MECHI KATI YA LEICESTER NA WEST BROM FAHAMU HAYA

Mchezo wa leo kati ya Leicester city na West Bromwich Albion utapigwa katika dimba la King Power Stadium, ambapo Leicester watakuwa ni wenyeji wa dimba hilo. Mtanange utaanza saa 4 na dakika 45 usiku saa za Afrika Mashariki. Novemba 1, 2013, West Brom alimfunga Leicester goli moja bila katika dimba la King Power Stadium. Mwaka 2015, April 11 West Brom wakiwa wenyeji katika dimba la nyumbani, The Hawthorns walipigwa bao tatu dhidi ya mbili na Leicister city. Lakini pia October 31, mwaka jana 2015, West Brom akiwa mwenyeji kwenye dimba la The Hawthorns alifungwa na Leicester city magoli 3 kwa mawili kama mechi iliyopita. Leicester City inaongoza ligi ikiwa na pointi 56 ambapo imecheza mechi 27 imeshinda mechi 16, imetoka sare mechi 8, na kupoteza mechi 3 ikiwa na magoli ya kifunga 20. Kwa upande wa West Brom wao wapo katika nafasi ya 13 wakiwa wamecheza mechi 27, wameshinda mechi 9, sare mechi 8 na kupoteza mechi 10 wakiwa wmemfungwa magoli10. West Brom wana pointi...

MAMBO YA KUFAHAMU KATI YA CHELSEA NA NORWICH CITY

Chelsea imeshinda mechi saba na haijapoteza katika mechi tisa ilizokutana na Norwich City kwenye EPL. Norwich City imefenikiwa kuifunga Chelsea magoli manne tu na kushindwa katika mechi nne ambazo walikutana mara ya mwisho na The Blues. Steven Naismith wa Norwich City amefanikiwa kuifunga Chelsea magoli sita katima mechi saba walizokutana na The Blues EPL. Norwich City imeshinda mechi nne tu, sare nne na kupotezaechi nane katika mechi 16 ilizocheza katika dimba lao la nyumbani, Carrow Road. (W4 D4 L8). Norwich City imepata magoli 10 tu katika dimba lao la nyumbani, hii ni baada ya kushinda mechi mbili kati ya tano za EPL katika dimba hilo. Katika mechi 7 za EPL na kufunga magoli 7 pamoja na kuwa na jumla ya magoli 19 kwenye ligi. Chelsea imeshuhudia wachezaji wake 15 wakiifungia magoli timu hiyo msimu huu. Rekodi ambayo ni ya juu zaidi katika mashindani msimu huu. Guus Hiddink amepoteza mechi moja tu kati ya mechi 23 kama kocha na meneja wa klabu katika...

ROBOTI XINGHZE1 ATEMBEA KILOMITA 134 KUWEKA REKODI MPYA

Roboti aliyepewa jina la Xinghze No. 1 aliyetengenezwa nchini China, amevunja rekodi ya Dunia ya 'Guinness World Records' kwa kutembea kilomita 134.03 ambazo ni sawa na maili 83.28 (83.28 miles). Roboti huyo aliyetengenezwa na team iliyoongozwa na Profesa Li Qingdu kutoka College of Automation of Chongqing University of Posts and Telecommunications. Roboti huyo aina ya Quadruped ametengenezwa kwa mashine moja ambayo inaongozwa na program ya kompyuta au sakiti moja ya umeme. Pia, roboti huyo ameundwa kwa miguu minne (Four legs) isiyo na magurudumu (wheels). Mwongozo uliotolewa na Guinness World Records ni kwamba ili Roboti avunje rekodi ya Dunia kutembeanumbali mrefu, anatakiwa kuchajiwa mara moja au kutumia tanki moja la mafuta na pia anatakiwa atembee mfululizo kwa masaa takribani 54 na dakika 34 ili kuipiku rekodi inayoshikiliwa na jopo Chuo Kikuu cha Cornell Ranger Robot ambapo roboti wao alitembea umbali wa kilomita 65.18 sawa na maili 40.5, roboti Walker 1, aliv...

BIBI WA MIAKA 85 AKAMATWA KWA KUIBA HERENI

Bibi kizee mmoja mwenye umri wa miaka 85 raia wa Marekani na ambaye amekuwa akiiba vito vya thamani kwa zaidi ya miaka 60 amehukumiwa tena kwa kosa la wizi. Doris Payne, anatuhumiwa kwa wizi wa herini ya thamani ya dola 690, kutoka katika duka moja la uuzaji wa vitu vya thamani la Saks katika kiunga kimoja mjini Atlanta-Marekani. Wakili wake anatafuta namna ataachiwa huru kwa sababu ya kudorora kwa afya yake. Payne, ambaye maisha yake ya wizi yaliwekwa katika filamu mwaka 2013, amewahi kufungwa jela mara kadhaa kwa makosa mengi tu ya wizi na uhalifu. Wakuu nchini Marekani wanasema kuwa, ametumia majina 22 ya bandia tangu alipoiba almasi kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 23, na akaweza kukwepa kutiwa mbaroni. Muungano wa Walinzi wa vitu vya thamani JSA, kampuni moja kubwa ya kibiashara, ilituma tahadhari kwa maduka yote yanayouza bidhaa na mapambo ya thamani kujihadhari na mwizi huyo sugu mapema miaka ya 70. Rais wa kampuni hiyo kubwa alitaja tabia ya bi kizee huyo ...

DOGMATIC BLUSTERY WEATHER A POEM BY VENANCE GILBERT

Poem: Dogmatic Blustery Weather Poet:  Venance Gilbert Composed September 27, 2015 Published on October 21, 2015. The blustery weather blows wherever By a hair's breadth in the oceans and ponds Wind vane regularly measure the breeze. The blustery weather has now turned to policies Particularly in this phase of the GE Propelling hard to the populations; the electorates Populations frequently size them lyrics Whichever the runners’ dogmas or troop expression. It is the blustery weather since it blows to constituents The dogmatic blustery weather will measured in the poll Majority, make it take place on October Be pacific under open and just environments. ALL RIGHTS RESERVED. Venance Gilbert © 2015

DOWNLOAD WIMBO MPYA: TOFA EMCEE-KUNG FU PANDA

Anaitwa Christopher Robert jina la kazi ya sanaa 'Tofa Emcee'.  Tofa Emcee katika picha. Picha kwa hisani ya Facebook account Christoper TofaEmcee Robert Donload Kung Fu Panda kwa kubofya HAPA.