MECHI YA ATLETICO & REAL MADRID KULINDWA NA POLISI 2,000

Polisi wa kukabiliana na fujo walikabiliana na mashabiki wa Bayern Munich mnamo 18 Aprili
Polisi wa kukabiliana na fujo walikabiliana na mashabiki wa Bayern Munich mnamo 18 Aprili
Walinzi zaidi ya 2,000 watatumiwa kudumisha usalama na kudhibiti mashabiki wakati wa mechi ya nusufainali ya mkondo wa kwanza kati ya Real Madrid na Atletico Madrid katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Mechi hiyo itakayochezewa Santiago Bernabeu siku ya Jumanne imeorodheshwa kama yenye "hatari kubwa" na usalama "utaimarishwa", maafisa wasimamizi wa jiji la Madrid walisema Ijumaa.

UEFA wameamrisha usalama katika mechi za klabu Ulaya uimarishwe baada ya shambulio kwenye basi la timu ya Borussia Dortmund mnamo 11 Aprili.

Atletico watakuwa na mashabiki 4,000 katika uwanja huo wa Real unaotoshea mashabiki 80,000.
Kawaida ni mashabiki wachache sana husafiri kuhudhuria mechi za ugenini Uhispania.

Idadi ya walinzi tarehe 2 Mei itakuwa ya juu zaidi ya waliokuwepo wakati wa mechi iliyopita ya Real Ulaya dhidi ya Bayern Munich polisi wa kukabiliana na fujo walipokabiliana na mashabiki wageni wakati wa mapumziko.

Kulikuwa pia na fujo mechi ya robofainali ya Atletico nyumbani, polisi wakikabiliana na mashabiki wa Leicester City.

Chanzo: BBC

WAFAHAMU MARAIS 10 WA AFRIKA WALIOFARIKI WAKIWA MADARAKANI

Leo nimekuandikia orodha ya marais 10 waliofariki wakiwa madarakani. Tuanze kuhesabu sasa:

Lansana Conté, President of Guinea 
10. Lansana Conte, Rais wa Guinea
Baada ya miaka 24 Lansana Conte alifariki na ugonjwa usiojulikana akiwa na umri wa miaka 74. Alipambana na matatizo ya kisukari na maradhi ya moyo. Kuanzia Aprili 1984 mpaka kifo chake Desemba 2008 alikuwa ni rais wa pili kushika madaraka nchini Guinea. Mbali na matatizo ya afya aliyokuwa nayo aliweza kushinda uchaguzi.


Flash - Galerie Verstorbene Persönlichkeiten 2009 Omar Bongo (AP) 

9. Omar Bongo, Rais wa Gabon

Saratani ya tumbo iliosambaa ndio iliyosababisha kifo cha Rais Omar Bongo June 2009 mjini Barcelona, Uhispania, baada ya kuwa rais kwa miaka 42 mfululizo. Alifariki akiwa na umri wa miaka 72 na pia alikuwa ni kiongozi aliyekaa madarakani kwa muda mrefu katika historia na alikuwa akiongoza katika mambo ya rushwa. Bongo alijikusanyia utajiri mkubwa huku akiiacha nchi yake katika hali ya umasikini. 


João Bernardo Vieira, President of Guinea-Bissau 

8. Joao Bernardo Vieira, Rais wa Guinea-Bissau

Joao Bernardo Vieira rais wa Guinea-Bissau aliuwawa nchi mwake Machi 2009, akiwa na umri wa miaka 69. Alikuwa kiongozi wa nchi kwa muda wa miaka 31. 1978 alikuwa waziri mkuu na kuchukua madaraka 1980 na alitawala kwa miaka 19. Alibadilika na kuwa kiongozi wa umma na aliongoza miaka minne mingine zaidi. 2005 alishinda tena uchaguzi wa uraisi. 


Umaru Musa Yar’Adua, President of Nigeria  

7. Umaru Musa Yar’Adua, Rais wa Nigeria

Umaru Musa Yar’Adua, alifariki akiwa na umri wa miaka 58 mwaka 2011 akisumbuliwa na matatizo ya moyo nchini Nigeria. Alikuwa madarakani kwa miaka mitatu pekee. Alikosekana katika kampeni za uchaguzi kwa sababu za kiafya. Baada ya kuchaguliwa kwake 2007, afya yake ilidhoofika kwa haraka. 


Muammar Gaddafi, Brotherly Leader and Guide to the Revolution of Libya  

6. Muammar Gadhafi, kiongozi na mwana mapinduzi wa Libya

Mwathirika wa mauaji, Muammar Gadhafi aliuawa akiwa na umri wa miaka 69 na vikosi vya waasi katika mazingira yasiyoeleweka nchini Libya, baada ya kuwa kiongozi wa taifa hilo kwa muda wa miaka 42. Aliuondoa uongozi wa kifalme bila ya kumwaga damu wakati wa mapinduzi ya kijeshi ya mwaka 1969 lakini utawala wake ulifikia kikomo baada ya matokeo ya vuguvugu la mapinduzi ya uarabuni. 


Malam Bacai Sanhá, President of Guinea Bissau 

5. Malam Bacai Sanha, Rais wa Guinea-Bissau

Kiongozi wa nne kufariki mwaka 2012 alikuwa ni Malam Bacai Sanha rais wa Guinea-Bissau. Aliugua ugonjwa wa kisukari na alifariki mjini Paris baada ya miaka minne kama rais akiwa na umri wa miaka 64. Katika kipindi chote cha utawala wake alisumbuliwa na matatizo kadhaa ya kiafya yalosababisha kwenda hospitali mara nyingi.

Bingu wa Mutharika, President of Malawi  

4. Bingu wa Mutharika, Rais wa Malawi

Rais mwingine aliyefariki mwaka 2012 ni Bingu wa Mutharika, rais wa Malawi. Alipata mshutuko wa moyo mwezi Aprili na kufariki siku mbili baadae akiwa na umri wa miaka 78. Uongozi wake ulikuwa ni wa miaka nane na alipata mafanikio makubwa katika sera zake za kilimo na chakula. Sifa yake iliharibika kufuatia maandamano makubwa yalopinga ununuzi wa ndege ya rais iliyogharimu Dola milioni 14


John Atta Mills, President of Ghana 

3. John Atta Mills, Rais wa Ghana

Pia mwaka 2012, John Atta Mills, rais wa Ghana alifariki akiwa nyumbani kwake kwa mshutuko wa moyo na saratani ya koo akiwa na umri wa miaka 68. Alishinda uchaguzi wa rais wa 2008 alishika madaraka kwa miaka mitatu pekee. Alianzisha mikakati mingi ya kiuchumi na mageuzi ya kiuchumi yalomletea sifa kutoka ndani na nje ya nchi. 

Meles Zenawi, Prime Minister of Ethiopia 

2. Meles Zenawi, Waziri Mkuu wa Ethiopia

Meles Zenawi alifariki Agosti 2012 nchini Ubelgiji akiwa na umri wa miaka 57 kwa maambukizi yasiyojulikana. Ameiongoza Ethiopia kwa miaka 5 kama rais kuanzia mwaka 1991 hadi 1995 na kama Waziri Mkuu kwa miaka 17 kuanzia 1995 hadi 2012. Anajulikana kwa kuanzisha mfumo wa siasa wa vyama vingi, lakini pia kwa ukandamizaji wa maandamano halali ya watu wa Oromia wa kaskazini mwa Ethiopia. 

Michael Sata, President of Zambia 

1. Michael Sata, Rais wa Zambia

Michael Sata ni kiongozi wa hivi karibuni aliyefariki madarakani akiwa na umri wa miaka 77 kwa maradhi ambayo hayakuwekwa wazi Oktoba 28 2014, nchini Uingereza. Baada ya uchaguzi wa 2011, uvumi juu ya afya yake ulisambaa nchini Zambia. Kukosekana kwake katika shughuli kubwa za kitaifa kuliibua wasiwasi wa afya yake ingawa msemaji wake alisema alikuwa katika afya nzuri.




Chanzo: DW Idhaa ya Kiswahili.

THE WHEEL A POEM BY VENANCE GILBERT

Venance on the sitting benches of Vikenge Hostels, Mzumbe University Main Campus Morogoro

Poet: Venance Gilbert
Poem: The Wheel
Composition: October 18, 2016
Publication: April 20, 2017
Copyright: Venance Gilbert  2016



The wheel was moving
But I never noticed
second counted, minutes gone,
hours died, days were numbered
weeks moved, months and years passed
I noticed it as the matter of living.

Mental pictures remind me
those days when the moments existed
Sometimes I wish to restore and start
I find the wheel moving fast following the line
Like the train on its pathway
Happy birthday takes back to those moments.

Today I am youth
Full capable to place the mind on motion
I often regret when I remember the moment
The moment when I was the driver of the wheel
But now the wheel drives, how possible?
I never drove it well and careful at the moment,
Drive the wheel careful before it drive you on its pathway.

DOWNLOAD JAY2 THE HUSTLER X CAST BEEZY-TIME IS NOW


Hii ni mpya kutoka kwa Jay2 th hustler & Cast beezy-Time is Now.

DOWNLOAD HARMONIZE & RICH MAVOKO-SHOW ME NEW SONG

Tokeo la picha la harmonize & mavoko show me 
Brand new track kutoka WCB. Harmonize & Rich Mavoko wametuletea hii, Show Me

DOWNLOAD

WANASAYANSI WAGUNDUA UHAI KATIKA SAYARI YA SATURN

Sayari ya Saturn
Sayari ya Sarateni "Saturn"

Mwezi wa Enceladus ambao uko kwenye sayari ya Saturn huenda ukawa mahali bora zaidi pa kwenda kutafuta maisha nje ya dunia.

Tathmini hii inatokea kufuatia uchunguzi katika sayari hiyo yenye kilomita 500 uliofanywa na Cassini.

Uchambuzi wa kemia wa Cassini unaonyesha matundu ya maji moto kwenye sakafu ya bahari ya Enceladus, maeneo ambayo yanahusishwa na kuwepo kwa maisha, hapa duniani.

Kuwepo kwa maji haya sio thibitisho kamili kwamba vitu vilivyo na uhai vinaishi katika mwezi huo mdogo lakini teknolojia zinaweza kutumika kupima maji hayo na kutoa ushahidi zaidi.

"Tuna uhakika kuwa kitu chenye uhai kinaweza kuishi kwenye bahari ya Enceladus lakini lazima tufanye utafiti zaidi," alisema mwanasayansi wa Cassini kutoka Taasisi ya Utafiti ya Southwest, San Antonio, Dkt. Hunter Waite.

"Iwapo hakuna maisha huko, ni sawa, lakini ikiwa maisha yapo itakuwa bora zaidi," alieleza BBC.
Bahari iliyopo kwenye Enceladus inakisiwa kuwa na kina kirefusana sana na yapo majimaji kwa sababu ya joto linalotokana na mvuto wa mara kwa mara kutoka kwenye sayari ya Saturn.

Cassini tayari amedhibitisha kwamba maji hayo yanashikana na sakafu ya bahari kutokana na aina ya chumvi na silika ambayo pia imeonekana katika mashimo.
 
Lakini wanachotaka kujua sana wanasayansi ni ikiwa maswala fulani yanayotendeka duniani pia yanaweza kufanyika katika Enceladus - kitu kinachoitwa serpentinisation, ambayo hutengeneza gesi ya hidrojeni.

"Kwa viumbe hai, hidrojeni huwa ni kama kama pipi - ni chakula wanachokienzi," alieleza Dkt Chris McKay, mwanabiolojia wa maswala ya anga wa shirika la Nasa.

"Ni nzuri sana kwa kuvipa nguvu, na inaweza kusaidia viumbe vidogo sana. Kupata hidrojeni itakuwa vizuri sana na itakuwa moja ya ushahidi utakaoonyesha uwezekano wa kuwepo na uhai."

Viumbe hai anavyozungumzia Dkt McKay vinaitwa methanojeni kwa sababu vinatengeneza gesi ya metheni vinapogusana na hidrojeni na gesi ya kaboni .

Nasa, ambayo inaongoza ujumbe wa Cassini , ilitakikana kufanya tangazo la hidrojeni miezi michache baada ya uchunguzi wa mwisho waroketi ya mwezini, Oktoba mwaka wa 2015.

Ziara ya Cassini sasa inakamilika . Baada ya kuizunguka Saturn kwa muda wa miaka 12, inaendelea kuishiwa na mafuta na sasa itawachiliwa kuingia kwenye anga ya dunia hiyo ya Saturn mwezi Septemba, kuhakikisha kuwa haiwezi kugongana na Enceladus na kusababisha kuchafuka kwake.


Chanzo: BBC

DOWNLOAD ACHA NIKAE KIMYA DOWNLOAD PLATNUMZ NEW SONG

Huu ni wimbo mpya kuhusu hali inayoendelea nchini hivi sasa. Diamond pia ameamua kuzungumza kwa namna yake.