KIONGOZI WA AL SHABAAB AJISALIMISHA

Mmoja wa viongozi wakuu wa zamani wa kundi la wapiganaji wa Al-shabaab, Hassa Dahir Aweyes amewasili mjini Mogadishu chini ya ulinzi mkali wa vikosi vya serikali. Hata hivyo haijulikani iwapo kiongozi huyo amesalimu amri auameamua kujiunga na vikosi hivyo vya serikali. Ijumaa iliopita, umoja wa mataifaulitangaza kuwa Bwana Hassa Dahir alikuwa amejisalimisha kwavikosi vya serikali ya Somali lakinimadai hayo yakapingwa na wazee wa koo za taifa hilo. Kiongozi huyo alikuwa amechukua hifadhi katika mji wa Kazkazini wa Adado baada ya makabiliano makali kuzuka kati ya kambi tofauti za wapiganaji wa Al Shabaab juma lililopita. Kiongozi huyo ametajwa kama gaidi na umoja wa mataifa pamoja na serikali ya marekani. ©2013 Venance

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI