IDADI YA WATU WALIOFARIKI UGANDA YAFIKIA 33

Moto mkubwa uliowaka baada yaajali mbaya ya barabarani iliohusisha lori la mafuta, umewauwa takriban watu 33 mjini kampala Uganda. Watu wengine 30 wanadaiwa kujeruhiwa vibaya kufuatia tukiohilo. Maafisa wa polisi wanasema kuwa kati ya waliofariki ni raia waliokuwa wanakimbilia eneo hilo la mkasa kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwa lori hilo. maafisa wa serikali walikuwa katika harakati za kutambua mili ya waliofariki baada ya wengi wao kuchomeka vibaya. Idara ya polisi imesema kuwa waliofariki waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI